Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Prof. Assad walikuwa na bifu na Magu kabla ya kuwa rais, hadi leo bado anamlalamikia marehemu, sasa huoni hiyo ni personal matter?
Bifu gani Hilo ambalo lilikuja baada ya Assad kuibua ufisadi wa Trilioni 1.5? Wacha usenge we jamaa
 
Mzee kweli unajuwa ku spin, nipatie mifano ya scandals kama za IPTL, Escrow, EPA, Radar, kuuzwa kwa NBC katika awamu ya 5.
Mkuuu nashukuru umekuja hapa, je ungeyajuaje kama sio ukaguzi , mambo mengi yaliibuliwa na ofisi ya Cag na yakafika bungeni wabunge wakajadili kwa uhuru.
Sasa nambie kipindi Cha magu ilikuwaje ? Magu alikubali mijadala kuwa wazi kama enzi za kikwete? Na kama kweli alikuwa anataka kudhibiti basi angeachia hiyo miradi ijengwe kwenye taasisi husika ila angebana na kuwachukulia hatu wakosefu
Kweli, rais ndiyo mtoa pesa ila kama siyo msimamizi mzuri, watu watakula kwa urefu wa kamba zao.
Mkuu raisi hawez kuwa sehem zote na ndo maana kukawa na taasisi kama usalama wataifa, pccp, Cag na kwa wakaguzi wandani wapo karibia Kila taasisi na ripoti zao hutoka Kila mwaka.
Nambie ni ripoti gani ya Cag iliyoibuliwa kipindi Cha magu akaifanyia kazi walau hata kuwaweka lockup wahusika.

Mbona haya ya kugushi ndiyo yaliyozuiwa zaidi amwamu ya 5? Hivi unafikiri wananchi ni wajinga kumpenda Magu? siyo rahisi kudangaya watu mil 60, kama unayosema ni kweli watu wangesema.
Wananchi wanampenda sababu alizuia watu wasijue uchafu kwa hiyo ikaonekana yeye ndo Bora kwa sababu hawakuwa na taarifa
 
Umeona mahali nampinga Rais Samia kwa kuendeleza miradi? Tunachohoji ni kujisahaulisha yale aliyoyafanya Magu. Yaani woote kuanzia Nyerere, Mwinyi, Mkapa hadi Kikwete wanapata credit kwa miradi yao isipokuwa Magu. Huoni kuna tatizo hapo?
Hakuna tatizo mkuu, muhimu project ipo accomplished.
 
Mkuuu nashukuru umekuja hapa, je ungeyajuaje kama sio ukaguzi , mambo mengi yaliibuliwa na ofisi ya Cag na yakafika bungeni wabunge wakajadili kwa uhuru.
Sasa nambie kipindi Cha magu ilikuwaje ? Magu alikubali mijadala kuwa wazi kama enzi za kikwete? Na kama kweli alikuwa anataka kudhibiti basi angeachia hiyo miradi ijengwe kwenye taasisi husika ila angebana na kuwachukulia hatu wakosefu
Mbona watu walikuwa wanamchana hadharani mitandaoni, tena kipindi chake ndo watu waliongea sana, mpaka magazeti ya nje yalimwandika. Kama kungekuwa na skendo ya kweli wangeongea tuu.
Mkuu raisi hawez kuwa sehem zote na ndo maana kukawa na taasisi kama usalama wataifa, pccp, Cag na kwa wakaguzi wandani wapo karibia Kila taasisi na ripoti zao hutoka Kila mwaka.
Rais hayuko sehemu zote ila ndiye kiongozi mwenye mamlaka ya juu. Kama akiwa mkali kwa wala rushwa na wakwepa kodi, wataogopa kuvunja sheria.
Wananchi wanampenda sababu alizuia watu wasijue uchafu kwa hiyo ikaonekana yeye ndo Bora kwa sababu hawakuwa na taarifa
Dah, uko vizuri ku spin aisee, yaani hata vitu wazi kabisa unazungurusha. Hivi kweli unaweza kudanganya Taifa zima bila ya watu kunung'unika chini chini? Kama hayo unayosema ni kweli basi hayo yangesikika.
 
Sasa si bora JPM kuliko huyu aliyepo low score , hata hajui anafanya nini . Inakuwa leo inakuwa kesho, ufala wa ccm kulazimisha kubalance gender to please the west’s madness. Wastage .
Labda mkuu ungetuambia mradi ambao umesimama au hauendelei
 
Mbona watu walikuwa wanamchana hadharani mitandaoni, tena kipindi chake ndo watu waliongea sana, mpaka magazeti ya nje yalimwandika. Kama kungekuwa na skendo ya kweli wangeongea tuu.
Mkuuu magazeti hayawez pata access ya vitu potential bila ya ukaguzi Sasa magu aliidhit ukaguzi na Wala pale uovu ulipotokea alikuwa anamshughulikia mtoaji mfano na Cag utoah kikwete aliacha watu waibue wizi .Kuna watu waliwahi wajibishwa mfano wa lowasa. Magu hajawahi muadhibu mtu tena mtu wake kwa sababu ya wizi
Rais hayuko sehemu zote ila ndiye kiongozi mwenye mamlaka ya juu. Kama akiwa mkali kwa wala rushwa na wakwepa kodi, wataogopa kuvunja sheria.
Mkuu unakwepa Nini, nimekupa mfano kama kweli alikuwa mkali kwanini alishindwa chukua hatua hasa kwa watu wake walipoumbuliwa kuiba. Hivi ndungai alipofoji kutumia bil 12 India alimshughulikia?
Magu aliwashughulikia vipapa yaan watu wasio na ngazi .
Dah, uko vizuri ku spin aisee, yaani hata vitu wazi kabisa unazungurusha. Hivi kweli unaweza kudanganya Taifa zima bila ya watu kunung'unika chini chini? Kama hayo unayosema ni kweli basi hayo yangesikika.
Mkuu hivi unajua hata serikali inavyofanya kazi? Hiv unajua voucher za malipo zinavyolindwa sana na hakuna mtu anaweza kuacceas zaid ya mkaguzi na mhusika tu, hakuna mwandishi Wala mtu idara nyingine anaweza ingia voucher room ? Unajua kwanini .
Sasa kwa sisi ambao hatuwez ingia muibuaj wa ufisadi ni mkaguz Sasa magu alikuwa anaadhibu wakaguzi au hulijui?
 
Mzee kweli unajuwa ku spin, nipatie mifano ya scandals kama za IPTL, Escrow, EPA, Radar, kuuzwa kwa NBC katika awamu ya 5.

Kweli, rais ndiyo mtoa pesa ila kama siyo msimamizi mzuri, watu watakula kwa urefu wa kamba zao.

Mbona haya ya kugushi ndiyo yaliyozuiwa zaidi amwamu ya 5? Hivi unafikiri wananchi ni wajinga kumpenda Magu? siyo rahisi kudangaya watu mil 60, kama unayosema ni kweli watu wangesema.
Mkuu awamu ya 5 ndo Ina kesi nyingi za kughushi na ndo Kuna wizi mkubwa sana fikiria watu walisomba tri 1.5 na hakuna aliyewajibishwa ila akawajibishwa aliyeibua
 
Labda mkuu ungetuambia mradi ambao umesimama au hauendelei
Miradi inaendelea sababu hakukuwa na namna zaidi ya kupambana kuendeleza, we ulitegemea watelekeze SGR , au bwawa la umeme ? Was it possible ?
Ningekuchukulia serious ungesema ni kitu gani kipya wamefanya baada tofauti na alivyoanzisha Jiwe ,
Nothing , and that proves how incapable they are , hawana jipya hawa hawawezi ,
Tulitegemea walau tuone hata barabara ya njia nne kibaha morogoro wajitutumue, but hata ile tu ya Kimara-Kibaha bado wanahaha kuimalizia hadi leo. Uwezo mdogo, only stealing and looting ,
Ile timu ya mpira ya ihefu ambayo sasa hivi inaitwa sijui singida black nini sijui waziri mmoja aliinunua bilioni 7 cash,
Unajiuliza mzigo wote huo aliutoa wapi ? Na anategemea kurejeshaje pesa yake ? Yaani ananufaika nini na timu ? Hapa kuna Siri gani ?
Ni vile tupo kwenye nchi isiyo na mifumo ya kuhold watu acountable,
Wonder you still have faith on such people ? We are doomed mateys.
 
concordile 101 wacha tukubaliane kuto kukubaliana.
Hapana mkuu tukiruhusu nchi yetu iende kwa hisia hatuwezi fika mahali popote. Mkuu hakuna sehemu rahisi kuiba kama kwenye miradi ya ujenzi na dalili Moja ya wizi ni cash payment. Sasa jiulize ikawaje mwenzetu akawa analipa cash kitu kama ununuzi wa ndege alibeba kiasi gani kwa mfuko.
Tukitaka tufanikiwe lazima tuzijengee uwezo taasisi zetu sio kuzikandamiza .
Mimi namlaumu magu kwa Sabab alizuia watu wasikague vitu alivyokuwa anasimamia na hata kuongea ilikuwa marufuku
 
Miradi inaendelea sababu hakukuwa na namna zaidi ya kupambana kuendeleza, we ulitegemea watelekeze SGR , au bwawa la umeme ? Was it possible ?
Ningekuchukulia serious ungesema ni kitu gani kipya wamefanya baada tofauti na alivyoanzisha Jiwe ,
Mkuu nadhan Inawezekana kwako ujenzi ni barabara labda ni kwasababu havitangazwi kama kipindi Cha magu kwako inakuwa ngumu kutambua. Kuna miradi mingi sio ya ujenzi kwa kada mbalimbali Mimi ntakutajia michache tu
1. Ajira almost 150,000 magu alikaa miaka mitano hakufikisha hata 4000 huo ni mrad sababu wananchi wanahitaji kazi
2. Ujenzi wa madarasa nchi nzima, shule za 3bil Kila mkoa, ujenzi wa shule mpya Kila kata .
3 , ujenzi wa miradi ya maji mipya ( ruvuma - Mangaka(30bil

Nothing , and that proves how incapable they are , hawana jipya hawa hawawezi ,
Tulitegemea walau tuone hata barabara ya njia nne kibaha morogoro wajitutumue, but hata ile tu ya Kimara-Kibaha bado wanahaha kuimalizia hadi leo. Uwezo mdogo, only stealing and looting ,
Ile timu ya mpira ya ihefu ambayo sasa hivi inaitwa sijui singida black nini sijui waziri mmoja aliinunua bilioni 7 cash,
Mkuu maendeleo sio barabara tu Kuna mpaka human development ikiwemo ajira. Ukitoa mfano wa mwigulu kumbuka alikuwapo enzi za magu Sasa Mimi naweww tuulizane kapata wapi Sasa au kipindi kile maana hata makonda umuweke kwa utajiri alionao maana kwa mshahara wa mkuu wa mkoa Hana uwezo wa kununua hata hiyo range

Unajiuliza mzigo wote huo aliutoa wapi ? Na anategemea kurejeshaje pesa yake ? Yaani ananufaika nini na timu ? Hapa kuna Siri gani ?
Ni vile tupo kwenye nchi isiyo na mifumo ya kuhold watu acountable,
Mifumo nyinyi ndo hamuitaki Cag alipoadhibiwa kwa kuibiwa wizi Kila mtu akisema ana bifu na magufuli hakuna aliyeangalia chanzo
Wonder you still have faith on such people ? We are doomed mateys.
Mimi simuamini yeyote ila naamini katika kutengeneza mifumo dhabiti na ukweli tu na ndo maana kwangu kikwete was the best of all Sabab aliachia watu watiririke wajuavyo tukayajua mawizi makubwa sana Dunia hii
 
Back
Top Bottom