concordile 101
JF-Expert Member
- Oct 13, 2013
- 6,314
- 14,357
Sidhani wako aggressive kwenye kukusanya mapato,bali hapo mwanzo waliwahi kuanzisha makampuni ya production huku sisi tukiwa kwenye subsistence.Kenya wanakusanya pesa vibaya sana.
TZ unakuta mtu ana duka na hana leseni.
Au mtu ana duka, lina Pombe, Vifaa vya ujenzi, umeme, sukari, viberiti na leseni moja tu ya rejareja shilingi Tsh 40,000.
Kwa Kenya hizo ni biashara 5. Na kila moja inatakiwa malipo.
Walijichanganya na ujinga wao wa DEVOLUTION, kulipa Wanasiasa mabilioni kutaka kuwa kama Marekani wakati uchumi wa Lodwar.
Sasa Kenya Mbunge anakula Milioni Tsh 36,000,000 mshahara tu.
Akikaa miaka 10, anapata pension maisha yote.
TZ Mbunge analipwa Milioni 18.
Hakuna pension, ila kuna malipo ya mkupuo ya Tsh 250M.
===
TZ Diwani anapata Tsh 380,000 kwa mwezi.
Kenya Diwani (MCAs) anakula Tsh 2M kwa mwezi tena huwa wanacheka kwamba wanapata pesa kidogo.
Wakati TZ kwa 2M ndio mishahara ya Wakurugenzi, wakuu wa mikoa na Wilaya.
Kenya wana usenge wa Bunge la Senate, kama Marekani😅
Maseneta wanalipa Tsh 20M kwa mwezi.
Pesa yote ni KULA tu.
====
TZ tungekuwa tunakusanya pesa AGGRESSIVELY kama Kenya mpaka tunapata makusanyo kama yao.
Tungekuwa mbali vibaya sana.
Kwa sasa ni kama wamejanjaruka maana hata viongoz wengi wameingia kwenye zile shughuli na kugundua kwamba kukiwa sera nzuri ni utajiri tosha kuliko kuiba .
Mfano ukiangalia rate ya viongoz waliojiingiza kwa kilimo ndo utapata majibu kwani bashe alikuwa mkali kwa Malawi.
Ukienda mkoa wa mtwara Ile stakabadhighalani ilivyoiingizia hela serikali,halmashauri kwenye mazao, sasa hivi Kila halmashauri inahamadisha kilimo zipo baadhi zimeanza kufikiria mipaka kuanza kutoa mbegu Bure ili waje wafidie kwenye ushuru.
Mifumo ya makusanyo imeboreshwa sana imebaki kuongeza vyanzo vya mapato.