Fikra za viongozi wa Africa ni za kipuuzi. Nyerere set us on a good path as a nation. Nakumbuka wakati huo Israel ilikuwa ikitusaidia na bado tukawatambua Palestina na kuwapa office Dar waisrael wakakasirika, pia South Korea, West Germany na Morocco walikasirika tulipowatambua mahasimu wao North Korea, East Germany na Sahara (POLISARIO) pamoja na umasikini wetu na uchanga kama taifa tukawaambia hamuwezi kutuchagulia marafiki kamwe kama vipi songa na tukafunga uhusiano wa kibalozi na nchi hizo zote. Ndio maana wakati ule passport ya TZ inaandikwa you can visit all countries in the world except South Korea, West Germany and Israel lakini baada ya muda wamerudi wenyewe baada ya kuona hatuyumbishwi na yeyote na pia tulikuwa founders wa Non Aligned Movement iliyoanzishwa na kina Nyerere Tanzania, Gamal Nasser Egypt na Jawarhal Nehru India. Pia Makaburu tukawa tunawapiga pini pamoja na USA kutushinikiza tuwatambue Makaburu tulikataa katakata ila jirani wa kaskazini kila anachooambiwa anatekeleza hana maamuzi yake mwenyewe.