Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

Wachawi na watu wao wanaoamini uchawi wamejiwekea loopholes nyingi sana, mara waseme uchawi haufanyi kazi benki, mara uchawi haufanyi kazi kwa mtu usiyemjua, mara uchawi hauvuki maji na upuuzi mwingine mwingi tu, ni mental gymnastics tu.
Wachawi ni nani hasa? Nakuuliza hivyo kwa sababu nimeona hapo kwamba unasema wachawi wamejiwekea loopholes kwamba wanasema hivi na vile, mimi binafsi hadi leo hii sijawahi kushuhudia mtu anayejitambulisha kuwa ni mchawi na akawa anaeleza mambo yenye kuwahusu wachawi na uchawi wao.
 
Anyway wewe unataka uchawi upi? Ule wa quran(sio mgumu kama inavyodhaniwa kwasababu inatumia maneno ambayo yamezoeleka)

Ama unataka ule wa kale? Japo huu ni mgumu kiasi inaweza kukuchukua kuanzia miez 6 mpaka kukamilika
Uchawi wa kale ni upi na unaanzia miaka ipi mpaka ipi?
 
kitambo sana wanasema huko benki wachawi wake ndo balaa sana 🤣
Ila hizi hoja zengine ni kama mnajitekenya na kucheka wenyewe, hivi wewe unavyohoji issue ya wachawi au kutumika uchawi kuiba bank, hivi hata ikitokea ukasikia kuna bank inasema wameibiwa pesa kichawi wewe utakubali hilo suala kuwa ni kweli pesa zinaweza kuibiwa kichawi?

Kama chuma ulete haukubali na habari hizo zimejaa kibao, sasa nashangaa hili la bank kuonekana hoja ya msingi wakati hata kungekuwa na story za malamiko ya bank kuibiwa pesa kichawi bado usingekubali tu kwa sababu kama zilezile za kutoamini story za chuma ulete.

Ndio maana nasema inakuwa kama mnajitekenya wenyewe na kucheka.
 
Uchawi upo ndugu zangu na sio jambo la kushabikia lengo la huu uzi sio kujionesha kujua kitu fulani lengo langu kuu ni kufungua uwepo wa muumba kwasababu wengi huamini njia za mkato pekee na wakati njia ya muumba ndio njia sahihi
Naomba unisaidie tu majina ya hivyo vitabu, kama hapa haiwezekani njoo hata PM
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Sasa na yeye akikuuliza swali kama hilo utajibu nini? Yani akikuuliza unahakika gani hakuna uchawi na si kwamba kutokujua kwako tu maarifa ya uchawi ndio kunafanya useme hakuna uchawi utajibu nini?

Kwa sababu ukiangalia sidhani kama katika experience yako ya maisha umewahi kushiriki ama kushuhudia mwenyewe katika mambo ambayo yalihusishwa na uchawi, kwako wewe uchawi ni issue za kusikia tu na si zaidi ya hapo.
Sayansi inathibitika kimantiki ila Uchawi haithibitiki

Sayansi inawekwa wazi ila Uchawi huwa ujafanywa kuwa siri KWANINI?
 
Na binafsi siamini kama kuna mtu humu ambaye ni mgeni wa maneno "UCHAWI"

UCHAWI ni neno ambalo likitajwa wote tunakuwa tunaelewa muktadha unalenga nini.

Lakini kama katika mjadala kuna mtu amehoji nini maana ya uchawi wala haiwezi kuwa jambo geni kwasababu kwenye mjadala premises za hoja zinaanzia katika definition.

Kuna uwezekano katika mazungumzo yenu kuna mambo umeyaongea ambayo hayaja match na taarifa zake juu ya jambo hilo hivyo anakuomba umpe maana ili aelewe zaidi.

Kwa mfano neno SHETANI tunaweza kuliona kama lipo universal likielezea kitu chenye maana moja inayogusa jamii nyingi.

Lakini kama neno SHETANI tutalifanya mjadala wa kuanza kujadili undani wake, basi hapo tunaweza kuona haja ya maana kwasabau katika ukristo SHETANI ni malaika muhasi wakati katika Uislamu stori ni tofauti.

Kwa hiyo kama mimi nilijenga hoja katika perception ya Ukristo kuhusu SHETANI halafu nikaona kuna sehemu hatuendi sawa basi ni sahihi kuhoji maana ya SHETANI ili nijue upande wako unatafsiri gani.
Umeeleza sawa sawia kabisa.

Sasa mtu amekuja humu akaeleza kwamba uchawi hakuna na akatoa hoja kwamba uchawi ungekuwepo basi afrika ingekuwa tajiri? Unamuuliza ki vp afrika ingekuwa tajiri kama uchawi ungekuwepo?
Hapo hapo haujaeleza kitu chochote chenye kupingana na maelezo yake wala hakuna ulichompinga, ila mtu badala ajibu anaanza kukuuliza definition ya uchawi? Wakati swali aliloulizwa halipo tofauti na huo muktadha tunao ukusudia.

Mwengine anasema uganga hauna nguvu yeyote, ni kwamba waganga wanacheza tu na akili za mtu. Unamuuliza vp mganga anaweza kucheza na akili yangu endapo mimi nikienda kwake mganga na kutaka huyo mganga amfanyie mtu uchawi yani amroge mtu mwengine?
Mtu anakuja kukuuliza kuroga ndio nini? Uchawi ndio nini?

Sasa ni vyema mtu mwenyewe ukaeleza mie najua definition hii ya neno uchawi, kuliko kudhani mtu mwengine hajakuelewa na kuanza kumtaka akupe definition ya uchawi, matokeo yake mnaweza mkaanza kubishana kuhusu definition tena.
 
Sayansi inathibitika kimantiki ila Uchawi haithibitiki

Sayansi inawekwa wazi ila Uchawi huwa ujafanywa kuwa siri KWANINI?
Sayansi ina misingi yake na mipaka yake, kuna aina tofauti za uthibitisho au kuthibitisha jambo kwenye nyanja tofauti na uthibitisho wa kisayansi ni mmoja wapo tu. Sasa huku kusema kwamba uchawi hauthibitiki au hakuna uthibitisho wa uchawi mara nyingi huwa mnakusudia uthibitisho wa kisayansi, na uchawi hauendani na zile kanuni za kisayansi.
 
sasa mbona wenye taarifa za uchawi hilo swali wakiulizwa wanaingia mitini? na uzi kimsingi mara nyingi hukwama mahali hapo
Labda waingie mitini kutokana na ubishi wenu kwa sababu ni kazi ngumu kujaribu kumuelewesha mtu kitu asichokielewa ilhali ametangulia kupinga hicho kitu asichokielewa.

Sasa mtu anatumia zile imani potofu za watu zenye kuhusishwa na uchawi na kusema hakuna uchawi ni imani potofu tu za watu kushindwa kuelewa mambo yalivyo, utafikiri imani potofu huwa zipo kwenye kwenye uchawi tu.
 
Kwaiyo unamaanisha yeye ni mkuu wa wachawi mpaka useme hivyo?

Nadhani kuna kitu utakua unachanganya, serikali yenyewe inaendesha nchi kulingana na vitu vinavyoonekana. Viongizi wengi wana imani zao tofauti ili kuepusha mkanganyiko wa kiimani serikali imeamua kutenganisha imani ya mtu binafsi na katiba

Leo hii kiongozi wa irani anaweza kusema wao wanashambuliwa kwasababu ya uislam wao na wao wanatetea uislam wao..hapa utaona kiongozi wa irani yupo huru kuingiza imani kwenye mambo ya kiserikali tofauti na ulivyosema hapa kwetu rais ahutubie bunge kama tumelogwa(kwetu haikuwa na nguvu kwasababu tupo imani tofauti)
mi nimesema ikitokea kasema hivyo wewe utakubali?
 
Wachawi ni nani hasa? Nakuuliza hivyo kwa sababu nimeona hapo kwamba unasema wachawi wamejiwekea loopholes kwamba wanasema hivi na vile, mimi binafsi hadi leo hii sijawahi kushuhudia mtu anayejitambulisha kuwa ni mchawi na akawa anaeleza mambo yenye kuwahusu wachawi na uchawi wao.
Wala usiende mbali, Wewe mwenyewe mchawi /mshirikina, mleta uzi naye pia mchawi
 
Nikikuambia mimi nilizaliwa mzungu wa denmark ila nilichoma sindano na kuwa mtanzania mwenye asili ya mbeya utakubali?
Labda kama umejichubua kwa kitaulo kama wanawake wa Mbeya
 
Luck, connections, exploitation, inheritance, crime etc
Sure,
Hizo huwa zinafichwa fichwa sana.
Mtu anaweza akavunja sheria na akatusua.

Ijapo nafikiri Connection and Luck zinachangiwa na:

—Kuonewa huruma,
—How you communicate,
—Family line (Ndugu yako anaweza kukutengenezea nafasi),
—Fiendship,
—Your habits (Uvumilivu, Ujasiri, Uaminifu etc),
—Mda mwingine ule ukaribu wenu tu.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Labda waingie mitini kutokana na ubishi wenu kwa sababu ni kazi ngumu kujaribu kumuelewesha mtu kitu asichokielewa ilhali ametangulia kupinga hicho kitu asichokielewa.

Sasa mtu anatumia zile imani potofu za watu zenye kuhusishwa na uchawi na kusema hakuna uchawi ni imani potofu tu za watu kushindwa kuelewa mambo yalivyo, utafikiri imani potofu huwa zipo kwenye kwenye uchawi tu.

mimi binafsi hadi leo hii sijawahi kushuhudia mtu anayejitambulisha kuwa ni mchawi na akawa anaeleza mambo yenye kuwahusu wachawi na uchawi wao.
naam, basi tusubiri watu wanaojitambulisha wachawi, au walioujua uchawi waje tuone maelezo yao mkuu, ili mambo yasiwe mengi

kwasababu story zilizopo ni za kusikia kama tunavyosikia hapa kwa mdau mtoa mada
story za kusikika miongozni mwao ndo hizo za kusababishia watu matatizo/magonjwa nk, hapo tukiwa tunauliza unafanyaje kazi lengo lake ni kuangalia mfano mkoloni kaja na bunduki nini kilishindikana kuwapiga magonjwa au kuwatoa akili wawe mazezeta wakoloni

wengine wanasema zinaleta pesa, mali nk au hata mtu tunaweza sema akaingia nyumbani kwa mtu kwa njia zisizo za kawaida sasa njia hii haiwezi tumika kwenda kuchukua hata madini au fedha madukani? zikatumika kujitajirisha?

sasa ukiuliza maswali kama haya wanasema hivyo sio uchawi unavyopiga kazi --- sasa watupe namna ulivyo na unapigaje kazi ili tupime upya tuachane na story za kusikia,

mwisho wa siku kama hapo mtoa mada kasema kasoma vitabu kama vinne, wadau wameomba avitume au hata aweke majina --- mpaka muda huu jambo hilo halijafanyika na anasema ni vitabu vya hatari

sasa kwa muktadha huo kwanini tusiendelee kutumia story zinazovuma tu huku mtaani mkuu?

mada za hivi karibu kila siku zinaishia kwa kutokukubaliana, hapa karibuni at least ule uzi wa yule jama aalienda kwao tanga "alsisi" niliishia mwanzomwazo tu sjui nini kiiendelea ila alikua anajaribu kueleza matukio mbalimbali kwamba huyo jamaa anaweza mwambia hata mambo ya mbele, watu wakawa wanamuuliza mambo ya uchaguzi 2025 utakuaje naye sidhani kama alikua anajibu kwenye sekta hiyo.

so mwisho wa siku watu wanataka kitu cha kutesti
 
Sayansi ina misingi yake na mipaka yake, kuna aina tofauti za uthibitisho au kuthibitisha jambo kwenye nyanja tofauti na uthibitisho wa kisayansi ni mmoja wapo tu. Sasa huku kusema kwamba uchawi hauthibitiki au hakuna uthibitisho wa uchawi mara nyingi huwa mnakusudia uthibitisho wa kisayansi, na uchawi hauendani na zile kanuni za kisayansi.
Uchawi unathibitishwa kwa kanuni zipi?
 
Zipo nyingi sana naweza kuzileta ikawa mada mpya kabisa kujadili ipi ni sahihi, ndio maana nimekuuliza kwa vile unavyoelewa hadi ukajenga hoja ya kwamba huo uchawi ungekuwepo afrika ingekuwa tajiri.

Uchawi unahusu utajiri?
Zilete kwanza.
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Kwahiyo hizi kafara, misukule, mali za kitajiri, kusababisha uchizi kwa watu na malimbwata ni vitu vya uongo? Mbona vina matokeo na tunaona watu wakivipitia..
Watakwam ia kuwa hao misukule ni watu wanaoigiza.. na hata hao matajiri ni matapeli wanaorubuni wajinga ili wawatapeli...
 
Back
Top Bottom