Hapana mkuu, kuhusu Machinga complex ni tofauti kabisa, lile lilikamilika enzi za Kikwete na ilishindikana wamachinga kuhamia pale enzi za Kikwete kutokana na mpangilio wa hovyo wa mkataba wa ujenzi ulioingiwa na halmashauri ya Ilala, Kikwete mwenyewe alishindwa.
Kiufupi ni kwamba, mkopo uliotumika na jinsi ya kulipa huo mkopo ni mzigo mkubwa kwa serikali, sio rahisi kwa machinga kulipa Kodi ya vizimba ni kubwa mno, Magufuli alipoingia madarakani pia aliona hilo tatizo Kama alivyoliona Kikwete na akakataa wamachinga kubeba uzembe uliofanywa na hamashauri ya Ilala.
Masoko yote aliyojenga Magufuli akiwa madarakani, na vituo vya mabasi, wamachinga na mama lishe wamepewa kipaumbele kikubwa Sana. Vitambulisho vya Magufuli vinampa uhuru machinga ya Kisutu kuhamia soko la Magomeni, au soko lolote bila kubughudhiwa au kulipa ada au Kodi yoyote Ile.