Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Unachosema ni Sawa kuna haja ya kuja kujenga station Kubwa eneo lingine litengwe nje kidogo ya mji ,kuongeza Station mpya kubwa .

Pia kama tutafanikiwa kumaliza SGR to Kigoma by 2030 .

Muhimu kufikiria ku link Dodoma to Mbeya by SGR na Dodoma to Tanga via Arusha na Moshi by SGR . Hii Itafanya Tanga Port na Dar Port zote kuwa linked na SGR na hivyo kuwa na Link Port 2 .
.Kipande cha Mbeya kama kikifika Ziwa Nyasa nayo itakuwa vizuri..Hii itafanya SGR iweze kubeba mizigo mingi zaidi
Stesheni si ndogo ile ni upuuzi wa Kadogosa ticketing machines zinapaswa kuwa at least 6 ndani na at least 2 kwenye platform na kuangalia jinsi ya ki-discourage watu kukata tiketi dirishani!

Mimi najiuliza hizo benchmark tours za Seoul walikuwa wanaenda kufanya nn kama hawakujifunza operations zinaenda vp?

There is no way SGR Station yenye route moja kuelekea Dodoma inaweza kuwa announced ndogo! Tembeeni duniani muone! Kuna ujinga mwingi pale kwenye management! Escalator imeharibika inaenda mwezi haijakarabatiwa!
 
Iringa 👇👇
wizarayamaliasilinautalii_1717682046844237.jpg
wizarayamaliasilinautalii_1717682046844819.jpg
wizarayamaliasilinautalii_1717682046844116.jpg


View: https://youtu.be/b0--YK07Q2U?si=Bb1FXzT9UIjZDuaX
 
Ni kweli kabisa, station ni ndogo kama watakuwa wanatoa abiria wote wa mikoani kwa wakati mmoja angalau wangekua wanawagawa kwamba abiria wa Dodoma wakae floor a abiria wa Morogoro wakae floor b wakati wanafanya ticketing na kusubiri train lakini kuwakutanisha wote ni uongo, abiria wa Morogoro tu wametosha kufanya floor yote kuwa busy, vipi kama wakikutana wa mikoa yote project ikikamilika? Pia waweke multiple take offs with at least 2 hours intervals na wasisitize watu wakate online, mtu afike station tu dakika 35 kabla ya safari ili kupunguza congestion,

Au kingine waende kinyume na utaratibu kwamba mtu akate ticket aende moja kwa moja ndani ya train hakuna wengi kukaa waiting lounge, au baadhi ya slots waziminimize waongeze waiting lounge au waongeze automatic ticketing machines na waziweke kule nje kabla mtu hajaingia terminal na ziwepo nyingi angalau 15

Milango pia ni midogo sana wafanye Milango iwe mipana
Nadhani solution ni kujenga station kubwa Pugu na kuionganisha na BRT alafu hii iwe inafeed hiyo station sio lazima abiria wote kuja kushukia mjini au kupandia mjini, unganisha SGR na BRT na major bus stations, abiria wa Mbeya anayekwenda Mwanza anashuka Magufuli Terminal anachukua BRT mpaka Pugu Terminal anaunga na train yake, hili linawezekana kirahisi sana na wakifanya ndipo utaona faida ya intergrated transport system. Lakini pia idea ya abiria wa MGR kupandia kwenye new station is off, naona wanarenovate former station ya MGR ili wa MGR wapandie kule na wawekewe na platform yao, hiyo space walitenga kwa MGR itumiwe na SGR tu.
 
Back
Top Bottom