Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Kwahiyo unataka kuendesha bandari vile utakavyo wewe, sio vile watakavyo wateja wa hiyo bandari?.

Wamiliki wa Meli wanalalamika kwamba bado bandari yetu haijafikia viwango vinavyohitajika kutokana na kutumia vifaa vya kizamani, wewe hutaki unang'ang'ana na kubanana na watu hao hao ambao hawana utalaamu, itabidi bandari yako uitumie kuvulia samaki, hakuna Meli zitakazo tumia bandari yako.

mkuu hujui biashara, tujadili kwanini Yanga na Simba zinafundishwa na wageni na watu hawalalamiki?, ila serikali ikiwapa wageni kazi za kuendesha miradi tunalalamika, inawezekana huko Ukatoa msaada mzuri zaidi.
Vifaa si vinanunuliwa tuu? Gharama za kununua vifaa siyo sawa na gharama za kuwapa DP World mkataba usio na kikomo. Ikitokea vita na wao wakashirikiana na adui kutuhujumu kupitia bandari utajuwa?

Nchi kama Uingereza wamefanya ubia na DP World kwenye vigati vichache tuu, siyo bandari nzima, huu ni ujuha. Hao jamaa mikataba yao mingi ni ya rushwa, nchi nyingi teyari zimewapeleka mahakamani.
 
Kusema ukweli kwa muda mrefu nimekuwa nikiwaza juu ya serikali kushirikiana na private sector kwenye ku-run/ku-manage baadhi ya mashirika na taasisi za umma ili kuleta ufanisi in a win-win situation. Kwa hiyo kwangu mimi Kuwapa DP-World kumanage shughuli za bandari zetu (as long as they have a good proved record in the sector) sio jambo baya wala jipya ila tatizo la sisi watz na waafrika kwa ujumla ni mikataba ya hovyo na ya kinyonyaji ambayo nchi zetu zinaingia na hawa private sector tena wengine ni incompetent kabisa/wababaishaji.
Unafahamu hawa DP world nchi ngapi wamepelekwa mahakamani kwa kutoa rushwa ili wapate mkataba?
Natamani kuona mashirika ya umma kama DART, TRC, Tanesco, na mengineyo yakiingia ubia (partnership) na private sector kwenye ku-run/ku-manage the business part ya hayo mashirika in a win-win situation. Serikali ilishaacha kufanya biashara na pale serikali inapolazimisha kufanya biashara hzi taasisi au mashirika mara nyingi kama si zote huwa ni hasara tu au faida kiduchu sana. PPP ikiwekewa utaratibu mzuri mi naona ndio njia pekee ya mashirika na taasisi zetu zinazofanya biashara zinaweza kukua na kuchangia vizuri kwenye pato la taifa otherwise kila siku tuatakuawa tunaona madudu tu kwenye riport ya CAG.
Uzalendo usio na tija ni sawa na zero tu. Kwa mantinki yako ni kwamba hata viwanda tulikosea kuwapa private sector au siyo? Hiyo TBL na viwanda vingine unavyoviona leo vinazalisha bidhaa bila mgogoro ni kwa sababu ya private sector ukivirudisha hivyo viwanda viendeshwe na umma hata mshahara wa kulipa wafanyakazi utakuwa kizungumkuti.

Hivi Rites ya India ilileta mafanikio gani kwenye shirika letu la reli, zaidi ya kuliua?
 
Vifaa si vinanunuliwa tuu? Gharama za kununua vifaa siyo sawa na gharama za kuwapa DP World mkataba usio na kikomo. Ikitokea vita na wao wakashirikiana na adui kutuhujumu kupitia bandari utajuwa?

Nchi kama Uingereza wamefanya ubia na DP World kwenye vigati vichache tuu, siyo bandari nzima, huu ni ujuha. Hao jamaa mikataba yao mingi ni ya rushwa, nchi nyingi teyari zimewapeleka mahakamani.
Inaonekana wewe ndiye juha, nani amekuambia kwamba tayari wamepewa mikataba ya kazi?, tuambie Kama wameshapewa, wamepewa kwa muda gani?. Toa ushahidi Kama hapa Tanzania wameshapewa gates zote, hata hapa Tanzania pia TICS hawakupewa bandari yote, mkuu Wacha kusikiliza maneno ya vijiweni.


Ninekuambia, inaonekana upande huu huna uwezo nako, tuzungumzie Simba na Yanga Mkuu.

Bunge ndio kwanza limepitisha mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi kati ya Tanzania na Dubai, hii Sasa inatoa nafasi kwa TPA na DPW kukubaliana "terms na maeneo ya kufanya kazi kwa pamoja, huyo aliyekuambia kwamba tayari muda na terms za kazi wameshakubaliana ni nani?

Wewe endelea kutoa maoni jinsi ya kushirikiana na wabia kuiendesha hiyo bandari, tayari bunge limeridhia DPW kuingia ubia, ukiendelea kupiga kelele za kupinga huu ubia haitokusaidia kwa Sasa.
 
Unafahamu hawa DP world nchi ngapi wamepelekwa mahakamani kwa kutoa rushwa ili wapate mkataba?



Hivi Rites ya India ilileta mafanikio gani kwenye shirika letu la reli, zaidi ya kuliua?
Mkuu unafahamu serikali ya Tanzania imepelekwa mahakamani mara ngapi na kushindwa kwa sababu ya kukiuka mikataba na wawekezaji bila sababu za msingi hadi Leo ndege zinakamatwa?, Je hiyo ni sababu tosha ya kufanya Tanzania isipate tena wawekezaji?.

Kwahiyo DPW akiwa na kesi maana yake ameshitakiwa au yeye ndiye ameshitaki?, Kesi ngapi DPW ameshindwa na kuamrishwa azilipe fidia hizo nchi?.

Lete ushahidi kwamba walipelekwa mahakamani kwasababu walitoa Rushwa Ili wapate mkataba, Wacha maneno ya vijiweni mkuu, sisi hapa ni wasomi.


Hivi serikali ilileta mafanikio gani wakati ilipokua ikiendesha TCC, TCL, TBL, Sungura Textile, Urafiki Textile, Kilimanjaro machine Tools, Viwanda vya Cement na viwanda vya tumbaku ambavyo hadi Leo vimekufa?
 
Oh Kenya. ...blah blah blah... Ahero interchange taking shape...We move.
FB_IMG_1686683636568.jpg
 
Inaonekana wewe ndiye juha, nani amekuambia kwamba tayari wamepewa mikataba ya kazi?, tuambie Kama wameshapewa, wamepewa kwa muda gani?. Toa ushahidi Kama hapa Tanzania wameshapewa gates zote, hata hapa Tanzania pia TICS hawakupewa bandari yote, mkuu Wacha kusikiliza maneno ya vijiweni.


Ninekuambia, inaonekana upande huu huna uwezo nako, tuzungumzie Simba na Yanga Mkuu.

Bunge ndio kwanza limepitisha mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi kati ya Tanzania na Dubai, hii Sasa inatoa nafasi kwa TPA na DPW kukubaliana "terms na maeneo ya kufanya kazi kwa pamoja, huyo aliyekuambia kwamba tayari muda na terms za kazi wameshakubaliana ni nani?

Wewe endelea kutoa maoni jinsi ya kushirikiana na wabia kuiendesha hiyo bandari, tayari bunge limeridhia DPW kuingia ubia, ukiendelea kupiga kelele za kupinga huu ubia haitokusaidia kwa Sasa.

Hakuna uwazi, unajuwa kilichosainiwa MOU feb 28 2022, kwenye Dubai expo? Unajua kilichosainiwa Oct '22 na serikali. Mbona walikaa kimya hawakutueleza kuhusu DP World mpaka taarifa zilipovuja ndo wanajibaraguza kujidai kutaka kujadiliwa bungeni.
 
Sasa unaanza kuelewa, bunge juzi lilitoa maelekezo ambayo yatasaidia TPA na Wizara husika kuingia mkataba rasmi na DPW. Subiri tutaelezwa maeneo gani na kwa muda gani hawa jamaa watakabidhiwa.
Eti naanza kuelewa, mimi naelewa tangu kitambo kuwa Samia hana uwezo wa kwakua hana utashi. Na pia najua kitambo kuwa serikali ya Samia imejaa matapeli wengi mno ndio maana tangu imeingia madarakani hatukuacha kuipinga.

Wewe ndio huna ujualo zaidi ya kufuata upepo. Eti bunge,

1. unajua kuna watu wame risk maisha yao kwa kuvujisha ule mkataba? Unafikiri ungeenda bungeji hila hivyo?

2. Kule Dubai wamesign mikataba kibao, hiyo mingine mbona haijadiliwi bungeni? Huu umejadiliwa, sio umejadiliwa, yaani wamefunika kombe kwa aibu kwakua umevuja.

Kama kuelewa, nitaanza kuelewa wakianika mikataba waliosign Dubai. We are not kids, brother. Sisi tumeelimika na tunajua nini tunapigania, tupo kwenye harakati kitambo. Hapa ni Geza tunajuana tango 20006/7 kama sikosei, hatujaanza huku JF.
 
Mkuu unafahamu serikali ya Tanzania imepelekwa mahakamani mara ngapi na kushindwa kwa sababu ya kukiuka mikataba na wawekezaji bila sababu za msingi hadi Leo ndege zimakamatwa, Je hiyo ni sababu tosha ya kufanya Tanzania isipate tena wawekezaji, kwahiyo DPW akiwa na kesi maana yake aneshitakiwa au yeye ndiye ameshitaki?, Kesi ngapi DPW ameshindwa na kuamrishwa azilipe fidia hizo nchi?. Lete ushahidi kwamba walipelekwa mahakamani kwasababu walitoa Rushwa Ili wapate mkataba, Wacha maneno ya vijiweni mkuu, sisi hapa ni wasomi.


Hivi serikali ilileta mafanikio gani wakati ulipokua ikiendesha TCC, TBL, Sungura Textile, Urafiki Textile, Viwanda vya Cement na viwanda vya tumbaku ambavyo hadi Leo vimekufa?
Wewe umezaliwa meaka gani? Unajua kilichopelekea hivyo viwanda kufa?

Wewe utakuwa umezaliwa 1990s kama ulizaliwa before 1980, then unamatatizo na shule.
 
Back
Top Bottom