Mpendwa Mheshimiwa Zitto,
Hivi karibuni katika moja ya thread humu JF, nilisema kuwa Rostam Aziz amenunua viongozi wetu wengi wa kisiasa, nikasema kuwa huyo bwana anamwagilia miche yote maana hajui upi utakao chipua. Nikawasema kwa majina watu ambao wamekuwa wakifadhiliwa na RA hata nikaandika kuwa Rostam alichangia kwenye kampeni za ODM ya Kenya.
Nilsema kuwa sijui nani anafadhili masomo yako huko ughaibuni lakini nikasema bayana kuwa Rostam ndiye aliyegharimia masomo ya Mbatia huko huko ughaibuni. Sasa mambo yanayoendelea kwenye chama chenu yanatia wasiwasi mpaka sisi wapiganaji tunaona kama kamanda wetu umenunuliwa na huyo huyo Rostam. Tuna wasi wasi mkubwa kwa sababu tunajua jinsi mbinu chafu za fisadi huyo. ninakuomba usije ukatumbukia katika mtego huu wa kifisadi na kujitoa CHADEMA ukaenda NCCR,
NCCR Mageuzi ni chama chenye historia ya kukumbatia mamluki, wapo wengi na wengi wamepitia hapo. Lakini kitendo chako cha hivi karibuni kufadhili swahiba wako aliyefulia na kuanza kutukana chama chako unachokiongoza, kimeleta wasiwasi mkubwa kwetu, sisi tunaokuamini na kukuheshimu.
Hatujui mbinu hiyo ya kuibomoa chadema ni ajenda ya nani!!! kamwe sitaki kuamini kuwa wewe Zitto Kabwe tunayekujua waweza kusaliti vuguvugu la kukomboa nchi hii na kujiunga na mafisadi wachumia tumbo! Hatutaki kukubalia na hoja zozote za kututenga wewe na sisi, maana bado tunakuhitaji mstari wa mbele wa mapambano.
Mpendwa Zitto, mbona umebadilika hivi kwa siku za karibuni? Kwanza ulianza kutetea kununuliwa kwa Dowans, baadaye ukaona vema kupimana nguvu na ikiwezekana umwondoe Freeman kwenye uenyekiti wa chama. Kukaa kidogo ukaanza kumsifia Idrisa Rashid, Fisadi na tapeli wa kutupwa aliyesababisha NBC kufilisika na kuuzwa kwa bei chee ambaye pia amehusika kwa tuhuma za ufisadi mkubwa mkubwa wote hapa nchini. Zitto mdogo wangu, bado hayo yalipokwisha ukaanza kuwakumbatia watu wanaovuruga chama unachoongoza na bado unawakumbatia!! kwani ungetegemea katibu wa chama awafanye nini wafanyakazi wa chama wanao kiuka utaratibu??
Zitto, kwa kweli sikubaliani na wewe kumtetea kafulia kwa vyovyote na kama ulishiriki kumshauri ajiondoe kwenye chama, ulifanya makosa makubwa na umejiunga na wahaini wengine wowote. Kwani Kafulila ilikuwa ni lazima awe Ofisa wa Chama? kwa nini hakukubaliana kuacha hiyo ofisi akajiimarisha na kisha kuwa kugombea na kuwa kiongozi?
CHADEMA ni kubwa kuliko mtu yeyote. Si Mtei, Mbowe, Slaa au wewe ambaye ni mkubwa kuliko Chadema, kwa hiyo ilikuwa ni vyema kama kuna hoja ambazo tumezisikia kwa Kafulia akupatie wewe au ampe mtu mwingine ziwasilishwe kwenye vikao vya chama. Kafulila alikuwa anahoji utiaji wa saini kama nani? Je mnataka sisi watu wa mitaani ndiyo tujadili na kuwashauri nyinyi kamati kuu ya CHADEMA nani atie saini na nani asitie? hilo si ni jambo la ki utendaji tu? au Freeman ndie amekuwa mwenyekiti wa kwanza kutia saini zake kwenye hundi?
Mpendwa Zitto kama umesukumwa na mafisadi kubadilika hivi, ujue umma wa watanzania tuliokuwa nyuma yako tutakuacha na utakuwa mwenyewe wewe na mbatia na Rostam. Hakika utapotea kama alivyopotea Marando, Lamwai na Kabouru. Fikiria sana kabla hujaamua chochote. Nyota yako inawaka kwenye CHADEMA na itazimika wakati wowote. Ebu Muheshimiwa, mtafute DK Slaa, mjadili a way forward kabla mambo hayajakuharibikia, najua thamani yako kwenye CHADEMA haitapungua hasa baada ya kuwa mkomavu na kuondoa jina lako kwenye uchaguzi ule.
Wasalaam