Vyuo vya Kagera tu ndio havikukidhi vigezo tu. Hicho chuo cha Askofu vipi mbona hakikudhi vigezo hata kabla hakijajengwa?
Walipimaje vigezo kwamba haviwezi kukidhi, kwingine.Kwani wananchi ndio wanatoa ithibati? Majengo mangapi sasa hivi ni makazi ya popo ambayo yalipigwa stop baada ya kujengwa ili yawe vyuo?
Kama ni vigezo kwanini wanaacha mtu anatafuta pesa, anapewa kibali cha ujenzi, akikaribia kumaliza anaambiwa haruhusiwi kuendelea na ujenzi. Ingekuwa ni wewe utakuwa na jeuri ya kuitunishia serikali misuli.
Tujadili kama watu wazima na siyo wapambe wa serikali kwa kuwa tunalipwa au tumepewa ahadi fulani fulani hivi hadi tunajitoa ufahamu na kupoteza lengo.