Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

Kwahiyo hizi kafara, misukule, mali za kitajiri, kusababisha uchizi kwa watu na malimbwata ni vitu vya uongo? Mbona vina matokeo na tunaona watu wakivipitia..
Watakwam ia kuwa hao misukule ni watu wanaoigiza.. na hata hao matajiri ni matapeli wanaorubuni wajinga ili wawatapeli...
 
Chumvi ya mawe humkinga mtu kwa muda. Na hapo utakapoitumia, ni kama umejichoresha kwao. Yaani hata kama hawakijui, ukishaitumia, ni kama umejiingiza kwenye rada yao.

Ili uwe salama basi yakupasa kuitumia mara kwa mara kama mtu atumiavyo ARV... Tazama watumiaji wanavyokuwa watumwa... Watu hawataki kusali, kutwa kucha ni kuoga dawa..
Mtu anazijua dawa mpaka anajiona keshakuwa mganga...

Imani za mambo ya kishirikina zinatesa sana watu.
 
Unaamini luck?
Ndio, naamini kuzaliwa Marekani, Canada, Australia, Ulaya, Korea Kusini, Japan au Gulf countries ni bahati inayokupa chance kubwa zaidi ya kufanikiwa na kuishi maisha mazuri kuliko kuzaliwa Sudan, Congo au Tanzania.

Kuzaliwa familia tajiri ni bahati,
Kuzaliwa na IQ kubwa ni bahati,
Kuzaliwa na genes zisizosumbuliwa na magonjwa ni bahati
Kama ni mwanamke kuolewa na tajiri ni bahati
Kwenda kuchimba madini na vifaa duni kisha kuibukia lundo la madini ni bahati
Zipo bahati nyingi sana tofauti kwa wanadamu mbalimbali
 
Kwanza hakuna Imani ya ukweli na imani ya uongo kwenye haya masuala ya superstitions, kinachotofautina ni kiwango tu cha msimamo, ujinga na madhara yanayotokana na hizo imani tofauti. Mtu akiamini paka mweusi aliyekatiza mbele yake au bundi aliyekuwa mlangoni kwake ni ishara ya jambo baya ni ujinga lakini hakuna madhara yoyote kwake au wanaomzunguka. Mtu anayeamini viungo vya binadamu vinaweza kumpa mafanikio au mtu ambaye hataki kwenda hospitali akiwa magonjwa kwa sababu ya hizo superstitions huo ni ujinga unaoweza kuambatana na madhara makubwa na maafa.
Shida mkuu mkiongea nyie maneno matupu hapa mnataka hayo mnayoeleza yachukuliwe kuwa ndio uhalisia mzima na ndio sahihi ila wengine wakieleza wanaonekana wanaeleza story za kubuni.
 
Kwahiyo hizi kafara, misukule, mali za kitajiri, kusababisha uchizi kwa watu na malimbwata ni vitu vya uongo? Mbona vina matokeo na tunaona watu wakivipitia..
Hakuna lolote mkuu.
Sayansi inaelezeaa yote Kwa usahihi.
Mambo ya limbwatwa ni uongo, sijui misukule na blah blah kibao.
Nikiwa mdogo tulikuwa tunaambiwa ukienda mtoni usiku sana huko ni vibaya, mashetani na vikaragosi wanafanya ibada zao, wanafua nguo na kuosha vyombo vyako.
Freshi nikakubali.
Nikiwa tabora mjini kukawa na stori kibao kuhusu makabuli Fulani Yako nje kidogo ya mji kwamba hapo makabulini usiku wa manane haukatizi pale maana kumejaa uchawi na misukule ndiyo muda wake, MIMI NIKAENDA KULALA HAPO HAPO MAKABULINI KUANZIA SAA 4 MPAKA NAONDOKA ALFAJIRI YA SAA 12 SIJAONA CHOCHOTE ZAIDI YA USUMBUFU WA MBU TU.
Baadae watu nawaambia nimelala pale makaburi ila sijaona chochote wanakataa wanasema haiwezekani nilale pale makabulini halafu asubuhi niamke salama.
Nikatulia zangu kimya maana sitaki migogoro na kubishana
 
Sijawahi kusikia story ya uchawi au miujiza isiyo na matobo mengi ya kutosha mpaka najiuliza mtu anawezaje kuamini ujinga wa jinsi hii wa wazi kabisa. Hata hivyo pia ubongo unaweza kutengeneza hallucinations, illusions na false reality kwa sababu nyingi mbalimbali ikiwemo madawa ya kulevya, njaa, ugonjwa, ndoto, maumivu, hofu, PTSD, uchovu, magic tricks n.k
Wewe umemaliza Kila kitu mkuu kunywa soda nalipia hapa
 
Ndio, naamini kuzaliwa Marekani, Canada, Australia, Ulaya, Korea Kusini, Japan au Gulf countries ni bahati inayokupa chance kubwa zaidi ya kufanikiwa na kuishi maisha mazuri kuliko kuzaliwa Sudan, Congo au Tanzania.

Kuzaliwa familia tajiri ni bahati,
Kuzaliwa na IQ kubwa ni bahati,
Kuzaliwa na genes zisizosumbuliwa na magonjwa ni bahati
Kama ni mwanamke kuolewa na tajiri ni bahati
Kwenda kuchimba madini na vifaa duni kisha kuibukia lundo la madini ni bahati
Zipo bahati nyingi sana tofauti kwa wanadamu mbalimbali
Unaweza ukaelezea hiyo bahati inafanyaje kazi? Nataka kujua inakuaje hadi bahati inawapata wengine na wengine hawaipati?

Halafu kuna kinachoitwa bahati mbaya, hii nayo vp ipo na unaamini ama vp?
 


Sijajifunga kwenye experience yangu, wala sihitaji kuona directly niamini, nahitaji hata maelezo yaliyonyooka tu yanayoelezea tukio hata moja tu la uchawi. Mambo ya uchawi ukiacha tu kwamba huwa hayana uthibitisho wowote hata story zenyewe huwa zina matobo na contradictions sana kiasi kwamba ni vigumu kuaminika.

Taarifa/Story kutoka sehemu tofauti tofauti wala sio uthibitisho wa chochote zaidi ya kwamba binadamu ni kiumbe wa kutengeneza story na kuziamini mfano utaifa, uzalendo, dini na pesa yote ni mambo yaliyotokana na story tu zilizoaminiwa kwa muda mrefu na watu wengi.

UKIMWI upo kwa sababu Kuna uthibitisho wa kutosha wa kisayansi wa virus na jinsi vinavyofanya kazi. Unaweza kufanya jaribio(experiment) la UKIMWI kwa watu bilioni kwa kurudia njia zile zile na ukapata matokeo yale yale kwa 99%, Huwezi kufanya jaribio la uchawi la kujirudia hata kwa watu kumi tu ili uweze kufanya majumuisho ni kitu gani.
Mbona sasa kuna wanasayansi na madaktari wenye kupinga issue ya uwepo wa virusi vya ukimwi? Kama upo uthibitisho wa kisayansi wa kuwepo hivyo virusi vya ukimwi mbona kuna wanasayansi wanapinga kuwa sio kweli?

Halafu hivi kila uthibitisho huwa ni wa kisayansi tu? Hivi kwa mfano kwenye masuala ya historia huwa pia inatumika sayansi kuthibitisha ukweli wa historia?
 
hivi mkuu siku samia akasimama bungeni au ikulu akahutubia kwamba nchi yetu imelogwa ndo maana watu wamekufa oct 29, mali zetu zinapotea bila habari we utakubali?
Kwani wewe ulikubali aliposema Tanzania ipo vizuri kiuchumi kushinda Marekani?
 
Unaweza ukaelezea hiyo bahati inafanyaje kazi? Nataka kujua inakuaje hadi bahati inawapata wengine na wengine hawaipati?

Halafu kuna kinachoitwa bahati mbaya, hii nayo vp ipo na unaamini ama vp?
Sijui kwa nini wewe umezaliwa Tandahimba na Mark Zuckerberg amezaliwa New York. Sijui kwa nini IQ yako ni ndogo kuliko ya kwake, sijui kwa nini Rizimoko na Abdul wamepata bahati ya kuishi Magogoni wakati Soka, Mdude na Ben Saanane hawakupata hiyo bahati, Sina majibu ya sababu zake, najua tu ni random chances.
 
Chumvi ya mawe humkinga mtu kwa muda. Na hapo utakapoitumia, ni kama umejichoresha kwao. Yaani hata kama hawakijui, ukishaitumia, ni kama umejiingiza kwenye rada yao.

Ili uwe salama basi yakupasa kuitumia mara kwa mara kama mtu atumiavyo ARV... Tazama watumiaji wanavyokuwa watumwa... Watu hawataki kusali, kutwa kucha ni kuoga dawa..
Mtu anazijua dawa mpaka anajiona keshakuwa mganga...

Imani za mambo ya kishirikina zinatesa sana watu.
Vile vile hauwezi kusali mara moja tu ukasema umemaliza, inahitaji kusali na kuomba kila mara, kuhudhuria sana kanisani au misikitini, kufunga na kushinda njaa mara kwa mara n.k

Pande zote mbili UTUMWA HAUEPUKIKI NA KUTESANA BURE TU iwe ni kwa washirikina au kwa wanaosali.

Ukibishi njoo na hoja...
 



Mbona sasa kuna wanasayansi na madaktari wenye kupinga issue ya uwepo wa virusi vya ukimwi? Kama upo uthibitisho wa kisayansi wa kuwepo hivyo virusi vya ukimwi mbona kuna wanasayansi wanapinga kuwa sio kweli?

Halafu hivi kila uthibitisho huwa ni wa kisayansi tu? Hivi kwa mfano kwenye masuala ya historia huwa pia inatumika sayansi kuthibitisha ukweli wa historia?
Kupinga au kubishania uthibitisho uliopo ni jambo moja, kutokuwepo uthibitisho ni jambo lingine kabisa. Wanaopinga uthibitisho wa kisayansi mfano Dunia kuwa duara (flat earthers), HIV kusababisha AIDS au uthabiti wa chanjo(anti-vaxxers) hao wanawekwa kwenye kundi la conspiracy theorists na pseudoscientists.

Kwenye Science Kuna
Natural Science
Social sciences
Archaeological science
Astronomy
Kwenye History kuna "scientific methods" za dating, Paleontology, forensic document examination n.k

Halafu unachosha sasa na maswali yako ambayo ulipaswa uwe unayafahamu wakati unamaliza kidato cha nne.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom