ingependeza zaidi unapoponda kidogo uwe unatoa na pendekezo/ushauri wa kipi kifanyike
Mapendekezo yametolewa Sana ila maccm huwa yanafanya mambo ambayo itawaletea sifa na kura kwa wajinga hata kama haiwasaidii.
Tumependekeza Sana lakini ccm haielewi kwa mfano washushe VAT hadi 12% kutoka 18% Ili tutumie zile mashine zao kwenye biashara.
Tumesema ccm ipunguze mlokongo wa mataasisi ya udhibiti imagine ukitaka kufanya biashara Halali ya let say timber supplier haitakaa upate kitu ,hapo fire,tfs,TRA,wakala wa vipimo, Halmashauri,mbrella ,leseni ya biashara na kibali cha kusafirishana .Kote huko unazungushwa unatumia mda na pesa wameshindwa kuweka window moja ya kulipia na kupunguza matozo matokeo yake kila taasisi inakomoa mfanyabiashara.
Huo ni mfano mmja tuu,nchi ya Tzn ina taasisi za udhibiti nyingi kuliko facilitors,na matokeo yake ukijifanya unafuata sheria hutoboi kwa hiyo lazima tukwepe kodi na tumalizane na maafisa Ili ku survive .
Kwenye miundombinu sasa Nako hawajengi miundombinu yenye tija kwa watu,nakupa mfano mdogo toka wameanza kujenga mastendi makuubwa yameleta tija gani? Jibu ni hakuna.
Kwa wale mnaofahamu mkoa wa Rukwa ccm walijenga barabara inatoka mjini kwenda port ya Kasanga hiyo road si tuu haina traffic bali hakuna inachozalisha,wakaacha barabarani inayotumiwa na watu wengi blonde la Rukwa na kuna uzalishaji.Miradi ya kipuuzi Kam hiyo iko mingi Sana nchi hii,Sasa serikali za watu dizaini hii si ni za wajinga tuu.