7seven
JF-Expert Member
- Mar 27, 2022
- 3,744
- 8,066
Waganda wameona fursa baada ya ujenzi wa SGR kutokea Dar to Mwanza kwasababu mizigo yao itakuwa inafika mapema inaingia kwenye meli siku hiyo hiyo na kusafirishwa hadi Port Bell Uganda.[emoji106][emoji106]
Kutokea Dar treni itatumia masaa manane 8hrs kufika Mwanza. Kwahiyo utaona hapo wanakuwa wameokoa muda wa mizigo yao kukaa barabarani ikisafirishwa ikiwa kama wangetumia malori.
Kwenye biashara au kazi ukishaweza kuokoa muda ambao ulikuwa unapoteza bure unakuwa umeweza kukwepa hasara au unaongeza faida kwa kuutumia huo huo muda kufanya hiyo kazi au kazi nyingine zaidi ya hiyo.
Kwahiyo reli haitaleta hasara bali faida kwa uchumi wa nchi na kwa Watanzania kwa ujumla.