Sio kwamba I am the wisest Kenyan hapa. Kuna Wakenya na Watanzania wengi hapa ambao ni werevu kunishinda. Mimi sio mwerevu sana. Mimi ni mtu wa kawaida tu kama wewe. Tatizo ni kwamba anataka kunipimia hewa. Yeye ndiye anataka kuniambia nitasema nini hapa na sitasema nini? Eti mimi nimekuwa pathetic kwa sababu hapendi jinsi ninavyo-interact na Watanzania humu. Approach yake ni ya kimabavu. Approach yake ni ya kutusi watu, kudharau watu, kudhalilisha watu. Mimi sina hio roho mbaya. Mimi huwa nashindwa kubeba chuki moyoni kama yeye anavyobeba chuki moyoni.
Yeye anawachukia Watanzania kiukweli. Hajui hapa tupo battle, yaani tupo hapa kujifurahisha. Mtu unapiga kazi, ukipata dakika tano unaingia JF kidogo kisha unaendelea na kazi yako. Yeye hanilipii chakula wala hanilipii bill ya umeme au maji sasa ataniambiaje cha kusema huku? Eti hapendi jinsi ninavyotangamana na Watanzania, yaani anataka niwe natukana na kudharau Watanzania ili kuonyesha kwamba mimi ni Mkenya?
Mimi nipo hapa kivyangu na wala sipo hapa kufurahisha mtu yeyote. Kama hapendi basi too bad for him kwa sababu hakuna chochote anachoweza kunifanyia. Hata hanijui na anakasirishwa na mtu asiyemjua? Mtu unayekutana naye mtandaoni unamchukia ili iweje?