🤣🤣🤣 Hizi andika za wajua kiingereza humu ndani ni ujinga tu, kwa mfano we bwana
Walker255 nimeona ukiongea kwamba tubadili mfumo wa elimu, lakini sijaona ukipendekeza ni kwenye eneo gani tubadili mfumo wetu wa elimu ambao labda utaonekana kuwa bora kama mfumo wa elimu wa kenya (inavyosemekana Ina mfumo mzuri wa elimu) 🤣🤣 au nyie ndio wale wa English iwe language of instructions kuanzia elimu ya msingi.? Leta hoja, usilalame tu ..
Specificity ya tatizo sio kazi yangu, ni kazi ya serikali kuchunguza. Still, I’ll break it down for you. Mfumo wa elimu wa Tanzania Una changamoto nyingi, na tafadhali, sikuwahi kulinganisha mfumo wa elimu wa Tanzania na ule wa Kenya. Usiweke maneno kunywani mwangu!
Mahitaji ya kielimu ya nchi moja ni tofauti na nchi nyingine.
Labda tuanze na elimu ya msingi. Lugha ya ufundishaji kwenye shule zote za msingi zinazomilikiwa na serikali ni Kiswahili. Na lengo kuu ni kuwasaidia watoto wajifunze lugha ya asili ya nchi yao toka wakiwa na umri mdogo.
Lakini wakifika sekondari, language of instruction imabadilika. All of a sudden, wanatakiwa wazungumze kiingereza, bila kuwa na foundation ya kutosha ya lugha hiyo. Unakuta kuna campaign za “Speak English” na wanafunzi unakuta wanachapwa viboko wakiongea Kiswahili. Hii hasira uliyonayo juu ya watu wanazungumza kiingereza kama mimi imetokana na ukatili uliofanyiwa shuleni.
Transition ya kutoka kusoma kila soma Kwa Kiswahili kwenda Kiingereza inamfanya mtoto ashindwe ku-adapt haraka. Unakuta masomo yanakuwa magumu Kwasababu ya language barrier. Wale wanaoonyesha bidii unakuta wanasoma kwa kukariri, Kwa hiyo passion ya masomo unakuta haipo.
Effects za madiliko ya lugha zinaenda mpaka wanafunzi wanapofika chuo. Pia hao wanafunzi waliopitia mfumo huu wanaenda kusoma ualimu na wanarudi mashuleni kufundisha wakiwa na mapungufu makubwa ya kilugha.
Unfortunately, Kiswahili si lugha ya kitaaluma, especially taaluma ya juu. Tumeweza kutengeneza curricula za Kiswahili kuwafundisha watoto wa shule za msingi lakini hatukufanikiwa kufanya hivyo hivyo kwenye ngazi za juu zaidi za elimu. Inabidi tuchague moja. Kiswahili ama Kiingereza kuwa lugha ya elimu yetu. Lugha ni fursa. Wafaransa, wakorea, Wachina, Warusi nk. Wanaendesha uchumi wa nchi zao Kwa lugha zao wenyewe. Lakini mfumo tulionao sisi hausaidii.