Dodoma nje ya mji hakuna shughuli yoyote inayofanyika sababu ni pakavu balaa .
Mbeya mazingira yanaruhusu kilimo karibia msimu wote ndo maaana Kuna tofauti kubwa sana .
Ukiangalia mikoa mingi kama njombe ,songea,mtwara nyingi mapato yake ni mazao.
Ukiangalia mapato ya wilaya zote za mtwara 70% ni korosho+ ufuta+mbaazi+ karanga
Njombe miti
Songea mazao
Usisahau factor kuu ya watu wa Mbeya-Wapambanaji na watata kweli kweli.
Mawilayani kwenye hiyo Mikoa Kuna shughuli wanafanya but Hazina Tija saana kulinganisha na Mbeya labda Kutokana na Hali ya Hewa nk.
Mbeya inategemea zaidi shughuli za Kilimo especially Viazi,Mahindi,Tumbaku,Kakao,Pareto,ampunga, agro industries na Madini (Dhahabu ya Chunya).Yaani kila Wilaya Ina kitu chake inazalisha.
1.Chunya-Dhahabu & Tumbaku ,namba 1 & 2 Tanzania
2.Mbeya DC-Pareto & viazi ,namba 1&2 Tanzania
3.Kyela-Kakao na mpunga ,namba 1 Kwa Kakao Tanzania
4.Rungwe & Busokelo -Ni kati ya Wilaya top producers wa Chai,Parachichi na Ndizi Tanzania.
5.Mbarali-Top producers wa mchele/Mpunga wa Mbeya around 90% na ni full irrigation.
6.Mbeya Jiji-agro and food industries na Biashara ,ni economic centre ya mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Mind you Mbeya ndio Mkoa unaongoza Tanzania nzima Kwa matumizi ya pembejeo ya Mbolea ikifuata Ruvuma.
Mkoa kama Mwanza siku wakianza irrigation ndio watabadilisha maisha Yao badala ya kujazana pale mjini Kila mtu mchuuzi badala ya kuwa producers,wiwanda vingi vinakimbilia Shinyanga.
Dodoma kulingana na massive investments za serikali miaka ya baadae hata huko Mawilayani kutakuwa poa maana wanawaletea irrigation schemes za kutosha so hao wote itawachukua mda kuwa na living standards za watu wa Mbeya..
Ieleweke vizuri,Kilimo na ufugaji ni Kati ya shughuli ambazo ni less taxed ni kama hakuna kodi so pesa nyingi inaingia Kwa mkulima Moja Kwa moja.