Al Mukheef
JF-Expert Member
- Dec 7, 2025
- 284
- 415
Faida zake ni kutenganisha watu,kufanya mtu au watu wakupende au wampende mwingine,kusababishia wengine matatizo na kudanganya machosasa una faida gani hata kama upo?
Faida zake ni kutenganisha watu,kufanya mtu au watu wakupende au wampende mwingine,kusababishia wengine matatizo na kudanganya machosasa una faida gani hata kama upo?
Kama mambo yako beyond our reasoning and thinking kwa nini unasema ni ya kiroho? Umejuaje ni ya kiroho? Umethibitishaje ni ya kiroho? Mambo ya kiroho ni mambo gani kwanza??Hebu tuwaze kwa kuweka Udini pembeni.
Tuwaze kwa kuweka Mungu. Uganga na Uchawi pembeni.
Tuwaze tukiwa Neutral ground.
Najua unaamini kuna mambo watu wanaweza kufanya ambayo kwa hali ya kawaida mtu asingeweza Kufanya.
Pia kuna mambo ya Kiroho ambayo hata ww unajua yako beyond our reasoning and thinking.
Je Haya tuyaiteje?.
mfano.
Ushawah kuota kitu alaf huko mbele kikatokea vile vile?.
Ushawah kumuwaza mtu na yeye anakuwaza muda huo huo?.
Ushawah kunuia kitu na kikatokea?.
Najua ushawah haya yote.
Je tuiwekeje hii?.
Kama mambo yako beyond our reasoning and thinking kwa nini unasema ni ya kiroho? Umejuaje ni ya kiroho?
Kama mambo yako nje ya uwezo wako wa kawaida wa akili ina huyaelewi na haufahamu, haithibitishi chochote kwamba ni mambo ya kiroho au yaliyo nje ya uhalisia, ni kwamba tu hujayafahamu na kuyaelewa kwa akili zako, ishia hapo.
Unaweza kumleta mchawi au mganga hata mmoja anayeweza kuelezea na kuthibitisha mtu ukitoa kafara, ukipewa dawa au ukizindikwa utapata pesa au mafanikio??Ww pia unajua na hujaelewa yanatokeaje.
Ila kuna watu wanajua na wanatumia kufanya yasiyowezekana kikawaida kuwezekana.
Uchawi upo. Mm nishashuhudia
Najua utasema ni story. Ila i wish siku moja ukutane nao.
Unaweza kumleta mchawi au mganga hata mmoja anayeweza kuelezea na kuthibitisha mtu ukitoa kafara, ukipewa dawa au ukizindikwa utapata pesa au mafanikio??
Mkuu wala usielezee zaid! Watakuja kukuponda wasomi uchwara wa JFHakuna shida naweza kufunguka ila ningependa kwa kujua unataka nikufahamishe kuhusu kitu gani kuhusu hayo mambo
Kujua mambo mengi sio tatizo ila shida inakuja kujua uhalisia wa hayo mambo. Unaweza ukawa unajua mambo mengi kwa kusikia na kusoma kuhusu Marekani lakini isiwe yote uliyosoma na kusikia ikawa ndio uhalisia wenyewe wa maisha ya huko Marekani yaliyvyo.Najua mambo mengi tu ya afya na sijawahi kusoma hata course moja ya udaktari au unesi. Najua mambo mengi ya Marekani japo sijawahi kufika huko, najua mambo mengi ya Waislamu na sijawahi kutia mguu msikitini au madrasa.
Me nisaidie kitu kimoja tu, njoo PM niachie majina ya hivo vitabu tuHabarini wakuu
Leo nimeona nikumbuke matukio niliyoyashuhudia ambayo yananiweka mdomo wazi na sijui nilikuwa nawaza nini(nitabase zaid upande wa kiroho)
Kwanza kabisa mimi ni aina ile ya watu ambao tunataka kujua kila kitu hata kama ni vya hatari ila nitajilazimisha nijue tu.
MImi ni mkatoriki ila sikua nyuma sana kuna kipindi niliamua kulivalia njuga swala la dini na kuchimba kidogo juu ya imani kwa ujumla na kupata mwanga fulani kuhusu imani niliyopo hasa swala la kuitwa wakatorik tunaabudu sanamu, ukweli ni kwamba hatuabudu sanamu ila kuna gap dogo sana ukiteleza kidogo utaangukia kwenye kuabudu sanamu
Maisha yakaenda mm kama binadamu nilipitia mapito fulani kimaisha nikayumba kiuchumi..nilijaribu kutatua changamoto zangu mwisho wa siku nikaangukia kwenye mambo ya waganga..uganga kweli upo na somehow unafanya kazi na matokeo yanaonekana japo fix zipo nyingi sana (kila mganga atakuambia hii dawa ninayokupa mtu akikugusa tu anakwenda na maji)
Nafsi yangu ilikuwa inagoma sana kuamini mambo ya kiganga na uchawi ila ndo hivyo tena maji yalikua yanaifika shingoni nikawa najikuta tu naenda kupata msaada
SIku moja nilikaa nikajiuliza kwanini naenda kwa mganga na huko kwa mganga natajiwa jina la mungu, nikaona ngoja niuchimbe kwanza huo uganga na uchawi unafanyaje kazi na kwanini upo
Nilifanikiwa kusoma vitabu vinne vya uchawi na uganga (jina kapuni kwasababu ni vya hatari kidogo)
Ndani yake nilifunguka kiakili sana nikaja kugundua uganga ama uchawi kwanza kabisa unaanza na wewe kuwa na imani ya hicho unachokifanya
Pili ni lazima kuwe na roho ambayo inakupa muongozo wa nini cha kufanya ili kufanikisha jambo lako
mtu ili kuwa mchawi kwa level wa chini kabisa inaweza kumchukua wiki tatu mpaka miezi 18 mpaka kuweza kufanya mambo ambayo yapo kinyume na mungu japo hivyo vitabu vinaita hiyo ni elimu safi na tuitumie kwa wema
TAtu. Uchawi ama uganga ni lazima uende kinyume na muumba hata kama majina yanayotamkwa ni ya muumba ila pale yanatamkwa kama dhihaka tu na hilo ndio lengo kuu ili uchawi uweze kufanya kazi
Uchawi unahusisha zaidi matumizi ya alama hasa nyota,duara na pembe, ukimaliziwa na maneno maalumu ili kuipa nguvu pamoja na imani ya kwamba unachokitamka kinakwenda kutokea
Matumizi ya vitu kama chumvi, hirizi,talasin ni mabaya sana kwasababu yanakufa uhisi nguvu inatoka kwenye hivyo vitu na sio muumba(mnaoshauriana kutumia chumvi ili kujikinga ama kusafisha nyota naomba mnisamehe bure)
NIliyoyashuhudia kwenye hiyo elimu ni makubwa sana na yalinifanya niujue ulimwengu na kujikita zaidi kwa muumba wangu na kuachana kabisa na hizo imani
Nguvu za giza zipo ila zile ni njia za mkato tu ambazo zinampumbaza mwanadamu na kumpeleka shimoni, ukiingia huko lazma upotee tu iwe kwa kujua ama kutokujua
Dunia ina mengi sana na mimi sio mwandishi mzuri wa magazeti hivyo naishia hapa kukiwa na swali lolote nitajitahidi kulijibu ama nikishindwa nitasaidiwa na mliopo humu
Ungeweza kufanikisha utajiri kwa kutumia hizo nguvu zinazo daiwa ni za kichawi.Mimi sipingi ila nahoji, umeleta hoja kwamba uchawi ungekuwepo afrika ingekuwa matajiri, sijapinga kutokuwepo kwa uchawi bali nimehoji huo uchawi ungekuwepo ungewezaji kufanikisha afrika kuwa matajiri?
Si huwa mnasema ndoto ni mawazo tu ya mtu kwa siku hiyo.Tuiwekeje mtu anayeota ndoto anakoja usingizini halafu anajikojolea kweli kitandani?
Kwani ni uchawi ni nguvu zenye kuhusu utajiri?Ungeweza kufanikisha utajiri kwa kutumia hizo nguvu zinazo daiwa ni za kichawi.
Wapi ulinisoma nikisema hivyo??Si huwa mnasema ndoto ni mawazo tu ya mtu kwa siku hiyo.
Nice story, but doesn't cut itNina amini wako.
Ila mm sina connection ya makafara . Hayo muombe Al-mukheef .
Nishashuhudia ndugu yangu kabisa wa karibu tunalala usiku anaongea na sisi vizur.
Alaf asubuh hawez kuongea. Anaongea kama bubu (aba aba aba nying).
hosp kadhaa ameenda. Mapicha na Xray za kutosha. Na hakuna kitu.
Ni dawa za usingiz alipewa ili Ubongo utulie maana waliamini ni Hitilaf ya Ubongo.
Miez 6 tukampeleka Handen kwa Mababu Zetu. Akakaa wiki 2. Akarud anaongea 😂😂😂😂.
Mm mwenyewe nishawah fanyiwa mavitu vitu. So naelewa.
Hizi nguvu hata usipoita Uchawi. Ila ziko bro.
Hata kwa mambo ambayo mtu anategemea kuona matokeo ya hiyo nguvu ya uganga nje ya huyo mtu? Mfano kwenda kumroga mtu mwengine?Hakuna uganga unaofanya kazi,
Wanacheza na akili yako,
Pseudo Effects.