Ibambasi
JF-Expert Member
- Jul 25, 2007
- 9,277
- 4,683
Ulipotelea wapi weweHapo kitambo mitaa ya MwanaNyamala kulikuwa na mapori na wakabaji, kwa hiyo kina mama wa kizaramo walivyokuwa wakifika mitaa hiyo wakawa wanawaambia watoto wao "Mwana Nyamala" maana yake "Mtoto Nyamaza" ili wasisikiwe na maharamia.
Kijito Nyama inawezekana ina uhusiano na Mwana Nyamala, kwamba unavuka kijito ukifika upande wa pili huko "Mwana nyamala" Nyamaa == Kijito Nyamaa mwisho ikawa Kijitonyama.
Mtoni kwa Aziz Ali pamepata jina kutokana na mkazi mmoja alwatani sana marehemu Aziz Ali. Mzee huyu alifariki miaka kadhaa iliyopita kukawa na kesi kubwa sana ya urithi kati ya wanawe.