Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Wengine January to December ni kupost tu apartments utadhani nchi zingine watu wanalala nje. 😂😂😂
Apartment's zenyewe kila mwezi zinadondoka kwa sababu ya kujengwa chini ya kiwango.
Tutatenga, tumetenga, tuta tuta.
Kwa wenzetu 🇰🇪 mfanya kazi au mfanya biashara wa kati kumiliki ardhi karbu na miji au majiji ni ndoto.Ndomaana matajiri wachache manaomiliki mapande makubwa ya ardhi hujenga magorofa kwa ability ya kupangisha kama ya chini au kuuza kwa kama ya kati.
 
Nikindi gani ambacho kulikuwa na ufisadi wa Richmond,EPA, Dowans hadi waziri mkuu akajiuzuru kuiokoa serikali aka mbuzi wa kafara maake watu wanatufanya kama hatujui kila awamu imefanya nini
Hilo la elimu lote mimi nalifidia kwa sera ya Magufuli ya elimu bure.
Utambue kuwa unapoweka huduma fulani bure serikalini kunatakiwa kuwe na fungu la uendeshaji hiyo huduma.

Kuna vituo vya afya hususan maeneo ya vijijini vingi tu vilijengwa kipindi cha Magufuli na hata mimi nimeshuhudia.
Morogoro mkoa naotembea sana kuna vituo vya afya vitatu vilijengwa kwa wakati mmoja katika vijiji vitatu vinavyofuatana mnamo 2017 kama sijakosea.
Pia kuna vifaa tiba muhimu kama CT-Scan nahisi vilianza kuingizwa ama kuagizwa kwa wingi kipindi cha Magufuli.
Sera ya kubobeza madaktari ili wabaki katika vituo vyao badala ya kuandika rufaa lukuki kwa wagonjwa hili lilianza kipindi cha Marehemu Magufuli.

Hapa sasa ndio patamu zaidi mkuu.
Hivi umeshajiuliza pesa za kulipa hao watumishi wa umma na kuajiri zaidi zinatoka wapi!?
Mnafurahia mishahara mikubwa pasi na kujua wapi inatoka.
Kwa pato gani la taifa kila awamu uongeze mishahara!?
Mwishowe mnakopa na nchi inazidi kuwa na madeni baadae kupelekea devaluation ya shilingi yako.
Magufuli alishasema wazi,serikali ya Tanzania haina hizo pesa kiuhalisia za kuongeza mishahara kila wakati na kuajiri kila wakati.
Ila usisahau kuwa aliwapa kipaumbele wajasiriamali wadogo wadogo na vijana na kina mama kwa kuwapa fedha za mikopo kutoka Halmashauri.Hili jambo halikuanzia kwa Samia lilianzia kwa Magufuli.
Alitengeneza mazingira wezeshi ya hadi wa mtu wa chini kupata pesa.
Ila uliza sasa hivi hali ikoje mtaani.

Mimi kila leo naingia ofisi za utumishi wa umma.
Sijaona huo uhaba unaousemea zaidi ya kurudi kwa uzembe na kutokujituma kwa watumishi wa umma na kukosa nidhamu ya utumishi wa umma.

Usiseme miradi midogo unakosea hilo.
*Ufufuaji wa reli ya Kaskazini Arusha.
-Uboreshaji wa reli kuwa continuos welded kutoka kuwa jointed rail.
Maana hii reli Kikwete aliirudisha toka kwa wahindi ikiwa mufrisi.
*Uboreshaji wa bandari.
*Uanzishwaji wa viwanda vidogo na vya kati.
*Uboreshaji wa sekta ya madini kwa kuweka mashine ya usafishaji dhahabu kuwa 99.99% pure na uozeshaji wa makinikia.
-Kuwapa fursa wachimbaji wadogo wadogo wa kufanya biashara ya madini na kupata mikopo wezeshi ya kuwezesha shughuli zao.

Hii unasema ni miradi midogo mkuu!??

Aya endeleeni kufurahia serikali za danganya toto kukopa ili iwaongezee mishahara na ajira ilhali nchi inaoza.
 
Nikindi gani ambacho kulikuwa na ufisadi wa Richmond,EPA, Dowans hadi waziri mkuu akajiuzuru kuiokoa serikali aka mbuzi wa kafara maake watu wanatufanya kama hatujui kila awamu imefanya nini
Mkuu kwa hii thread tungeacha hii discussion labda tuanzishe thread nyingine ya kufanya comparison kati ya magu versus kikwete na magu versus Samia . Hapa tunawakwaza wengi kwa sababu sio lengo la thread husika. Kama ntakuwa nimekukera natanguliza samahani
 
Nikindi gani ambacho kulikuwa na ufisadi wa Richmond,EPA, Dowans hadi waziri mkuu akajiuzuru kuiokoa serikali aka mbuzi wa kafara maake watu wanatufanya kama hatujui kila awamu imefanya nini
Mkuu tunyamaze tu maana watu wanalalamika kuwa tunaharibu uzi wao.
Ila ukweli unajulikana hivyo vyote vilitokea awamu ya Kikwete na Lowassa akiwa waziri.
 
Eti tuache kutumia unyama huu, tutumie zile kopo wanazotengeneza kunyans 😂😂😂 Ndani ya Sama luxury on my way to Rock city. 👇🏾
IMG_2229.jpeg
 
Huwezi kupunguza foleni kwa kupanua barabara. Baada ya muda zitakuwa hazitoshi,tE mpaka wapi? RELIABLE PUBLIC TRANSPORT NDIO INAONDOA KERO YA FOLENI. una majiji makubwa duniani yana barbara pana na za kisasa lakini foleni iko pale pale. Mwendokasi haijawekwa kuremba mji ni njia sustainable ya kuondoa kero ya foleni. Inakupoa option uamue kukaa kwenye gari yako masaa mawili au upande bus 25 minutes kufika mjini. Tumefanya uzembe kwenye uendeshaji awamu ya kwanza ndio maana tumefika hapa. Mradi ulianza vizuri na watu wengi walikuwa wanaacha magari lakini kama kawaida yetu upuuzi wa jadi tujauharibu mradi wenye wamagari wakarudia magari yao.
sikatai wazo lako kabisa BRT ni muhimu sana, city rail ni muhimu sana lakini lazima iendane na barabara pia, haimaanishi ukiwa na BRT na city train basi barabara ziwe finyu hapana bro lazima kila infastructure ijengwe kwa upana wake hasa kwa kuzingatia ukuaji wa population, ni muda barabara zipanuliwe ziwe hata 8 lanes njia ya airport etc, unazungumzia watu million 10 by 2030 dar pekee bro bila kua na barabara pana zenye kupitika muda wote usitegemee BRT na City train itamaliza kero never ever ndio maana nchi za wenzetu wana kila aina ya infastructures na still wana barabara mpaka 16 lanes, tuseme wao hawana akili ???
 
sikatai wazo lako kabisa BRT ni muhimu sana, city rail ni muhimu sana lakini lazima iendane na barabara pia, haimaanishi ukiwa na BRT na city train basi barabara ziwe finyu hapana bro lazima kila infastructure ijengwe kwa upana wake hasa kwa kuzingatia ukuaji wa population, ni muda barabara zipanuliwe ziwe hata 8 lanes njia ya airport etc, unazungumzia watu million 10 by 2030 dar pekee bro bila kua na barabara pana zenye kupitika muda wote usitegemee BRT na City train itamaliza kero never ever ndio maana nchi za wenzetu wana kila aina ya infastructures na still wana barabara mpaka 16 lanes, tuseme wao hawana akili ???
Njia ya airport kimsingi ilifaa kuwa na lanes 6 za gari za kawaida+ lanes 2 za brt, ile barabara sasahiv tu tayari imeshazidiwa
 
Back
Top Bottom