Mkuu wangu katika swala la kuanguka kiuchumi nadhani hatuna sababu ya kulinganisha na nchi nyinginezo kwa sababu itakuwa utnaukimbia ukweli. Sisi tuli fail, so are many nations kama vile leo Greece wanavyolia haina maana Ureno na nchi nyingine za Ulaya ziko salama. Kifupi leo hii uchumi umeshuka kila mahala lakini, picha kubwa ipo Ugiriki na inabidi tuseme rais wao au wagiriki wame fail, ingawaje Taifa halitakufa kesho .
Na labda niseme Nyerere failed sio kwa sababu ya Ujamaa bali ni sawa na nyumba ziliyojengwa kwa drywall na mbao zikapigwa na dhoruba ya kimbunga (Tornado), sasa ziole zilizokuwepo katikati ya dhoruba zitaathirika zaidi ya zile za pembeni na pia hatuwezi kusema zile zilizoweza kupona zimejengwa imara zaidi ya zile zilizoharibiwa. Factors za ku detarmine uimara wa nyumba haupimwi baada ya madhara bali wakati wa ujenzi...
Na ndipo napomsifu Nyerere kwamba yeye aliwekeza sana ktk miundombinu na viwanda ambayo ilimchukua zaidi ya miaka 15 ya utawala wake kuijenga (toka 1967 to 1982) lakini wazalendo hawakuweza kuona faida yake kwa sababu ujenzi wa miundombinu na viwanda hivyo ulitufiksha kula Bulga na maziwa ya msaada kwani walichotegemea ni ujenzi wenye kuzaa kama dhahabu. Wanahesabu madeni ya kujenga miundombinu hiyo kama hasara wakati ni miundombinu hiyo na viwanda ambavyo leo vinatumika kuendesha uchumi wa serikali hizi toka Mwinyi hadi Mkapa.
Yote haya yamesaulika na kuitwa FAILURE simply because kimbunga cha 1982 na leo tumesahahu kwamba ni wakati nchi kubwa zinazotoa mafuta duniani zilikuwa ktk hekaheka ya vita (Iran vs Iraq) dunia nzima iliyumba kiuchumi leo Taifa ambalo fedha yake yote limewekeza ktk miundombinu na viwanda lingeweza vipi kuhimili vishindo tena baada ya vita ya Uganda.
Pamoja na yote yale na sababu zote zilizokuwepo lakini bado tukubali kwamba tulishindwa! we failed kama mzee wa Kariakoo aliyejenga nyumba ya vyumba sita ataonekana hakuwa na akili kuliko huyu mtoto wake aliyewtumia nyumba ile ile kuipangisha au kuivunja na kujenga ghorofa ambalo limewapa watoto hawa maisha bora zaidi ya yale waliyokulia chini ya himaya ya mzee baba yao.
Na hakika hawatakumbuka nguvu ya mzee kuijenga nyumba ile ambayo pengine ili cost only Tsh 5,000 lakini kwa mshahara wa Tsh 50 kwa mwezi (a thousand times) lakini sisi wenyewe kizazi kipya na mshahara wa Tsh 500,000 tunashindwa hata kununua kiwanja.
Imagine our elderly sacrifice, lakini waulize hao MasharoUharo wa Kariakoo utasikia makosa yote ya dingi, he failed us! angenizaa mimi ktk tajiri - NINGEKUWA bl;aa! blaa! blaaa!
Kwa hiyo mawazo mengi against Nyerere ni ya hawa Masharouharo ambao walitaka watengewe kila kitu mezani wao waje kujichana kama vile hakuna najsi!..Miafrika ndivyo Tulivyo!