Did Nyerere admit he was a "failure"? Some say "Yes he did"...

Did Nyerere admit he was a "failure"? Some say "Yes he did"...

Wakati wote wa nyerere tumeona kila kitu kikifa hata viwanda alivyotaifisha, mashamba aliyotaifisha yakawa mapori, mashule yakadidimia, mabarabara yakafa, tulikuwa tukienda Mwanza na Tanganyika bus kupitia njia ya kati, ikafa kabisa mpaka inabidi uzunguke Kenya. Halafu anaposema kashindwa nyie mkatae. Makubwa haya.Nini alichokiweza?

aisee.... kweli gubegube ni sawa nini sjui
reli, atc, urafiki, nyanza, mwadui, uvinza etc kumbe haya yalifia kwa nyerere??

haya asante kwa kutujuza..... na barrick, afgem yakazaliwa na JK sio.... haya bhana

na mwinyi hakuwahi kutawala siyo?? kwahiyo hakuna kilichokufa wala kukufukia kwake siyo??

mnahangaika bure bandugu.... nature is taking its course
 
Dah!! Huu uzi umenisikitisha na kunidhihirishia kua sasa kweli uzalendo wa sisi wananchi haupo.. Tanzania tupo wakati mgumu na complicated kisiasa like never before (achana na mambo ya kugombea uhuru); Nina maana ugumu in the sense kua wale ambao wamebahatika kua wenye utafakari , uwezo wa kupambua mambo na pia kuwakilisha walau basi ifanywe hivyo kwa kuangalia tuliko toka, kujifunza makosa yetu and learn from them... kwa kufanya hivyo yaani kuthamini tuliko toka na akina nani waliwezesha kwa njia yoyote ile ndo itafanya sisi na vizazi vijavyo viwe bora zaidi..

Tatizo kwa sisi wa Tanzania ni wavivu saana wa kusoma litratures, kusoma biographies and hata anaesoma yuko soo very critical as if s/he would have done better… Mtu anaongea na kudefend issues alizopokea katika kinywa cha mtu ambae yuko prejudge or even not... The late Mwalim Nyerere (may he rest in peace) was a great man; na sisi Watanzania kutoheshimu nguvu zake na kuapppreciate his efforts then... yes we don't know or we do not treasure or heritages in a level headed mind.. ideas zake ingawa misunderstood by some critics ni sawa na kusema huelewi what is best for your nation. The man knew in advance jinsi Tanzania itakua leo as much as he is dead.. Madeni, utegemezi wa kupindukia, kuchakachulika kwa mwananchi wa kawaida ... and a lot more..

Mfano mdogo tu kwa kutolea but mkubwa in the results ni lugha ya Kiswahili.. succeeding in those times of difficulty with impossible environments and circumstance he was able to Unite this nation in one, with focus, determination, Vision so powerful for Tanzanians (ambayo mpka leo personally sijaona nani anaweza prove uzalendo…

Viongozi wetu woote sasa hivi awe (MAGAMBA au MAGAMBALESS) wanapiga/pigiana propaganda tu… Woote wanasiasa tu.. Kundi moja maarufu kwa kujirusha na kuzima moto (ambao inaelekea kuwashinda..) kundi linguine maarufu kwa kuchokoa na kupiga mbizi wabadili nafasi (ambao possibility kubwa ya kufanikiwa kupo..) Naamini the only changes zitatokea kwa Mtanzania wa kawaida Chama kikibadilika ni roho zao kupoa kwa to ile kwamba wahusika wa Magamba woote watapata cha moto!!! Whether watabadilisha maisha… that is another story..

Mwl Nyerere is a man a human being ambaye pia anaruhusiwa kufanya mistakes… anaweza akawa hakua perfect but he was the best in doing what was best for his country he loved as much as it was with strain.. Na kwa attitude na nidham ya Watanzani at that time what he did was rite kwa mda ule (my stand!! )

@FAIZAFOXY (Presumably my alter self…)

Nimeshangaa saana… I have noticed you are CCM damu… what is wrong or what went wrong??? I am not sure if he really admitted to failure but does it matter?? REALLY… He failed unasema… The man is dead… kuna haja, Why don’t we start na viongozi wetu ambao wame faili mpaka kila Mtanzania acknowledges that… I believe right now Nyerere is turning in his grave right now the way the issue of Mapacha watatu is being treated!
From hii Link umetoa..

Julius Kambarage Nyerere (April 13 1922 - October 14 1999), also known as Mwalimu (teacher), was President of Tanzania from 1964 to 1985, though he was still influential in politics until his death in 1999 because of his popularity. He is remembered as an unusually honest leader, especially for Africa, and for helping refugees. When his attempt at using his socialist ideas of Ujamaa failed , he said, "I failed. Let's admit it." He was also responsible for the overthrow of the murderous Idi Amin regime in Uganda.


Hii evidence umetoa… source ni WIKIPEDIA nikitaka ku edit hata mimi naweza but ilo si la muhimu.. kuna positive points katika hio paragraph kuliko hata negative… Hivi what explains the habit of a person – all humans have a positive and negative side bu we define someone with what runs over the other..

POSITIVE

  • Was Influencial in politics until his death as a result of his popularity..
  • He is remembered as being a honest leader.. especially for Africa…
  • He is remembered in helping refugees…
  • He was responsible for the overthrow of the Iddi Amin regime in Uganda (a discussion to date to its necessity)
All those positive and you conclude with a failure, a failure in a small nation where it was still young and fragile just from independence… expecting to succed where as there was sharks like US??


Thanks, He said i failed... we didnt say he failed.....

JK will never say i failed, we will say he failed!!

read it carefully

Nyerere didnt fail IMO, JK has failed IMO... tunaopima ni sisi na si self assessment kwani they are not lading themselves, they are leading people (sisi)
 
Bukuku, nimepitia taratibu hayo ambayo umeyaita ni "academic" works. Na nimeelewa kinachosemwa vizuri sana. Na inafurahisha kuwa mtu ambaye wewe unamuita "dikteta" anaoneshwa katika mwanga wa sifa na shangwe labda kuliko Mwafrika mwingine yeyote. Dikteta Nyerere anasifwa na ukiondoa wewe na wachache wa siku hizi hakuna mtu yeyote kati ya hao uliowanukuu hapo amemtaja Nyerere kama Dikteta. Dikteta asiyejulikana na watu wake.

Tunaambiwa Nyerere ndiye aliyeweka mkazo katika hili la uvumilivu wa kidini na sifa hizo hapewi mtu mwingine yeyote.



Kikwete ambaye leo hii amekuwa muumini kuwa Nyerere aliwakandamiza Waislamu na kuwa chini yake ndiko kulikuwepo udini (japo hasemi hivyo wazi lakini kwa ukimya wake na wa serikali yake anabariki) amekiri miaka miwili tu iilyopita maneno hayo. Na tunaambiwa Umoja wa Mataifa miaka kumi baada ya kifo chake ukampa heshima ya kuwa Shujaa wa Haki za Jamii.



Katika legacies zake waandishi wetu wanabalance ukweli wa kihistoria juu ya Nyerere.

Ali Mazrui (a contemporary of Nyerere) anasema eloquently -

Mazrui hamuoni Nyerere kama Dikteta!

Mwandishi mwingine anasema,



Ambacho nimependa ni hitimisho la hawa wasomi uliowaleta;



Kwamba Nyerere anaweza kupimwa kwa mafanikio na mapungufu yake halina shaka ni jukumu la kihistoria na msomi yeyote yule. Lakini kufikia hitimisho kuwa Nyerere alikuwa ni dikteta na kuwa alikuwa mbaya na hakufanikiwa ni kinyume na ushahidi wote uliopo kuhusu Nyerere. Bahati nzuri ni miongoni (yawezekana ni mtu pekee) katika Tanzania aliyewahi kuandikwa vya kutosha na ambaye legacy yake inaweza kuangaliwa kisomi na si kihisia. Hadi hivi sasa sijaona kazi yoyote ya Kisomi ambayo imeweka ushahidi wa Udikteta wa Nyerere; none kama vile hakuna ushahidi kuwa aliwahi kusema kuwa "I failed, lets admit it".

Hata maandishi mekundu ambayo umeyanukuu ambayo mwandishi anasema:



Huyu naye hasemi maneno hayo Nyerere aliyatoa wapi.

Hakuna ushahidi wowote kuwa Nyerere alikuwa

a. Kiongozi mbaya
b. Dikteta
c. Hakujali wananchi
d. Alitumia vibaya madaraka yake
e. Alijinufaisha yeye na watu wake wa karibu

n.k

Najiuliza hivi watoto wa Mramba wanaweza kumuona Kikwete ni mtu mzuri kwao? Najiuliza kama watoto na familia ya Mgonja wanamuona Kikwete ni kiongozi mzuri? Najiuliza kama familia ya Kiula inamuona Mkapa kuwa ni kiongozi mzuri?



Watoto wa Thomas Zangira, Ed Barongo n.k.

Wale wanaosimamia hotuba ya 1985 tupeni siku, mahali na saa tutakwenda au kuomba hotuba hiyo kutoka kwa mzee Butiku ili tupate ukweli.
Kuchukua opinion za waandishi kutoka NY times na kuzifanya fact ni ututusa wa kiwango cha kimataifa.

Ninashangaa kuna mtu anasema kama yapo mazuri mbona hayaonekani? ah! sasa kama ameacha viwanda 400 mkauza mtaviona wapi, mbona UDSM ambayo hamkuuza ipo pale. Watu hawaoni taa wanazowasha ni jitihada za kujenga Mtera, Nyumba ya mungu, kidatu n.k tangu aondoke kuna chanzo gani cha umeme kimejengwa kama si kuuza Kiwira ya mwalimu.
Hivi hamuoni sisi kuishi kama watu wa taifa moja ni sehemu ya mafanikio na mambo aliyoyaacha n.k

Lakini la muhimu zaidi kuhusu Nyerere ni kuwa 10 yr baada ya kifo chake bado umma unamjadili iwe kwa mazuri au mabaya. Ali Hassan amefutika, Jomo Kenyatta, Ben Mkapa, Kaunda, Neto, Marchel, Senghor, Tolbert, Nandi, Gamal, Haille selasi n.k ni kama hawakuwepo.
Tena umma unaomjadili ni ule wa wasomi kama akina Wole, Shivji, walter, profesa wa international universities n.k yeye amekuwa reference kwasababu hakuna reference so far.
Nilishangaa mwananfunzi asiye mtanzania kuandika thesis ya political science kuhusu success and failure ya Nyerere. ! Sisi hatuwezi kuandika mazuri na mabaya yake tunachagua neno mistake na kuligeuza kuwa fail tunawalisha watoto wetu ii kuzifurahisha nafsi zetu.

Mkuu MKJJ kwanza unakosea tena na tena kusema kuwa nasema Nyerere ni dikteta bila kutoa sababu ya kwa nini nimesema hivyo

Nimekuambia kuwa neno DIKTETA halina maana kamili, lina vary kutokana na mtu na mtu

watu walisema Mkapa dikteta simply kwa sababu ya misimamo yake kwa vyombo vya habari n.k
Kikwete mara kadhaa na hasa first term aliitwa dikteta
Mwinyi sijasikia sikia sana kuita dikteta!

NENO DIKTETA AMBALO WEWE UNASEMA NYERERE HATAKIWI KUITWA HIVYO LINA VARY..KIBAYA SANA na aibu ya mwaka umeweka jibu mwenyewe kwenye paragraph ya mwisho umetoa mifano ya akina Mramba, Mahalu n.k!!!!! SEE!!!

NIKASEMA KUWA WANAOSEMA NYERERE DIKTETA WANASABABU, single reason inampa demokrasia mtu kusema lolote na WOTE TUNAJUA DEMOKRASIA YA KWELI UANZIA MAWAZONI MWA MTU! MTU ANA UHURU WA KUWAZA NA KUSEMA!!!

WENGI wanamwita Nyerere dikteta na wana sababu zao kama vile;

1. Kuondoa mfumo wa vyama vingi toka 61-67 na kuingiza mfumo wa chama kimoja
2. Kuwa haambiliki
3. kuwa aliweka watu wengi vizuizini
4. aliua wengi kwa siri
5. aliongoza nchi kwa nguvu ya giza (uchawi)
6. alitumia polisi na usalama wa taifa kuwatisha watu
7. Kuitisha uchaguzi wa kivuli na mtu
8. kutosikiliza ushauri wa wataalamu wake
9. etc

yako mengi MKJJ ambayo kwa sababu moja mtu anaweza kumuita Nyerere dikteta! we are using this word everyday!!!!!

Personally MSIMAMO WANGU NI KUWA HUWEZI KUZUIA WATU KUMUITA NYERERE DIKTETA!!!! I have warned you several times.....mapaka wazazi na wajomba huitwa madikteta wakati hawana jesho wala mahakama!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

watu huita mpaka wachungaji na mashekh madikteta...

HII NI KAWAIDA NA NI HULKA YA BINADAMU

SASA KUTOKANA NA UBORA WA UONGOZI WA NYERERE INAWEZEKANA WENGINE ALIWAGUSA NA PIA WAMEWEKA VINYONGO NA WANAMWITA NYERERE DIKTETA....you see bado hujaondoa neno dikteta

Ukiangalia jibu la Nguruvi hapo juu unaona anasema tena KISOMI kuwa ombwe la uongozi wa sasa linafanya watu warudi na kumkumbuka Nyerere kwa mazuri au mabaya

Juzi nimesema tena kwa crown yake ya kuwa yeye ni baba wa taifa still watu watamsema tu kwa mazuri au mabaya!!!! it is normal it is HUMAN!!!

Kesho ukifa, still watu watamwita Nyerere dikteta, na wako watasema mwenye HERI..wako ambao watafanya ziara mpaka makaburini kwakwe wakimsifia na wengine wataaandika ubaya wake woooote, MAISHA YATAENDELEA!!!

SIJAONA MANTIKI YA LIGI HII YA WEWE NA FAIZAFOXY FAIZA ANA UHURU WA KUSEMA NYERERE DIKTETA NA AKATOA SABABU...KWA HAPA DIKTETA LINAWEZA LIKAWA NI
NEOLOGISM


Kwahiyo, hiyo paper ambayo nimeweka nimeweka kuhakikishia umma kuwa sina tatizo na mtu yeyote kumsema Nyerere kwa mazuri au mabaya, ULIPOSIMAMA WEWE NI KUWA HUTAKI NYERERE ASISEMWE KWA MABAYA...huwezi kuzuia hilo SOMEBODY help mwanakijiji please!!! you will never!! utaishia kuanzisha thread kila siku za 'dikteta' NYERERE mwishowe ukiwa na lengo zuri la kumtetea Nyerere wasiojua wataondoka na hiyo vocabulary mkuu!!! utatangaza ubaya wa NYERERE!!!


Unapotumia emotion kubishana na FAIZA ambaye amekushinda kila kona, maana unabaki kujieleza na kutetea kitu ambacho hata FAIZA ANAKIJUA!!!! we are laughing!!! amekuteka dada wa watu HAUPUMUI, HAULI, KISA NYERERE!!! what is a big deal? yaani unataka kusema member woote elfu thelathini hawana akili ya kuchambua ukweli na ubaya au wewe unampenda Nyerere kuliko wengine wooote humu.?

NYERERE HAWEZI KUTETEWA NA MTU KAMA WEWE MWANAKJIJI, NYERERE ATAJITETEA NA KAZI ZAKE ZITASIMAMA, UBORA WAKE UTASIMULIWA VIZAZI VYOTE VIJAVYO, UBOVU WAKE UTASIMULIWA VIZAZI VYOTE VIJAVYO..wewe kazi hii uliyojivika voluntarily huwezi!!!

Nyerere siyo dini! Nyerere siyo mtume...Nyerere alikuwa binadamu na ndiyo maana amekufa!! amekufa na kinachobaki ni wasifu wake na kazi zake, sasa kama kuna mabaya asisemwe? why??

Yes he was great leader, yet he was fallible, kwa sababu hatuna standard ya kosa au udhaifu wa mtu tuuweke kwenye rank gani basi wengine kumwita dikteta as
neologism to describe his character sioni tatizo!!

Kama is a.k.a za Nyerere zimekuwa alama ya uadui na kutumiwa na kutokuwa mzalendo then count me in-proudly!!

Key words:

Neologism, dikteta, Nyerere,




 
Wakati wa nyerere Tanzania siku zote ilikuwa katika nchi tatu za mwisho kwa umaskini duniani. Kama sio kushindwa huko nini?

How old is Tanzania?? and how many countries zimeongezeka since Nyerere haa duniani

and how many indices za maendeleo (forget resources which he left for the mooses to munch like squirrels) zilikuwepo

what about development indicators

what was the prime role of Mwalimu's first 15 years???

You are bragging your bra all ove the table i cant even see where i did put my ketchup, can just lift your boobs a little??
 
Thanks, He said i failed... we didnt say he failed.....

JK will never say i failed, we will say he failed!!

read it carefully

Nyerere didnt fail IMO, JK has failed IMO... tunaopima ni sisi na si self assessment kwani they are not lading themselves, they are leading people (sisi)


That's the thing MTM whether he said it or not... He was for Tanzanians not for himself...
JK is a juggler he knows what he is doing thou saying otherwise...
And he knows... we know what he knows.. and that is that he has FAILED..
thus i believe the most common opinion at present.. that also being proved with
his poor relations even with his alumni president members....
WHAT is leading us ni muhimu mno... imagine hapa we are discussing of
Nyerere wakati kuna urgent matters at Hand... saddening...
 
That's the thing MTM whether he said it or not... He was for Tanzanians not for himself...
JK is a juggler he knows what he is doing thou saying otherwise...
And he knows... we know what he knows.. and that is that he has FAILED..
thus i believe the most common opinion at present.. that also being proved with
his poor relations even with his alumni president members....
WHAT is leading us ni muhimu mno... imagine hapa we are discussing of
Nyerere wakati kuna urgent matters at Hand... saddening...

so does this mean for the first time since i was born you ahve agreed with me?? for once

FF is dragging here so that we dont talk of her inlaw makinda, her idol JK and her peers magambaz
 
so does this mean for the first time since i was born you ahve agreed with me?? for once

FF is dragging here so that we dont talk of her inlaw makinda, her idol JK and her peers magambaz


Come on Man!! What did we discuss on and disagreed??? Unfortunately am doing that to this post on Makinda..
I believe she is a great woman given a Great responsibility... She is good in others BUT u speaker (she was not ripe yet) and a
Woman at that she had to work twice as hard and not necessarily like a MAN but radher like a woman
Who could have used the extra sense we Mothers are given by God.. in making sure there is harmony around..
Yeye ilitakiwa tu a relax... asitumie nguvu.. she would have done Great... And bahati mbaya i believe the washauri
ni wanaume... hivyo hutumia technique hizo kuonesha power instead of following instics (which i presume ni better..)
 
Sasa kama hapa ndio mtu ananukuu kama ukweli bado tuna matatizo. Wikipedia hiyo inasema "he said, "I faield. Let's admit it" na mtu anaamini kuwa Nyerere kweli alisema hivyo. Hajui ilisemwa wapi bali kwa vile Wikipedia imesema basi mtu anaamini na kuichukulia kama ukweli. Ndio maana baadhi ya vyuo sasa vinapiga marufuku watu kuicite Wikipedia kama authority katika masuala ya academic. Tatizo la Faiza kaenda kuongeza kabisa kuwa hiyo sentensi ipo kwenye "farewell speech"; uzuri wa farewell speech ni kuwa iko moja tu ambayo Nyerere aliliaga taifa.

Sasa kama kuna uungwana wowote basi angekubali tu kuwa kweli pale nilikosea na suala linakufa tunasonga mbele. But that aint gonna happen.

Mkuu wa Kijiji
Hapa umemaliza kazi, kwanza umetuwekea hotuba yote ambayo waliobahatika kuisoma wameisoma. na wengine waliobahatika kuwepo siku hiyo ya hotuba watakumbuka.

Sasa basi tuangalie tu tusibishane na asiyelelewa tusionekane wote hatuelewi(nimetumia lugha ya kidiplomasia hapa maana methali yenyewe huwa ni kali kidogo kuitamuka).
 
Come on Man!! What did we discuss on and disagreed??? Unfortunately am doing that to this post on Makinda..
I believe she is a great woman given a Great responsibility... She is good in others BUT u speaker (she was not ripe yet) and a
Woman at that she had to work twice as hard and not necessarily like a MAN but radher like a woman
Who could have used the extra sense we Mothers are given by God.. in making sure there is harmony around..
Yeye ilitakiwa tu a relax... asitumie nguvu.. she would have done Great... And bahati mbaya i believe the washauri
ni wanaume... hivyo hutumia technique hizo kuonesha power instead of following instics (which i presume ni better..)
Thanks Asha... and for that only i am giving you the attachde photo....

the_identity_of_vancouvers_famous_kissing_couple_is_revealed.jpg
 
Wanaomchukia Nyerere kimsingi wanamchukia kwa mengi. Pamoja na chuki zao ambazo kwa uzoefu wangu sizishangai, hata ukiwaambia wamzungumzie kuhusu mavazi watasema alivaa vibaya, kuhusu nywele watasema alichana vibaya n.k.

Pamoja na wadau kukataa kuhusisha mambo ya dini katika mjadala huu, binafsi nayaona wazi kabisa. Naruhusu mods wa-delete post yangu. Sitaficha ukweli. Afrika haina kazi za kufanya. Watu wako tayari kufanya uzinzi halafu wakaenda kupigana vita kutetea dini zao. Afrika haina kazi za kufanya. Watu watambishia Dr. James Watson aliposema Waafrika wana akili kidogo kuliko wazungu, mi binafsi bado natafuta hoja za kumpinga Dr. Watson, badoo sijapata maana kila dalili inaonesha yuko sahihi. Najua uzito wa kauli yangu, lakini niiseme, leo au kesho niko tayari kufa na kamba shingoni lakini si kuukana ukweli ambao kwa wakati huo ntakuwa nauamini, wanaoweza kuninukuu wafanye hivyo sasa. Afrika haina kazi za kufanya. Tunafarijika na "mvinyo wa Karl Marx" - Dini. Unafiki tu! Unafiki tu! Unafiki tu!

Afrika haina kazi ya kufanya. Unafiki tu! Na hapa ndipo mimi huwa naishusha sana JamiiForums. Pamoja na "matao" yote ya "u-Great Thinker" lakini uzezeta wa kiafrika unaendelea. Huu ni upumbavu ambao hautaondoka kwa kuingia darasani bali kwa kizazi hiki kilichochanganyikiwa kuondoka duniani na kuruhusu fikra mpya zizaliwe. Afrika haina kazi ya kufanya. Afrika haina kazi za kufanya.

Hadi pale nitakapopata hoja za kumpinga Dr. Watson, ukweli kuwa Wazungu wana akili kuliko Waafrika utaendelea kuwepo.
 
Wanaomchukia Nyerere kimsingi wanamchukia kwa mengi. Pamoja na chuki zao ambazo kwa uzoefu wangu sizishangai, hata ukiwaambia wamzungumzie kuhusu mavazi watasema alivaa vibaya, kuhusu nywele watasema alichana vibaya n.k.

Pamoja na wadau kukataa kuhusisha mambo ya dini katika mjadala huu, binafsi nayaona wazi kabisa. Naruhusu mods wa-delete post yangu. Sitaficha ukweli. Afrika haina kazi za kufanya. Watu wako tayari kufanya uzinzi halafu wakaenda kupigana vita kutetea dini zao. Afrika haina kazi za kufanya. Watu watambishia Dr. James Watson aliposema Waafrika wana akili kidogo kuliko wazungu, mi binafsi bado natafuta hoja za kumpinga Dr. Watson, badoo sijapata maana kila dalili inaonesha yuko sahihi. Najua uzito wa kauli yangu, lakini niiseme, leo au kesho niko tayari kufa na kamba shingoni lakini si kuukana ukweli ambao kwa wakati huo ntakuwa nauamini, wanaoweza kuninukuu wafanye hivyo sasa. Afrika haina kazi za kufanya. Tunafarijika na "mvinyo wa Karl Marx" - Dini. Unafiki tu! Unafiki tu! Unafiki tu!

Afrika haina kazi ya kufanya. Unafiki tu! Na hapa ndipo mimi huwa naishusha sana JamiiForums. Pamoja na "matao" yote ya "u-Great Thinker" lakini uzezeta wa kiafrika unaendelea. Huu ni upumbavu ambao hautaondoka kwa kuingia darasani bali kwa kizazi hiki kilichochanganyikiwa kuondoka duniani na kuruhusu fikra mpya zizaliwe. Afrika haina kazi ya kufanya. Afrika haina kazi za kufanya.

Hadi pale nitakapopata hoja za kumpinga Dr. Watson, ukweli kuwa Wazungu wana akili kuliko Waafrika utaendelea kuwepo.


3D Daima uki present kitu kimekuboa unawakilisha bluntly.. would have not been more blunt... which is good sometimes.. Nakubalina na most unayo sema but as much as ume conclude hivyo ni vizuri tukaulizana hapa as in why do we think iko hivyo... Kwa nini GT wako behind the Avatar and just above the Signatures but the no true revealing ya mtu ni nani? anayowakilisha ndo anaamini? Je yuko upande alosema yuko? Je ni mwema kama anavyo ji pain? Na maswali kibao...

Fikra za watu, maisha ya watu, mazingira ya watu huabadilika taratibu (thou pace ni kali sasa) but for the next two or more generations to be better people ni lazima wa evolve from us kama sie tulivyo evolve from the past generations... Change will always be brought by the people themselves for it to suceed... Ndio tokana na umaskini wetu wa kua na majukumu na wategemezi kibao tunandecy ya kukwepa litalo kuletea matatizo kuepusha shari yoyote ile...

Ukisema hatuna kazi ya kufanya ... really.. bado personally naona hujajustify vya kutosha.. Ila nakuunga mkono kuhusu udini unaokuja kwa kasi.. ni mpaka nilipo jiunga JF ndo nimegundua hii issue... I DID NOT KNOW KUA kuna udini mkubwa kiasi hiki... na nimefuatilia saana, Most wachangiaji uelewa na upambanuzi wao ni wa Primary level pande zoote za Wakristo na Waislam... hakuna anaetoa constructive arguments kwamba mwenzangu ni Muislam/Mkristo anaelewa hili jambo hivi but i feel it is Wrong ngoja nimueleze vizuri... zimejaa kejeli na short arguments... ambazo hazielimishi wala kuongeza knowledge... mjadala kati ya these two groups unanuka!!! na ni katika uzi mbali mbali za jamii wala sio za dini..
 
Kwa hiyo, hiyo ni conclusion ya moja ya muandishi aliyemnukuu nyerere kusema failure? Kama ndio hivyo kuna tatizo lipi hapo?

He simply failed. No one with his right mind can argue with this. Muwandanganye wale ambao hawakuwepo wakayi wake.

Nyerere kaiacha nchi njaa, kiza, hakuna hata mafuta ya taa, foleni ma petrol station, foleni hata sukari, ashaakum si matusi hata pamba zetu za kujistiri tulikuwa hatupati mpaka tuzinunue za magendo, sijui kama wanaume wanalijuwa hilo? ukipita njiani umebeba hata kikapu, kinapekuliwa na mgambo. Vizuizi vimewekwa Tanzania nzima eti vya kuzuia kipindupindu! jamani? mlikuwepo au mnabisha tuu?

Hivi mkiambiwa ukweli wa nyerere kwanini hamuupendi? nyerere alikuwa "orater" mzuri sana. Lakini mama yangu, ikifika kwenye maamuzi ya utendaji, yote bogus, hakuna kilicho fanikiwa.Viwanda vya umma, viko wapi? majumba aliyotaifisha, yako wapi? mabenki aliyotaifisha. yako wapi, shule alizotaifisha, ziko wapi? mashamba aliyotaifisha, yako wapi? vijiji vya ujamaa alivyolazimisha watu wahamie, viko wapi? mashirika umma aliyoanzisha, yako wapi? Hivyo vyote vimeanza kufa kabla yeye haja ng'atuka. Kaondoka benki kuu haina senti tano ya kigeni na ikachowa moto kuficha madudu yake, wizara ya mambo ya ndani ikachomwa moto kuficha madudu yake. Na ndio maana tukasikia mpaka kaburi lake liliwaka moto kwa dhulma alizofanya, siku aliyozikwa mpaka ardhi ikatetemeka kwa dhambi alizonazo.

Hao wanaojidai, oooh kaondoa udini. Ni waongo, kabla ya nyerere kulikuwa hakuna tatizo la udini Tanzania. Kungekuwa kuna tatizo la udini hata yeye asingepokelewa na kufadhiliwa na waIslaam wa Kariakoo. Oooh eti ukabila, ni nani aliyenyanyaswa kwa kabila yake Tanzania kabla ya nyerere? baada ya kuja nyerere ndio tukaona udini unaanza kwa kuwafunga mashekhe wote wwakubwa Tanzania, kuwahamisha makazi yao, kuwakejeli. Ukabila ukaanza alipoanzisha mashirika ya umma.

He was simply a failed dictator.

Hatimaye Faiza umejifunua wale wanaoelewa watajua wewe ni mtu gani.
 
Mkuu MKJJ kwanza unakosea tena na tena kusema kuwa nasema Nyerere ni dikteta bila kutoa sababu ya kwa nini nimesema hivyo

Nimekuambia kuwa neno DIKTETA halina maana kamili, lina vary kutokana na mtu na mtu


Well.. neno Dikteta lina maana na kama yalivyo maneno mengine linabeba maana. Ukisema "dikteta" unataka kumaanisha kitu. Lakini huwezi kujitengenezea maana ya "dikteta" kwa ababu tu lina "vary kutokana na mtu na mtu". Hapana. Neno dikteta lina maana iliyokubalika na mimi na wewe hatuwezi tu leo kuipa maana ya "kiongozi mpendwa" au "mwalimu mahiri". Kamusi inatuambia kuwa neno dikteta lina maana ya:

"a person exercising absolute power, especially a ruler who has absolute, unrestricted control in a government without hereditary succession." au " [TR="class: tr3"]
[TD="class: td3n2"]a. a ruler who is not effectively restricted by a constitution, laws, recognized opposition, etc [/TD]
[/TR]
[TR="class: tr3"]
[TD="class: td3n1, width: 1%, align: right"] [/TD]
[TD="class: td3n2"]b. an absolute, esp tyrannical, ruler"

Sasa ukisoma utaona kuwa dictator ina maana na vigezo. Lakini tuangalie vigezo vya maana yako wewe.
[/TD]
[/TR]



watu walisema Mkapa dikteta simply kwa sababu ya misimamo yake kwa vyombo vya habari n.k
Kikwete mara kadhaa na hasa first term aliitwa dikteta
Mwinyi sijasikia sikia sana kuita dikteta!

Tatizo bado liko pale pale, hawakuwa madikteta - not in the strickiest meaning of the term.

NENO DIKTETA AMBALO WEWE UNASEMA NYERERE HATAKIWI KUITWA HIVYO LINA VARY..KIBAYA SANA na aibu ya mwaka umeweka jibu mwenyewe kwenye paragraph ya mwisho umetoa mifano ya akina Mramba, Mahalu n.k!!!!! SEE!!!

Kama unataka kumaanisha ni kiongozi mwenye mamlaka au mwenye madaraka inabidi utoe maana.

NIKASEMA KUWA WANAOSEMA NYERERE DIKTETA WANASABABU, single reason inampa demokrasia mtu kusema lolote na WOTE TUNAJUA DEMOKRASIA YA KWELI UANZIA MAWAZONI MWA MTU! MTU ANA UHURU WA KUWAZA NA KUSEMA!!!

Hata nikikubali tu kuwa demokrasia inampa mtu "kusema lolote" demokrasia hiyo hiyo inampa mtu mwingine kusema lolote kuhusu lililosemwa na mtu mwingine. Ni sehemu hiyo hiyo.

WENGI wanamwita Nyerere dikteta na wana sababu zao kama vile;

Angalau hapa tuangalia hii msingi ya Nyerere kuitwa Dikteta na wewe na hao wengine.


1. Kuondoa mfumo wa vyama vingi toka 61-67 na kuingiza mfumo wa chama kimoja

Well, hili ni rahisi kuliangalia, Je Nyerere alitumia kauli yake tu kufuta mfumo huo au kulikuwa na utaratibu uliofuatwa? Je kulikuwa na sababu gani zilizotolewa za kuwa na mfumo wa chama kimoja? Je, Demokrasia haikuwepo kwenye mfumo wa chama kimoja? Kwani kuwa na vyama vingi ndio kigezo pekee cha kuwa na demokrasia? Swali la msingi hapa ni kuwa Nyerere alifuta mfumo wa vyama vingi kwa kutumia amri yake bila kuwashirikisha viongozi na wananchi? Hivyo ndivyo madikteta wanavyofanya. Nyerere hakufanya hivyo - Rejea Tume iliyoundwa kuangalia mfumo wa chama kimoja uweje.

2. Kuwa haambiliki

Mojawapo ya hoja dhaifu. Kuambilika katika lipi? Aliambiwa nini hakuwa sikia na kukubali kila unachoambiwa ndio alama ya kuwa kiongozi mzuri? Je kutowaengage wanaokuambia ili watetee hoja zao ni jambo baya. Hakuna mtu ambaye ametuambia Nyerere alikataa nini na hoja zilizotolewa ni zipi? Hukuweza kwenda kwa Nyerere na hoja ya kipuuzi au ambayo hukuwa umejiandaa kuitetea halafu akukubalie tu. Waulizeni kina Salim na wengine. Nyerere alikuwa na uwezo wa kuhoji. Tatizo waliokuwa wanatakiwa kufafanua wengi hawakuwa na uwezo wa kuteta hoja zao - si wapo hadi leo tunawaona jinsi wanavyojenga hoja? Nani anaweza kumsikiliza Kingunge leo na kusema anatoa pointi za kusikilizwa?

3. kuwa aliweka watu "wengi" vizuizini

Hakuna mfano. Ni kina nani waliowekwa kizuizini hadi kufikia kusema "wengi". NI sawa na mtu aliyesema "aliuawa wengi" na tukiuliza namba hakuna mtu anayeweza kutupa majibu. Hivi, kama mtu alistahili kuwekwa kizuizini asingewekwa kizuizini? Leo hii USA, UK na nchi nyingine wana sera hizi za kuweka watu kizuizini na wamewaweka watu kizuizini lakini watu hawaamki na kuanza kusema Obama ni Dikteta. Kuna watu walikamatwa wakachallenge kwenye mahakama zetu wakaachiwa! Nyerere hakwenda na kusema warudisheni ndani! Labda utusaidie ni kina nani hao "wengi" waliowekwa kizuizini:
a. kwa amri tu ya Nyerere bila Sheria
b. Kwa kusingiziwa pasipo makosa au reasonable cause.


4. aliua wengi kwa siri

"Wengi" inarudiwa tena - ni kina nani hao waliouawa na Nyerere kwa Siri. Changamoto yangu bado inasimama kwa wale wenye imani hii: Tutajieni japo hao watu 10 waliouawa kwa "siri" na Nyerere. Hii ni myths tu.

5. aliongoza nchi kwa nguvu ya giza (uchawi)

I'll not even comment on that lest I give it a measure of credibility.

6. alitumia polisi na usalama wa taifa kuwatisha watu

Jinsi gani? Hivi watu walikuwa wanaogopa Polisi kama wanavyowaogopa leo? Usalama wa Taifa was the most professional organization then kuliko sasa. Usalama wa Taifa unatakiwa uwe katika level hiyo huwezi kuwa na usalama wa taifa ambao watu wanaweza kuchezea tu. Nyerere hakuwatisha, wahalifu na watu waliokuwa na dili zao ndio walikuwa wanaogopa.

7. Kuitisha uchaguzi wa kivuli na mtu

Angalau huo ulikuwa ni uchaguzi; leo mna wabunge wangapi ambao hata hawakuchaguliwa hata kuwekwa na kivuli? Leo hii katika "demokrasia ya vyama vingi" mna kitu mnakiita "waliopita bila kupingwa" hii demokrasia ndio bora kuliko ya kupewa uchaguzi? Nyerere aliruhusu mgombea binafsi leo hakuna ndio demokrasia? Hivi unakumbuka ni viongozi wangapi walikuwa wanaangushwa katika hizi chaguzi za watu wawili toka chama kimoja?


8. kutosikiliza ushauri wa wataalamu wake

Wataalamu gani ambao hawakuwasikiliza ushauri wake? Waliomshauri nini? Ni rahisi kusema kuwa "kutosikiliza wataalamu wake" kwenye jambo gani? Mtaalam akishauri ina maana lazima umkubalie? Watalaamu hawa hawa? Yaani mtu akiwa mtaalam ina maana ushauri wake lazima ukubaliwe? Si wapo wataalamu bwelele leo wanasikilizwa na hawa viongozi wana demokrasia mambo leo.

Sasa utaona kuwa watu wanaomuita Nyerere Dikteta kwa maana hiyo wana mlima mrefu kweli kuweza japo kuthibitisha kwa mbali.

yako mengi MKJJ ambayo kwa sababu moja mtu anaweza kumuita Nyerere dikteta! we are using this word everyday!!!!!

Well.. sasa mtu anaweza kumuita Nyerere "dikteta" kwa sababu anajisikia hata kama hakuna ushahidi wa kiakili wa kufanya hivyo isipokuwa hisia. Kama hoja ni hiyo basi kuita huko hakuna nguvu zaidi ya kujaribu kutumia maneno mazito kirahisi rahisi bila kuyamaanisha.

Personally MSIMAMO WANGU NI KUWA HUWEZI KUZUIA WATU KUMUITA NYERERE DIKTETA!!!!

Na vile vile huwezi kunikatalia kuwapinga wanaomuita Nyerere Dikteta. Haki waliyonayo wao kumuita Dikteta, ni haki niliyonayo kuwapinga wao kumuita Dikteta!


I have
warned you
several times.....mapaka wazazi na wajomba huitwa madikteta wakati hawana jesho wala mahakama!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

I'll purposely ignore the sentiment za wewe kunionya au kunitahadharisha.

watu huita mpaka wachungaji na mashekh madikteta...

HII NI KAWAIDA NA NI HULKA YA BINADAMU

SASA KUTOKANA NA UBORA WA UONGOZI WA NYERERE INAWEZEKANA WENGINE ALIWAGUSA NA PIA WAMEWEKA VINYONGO NA WANAMWITA NYERERE DIKTETA....you see bado hujaondoa neno dikteta

Sina tatizo na neno "dikteta"; tatizo langu ni mlimaanishe lakini mkishalimaanisha muwe tayari kujibiwa. Ukisema Nyerere ni Dikteta be willing to defend that siyo kulazimisha kwa madai kuwa "naweza kusema lolote". Kama mna maana nyingine ya dikteta basi iwekeni ili angalau tuwaelewe na kuwaccommodate.

Ukiangalia jibu la Nguruvi hapo juu unaona anasema tena KISOMI kuwa ombwe la uongozi wa sasa linafanya watu warudi na kumkumbuka Nyerere kwa mazuri au mabaya

Juzi nimesema tena kwa crown yake ya kuwa yeye ni baba wa taifa still watu watamsema tu kwa mazuri au mabaya!!!! it is normal it is HUMAN!!!

Kesho ukifa, still watu watamwita Nyerere dikteta, na wako watasema mwenye HERI..wako ambao watafanya ziara mpaka makaburini kwakwe wakimsifia na wengine wataaandika ubaya wake woooote, MAISHA YATAENDELEA!!!

Hata wewe utakapokufa watakuwepo watu watakaomtetea Nyerere na kuwabeza wanaomuita Dikteta. Ni jambo moja kuzungumzia mazuri na mabaya ya mtu kwani hiyo ndio sehemu ya usomi na kujifunza. Tatizo ni kuwa watu wanataka kuweka msisitizo katika huo ubaya wa mtu na kuweza kuufanya uonekane ndio pekee unastahili kukubalika.

SIJAONA MANTIKI YA LIGI HII YA WEWE NA FAIZAFOXY FAIZA ANA UHURU WA KUSEMA NYERERE DIKTETA NA AKATOA SABABU...KWA HAPA DIKTETA LINAWEZA LIKAWA NI
NEOLOGISM


sina ligi na FF.

Kwahiyo, hiyo paper ambayo nimeweka nimeweka kuhakikishia umma kuwa sina tatizo na mtu yeyote kumsema Nyerere kwa mazuri au mabaya,


Hata mimi mbona sina tatizo hilo.

ULIPOSIMAMA WEWE NI KUWA HUTAKI NYERERE ASISEMWE KWA MABAYA...huwezi kuzuia hilo SOMEBODY help mwanakijiji please!!! you will never!! utaishia kuanzisha thread kila siku za 'dikteta' NYERERE mwishowe ukiwa na lengo zuri la kumtetea Nyerere wasiojua wataondoka na hiyo vocabulary mkuu!!! utatangaza ubaya wa NYERERE!!!

ooh no.. sitaki Nyerere asemwe kwa mabaya ya uongo au yale mapungufu yafanywe kuwa ni maovu. Mnajaribu kufanya mapungufu ya Nyerere kuwa "udikteta" huku mkishindwa kuonesha Udikteta katika mapungufu yake. Ubaya wa Nyerere ni nini hasa? Makosa ya uongozi ni sawa na ubaya wa mtu? Kila anayekosea ni mbaya.

Unapotumia emotion kubishana na FAIZA ambaye amekushinda kila kona, maana unabaki kujieleza na kutetea kitu ambacho hata FAIZA ANAKIJUA!!!! we are laughing!!! amekuteka dada wa watu HAUPUMUI, HAULI, KISA NYERERE!!! what is a big deal? yaani unataka kusema member woote elfu thelathini hawana akili ya kuchambua ukweli na ubaya au wewe unampenda Nyerere kuliko wengine wooote humu.?

Unlike you, I don't use emotions to respond to arguments. My arguments are soley based on rational thought. Unaandika kutoka katika hisia ukifikiria ninavyojisikia mimi. I don't do that. Wenye hisia wanaonekana kati yenu kwa sababu mkisikia jina la "Nyerere" mnajisikia kusisimka kwa ubaya. Mnaanza kuwa conditioned kuwa jina la "Nyerere" linawalazimisha kuzungumzia "mabaya yake".

NYERERE HAWEZI KUTETEWA NA MTU KAMA WEWE MWANAKJIJI, NYERERE ATAJITETEA NA KAZI ZAKE ZITASIMAMA, UBORA WAKE UTASIMULIWA VIZAZI VYOTE VIJAVYO, UBOVU WAKE UTASIMULIWA VIZAZI VYOTE VIJAVYO..wewe kazi hii uliyojivika voluntarily huwezi!!!

Emotional response; ad hominem per excellence. Nimezoea nikiwazidi kwa hoja mnaanza "mtu kama wewe"!

Nyerere siyo dini! Nyerere siyo mtume...Nyerere alikuwa binadamu na ndiyo maana amekufa!! amekufa na kinachobaki ni wasifu wake na kazi zake, sasa kama kuna mabaya asisemwe? why??

Well wote tutakufa kwani wote ni binadamu lakini hatuwezi kuacha watu kupotosha legacy ya mtu kwa sababu amekufa wakifikiri kwamba watu wengine wote watakaa kimya. Sehemu ya historia ni kuweza kufanya utafiti wa kuweza kumjadili mtu pasipo kulazimishwa kukubaliana na position moja. Tunachojaribu kupinga siku hizi ni hili jaribio la kujaribu kulazimisha historia ya "ubaya wa Nyerere" na maneno makali dhidi yake - Dikteta, na siku si nyingi mtaanza "muuaji" n.k It ain't gonna happen - at least not as long as I have the right mind.

Yes he was great leader, yet he was fallible, kwa sababu hatuna standard ya kosa au udhaifu wa mtu tuuweke kwenye rank gani basi wengine kumwita dikteta as
neologism to describe his character sioni tatizo!!


Kumuita mtu muuaji, mbakaji, dikteta nk ina connotations zake. You don't throw names loosely like that for the sake of political expediency. Kumuita "Dikteta" is not neologism sir; not its not unless you have also decided to change the meaning of what a neologism actually is.

Kama is a.k.a za Nyerere zimekuwa alama ya uadui na kutumiwa na kutokuwa mzalendo then count me in-proudly!!

Hapana bro, hakuna uadui na walahuna sababu ya kutafuta uadui kwa namna hiyo. Ni tofauti tu za kimtazamo na ni muhimu kuziheshimu hivyo. Nina maadui wa kutosha tu nikiongeza wengine watapata shida zaidi.


 
3D Daima uki present kitu kimekuboa unawakilisha bluntly.. would have not been more blunt... which is good sometimes.. Nakubalina na most unayo sema but as much as ume conclude hivyo ni vizuri tukaulizana hapa as in why do we think iko hivyo... Kwa nini GT wako behind the Avatar and just above the Signatures but the no true revealing ya mtu ni nani? anayowakilisha ndo anaamini? Je yuko upande alosema yuko? Je ni mwema kama anavyo ji pain? Na maswali kibao...

Fikra za watu, maisha ya watu, mazingira ya watu huabadilika taratibu (thou pace ni kali sasa) but for the next two or more generations to be better people ni lazima wa evolve from us kama sie tulivyo evolve from the past generations... Change will always be brought by the people themselves for it to suceed... Ndio tokana na umaskini wetu wa kua na majukumu na wategemezi kibao tunandecy ya kukwepa litalo kuletea matatizo kuepusha shari yoyote ile...

Ukisema hatuna kazi ya kufanya ... really.. bado personally naona hujajustify vya kutosha.. Ila nakuunga mkono kuhusu udini unaokuja kwa kasi.. ni mpaka nilipo jiunga JF ndo nimegundua hii issue... I DID NOT KNOW KUA kuna udini mkubwa kiasi hiki... na nimefuatilia saana, Most wachangiaji uelewa na upambanuzi wao ni wa Primary level pande zoote za Wakristo na Waislam... hakuna anaetoa constructive arguments kwamba mwenzangu ni Muislam/Mkristo anaelewa hili jambo hivi but i feel it is Wrong ngoja nimueleze vizuri... zimejaa kejeli na short arguments... ambazo hazielimishi wala kuongeza knowledge... mjadala kati ya these two groups unanuka!!! na ni katika uzi mbali mbali za jamii wala sio za dini..

Naposema Afrika haina kazi za kufanya simaanishi majukumu hayapo. Nachomaanisha badala ya kufanya mambo ya msingi Afrika inaona ina muda wa kutosha kujikita katika mabishano ya kijinga namna hii. Sijui Asha we uko nchi gani!! Hii chuki ya dini haiko hapa JF pekee. Leo hii kwa bahati mbaya nimeona Headlines za Magazeti ya Al-Huda, An-nuur na Kiongozi..... mi naishangaa serikali. Tafuta haya magazeti angalia yalichoandika, actually si yote yaliyoandika chuki ila ni theluthi mbili ya magazeti hayo. Kuna redio Morogoro, nadhani inaitwa Imaan... fuatilia, juzi hapa kuna wadau waliweka post ya kuilalamikia redio Wapo ya wapendwa. Hii michezo hii ndiyo inayotuudhi sisi makafiri na wapagani. Hao watakatatifu wanataka kutuharibia nchi yetu. Aisee, hatutakubali.

Afrika haina kazi za kufanya.
 
Naposema Afrika haina kazi za kufanya simaanishi majukumu hayapo. Nachomaanisha badala ya kufanya mambo ya msingi Afrika inaona ina muda wa kutosha kujikita katika mabishano ya kijinga namna hii. Sijui Asha we uko nchi gani!! Hii chuki ya dini haiko hapa JF pekee. Leo hii kwa bahati mbaya nimeona Headlines za Magazeti ya Al-Huda, An-nuur na Kiongozi..... mi naishangaa serikali. Tafuta haya magazeti angalia yalichoandika, actually si yote yaliyoandika chuki ila ni theluthi mbili ya magazeti hayo. Kuna redio Morogoro, nadhani inaitwa Imaan... fuatilia, juzi hapa kuna wadau waliweka post ya kuilalamikia redio Wapo ya wapendwa. Hii michezo hii ndiyo inayotuudhi sisi makafiri na wapagani. Hao watakatatifu wanataka kutuharibia nchi yetu. Aisee, hatutakubali.

Afrika haina kazi za kufanya.


3D genuinely it seems i am hanging out with the wrong crowd nashinda na wakristo
na waislam kila siku but never had that discussion ila during na baada ya uchaguzi...
Kamba kulikua na those elements.. I can not go further... i think am confused...
 
3D genuinely it seems i am hanging out with the wrong crowd nashinda na wakristo
na waislam kila siku but never had that discussion ila during na baada ya uchaguzi...
Kamba kulikua na those elements.. I can not go further... i think am confused...

Binafsi hizi arguments nimeanza kuzisikia tangu 1990 (kama sijasahau, I was young). Kuna tapes zilikuwa zinasambazwa, nakumbuka kuna dini moja ilitoa tapes zilizokuwa zinadai fulani nabii mkubwa sana katika dini moja kahamia dini nyingine huko huko "ahera aliko." Baadaye zilianza tapes zilizokuwa zimerekodi mabishano ya Waislam na Wakristo ambapo mwisho wake ilikuwa inaoneshwa dini moja imeshindwa na waumini wake kujiunga na dini iliyoshinda mabishano. Nilipokwenda O'level kuna vijana walikuwa wanakuja kutu-challenge juu ya makosa katika vitabu tunavyoviamini. Tulizoea. Nilipokuwa A'level kuna watu wa dini moja walilalamika kuwa walibaguliwa dini yao pale waliposahaulika kuachiwa chakula walipokwenda katika ibada. Nilishangaa. Uchaguzi wa mwaka jana umeleta mzozo sana wa dini. Sijaridhika na namna Rais alivyolishughulikia suala hili. Ana majukumu mengi lakini hili ni suala la msingi katika mustakabali wa nchi. Mi nimemwona Jk mara ya kwanza nadhani mwaka 1988 hivi, alikuwa kijana mdogo lakini alikuwa amechangamka, Jk wa sasa amekuwa mzito sana kuamua.

Nilipowekea bold maneno yako........... oh, may be you didn't have to say that, 'cause you have now made me sad.
 
Umeshushuka shuu! Siku zingine msijidai ku "challenge" just kwa ubishi tu. Unanini babuwee? Unachekeshaa.


next time jaribu kuwa mstaarabu! mtu akisha concede defeat si busara kumshushua bali mpe pongezi kwa kukubali kuelimishwa, sababu kuna mwingine angeweza kuamua kuweka ligi kwa ubishi tu bila sababu maalum. Nadhani una kaukosefu ka hikma kidoogo so jirekebishe, na masuala ya kushushua na mipasho it's best ukipeleka kulee saluni! ni vizuri tukitumia hii forum kwa kuelimishana na kujuzana na si kuzodoana bila sababu.
 
It ain't gonna happen.

Kama kumbukumbu haijanitoka aliwahi kuulizwa hilo swali na bbc kwamba sera zake zimefeli, alijibu ndiyo idea imefeli,mtangazaji kaendelea kwahiyo unatuambia kwamba na ulifeli ndo maana ukaamua kung'atuka ya kwamba idea zako zilikuwa mbovu?

Nyerere akajibu: Si kweli, akatoa mfano, Yesu alikuja hapa dunia kutuhubiria tufanye mambo mazuri, tusiibe, tusiseme uongo, tusizini, tusijambazi nk, lakini leo watu tunaiba, tunazini, tunaongopeana nk je unaweza sema Yesu alifeli na habari zake zilikuwa mbovu? kicheko ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaa mchezo ukaisha.

Nyerere alikuwa anajibu kisayansi, lakini hajawai kukili kwamba alishindwa yeye alichokili ni kwamba watanzania ndo wagumu wamekataa kufuata mafundisho mema na kufuata njia zao, ndio hao waliofeli sio mimi.

Na ndiyo maana ukimsikiliza zaidi kwingine utamsikia anasema"hua natembea na vitabu 2, kimoja Biblia na kingine kaazimio la arusha, haka ka azimio huwa nakarudia rudia lakini sijapata kuona sehem kalipo na makosa".

Hapa anawaambieni mlikataa kitabu chenye misingi mizuri na kukataa miiko itayowaongoza kenda kwenye heri. Sasa nang'atuka ili mfuate misingi yenu mibovu mnayotaka, kwani lulu hutupiwa nguruwe?
 
Kama kumbukumbu haijanitoka aliwahi kuulizwa hilo swali na bbc kwamba sera zake zimefeli, alijibu ndiyo idea imefeli,mtangazaji kaendelea kwahiyo unatuambia kwamba na ulifeli ndo maana ukaamua kung'atuka ya kwamba idea zako zilikuwa mbovu?

Sijui kama unakumbuka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom