Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

Ni sahihi kusema kwamba neno bahati hutumika kumaanisha kukosa ujuzi wa kujua sababu za hayo matukio kutokea kwa namna yalivyotokea au yanavyotokea?
upo sahihi pia, ila muktadha mfano wa kuzaliwa leo hii, elon musk, mo dewji, bakhresa, dangote na matajiri wengine wakipata mtoto hatujui nani atazaliwa ila ni wazi huyo mtoto shida za fedha, kupata elimu nzuri, nafasi ya kupata huduma bora zozote zinakua jambo la kusema tu.

tofauti na kuzaliwa ukanda wa Turkana kule kenya wanapopakana na kina sudan --- kupata janga la njaa ni suala la kufumba na kufumbua


View: https://youtube.com/shorts/HjmRIhvDcLg?si=fyp1Scdt18DzfWFl
 
Ni sahihi kusema kwamba neno bahati hutumika kumaanisha kukosa ujuzi wa kujua sababu za hayo matukio kutokea kwa namna yalivyotokea au yanavyotokea?
Kwani lazima kila jambo liwe na sababu au meaning??
 
Kwa sababu ni makisio dhaifu sana , makisio ya historia na evolution watu wanayosoma wanayafanyia utafiti na bado wanaacha mlango wazi kwa mawazo mbadala ukosoaji na hata kurekebisha ikibidi, sio kama nyie wachawi ambao tayari mmeshafikia conclusion na ni experiences zenu binafsi tu.
Nyie ndio mmefanya conclusion na mmefunga mlango na ndio maana kuna wakati mnafikia kusema hakuna uchawi ila ni mambo tu ambayo hatujayaelewa bado. Na bora sie tunaeleza experience zetu kuliko nyie mnatumia nadharia, mtu anakuja hapa anasema waganga wanacheza na akili zetu tu hakuna ukweli halafu huyo mtu mwenyewe hajawahi hata kwenda kwa mganga ila anajifanya anajua yanayotendeka huko kwa waganga.
 
uganga kweli upo na somehow unafanya kazi na matokeo yanaonekana japo fix zipo nyingi sana (kila mganga atakuambia hii dawa ninayokupa mtu akikugusa tu anakwenda na maji)
Dawa ninayokupa imwagie uwanjani kwako asubuhi ukiamka utamkuta mchawi kadondoka hawezi kuruka.
Hii dawa ninayokupa ifunge mlangoni kesho asubuhi ukiamka utamkuta mchawi kanasa haondoki hadi umfungue mwenyewe.
Hahaha waganga wanacheza na saikolojia yako tu kukunasa wakupige hela asilimia 90 wanaishi kwa janjajanja
 
Yoda sasa hiyo Nguvu.
Wanaiojua inavutwaje na kuipata ndio wanaitumia kwa namna mbali mbali.

Wengne Kuanzisha Dini.
Wengne Uchawi na Uganga.
Wengne kuongoza watu nk.

Ila kuna Nguvu iko ndan yetu. Na inatuzunguka.
kwasababu ya hiyo nguvu ndio Uchawi, Mungu, Uganga upo na mengne yapo na yanawezekana.
Wengine kuanzisha dini

Hii point ndio yenye mashiko haswaa
Dini zote chanzo chake ni mizimu na Majini wao ndio waasisi wa hizo so called sheria 10 and the likes but Kuna machache yameongezewa na watu


Siko hapa kwaajili ya kubishana I'm nazungumza kile Ambacho ninacho kifahamu Tena indeep
 
Kwanza Mungu tunayemwamini ndiye? Ukikonekti doti zote unagundua uhusiano mkubwa sana uliopo kati ya Mungu wa wakristo na Miungu ya dini zingine, yaani Wahindu, Budha na hata waislamu, halafu unagundua kuwa ni Mungu kutoka katika familia ya Miungu(Yaani uzao wa EL), Pia unagundua kuwa Ukisema Mungu sio mmoja isipokuwa imelazimishwa haonekane kuwa ni mmoja(From Polytheism to Monoitheism).
Alama zote za Miungu ya dini zote zinazopatikana toka Mesopotamia(Iran na Iraq),Teotihuacan,Egypt, Maya na Zimbabwe zote zinafanana na zinahusiana na Mungu wa Wakatoliki( Annunaki).
Alama zote zinahusiana na Miungu Annunaki ambao ni uzao wa Anu(EL), Kumbuka jina Israel ni kifupi cha ISIS(Mungu mke), RA(Mwana wa Mungu) na EL(Mungu mkuu-Baba) dhana ya utatu.
Israel ni jina linaloonyesha uzao wa ISIS,RA NA EL.
Na mwendelezo wa EL unaonekana kwa GabriEL,EmmanuEL,MichaEL.
Unaongea mambo mazito sana ngumu kueleweka na baadhi ya watu
 
📌📌🔨
mambo ya kiroho/kimungu au ya ulimwengu usioonekana, niyakufanya wewe mwenyewe na roho yako. Maana mungu ni roho na roho iko ndani yako na wewe upo ndani ya ulimwengu wa kiroho.
Itoshe kusema hakuna padre wala katekista, hakuna askofu, nabii wala mchungaji, hakuna sheikh wala ustaadh anayeweza kukusaidia katika mambo ya kiroho sana sana atakupa miongozo tu ya hapa na pale kutokana na kitabu cha dini husika, miongozo ambayo hata yeye haijawahi kumsaidia.
Safari ya kiroho ni ya mtu mmoja na muongozo mkuu ni roho iliyopo ndani yako, au Mungu aliyepo ndani yako.
Huko nyumba za ibada pelekeni sadaka tu ila mtatoka kama mlivyoingia.
Dig deep to the root,
Dig deep to the truth.
 
Unaelewa nini maana ya elimu ni bahari?? Njoo Zanzibar, sehemu inaitwa Matemwe nikuonyeshe uchawi kwa macho yako ,halafu uje uhadithie humu.

Uliwahi kuona ngamia anazama ardhini mwenyewe na kupotea?? Njoo ujionee kwa macho yako kinachofanyika mpaka anazama mwenyewe.

Tupunguze ujuaji kwenye vitu ambavyo hatuna uwezo navyo coz elimu ni bahari.

Yaani wewe hujiulizi Rais wa nchi anavalishwa mangozi ya wanyama na kusimikwa uchifu kila anapokwenda, unafikiri ni kawaida ile??

Yaani wewe na kidigrii chako au kimaster unahisi unajua kuliko serikali plus wale wazee??
😁😁😁🤣🤣🤣

Tatizo ukishaleta jambo online humu Kila mtu ni mjuaji sometimes unasoma comments za watu unaishia kucheka tu ,

Maisha the way yalivyo sio wote tunao uwezo wakujua Kila kitu but Honestly guys Kuna mambo ambayo yapo Juu yetu na hayaeleweki Katka ulimwengu wa kawaida kirahisi
 
sasa mkuu middle east wanadundana Allah na Yahweh wanahusika vipi mkuu,

wakati nikiwasikiliza analyst wa kimarekani wanasema israel huwa aridhiki na anachopewa marekani F35 hawakutaka mtu yeyote atumie ila wakafosi kama kawaida yao ikabidi waundiwe F35i, hali kadhalika Iran humwambii kitu kwenye kuziunda drone na missile,


sasa mkuu kiroho ila umesema twende zenji tukaone ngamia anavyozama , hii imekaaje?
😁😁😄😄
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
hapo naweza kukubaliana na wewe kwa kiasi chake, kwa sababu wote tunataka kuwasikia hao wachawi ila inakua ngumu.


dhana ya ukoloni binafsi unaweza sema ndo kipimo changu cha juu sana kwa story za uchawi , kama tunaweza kukubaliana mtu anaweza tumia uchawi akamdhuru mtu mtu, akafanya aumwe, arukwe na akili, afe hapa afrika sidhani kama tungehitajika kubeba bunduki kupambana na mkoloni au wala tungehitaji kwenda UN kuomba uhuru wala kumuomba malkia uhuru --- magavana wa kikoloni wale na wanajeshi wao wangekua wanapigwa kipapai tu kweisha habari yao, sasa hapa hua kuna mgogoro kwa kua tunaambiwa haufanyi kazi katika namna hii --- na ukiuliza sasa unafanya kazi vipi , wanaoleta story za uchawi mara nyingi wanakimbia


mkuu story za uchawi tunazozisikia basi yawezekana hata wanaotupa hizo story na wao hawafahamu wanachosema --- kama tutakubaliana hapo litakua jambo jema.

bro uchawi mimi binafsi angekuja mtu akanipa huu apa atleast huu wa story tulizozisikia hapa bongo tusingekua tunailalamikia serikali jambo lolote
Huwezi kusema dhana ya ukoloni ndio kipimo chako cha uchawi kwa sababu hakuna mahusiano ya moja kwa moja na uchawi na hilo suala la ukoloni hadi ikawa ndio kipimo chako, hao wazee wetu hawakuwa na tawala za kichawi kiasi cha kudhani wangetumia huo uchawi kama silaha au kujilinda katika mapambano.

Lakini pia kama nilivyosema kwamba kushikilia hili la ukoloni hiyo tena sio kutaka kupata ukweli wa uwepo wa uchawi bali mie naona ni kama unahoji nguvu ya uchawi.

Sasa mkuu badala ya kukaa na kusikiliza tu story za watu kuhusu uchawi na sijui kusubiri wakuletee uthibitisho, kwanini usichunguze mwenyewe? Mfano min-me yeye anasema kafanya utafiti masuala ya imani za kichawi katika upande wa afya, mimi ndio napenda kuona vitu kama hivyo hata mkijadiliana kuna hatua mnasogea.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Back
Top Bottom