Nimekuambia hakuna ulinganisho wa kimpira kwa sasa baina ya kenya na Tanzania, wewe unaongelea past ambapo tulikuwa sawa kiuwezo ila kwa sasa hatupo sawa katika level zote, kuanzia national team both men and women mpaka youth level, huku kwenye level ya clubs ndiyo kabisa tumewaacha mbali mnooooo.
Uthibitisho:
1. Fifa rankings tupo juu yenu kwa timu za taifa (men & women).
2. Timu zetu za taifa za football zote zimeingia kwenye michuano mikubwa, nyinyi hamna hata moja, mnaingia Afcon kwa mgongo wa timu mwenyeji (ambapo ata hivyo hamtoandaa)
3. Clubs zetu na zenu kwa sasa ni mbingu na ardhi, kuanzia revenues mpk mpira uwanjani, huwezi kuiongelea Gor Mahia au police, au bandari au shabana ambazo ndiyo giants wenu huko dhidi ya giants wa Tanzania.
4. Recently, timu zenu zote kubwa zimefungwa na timu za Tanzania,
(a). shabana kapokonywa kombe kabisa nyumbani kwake dhidi ya timu dhaifu ya Tanzania iliyopanda daraja ya Pamba FC,
(b). Gor Mahia kapigwa na Simba jana 2-0.
(b). Police bingwa wenu kafungwa na Singida ambayo ni timu ya 4 huku kwetu.
Kesho mabingwa wa nchi Dar es salaam Young Africans (Yanga) inacheza na bandari, nakushauri nunua kifurushi cha azam mapema ukiangalia jinsi timu yako inavyodhalilishwa 🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Hivyo basi, itoshe kusema kwamba kwa faida ya battle tunawaruhusu kujitutumua ili battle isife lkn hakuna ufanano kabisa kwenye soka kwa sasa.