Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Battle: Dar es Salaam vs Nairobi

Eti hilo neno "pesa" la wapi

Mungu wangu! Naishia hapo hapo!

Wakenya tunaopigishana nao humu ndani IQ yao no ndogo sana. Yani mpaka najisikia kuachana na huu uzi.
Peso- Portuguese meaning money. Contact between Swahili and Portuguese explorers - pesa. Utohozi
 
HQ ya sport pesa iko wapi?? 😅😅😅 na je inamilikiwa na nani? Ukipata majibu unitag kwanza kenge wewe
Pesa zetu ndo zilifungua hizo ofisi za Liverpool, source guardian newspaper
Screenshot_20230613_202311.jpg
 
Mkuu, kwani tatizo ni management pekee?.
1)Mtaji
2)Utaalamu
3)Network
5)Experience

Hawa DPW wanamiliki zaidi ya Meli 500 za mizigo zikizunguka Dunia nzima kufanya biashara, Wana mtandao mkubwa Sana wa biashara.

Mkuu, hivi mbona hujiulizi inakuaje team zetu za mipira barani Afrika zinafundishwa na wageni?.

Mkuu, hapa Tanzania wafanyabiashara wakubwa 10, unaweza kukuta sisi waswahili ni wawili au mmoja. Afrika Migodi yote mikubwa na miradi yote mikubwa ya Ujenzi inaendeshwa na wageni, Why?.

Leo hii waafrika wakishindwa kutibiwa Afrika wanaenda kutibiwa hukohuko, hasa viongozi, bado wasomi wetu bila kwenda kupata Elimu nje ya Afrika, bado anaonekana hajasoma vizuri, machine na mitambo yote inatoka nje.

Mkuu tuache kujitutumua na kujipiga kifua, kwasasa Afrika bado sana, lazima tuweke juhudi za makusudi tuweze kujitegemea ktk technology na kujisimamia, lakini kwasasa tusijidanganye.
Unajichosha Bure,Huwa nasema mara zote kwamba Watu wenye Itikadi za Kijamaa ni wapuuzi na hivyo kabisa..

Hao wajinga walijaza wanajeshi bandarini,Tiss wa kuzidi ila mwisho wa siku upuuzi ulikuwa pale pale na hakuna Ufanisi wowote wa maana ulitokea..

Hapo bandarini huwezi pata kazi on merit ila connection na kazi za connection unajua madhara yake kwenye performance..
 
Kusema ukweli kwa muda mrefu nimekuwa nikiwaza juu ya serikali kushirikiana na private sector kwenye ku-run/ku-manage baadhi ya mashirika na taasisi za umma ili kuleta ufanisi in a win-win situation. Kwa hiyo kwangu mimi Kuwapa DP-World kumanage shughuli za bandari zetu (as long as they have a good proved record in the sector) sio jambo baya wala jipya ila tatizo la sisi watz na waafrika kwa ujumla ni mikataba ya hovyo na ya kinyonyaji ambayo nchi zetu zinaingia na hawa private sector tena wengine ni incompetent kabisa/wababaishaji.

Natamani kuona mashirika ya umma kama DART, TRC, Tanesco, na mengineyo yakiingia ubia (partnership) na private sector kwenye ku-run/ku-manage the business part ya hayo mashirika in a win-win situation. Serikali ilishaacha kufanya biashara na pale serikali inapolazimisha kufanya biashara hzi taasisi au mashirika mara nyingi kama si zote huwa ni hasara tu au faida kiduchu sana. PPP ikiwekewa utaratibu mzuri mi naona ndio njia pekee ya mashirika na taasisi zetu zinazofanya biashara zinaweza kukua na kuchangia vizuri kwenye pato la taifa otherwise kila siku tuatakuawa tunaona madudu tu kwenye riport ya CAG.
Mengi sana yanatakiwa kufanyiwa ubinafsishaji ,tunapoteza hela kulipa watu wapuuzi huko kwenye mashirika yasiyojitambua..

Kwanza Mimi natamani mengi Yao yafutiliwe mbali na Samia ndio anaweza hii kazi ya kushughulika na mambo magumu..

Mkapa alijitahidi kiasi kuyabinafsisha licha makelele ya wapuuzi ooh anauza Nchi na blaa blaa za kijinga kama hizo..

Mwisho wa Siku historia ilimtaja kama shujaa wa Uchumi na Mageuzi.
 
Wawekewe mazingira mazuri ya uwekezaji itakuwa labda kuna shida somewhere kwenye government
Waongoze kasi za viwanda sema serikali inazingua sana

Viwanda viwe vingi mbalimbali wasiishie hicho cha pombe ili wakulima wauze kwa sana malighafi ndani na nje hapo tunapunguza ku import . Hizi nido, blueband , nakadhalika .

Hapo inakuwa game over
Umeme unazingua.bei ya umeme ni kubwa sana kwa Nchi kama yetu. China unapata unit moja kwa US cents 8.1 Ambayo ni kama shilingi 190 za kitanzania. Lakini hapa kwetu unauziwa unit shilingi 350 ukiongeza na matozo basi unalipia unit sh 370.

kwa bei hii ya umeme,huwezi piga hatua kubwa kiviwanda. Viwanda pekee vinavyoweza shamiri bongo ni light industries kama utengenezaji magodoro,vinywaji,sabuni,n.k, viwanda ambavyo havina matumizi makubwa ya umeme.

Lakini ili uibadilishe TZ kiviwanda na uchumi,inabidi ujenge viwanda vyenye kutumia malighafi zetu za ndani.Na hapa ndio suala la umeme rahisi linapohitajika. Tukiweza kua na umeme huo rahisi, viwanda kama vya chuma vitashamiri sana,na tunacho chuma ghafi. Viwanda vya bid has za shaba, viwanda vya ceramic, vioo, vitakuwa sana kwakua madini kama feldspar,dolomites,n.k. tunayo ya kutosha. Hata viwanda vya cement vitaongezeka kwakua tuna gypsum na chokaa ya kutosha.Hayo ndio mapinduzi.

Lakin imekua aibu tunaagiza hadi majembe toka China kisa tuu umeme wetu ni ghali na wakati tumebarikiwa mito mingi ya kuzalisha umeme bei nafuu. Cha ajabu, eti wanataka kujenga umeme wa jua na wind power ambao ni ghali sana

Serikali kama wameshindwa kushusha gharama za umeme Nchi nzima pengine kwasababu ya maslahi ya viongozi wachache,basi waache baadhi ya mikoa ijengewe umeme maalum kwaajili ya viwanda.Mfano, mkoa kama morogoro wangepewa umeme wa maji kwa bei nafuu ili viwanda vyenye mahitaji makubwa ya umeme vingejengwa huko. Mikoa ya ruvuma,njombe, rukwa,na mbeya nao wangejengewa vinu cha umeme wa makaa kila mkoa kwa kua wana makaa mengi ya mawe,Na viwanda vyenye kuhitaji umeme mwingi vingejengwa huko kwani malighafi za chuma,gypsum, shaba, zinc ziko Tele huko.
 
Back
Top Bottom