Ansbert Ngurumo (Video): Mlipata wapi kura 32,000,000 za Samia?

The Palm Beach

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2015
Posts
3,622
Reaction score
9,301

View: https://youtu.be/a3x3e1QFasQ?si=WxGatqMY68D7RZ8v
Hili ni swali la Ansbert Gurumo kupitia Youtube Channel yake (SK Media Online TV)

Na huyu hapa 👇🏻👇🏻ni mmoja wa watazamaji wake waliotoa maoni yake akijitambulusha kuwa yeye alikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura huko Shintanga, Manispaa ya Shinyanga, Kata ya Ndala, kituo cha kupigia kura ✖ akieleza kilichofanyika kwenye vituo vya kupigia kura ili kumshindisha Samia
===============================================

"....Ansbert Ngurumo mimi nilikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura katika uchaguzi huu mkoa wa Shinyanga, manispaa ya Shinyanga kata ya Ndala.

Si unajiuliza Tume ya Uchaguzi wamewatoa wapi wapiga kura 32,000,000 nchi nzima waliompa ushindi wa 98% Samia? Soma kwa makini utapata jibu

Sikiliza bwana. Mpango mzima ulikuwa hivi ndugu Ansbert Ngurumo:

Matokeo tokana na wapiga kura hewa ya kura za Rais yalishaandaliwa na kupelekwa majimboni hata kabla ya siku ya uchaguzi kwa kuwatumia wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi na wa kata kwa idadi ya kata na vituo vya kupigia kura vilivyomo kwenye maeneo yao.

Wenyewe walikuwa wanasema kila mtu alipewa target "special votes target" kwa kila jimbo, kila kata na kila kituo chakupigia kura" bila kujali wapiga kura wangekuja kupiga kura ama la. Wakati wa kujumuisha matokeo ya kura kuanzia ngazi ya kata na jimboni, sisi wasimamizi wa vituo vya kupigia kura hutukutakiwa kabisa kwenda ktk kituo cha kujumuisha matokeo ya kura na matokeo halisi ya waliopiga kura isipokuwa yale ya target ya NEC kwa kila ngazi; kata (diwani), jimbo (mbunge) na Rais..!!!.

Jimbo lilishusha matokeo hayo kwa kila kata na wasimamizi wa kata wakayapeleka kwenye kila kituo cha kupigia kura na kutulazimisha wasimamizi kutangaza hayo.

Kwa mfano, mimi kwenye kituo changu ✖ (kwa usalama wangu sitakitaja kwa sasa) nilikuwa na wapiga kura 439.

Siku hiyo ya uchaguzi tarehe 29/10 mpaka kufikia saa 10:00 jioni muda wa kufunga vituo vya kupigia kura, ni wapiga kura 32 tu kati ya 439 waliokuwa wamekuja kupiga kura.

Kabla hata ya kuanza kuhesabu hizo 32 kisha tutangaze matokeo, ikaletwa fomu za matokeo yaliyokwisha kujazwa tayari kwa diwani, mbunge na Rais na kutulazimisha wasimamizi wa kituo kugonga muhuri na kusaini na kisha kuyabandika kana kwamba ndiyo matokeo halisi ya kituo. Ilifanyika hivyo kwenye vituo vyote. Matokeo hayo ya kubumba kwa Urais, yalionesha kuwa kura zilizopigwa ni 411 na Samia ana kura 367 kwenye kituo chetu🤔🤔 na 44 waligawiwa wagombea wengine, mwenye kupata 2, 1, 3 na 0 walipewa. Hatujui hizo kura zilipigiwa wapi maana sisi ndio tuliokuwa wasimamizi wa kituo.

Nilipiga picha fomu hizo zote za matokea ya kubumba na za matokea halisi (wale 32 kati ya 439 waliopiga kura kwenye kituo chetu) na ninayo kwenye simu yangu. Siku yakihitajika na mazingira kuruhusu kuyatoa kama ushahidi, nitakuja kuyatoa. Katika zile kura za kweli, kura halisi baada ya kuzihesabu, Samia wa CCM alipata kura 08 tu na 24 ziligawanwa na wagombea wengine.

Kwa hiyo unaweza kuona kuwa,hata waliokuja kupiga kura wengi walimkataa kabisa huyu mama na bila shaka ni CCM wenzake. Hiyo ndiyo mbinu na mkakati waliotumia wahuni hawa na kusema nchi nzima wapiga kura 32,000,000 ndio walipiga kura. Ndugu Ngurumo, huo ulikuwa uchafu na uhuni mtupu na kamwe haukuwa uchaguzi. Inaumiza na kuudhi sana.

Na sielewi wao wenyewe (Emmanuel Nchimbi na Samia Suluhu Hassan) wanajisikiaje kuwa hapo walipo kwa matokeo ya uchaguzi wa uongo na udanganyifu huku wakiwa na damu za watoto, kinamama na kinababa wasio na hatia waliowaua kuhalalisha upuuzi wao. Hawa hakika, wanatembea na kuishi katikati gadhabu ya hukumu ya Mungu na ni lazima iwamalize hapa hapa duniani!..."
 
Na safari hii wasimamizi wa vituo msipoungama, damu za watanzani zitawalilia. Dhuluma ni mbaya. Hakuna kituo kilichozidi wapiga kura 50, kama vipo basi havifiki hata 100 kati ya elfu 99+
 
Naisikitikia sana nchi yangu Tanzania. Maana huko mbeleni hatima yake itakuwa mbaya kwani CCM imezidi kuendekeza ulafi na uroho wa madaraka.
Kwa dhuluma iliyofanyika tarehe 29/10 huwa naona aibu viongozi wa chama wanavyojinasibu kuwa walishinda kwa 98%.
Kuna haja viongozi wa dini zote kukemea hizi dhulma.
 

View: https://youtu.be/a3x3e1QFasQ?si=WxGatqMY68D7RZ8v
Hili ni swali la Ansbert Gurumo kupitia Youtube Channel yake (SK Media Online TV)

Na huyu hapa 👇🏻👇🏻ni mmoja wa watazamaji wake waliotoa maoni yake akijitambulusha kuwa yeye alikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura huko Shintanga, Manispaa ya Shinyanga, Kata ya Ndala, kituo cha kupigia kura ✖ akieleza kilichofanyika kwenye vituo vya kupigia kura ili kumshindisha Samia
===============================================

"....Ansbert Ngurumo mimi nilikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura katika uchaguzi huu mkoa wa Shinyanga, manispaa ya Shinyanga kata ya Ndala.

Si unajiuliza Tume ya Uchaguzi wamewatoa wapi wapiga kura 32,000,000 nchi nzima waliompa ushindi wa 98% Samia? Soma kwa makini utapata jibu

Sikiliza bwana. Mpango mzima ulikuwa hivi ndugu Ansbert Ngurumo:

Matokeo tokana na wapiga kura hewa ya kura za Rais yalishaandaliwa na kupelekwa majimboni hata kabla ya siku ya uchaguzi kwa kuwatumia wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi na wa kata kwa idadi ya kata na vituo vya kupigia kura vilivyomo kwenye maeneo yao.

Wenyewe walikuwa wanasema kila mtu alipewa target "special votes target" kwa kila jimbo, kila kata na kila kituo chakupigia kura" bila kujali wapiga kura wangekuja kupiga kura ama la. Wakati wa kujumuisha matokeo ya kura kuanzia ngazi ya kata na jimboni, sisi wasimamizi wa vituo vya kupigia kura hutukutakiwa kabisa kwenda ktk kituo cha kujumuisha matokeo ya kura na matokeo halisi ya waliopiga kura isipokuwa yale ya target ya NEC kwa kila ngazi; kata (diwani), jimbo (mbunge) na Rais..!!!.

Jimbo lilishusha matokeo hayo kwa kila kata na wasimamizi wa kata wakayapeleka kwenye kila kituo cha kupigia kura na kutulazimisha wasimamizi kutangaza hayo.

Kwa mfano, mimi kwenye kituo changu ✖ (kwa usalama wangu sitakitaja kwa sasa) nilikuwa na wapiga kura 439.

Siku hiyo ya uchaguzi tarehe 29/10 mpaka kufikia saa 10:00 jioni muda wa kufunga vituo vya kupigia kura, ni wapiga kura 32 tu kati ya 439 waliokuwa wamekuja kupiga kura.

Kabla hata ya kuanza kuhesabu hizo 32 kisha tutangaze matokeo, ikaletwa fomu za matokeo yaliyokwisha kujazwa tayari kwa diwani, mbunge na Rais na kutulazimisha wasimamizi wa kituo kugonga muhuri na kusaini na kisha kuyabandika kana kwamba ndiyo matokeo halisi ya kituo. Ilifanyika hivyo kwenye vituo vyote. Matokeo hayo ya kubumba kwa Urais, yalionesha kuwa kura zilizopigwa ni 411 na Samia ana kura 367 kwenye kituo chetu🤔🤔 na 44 waligawiwa wagombea wengine, mwenye kupata 2, 1, 3 na 0 walipewa. Hatujui hizo kura zilipigiwa wapi maana sisi ndio tuliokuwa wasimamizi wa kituo.

Nilipiga picha fomu hizo zote za matokea ya kubumba na za matokea halisi (wale 32 kati ya 439 waliopiga kura kwenye kituo chetu) na ninayo kwenye simu yangu. Siku yakihitajika na mazingira kuruhusu kuyatoa kama ushahidi, nitakuja kuyatoa. Katika zile kura za kweli, kura halisi baada ya kuzihesabu, Samia wa CCM alipata kura 08 tu na 24 ziligawanwa na wagombea wengine.

Kwa hiyo unaweza kuona kuwa,hata waliokuja kupiga kura wengi walimkataa kabisa huyu mama na bila shaka ni CCM wenzake. Hiyo ndiyo mbinu na mkakati waliotumia wahuni hawa na kusema nchi nzima wapiga kura 32,000,000 ndio walipiga kura. Ndugu Ngurumo, huo ulikuwa uchafu na uhuni mtupu na kamwe haukuwa uchaguzi. Inaumiza na kuudhi sana.

Na sielewi wao wenyewe (Emmanuel Nchimbi na Samia Suluhu Hassan) wanajisikiaje kuwa hapo walipo kwa matokeo ya uchaguzi wa uongo na udanganyifu huku wakiwa na damu za watoto, kinamama na kinababa wasio na hatia waliowaua kuhalalisha upuuzi wao. Hawa hakika, wanatembea na kuishi katikati gadhabu ya hukumu ya Mungu na ni lazima iwamalize hapa hapa duniani!..."

My only concern ni usalama wa huyo msimamizi. Kama hizi details zote alizotoa ni sahihi yuko hatarini, ushauri wangu ahamishe hizo picha na ushahidi wote kutoka kwenye simu yake ikiwemo na kulog out kutoka kwenye account aliyotuma nayo haya maelezo yake kwenye YouTube Channel ya Ngurumo.
 
Wife alisimamia kituo kimoja huko arusha,mpaka jioni hakukua na mpiga kura hata mmoja.
Kiongozi wao akawaambia wafanye wanavyojua ila kituo chao kinatakiwa kuwa na kura 300 za samia.
Walichofanya ni wao wenyewe kujaza kura feki za ndio kwa Samia.
 
My only concern ni usalama wa huyo msimamizi. Kama hizi details zote alizotoa ni sahihi yuko hatarini, ushauri wangu ahamishe hizo picha na ushahidi wote kutoka kwenye simu yake ikiwemo na kulog out kutoka kwenye account aliyotuma nayo haya maelezo yake kwenye YouTube Channel ya Ngurumo.
I don't think so...

Youtube accounts holders credentials/details zao ziko secured vizuri sana...

Hawana access ya kuweza kumpata..

After all, mbona ni taarifa ya kawaida sana...

Na wapende au wasipende, mazingira ya kutoa ushahidi huu yakitegenezwa na kuwa salama, basi maelfu ya wasimamizi wa vituo vya kupigia kura wako tayari kutoa ushahidi wao kuonesha kuwa matokeo hayo ni ya kupikwa, sio halisi.

Kuna sauti na video zilizorekodiwa za maofisa wa Tume ya Uchaguzi wenyewe katika maeneo mbalimbali wakitoa maelekezo kwa wasimamizi wanachotakiwa kwenda kufanya ili "kumshindisha mama yao". Zilirekodiwa bila wao kujua..

Wana ushahidi wa karatasi, picha na sauti (audio) za wasimamizi wa tume wakitoa maelekezo ya wao waliita "kumsaidia mama kushinda ushindi wa kishindo🤔🤔"
 

View: https://youtu.be/a3x3e1QFasQ?si=WxGatqMY68D7RZ8v
Hili ni swali la Ansbert Gurumo kupitia Youtube Channel yake (SK Media Online TV)

Na huyu hapa 👇🏻👇🏻ni mmoja wa watazamaji wake waliotoa maoni yake akijitambulusha kuwa yeye alikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura huko Shintanga, Manispaa ya Shinyanga, Kata ya Ndala, kituo cha kupigia kura ✖ akieleza kilichofanyika kwenye vituo vya kupigia kura ili kumshindisha Samia
===============================================

"....Ansbert Ngurumo mimi nilikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura katika uchaguzi huu mkoa wa Shinyanga, manispaa ya Shinyanga kata ya Ndala.

Si unajiuliza Tume ya Uchaguzi wamewatoa wapi wapiga kura 32,000,000 nchi nzima waliompa ushindi wa 98% Samia? Soma kwa makini utapata jibu

Sikiliza bwana. Mpango mzima ulikuwa hivi ndugu Ansbert Ngurumo:

Matokeo tokana na wapiga kura hewa ya kura za Rais yalishaandaliwa na kupelekwa majimboni hata kabla ya siku ya uchaguzi kwa kuwatumia wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi na wa kata kwa idadi ya kata na vituo vya kupigia kura vilivyomo kwenye maeneo yao.

Wenyewe walikuwa wanasema kila mtu alipewa target "special votes target" kwa kila jimbo, kila kata na kila kituo chakupigia kura" bila kujali wapiga kura wangekuja kupiga kura ama la. Wakati wa kujumuisha matokeo ya kura kuanzia ngazi ya kata na jimboni, sisi wasimamizi wa vituo vya kupigia kura hutukutakiwa kabisa kwenda ktk kituo cha kujumuisha matokeo ya kura na matokeo halisi ya waliopiga kura isipokuwa yale ya target ya NEC kwa kila ngazi; kata (diwani), jimbo (mbunge) na Rais..!!!.

Jimbo lilishusha matokeo hayo kwa kila kata na wasimamizi wa kata wakayapeleka kwenye kila kituo cha kupigia kura na kutulazimisha wasimamizi kutangaza hayo.

Kwa mfano, mimi kwenye kituo changu ✖ (kwa usalama wangu sitakitaja kwa sasa) nilikuwa na wapiga kura 439.

Siku hiyo ya uchaguzi tarehe 29/10 mpaka kufikia saa 10:00 jioni muda wa kufunga vituo vya kupigia kura, ni wapiga kura 32 tu kati ya 439 waliokuwa wamekuja kupiga kura.

Kabla hata ya kuanza kuhesabu hizo 32 kisha tutangaze matokeo, ikaletwa fomu za matokeo yaliyokwisha kujazwa tayari kwa diwani, mbunge na Rais na kutulazimisha wasimamizi wa kituo kugonga muhuri na kusaini na kisha kuyabandika kana kwamba ndiyo matokeo halisi ya kituo. Ilifanyika hivyo kwenye vituo vyote. Matokeo hayo ya kubumba kwa Urais, yalionesha kuwa kura zilizopigwa ni 411 na Samia ana kura 367 kwenye kituo chetu🤔🤔 na 44 waligawiwa wagombea wengine, mwenye kupata 2, 1, 3 na 0 walipewa. Hatujui hizo kura zilipigiwa wapi maana sisi ndio tuliokuwa wasimamizi wa kituo.

Nilipiga picha fomu hizo zote za matokea ya kubumba na za matokea halisi (wale 32 kati ya 439 waliopiga kura kwenye kituo chetu) na ninayo kwenye simu yangu. Siku yakihitajika na mazingira kuruhusu kuyatoa kama ushahidi, nitakuja kuyatoa. Katika zile kura za kweli, kura halisi baada ya kuzihesabu, Samia wa CCM alipata kura 08 tu na 24 ziligawanwa na wagombea wengine.

Kwa hiyo unaweza kuona kuwa,hata waliokuja kupiga kura wengi walimkataa kabisa huyu mama na bila shaka ni CCM wenzake. Hiyo ndiyo mbinu na mkakati waliotumia wahuni hawa na kusema nchi nzima wapiga kura 32,000,000 ndio walipiga kura. Ndugu Ngurumo, huo ulikuwa uchafu na uhuni mtupu na kamwe haukuwa uchaguzi. Inaumiza na kuudhi sana.

Na sielewi wao wenyewe (Emmanuel Nchimbi na Samia Suluhu Hassan) wanajisikiaje kuwa hapo walipo kwa matokeo ya uchaguzi wa uongo na udanganyifu huku wakiwa na damu za watoto, kinamama na kinababa wasio na hatia waliowaua kuhalalisha upuuzi wao. Hawa hakika, wanatembea na kuishi katikati gadhabu ya hukumu ya Mungu na ni lazima iwamalize hapa hapa duniani!..."

Duh Hadi tumbo limeunguruma Kwa dhulumu inayofanyika kwenye nchi yangu

Hii serikali itawafundishaje watoto wetu uadilifu
 
Na safari hii wasimamizi wa vituo msipoungama, damu za watanzani zitawalilia. Dhuluma ni mbaya. Hakuna kituo kilichozidi wapiga kura 50, kama vipo basi havifiki hata 100 kati ya laki 9+
Uko sahihi kaka,mimi nimeshuhudia kwa macho yangu,sisi wengine tulikataa ila wasimamizi wakuu wa vituo walishapangwa.
Nilipokua kua mimi hakuna waliozidi 70 waliopiga kura,yaani kile kitabu kina karatasi 50,wengi hawakumaliza kitabu wengine hawakufika hata nusu,walimu,walimu,walimu na watendaji wa kata ndio maana tunadharaulika hii nchi kwa kubeba laana za dhulma.
 
Uko sahihi kaka,mimi nimeshuhudia kwa macho yangu,sisi wengine tulikataa ila wasimamizi wakuu wa vituo walishapangwa.
Nilipokua kua mimi hakuna waliozidi 70 waliopiga kura,yaani kile kitabu kina karatasi 50,wengi hawakumaliza kitabu wengine hawakufika hata nusu,walimu,walimu,walimu na watendaji wa kata ndio maana tunadharaulika hii nchi kwa kubeba laana za dhulma.
Inasikitisha sana!
 
Na safari hii wasimamizi wa vituo msipoungama, damu za watanzani zitawalilia. Dhuluma ni mbaya. Hakuna kituo kilichozidi wapiga kura 50, kama vipo basi havifiki hata 100 kati ya laki 9+
Nimeshuhudia.. Walimu ndio wasimamizi wa kila Uchaguzi mkuu, waulizwe vizuri wataeleza kila kitu, uzuri walimu sio wachoyo wa kufundisha na Walimu wana Siri nyingi za chaguzi nyingi tena Siri za huu uchaguzi wamezihifadhi kwa muda tu waliodhani ni Siri wanajidanganya zitawekwa hadharani zote
 

View: https://youtu.be/a3x3e1QFasQ?si=WxGatqMY68D7RZ8v
Hili ni swali la Ansbert Gurumo kupitia Youtube Channel yake (SK Media Online TV)

Na huyu hapa 👇🏻👇🏻ni mmoja wa watazamaji wake waliotoa maoni yake akijitambulusha kuwa yeye alikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura huko Shintanga, Manispaa ya Shinyanga, Kata ya Ndala, kituo cha kupigia kura ✖ akieleza kilichofanyika kwenye vituo vya kupigia kura ili kumshindisha Samia
===============================================

"....Ansbert Ngurumo mimi nilikuwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura katika uchaguzi huu mkoa wa Shinyanga, manispaa ya Shinyanga kata ya Ndala.

Si unajiuliza Tume ya Uchaguzi wamewatoa wapi wapiga kura 32,000,000 nchi nzima waliompa ushindi wa 98% Samia? Soma kwa makini utapata jibu

Sikiliza bwana. Mpango mzima ulikuwa hivi ndugu Ansbert Ngurumo:

Matokeo tokana na wapiga kura hewa ya kura za Rais yalishaandaliwa na kupelekwa majimboni hata kabla ya siku ya uchaguzi kwa kuwatumia wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi na wa kata kwa idadi ya kata na vituo vya kupigia kura vilivyomo kwenye maeneo yao.

Wenyewe walikuwa wanasema kila mtu alipewa target "special votes target" kwa kila jimbo, kila kata na kila kituo chakupigia kura" bila kujali wapiga kura wangekuja kupiga kura ama la. Wakati wa kujumuisha matokeo ya kura kuanzia ngazi ya kata na jimboni, sisi wasimamizi wa vituo vya kupigia kura hutukutakiwa kabisa kwenda ktk kituo cha kujumuisha matokeo ya kura na matokeo halisi ya waliopiga kura isipokuwa yale ya target ya NEC kwa kila ngazi; kata (diwani), jimbo (mbunge) na Rais..!!!.

Jimbo lilishusha matokeo hayo kwa kila kata na wasimamizi wa kata wakayapeleka kwenye kila kituo cha kupigia kura na kutulazimisha wasimamizi kutangaza hayo.

Kwa mfano, mimi kwenye kituo changu ✖ (kwa usalama wangu sitakitaja kwa sasa) nilikuwa na wapiga kura 439.

Siku hiyo ya uchaguzi tarehe 29/10 mpaka kufikia saa 10:00 jioni muda wa kufunga vituo vya kupigia kura, ni wapiga kura 32 tu kati ya 439 waliokuwa wamekuja kupiga kura.

Kabla hata ya kuanza kuhesabu hizo 32 kisha tutangaze matokeo, ikaletwa fomu za matokeo yaliyokwisha kujazwa tayari kwa diwani, mbunge na Rais na kutulazimisha wasimamizi wa kituo kugonga muhuri na kusaini na kisha kuyabandika kana kwamba ndiyo matokeo halisi ya kituo. Ilifanyika hivyo kwenye vituo vyote. Matokeo hayo ya kubumba kwa Urais, yalionesha kuwa kura zilizopigwa ni 411 na Samia ana kura 367 kwenye kituo chetu🤔🤔 na 44 waligawiwa wagombea wengine, mwenye kupata 2, 1, 3 na 0 walipewa. Hatujui hizo kura zilipigiwa wapi maana sisi ndio tuliokuwa wasimamizi wa kituo.

Nilipiga picha fomu hizo zote za matokea ya kubumba na za matokea halisi (wale 32 kati ya 439 waliopiga kura kwenye kituo chetu) na ninayo kwenye simu yangu. Siku yakihitajika na mazingira kuruhusu kuyatoa kama ushahidi, nitakuja kuyatoa. Katika zile kura za kweli, kura halisi baada ya kuzihesabu, Samia wa CCM alipata kura 08 tu na 24 ziligawanwa na wagombea wengine.

Kwa hiyo unaweza kuona kuwa,hata waliokuja kupiga kura wengi walimkataa kabisa huyu mama na bila shaka ni CCM wenzake. Hiyo ndiyo mbinu na mkakati waliotumia wahuni hawa na kusema nchi nzima wapiga kura 32,000,000 ndio walipiga kura. Ndugu Ngurumo, huo ulikuwa uchafu na uhuni mtupu na kamwe haukuwa uchaguzi. Inaumiza na kuudhi sana.

Na sielewi wao wenyewe (Emmanuel Nchimbi na Samia Suluhu Hassan) wanajisikiaje kuwa hapo walipo kwa matokeo ya uchaguzi wa uongo na udanganyifu huku wakiwa na damu za watoto, kinamama na kinababa wasio na hatia waliowaua kuhalalisha upuuzi wao. Hawa hakika, wanatembea na kuishi katikati gadhabu ya hukumu ya Mungu na ni lazima iwamalize hapa hapa duniani!..."

Duuh, hii hatari kweli!!

Hawa waliopanga kuendelea na uchaguzi kwa kuiba kura ndio hasa wahaini na wahalifu wanaopaswa kupambana na mkono wa sheria.

Si wengine na Samia na genge lake la kihuni!
 
Na serikali isiyoheshimu kura ya Mwananchi haiwezi kuheshimu rasilimali za taifa. Kile kiduchu tulichokuwa tumebaki nacho kitataifishwa/kuuzwa bila kuzingatia maslahi ya taifa. 🙆
 
Uko sahihi kaka,mimi nimeshuhudia kwa macho yangu,sisi wengine tulikataa ila wasimamizi wakuu wa vituo walishapangwa.
Nilipokua kua mimi hakuna waliozidi 70 waliopiga kura,yaani kile kitabu kina karatasi 50,wengi hawakumaliza kitabu wengine hawakufika hata nusu,walimu,walimu,walimu na watendaji wa kata ndio maana tunadharaulika hii nchi kwa kubeba laana za dhulma.
Inasikitisha sana..

Kama wanapanga matokeo kuna umuhimu gani wa kutumia mabilioni ya walipa Kodi kuendesha ubatili?.... kwanini raia wanyimwe haki ya kuchagua viongozi wanaowataka mpaka wachache tu ndio wapange nani mshindi?..

Dhambi hii itaendelea kulitafuna hili taifa.
 
Comrade!
Duniani kite Huwa Kuna uchakachuzi wa matokeo Ili mlengwa ndio ashike dola Kwa malengo maalum!

Huku kwetu kufoji kulizidi kiwango Cha fojari yenyewe!

Ingekua 55% vs 45 inakua reasonable fojery kuliko hiii iliyofnyika yaani upinzani 45 na ccm 55 Ili iu balance mambo ya uchaguzi na demokrasia!

Ni rasmi washauri na majasusi wamemshauri vibaya madam president ili uchaguzi usiwe na mantiki kiuhalisia!

Fodging ya hivi ni zaidi ya kawaida kabisa na isiyo wezekana kisayansi,kimantinki na kiuhalisia!

Tumeharibu na kumharibia madam president Kwa hicho kilichotokea!!
 
Kuna msimamizi mmoja wa INEC wa wilaya anasema tarehe 30/10/2025 alikuwa anahangaika kuwatafuta wasimamizi wa vituo ili wajumlishe kura za wabunge na Rais.
Akaambiwa na mtu Mbona matokeo ya Jimbo lake Tayari yameshatangazwa na tume ya uchaguzi?
Kwahiyo hawakuendelea tena na zoezi la kuhesabu kura. Amebaki anashangaa mpaka leo🤣🤣🤣
 
Kuna msimamizi mmoja wa INEC wa wilaya anasema tarehe 30/10/2025 alikuwa anahangaika kuwatafuta wasimamizi wa vituo ili wajumlishe kura za wabunge na Rais.
Akaambiwa na mtu Mbona matokeo ya Jimbo lake Tayari yameshatangazwa na tume ya uchaguzi?
Kwahiyo hawakuendelea tena na zoezi la kuhesabu kura. Amebaki anashangaa mpaka leo🤣🤣🤣
Haa haa🤔🤔

Jaji Mwambegele na Ramadhani Kailima wa inayoitwa INEC ndio hasa wahaini wa kwanza...

Hawa ndio chanzo cha vurugu na mauaji yaliyotokea...

Baadae wanafuata wasemaji fulani fulani wa Jeshi la Polisi waliokuwa na kauli za kuhamasisha mauaji kama: Tutavunja miguu, kama hujui kufa Andamans trh 29/10 nk

Hawa ni kama Jumanne Muliro, ZCO Faustine Mafwele, Awadh, MKUU wa mkoa wa DSM Albert Chalamila na wengine wengi tu
 
Back
Top Bottom