Nimekusoma na kukuelewa, vile nilivyo elewa...! Kufananisha Kenya na Tanzania (Tanganyika) yenye makabila 123, unakosea kabisa. Kiufupi Nyerere aliendeleza kile alichowakuta nacho Watanzania.
Mkuu wangu labda mimi nikueleze kinagaubaga upate kuelewa matatizo ya kuchukua nchi iliyokuwa imetawaliwa kwa mabavu ama Ukoloni.
Pengine hufahamu kwamba Kabla ya Uhuru kulikuwepo na makundi ya kikabila na baina yetu hatukukubaliana kiutawala zaidi ya kuwa chini ya mkoloni. Waasisi wa chama chetu TANU iwe toka AbdulWakil au Nyerere swala kubwa lililowatatizo zaidi iulikuwa kuunganisha nguvu ya kupata kudai uhuru wetu ambao ulikuwa na masharti na moja kubwa lilikuwa kupata kura toka majimbo yote na kazi hii ilianza baada ya Nyerere kuwa mwenyekiti wa chama.
XPASTER, kabla ya Uhuru sisi tulozaliwa bara hatukuzungumza kiswahili kama lugha ya kwanza na wala haikuwa lugha ya biashara..Na nakumbuka vizuri sana ingawa nilizaliwa na wazazi wanazungumza kiswahili ilikuwa taabu sana ku communicate na wengine hadi nilipokuwa fluent kwa Kijita na Kikerewe.
Sisi tulokuwa tukizungumza kiswahili tuliitwa waswahili na Waislaam na hakika ni Waislaam na waswahili ndio walizungumza kiswahili hata kiwe cha kuokoteza, tena basi huwezi kuamini Biblia ya kwanza niliyoiona mimi ilikuwa kwa Kikererewe na hata nyimbo za kanisani zilikuwa za kikerewe.
Labda kwa kifupi nikwambie kwamba sisi tumepitia muda wa mabadiliko na tunayozungumza sii historia iliyoandikwa mahala popote isipokuwa watu wengi wanafikiria maisha ya Dar ama Pwani yalikuwa vile vile huko bara.. hapana mkuu wangu.
Na kumbuka tu kitu cha kwanza ktk kujenga utamaduni wa watu ni lugha, siku Nyerere alipotangaza kiswahili kuwa lugha ya taifa kulipita malalamishi mengi tena huwezi kuamini. Na ilichukua kazi kubwa sana Nyerere kubadiulisha masopmo yote kuwa kwa kiswahili jambo ambalo hadi leo wasomi na wataalam wanamlalamikia kwa sababu Kiswahili kiliharibu upana wa elimu lakini wakati huo huo ukijenga Umoja wa Utaifa letu.
Nakuhakikishia kama Kiswahili kisingekuwa lugha ya Taifa na tukaendelea na lugha za makabila huku Kiingereza kikitumika kama lugha ya kufundishia ingekuwa kazi kubwa sana hata kuelemisha wananchi kwa mwalimu kutoka Lindi aje fundisha Ukerewe, lakini maadam ku learn lugha haichukui muda kama elimu watu wengi walishindwa kuelewa kwa nini kiswahili kiwe lugha ya kufundishia ikiwa wananchi wengi (asilimia kubwa) hawazungumzi kiswahili, lakini leo hii wanakubali kiingereza kiwe lugha ya kufundishia hata kama ni asilimia ndogo sana wanazungumza lugha hiyo, tena basi pasipo kujali kama lengo ni kukifanya kiswahili kiwe lugha ya mawasiliano isipokuwa lugha ya kibiashara...
Hivyo ukitazama malengo ya lugha ya biashara kinachotakiwa ni wananchi kufundishwa lugha kuizungumza basi, lakini unapoifanya lugha kuwa ya kufundishia siku zote unaua lugha zingine ktk mawasiliano kwa sababu huyo msomi hataweza kujieleza ktk lugha yeyote isipokuwa ile aofundishiwa hhivyo kuzoea kutumia lugha hiyo ktk mawasiliano yake..
Na ukitazama sasa hivi TZ kiswahili kinapotea taratibu, vijana wengi wanashindwa kunyoosha kiswahili pasipo kuweka maneno ya kiingereza na sii kwamba wanadengua laa hasha! hawajui maana ya maneno hayo kwa kiswahili ingawaje yapo.. Hii ni mpoja ya mwanzo wa kututenganisha.. Lugha ni kiungo na lugha inaweza kuwasambaratisha ndio maana unaona nchi zote za magharibi wanaprotect lugha zao na mara zote hujifunza lugha ya kigeni kama lugha ya kibiashara (somo) na sii ya kufundishia..
Na kwa bahati leo hii mimi na wewe na wengine wote hapa JF tunajumuika ktk mijadala mbalimbali kutokana na maamuzi ya utawala wa JKN laa sivyo tungekuwa kama Mataifa mengine yaliyoshindwa kutumia lugha moja kuwa ya mawasiliano na hakika lugha ina picha pana sana ktk Ubaguzi wa makabila kama tunavyozungumzia Udini kutokana na majina ya watu na ubaguzi mwingineo..