Did Nyerere admit he was a "failure"? Some say "Yes he did"...

Did Nyerere admit he was a "failure"? Some say "Yes he did"...

Safi sana kwa kuwa wewe ni muungwana, lakini sifa mojawapo ya uungwana ni kukubali ukweli hiyo sifa mkuu wangu wewe uliitelekeza wapi? maana hutaki kukubali japo kidogo kwamba Mwalimu nyerere kuna mambo aliyofanikiwa katika uongozi wake.
Kweli kuna ambayo alifanikiwa kuyatekeleza, kama vile kuunganisha Tanganyika na Zanzibar, kupeleka majeshi nje ya Tanzania, kuuwa maduka ya Ushirika, kuanzisha Azimio la Arusha na kunyang'anya mali za wananchi, alisababisha watu kuvaa magunia na makatambuga, foleni za unga kwenye maduka ya kaya, pia alizuiya watu wasiendeshe magari siku za mwisho wa wiki, yaani kuendesha gari siku ya jumamosi na jumapili ilikuwa kwa kibali maalum.
 
X-Paster,
Nyerere alikuwa mwanafalsafa. He could speak tongue in cheek. Hii ya kufananisha kushindwa kwa ujamaa na ukristo inaangukia kwenye ligi hiyo hiyo. Last time I looked Christianity was doing well.
Kwani unafikiria alivyosema hivyo, wenye imani zao walikaa kimya, walijaribu kumpinga ati... Ndio wakamwambia kuwa ujamaa ndio ulioshindwa...!
 
Nakubaliana na wewe kua Nyerere aliondoka baada ya nchi kwenda mrama na hakuwa tena na njia ya kurekebisha mambo. Alikua na tatizo kuwa kubadilisha muongozo ni aibu au atageuka jiwe

Kuhusu vyama vingi wewe umerudi sana nyuma 1964 mimi nazungumzia pale alipong'atuka 1985 kama sikosei ndipo alipo pendekeza kuruhusiwa vyama vingine na pia kuweka kikomo cha vipindi viwili kwa rais kukaa madarakani.
Nimekuelewa mkuu, sasa kama alipendkeza hao aliyo yapendekeza, tungemuona wa maana sana hayo mambo yangekuwa kipindi yupo madarakani, yamemshinda ndio anatoa mapendekezo.
 
Was it necessary to make a public admission to see the obvious that he failed miserably?
 
Hilo linatakiwa kumaliza mjadala.
[/URL][/B]


Sasa hii ni hoja nzuri tu; he failed economically compared to what other country's economy? Are there any rational and scientific reasons why our economy failed beside blaming it on Nyerere as a person - we will have to compare with the economy of other nations at the same time. If Our economy was the only one that didn't do well (compared to other nations similar to ours) then Nyerere should be blamed for it.



Well.. hapa unaleta proposition nzuri - yawezekana kulikuwa na matatizo zaidi ya watu waliokuwa juu - maana Nyerere tunaambiwa ni sababu ya Ujamaa lakini Moi alikuwa anafuata Ubepari! Banda alikuwa anafuata Ubepari na Kaunda Ujamaa wa aina yake? Mobutu alikuwa anafuata ubepari na per capita ilionekana kubwa - was it a success? Yawezekana kulikuwa na factors nyingine zilizochangia kuvurugika kwa uchumi?

Ukisoma huu Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano uliopitishwa na Kikwete juzi hakuna sehemu yoyote ambayo wanaseema uchumi wetu ulianguka kwa sababu ya Nyerere na wanataja sababu mbalimbali zilizokabili uchumi wetu.
Mkuu wangu katika swala la kuanguka kiuchumi nadhani hatuna sababu ya kulinganisha na nchi nyinginezo kwa sababu itakuwa utnaukimbia ukweli. Sisi tuli fail, so are many nations kama vile leo Greece wanavyolia haina maana Ureno na nchi nyingine za Ulaya ziko salama. Kifupi leo hii uchumi umeshuka kila mahala lakini, picha kubwa ipo Ugiriki na inabidi tuseme rais wao au wagiriki wame fail, ingawaje Taifa halitakufa kesho .

Na labda niseme Nyerere failed sio kwa sababu ya Ujamaa bali ni sawa na nyumba ziliyojengwa kwa drywall na mbao zikapigwa na dhoruba ya kimbunga (Tornado), sasa ziole zilizokuwepo katikati ya dhoruba zitaathirika zaidi ya zile za pembeni na pia hatuwezi kusema zile zilizoweza kupona zimejengwa imara zaidi ya zile zilizoharibiwa. Factors za ku detarmine uimara wa nyumba haupimwi baada ya madhara bali wakati wa ujenzi...

Na ndipo napomsifu Nyerere kwamba yeye aliwekeza sana ktk miundombinu na viwanda ambayo ilimchukua zaidi ya miaka 15 ya utawala wake kuijenga (toka 1967 to 1982) lakini wazalendo hawakuweza kuona faida yake kwa sababu ujenzi wa miundombinu na viwanda hivyo ulitufiksha kula Bulga na maziwa ya msaada kwani walichotegemea ni ujenzi wenye kuzaa kama dhahabu. Wanahesabu madeni ya kujenga miundombinu hiyo kama hasara wakati ni miundombinu hiyo na viwanda ambavyo leo vinatumika kuendesha uchumi wa serikali hizi toka Mwinyi hadi Mkapa.

Yote haya yamesaulika na kuitwa FAILURE simply because kimbunga cha 1982 na leo tumesahahu kwamba ni wakati nchi kubwa zinazotoa mafuta duniani zilikuwa ktk hekaheka ya vita (Iran vs Iraq) dunia nzima iliyumba kiuchumi leo Taifa ambalo fedha yake yote limewekeza ktk miundombinu na viwanda lingeweza vipi kuhimili vishindo tena baada ya vita ya Uganda.

Pamoja na yote yale na sababu zote zilizokuwepo lakini bado tukubali kwamba tulishindwa! we failed kama mzee wa Kariakoo aliyejenga nyumba ya vyumba sita ataonekana hakuwa na akili kuliko huyu mtoto wake aliyewtumia nyumba ile ile kuipangisha au kuivunja na kujenga ghorofa ambalo limewapa watoto hawa maisha bora zaidi ya yale waliyokulia chini ya himaya ya mzee baba yao.

Na hakika hawatakumbuka nguvu ya mzee kuijenga nyumba ile ambayo pengine ili cost only Tsh 5,000 lakini kwa mshahara wa Tsh 50 kwa mwezi (a thousand times) lakini sisi wenyewe kizazi kipya na mshahara wa Tsh 500,000 tunashindwa hata kununua kiwanja.
Imagine our elderly sacrifice, lakini waulize hao MasharoUharo wa Kariakoo utasikia makosa yote ya dingi, he failed us! angenizaa mimi ktk tajiri - NINGEKUWA bl;aa! blaa! blaaa!

Kwa hiyo mawazo mengi against Nyerere ni ya hawa Masharouharo ambao walitaka watengewe kila kitu mezani wao waje kujichana kama vile hakuna najsi!..Miafrika ndivyo Tulivyo!
 
Kuddddaddaadadadake..... haki ya nani tena JF darasa, tena lile la kitivo cha sayansi chuo kikuu!!!

Nyie nipeni mwaka mwingine mmoja tu hapa, ashakum si matusi, lazima niiondoke na PhD ya JF 🙂

Kamanda Mkandara, yaani unashuka nondo utafikiri umetafuna encyclopedia ya ulimwengu na kuimeza yote bila kusikia kiu wala kupata ukakasi mdomoni.... yaani mi pointi inateleza tu bang bang bang bang bila nyodo wala huruma na kutapakaa JF!! Luv it man🙂
 
Na labda niseme Nyerere failed sio kwa sababu ya Ujamaa bali ni sawa na nyumba ziliyojengwa kwa drywall na mbao zikapigwa na dhoruba ya kimbunga (Tornado), sasa ziole zilizokuwepo katikati ya dhoruba zitaathirika zaidi ya zile za pembeni na pia hatuwezi kusema zile zilizoweza kupona zimejengwa imara zaidi ya zile zilizoharibiwa. Factors za ku detarmine uimara wa nyumba haupimwi baada ya madhara bali wakati wa ujenzi...

Kweli wanasema "penye wazee..". Inafahamika vizuri tu kuna mambo mengi ambayo Nyerere hakufanikiwa kuyatimiza kama alivyotaka au alivyoona intellectually. Kushindwa huku kwa kiuongozi ni sehemu ya utawala wowote duniani; ni viongozi wachache sana (kama wapo) ambao waliweza kurelialize maono yao yote. Nyerere kama viongozi wengine aliongoza taifa katika maono ya aina fulani na kwa kiasi chake alifanikiwa na kwa kiasi chake hakufanikiwa.

Hii ndio sababu ya ile hotuba yake ya "mambo ya kijinga mnayaacha na mazuri mnayaendeleza"; yaani uongozi ni kuachiana mafanikio na mapungufu. Kama Nyerere angeweza kusolve matatizo yote yaliyoikabili Tanzania kama wengine wanaoashiria kuwa ilimpasa angekuwa Mungu! Kiini cha changamoto alizokutana nazo Nyerere mwanzo wa taifa letu huwa najiuliza kama Kikwete ndiyo angekuwa Rais wetu au Mkapa sijui tungekuwaje!

That aside, mgogoro uliopo ukiuangalia si wa kujadiliana mapungufu na makosa ya utawala wa Nyerere bali ni kile ambacho kinaitwa demonizing Nyerere kwa kuanza kumuita majina mbalimbali. Ukiangalia sana Nyerere anabebeshwa lawama za kila kitu ili kujaribu kufuta na kulazimisha kusahauliwa mchango wake katika ujenzi wa taifa.

Leo tunawasikia watu wakisema waziwazi:

a. Nyerere hakuleta umoja aliukuta
b. Nyerere alikuwa mbaguzi wa kidini
c. Nyerere alikuwa mbaguzi wa kikabila
d. Nyerere alikuwa muuaji
e. Nyerere hakufanya jambo lolote la maana
n.k n.k

Hawataki kujadili kuonesha mapungufu au makosa ambayo hata yeye mwenyewe alikuwa wazi kuyakiri na mtu yeyote ambaye anajua historia yetu anajua yalifanyika - hayakuwa siri - nimewaambia watu mara nyingi wasome kijitabu cha "tujisahihishe" hadi natamani kukiweka digital ili kuwapa mwanga watu waelewe kuwa Nyerere hakuwa mtu aliyelewa sifa za kijinga kuwa hakuweza kuona makosa yoyote.

Lugha inayotumika kufikia lengo hili ndio inazidi kuchochea mgongano huu. Makosa (mistakes) yanaanza kuitwa "Mabaya ya Nyerere", mapungufu yanaitwa "failures of Nyerere" n.k Sitoshangaa (baada ya kuweza kufanikiwa kuliweka jina la dikteta) the logical progression itakuwa ni "maovu ya Nyerere". Yote ni katika kuhakikisha kuwa nostalgia ambayo baadhi ya watu wanayo juu ya Nyerere inafutika kwani ukishafuta mchango wa Nyerere hakuna kilichobakia. Ndio maana kina Kikwete hawawezi hata kusema Baba wa Taifa kwa sababu hawaamini the unique contribution of Nyerere to the founding of our nation. Wanafikiri kwa kufanya hivyo tunakataa hakukuwa na 'waasisi' wa Taifa letu.

Kama nilivyosema mahali pengine, wanashindwa kuongoza na hata kutawala inakuwa ngumu kwao na wanajaribu kuhalalisha hayo kwa kujipima na Nyerere na kusema "mbona hata Nyerere alishindwa". Ni sawasawa na mtoto anapokiri kushindwa kwake na kusema "hata baba alishindwa" na hajui kwamba kwa kufanya hivyo anamuiunua baba yake zaidi kuliko yeye hamshushi.
 
...
...
Hii ndio sababu ya ile hotuba yake ya "mambo ya kijinga mnayaacha na mazuri mnayaendeleza"; yaani uongozi ni kuachiana mafanikio na mapungufu. Kama Nyerere angeweza kusolve matatizo yote yaliyoikabili Tanzania kama wengine wanaoashiria kuwa ilimpasa angekuwa Mungu! Kiini cha changamoto alizokutana nazo Nyerere mwanzo wa taifa letu huwa najiuliza kama Kikwete ndiyo angekuwa Rais wetu au Mkapa sijui tungekuwaje!
...
...
By now kungelikuwepo na tu-nchi kama 7 hivi ndani ya mipaka yetu tuliyonayo sasa... na twingine tungelikuwa tuna mabomu hata ya nyuklia kwa ajili ya kutishia twenzao!! Twingine tungeshakuwa himaya ya Uingereza, Saudi Arabia na twingine tungelikuwa tunaongea Kichina na tu-nchi twingine Kifaransa!!!
 
Kuna neno linatumika vibaya na kwa dhamira isiyosahihi 'Failure'. Kwa def kutoka katika dictionary, failure; be unsuccessful, be or judged below standard in a test, dissappointing or to be useless (to someone), be unable to do something. Neno hilo linalisitizwa ili kufunika hata kile kizuri kilichofanyika, na hapa ndipo hoja ilipo, je mistakes zilizofanyika zinaondoa success zilizopatikana?

Nyerere alichukua nchi ikiwa na changamoto nyingi sana. Hakuwahi kuwa waziri au mkuu wa mkoa kama viongozi waliomfuata, lakini hii sio excuse!
Nchi ilikuwa haikuwa na wasomi, wananchi kuwa na matarajio makubwa na uchumi hafifu. Kazi haikuwa kujenga uchumi tu bali kuliunganisha taifa lielewe kujitawala maana yake ni nini. Vurugu (sio jaribio la mapinduzi) kambi ya Colito(Lugalo 1964) ni mfano mzuri wa matarajio ya wananchi baada ya uhuru.

Nchi ilipita katika wakati mgumu, 1974 njaa kali kutokana na ukame(sio ujamaa), 1977 kuvunjika kwa EA, 1978 vita ya Kagera, 1980 vita ya Iran na Iraq, 1980.. vita baridi. Kuvunjika kwa EA kuliifanya serikali ya Tz ibaki tupu. Nchi ikaanza upya kwa kila kitu, kila shirika na kila taasisi.

Licha ya changamoto hizo tulikuwa na maendeleo ya ujenzi wa vituo vya afya, elimu na vyuo vya kada ya kati kuliko wakati wowote ule.
Nyerere aliwekeza katika reli,usafiri majini,Anga na kujenga viwanda.
Infrastructures na Industries ndivyo vilitegemewa kulikuza taifa hili kiuchumi (foundation)
Akiondoka madarakani vitu vyote hivyo vilikuwa vinaonekana na vinafanya kazi.

Marekani inatumia infrastructure zilitojengwa wakati wa industrial revolution na great depression. Uingereza inatumia infrastructure kama reli na bandari hadi leo , vyote vikiwa mwendelezo wa misingi iliyojengwa na watangulizi.

Kama hatuwezi kuweka mabehewa au kuendesha ATC ni failure ya nani?
Tuna acha mahindi yaoze mbeya tumeshindwa kuendesha Tazara, ni failure ya nani?
tunageuza vyuo alivyojenga Nyerere ( mfano, IFM, Mzumbe kuwa vyuo vikuu) ,hatuwezi kujenga mabwawa ya umeme, tunaagiza jenereta hewa ni failure ya nani?
Hatuwekezi katika shule na vyuo tunawekeza katika VX na posho,tumeua kibo match tunaagiza kutoka pakistan ni failure ya nani?
Tumeua Moproco tunaagiza kutoka malaysia, tumeua magunia tunaagiza rambo india, tumeua general tyre tunaagiza mitumba ni failure ya nani?
Tumeua Tanganyika packers tunaagiza kutoka brazil,tumeua STAMICO mchanga unabebwa usiku, failure ya nani?
Tumeua mgololo tunauziana plot,tunaacha twiga wanabebwa usiku, tunasema mwl kafeli!!
Hospitali gani kiwango cha rufaa imejengwa baada ya mwalimu kuondoka!! nani ka fail hapo!

PM Churchil anaheshima sana uingereza, baada tu ya vita alivyoshinda aliondolewa madarakani, je Sir Churchil anapewa heshima ya failure au success? Hakuna kiongozi duniani aliyewahi kukamilisha ndoto zake 100%, je nao ni failure!!!

Ni ukweli kuwa failure inapimwa kwa viwango kama vile chuo au shule inapoweka pass mark, swali ni je Nyerere anapewa pass mark kiasi gani hadi tuseme 'failure'? kwa definition inaonekana anapewa 0 au 5%, fair enough! Ili tupate pass mark ya haki ya Nyerere basi uzuri na uovu viwekwe katika mizani, si kusema 'mbaya' au failure bali ielezwe ni kwa vipi kama ilivyo kwa wanaosema pass wakionyesha ABCD.

Swali litakuja 'investment katika intellectual' inapimwa vipi, maana viongozi wote wazuri na wabaya ni zao la mwalimu wakiwemo maprofesa, JK,BWM n.k. Kama E.Lowassa ni 'failure' ya Nyerere, Salim A Salim ni success ya mwl, tunapata wapi ushajaa wa ku generalize kila kitu cha Nyerere kama 'failure' endapo hatuangalii pande zote.
 
..samahani, najua kuna watakaokwazika na maandishi yangu.

..jamani mimi naona kama Maraisi wote nchi hii wamefeli.

..kinachotofautiani ni kwa kiwango gani, na mazingira ya kufeli huko.

..namheshimu Mwalimu kwasababu tofauti na wenzake yeye hakuiba.

..I would never ever question Mwalimu's personal integrity.

..Mwalimu's sincerity is what elevates him compared to his successor, even though some decisions he made really affected our economy in a negative way.

..Mwalimu erred while trying his best to do good for his country. waliomfuatia are failures kwasababu ya tamaa ya mali na ngawira.
 
Achen ujinga grit thnkers mnabishania upuuzi mkishajua then ndo itakuwaje.anyway let me prove to you kuwa Nyerere ameshawai kir udhaifu.mfano ni ule wakat nkurumah anatoa mawazo ya kuunganisha Afrika yeye alipinga vikali na badae akaja sema,nilifanya upuz mkubwa mno kupinga ilo mana kuiunganisha africa sasa iv ni ngumu kuliko zaman.
 
Toa umbea hapa
Qur'an sio lugha ni kitabu, lugha ni kiarabu ambacho haukielewi.
Labda tu nikudoze, ndo ishakuwa, Nyerere alikuwa rais wa kwanza wa Taifa hili,
na anaheshimika ndani na nje ya taifa hili kama baba wa Taifa la Tanzania.
kama kuna kosa lolote alifanya tunaweza tukajidili kama ambavyo tunaweza
kujadili kosa la baba yako kukurithisha imani ambayo wewe mwenyewe hauwezi
kuyasoma maandiko yake na kuyaelewa.

hata kama umeenda shule, chuo whatever, haita kusaidia kitu hiyo elimu kama unayo. kwanza futa hayo mawazo "MGANDO" ya kuendelea KUMUABUDU yule mzee DİKTETA. I have seen fools with PhD ...I will not be surprised with what you have,if you have any...
 
Mwanakijiji, unapodai kuwa Nyerere alileta umoja, hivi alikuta hii nchi haitawaliki, watu hawasikilizani, kulikuwa na mapigano ya kikabila akayakomesha, alikuta Watanganyika wametawanyika akawaweka pamoja au...!?

Fafanua tafadhali, ina maana hata kwenye kupiga kampeni zake alikwenda na wakalimani au alitumia Kishwahili bila ya wakalimani?
 
Kwani unafikiria alivyosema hivyo, wenye imani zao walikaa kimya, walijaribu kumpinga ati... Ndio wakamwambia kuwa ujamaa ndio ulioshindwa...!
Kwa sababu 1. Hiyo interview ya CNN niliiona. na 2. Kama Ukristo ulishindwa mbona bado twaenda makanisani? That is the point he was trying to impress upon the interviewer, kufananisha kushindwa kwa ujamaa na kushindwa kwa Ukristo.
 
Achen ujinga grit thnkers mnabishania upuuzi mkishajua then ndo itakuwaje.anyway let me prove to you kuwa Nyerere ameshawai kir udhaifu.mfano ni ule wakat nkurumah anatoa mawazo ya kuunganisha Afrika yeye alipinga vikali na badae akaja sema,nilifanya upuz mkubwa mno kupinga ilo mana kuiunganisha africa sasa iv ni ngumu kuliko zaman.
The problem with your statement is Nyerere never said that. Alitofautiana na Nkrumah ambaye alitaka bara la afrika liunganike kwa mara moja, jambo ambalo halikuwezekana na Nyerere aliunga mkono nchi za eneo moja kuunganika hatua kwa hatua, jambo ambalo linawezekana. Mfano ni ECOWAS na sasa jumuiya ya Afrika mashariki.
 
Hivi nyerere angekuwa haja "fail" tungekuwa tunapewa sukari kwa foleni wiki kilo moja kwa kaya moja? Hivi nyerere agekuwa haja "fail" si ageachia ngazi na huku nchi kidogo iko kwenye ahueni? kaiacha hata benki kuu kaichoa moto. Loooh, corruption mtindo mmoja, sisi tuliobahatika kuikimbia nchi wakati wake, tukija kutembea hapa, Wallahi zawadi kubwa ni dawa za meno (colgate) na sabuni za kuogea.

Nakumbuka airport maaskari walivyokuwa wajinga walikuwa wanashangalia saa ya "digital", Kama wameona kitu cha ajaaabu. He was simply a total failure.
 
Kwa sababu 1. Hiyo interview ya CNN niliiona. na 2. Kama Ukristo ulishindwa mbona bado twaenda makanisani? That is the point he was trying to impress upon the interviewer, kufananisha kushindwa kwa ujamaa na kushindwa kwa Ukristo.

Hivi wewe hujawahi kukaa foleni ya sukari wakati wa nyerere? au ulikuwa haupo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom