Abdulrahman Kinana: Chaguzi za 2019 na 2020 zilileta hofu, Mwaka 2024 na 2025 zitakuwa za Huru na Haki

View attachment 2925116

"Uchaguzi mwaka huu na mwaka ujao utakuwa wa huru na wa haki, wakati nazungumza hivi nina hakika wapo ambao wana mashaka na kauli hii, na hao wenye mashaka wanazo sababu, na sababu zao zinatokana na 2019 na 2020 huo ndio ukweli"

"Sheria tuliyokuwa nayo ya uchaguzi ambayo ilitupeleka kwenye uchaguzi wa 2015 iliwezesha wanachama kutoka upinzani 117 kuingia bungeni, sheria hiyo hiyo iliwezesha karibu asilimia 40 ya madiwani kuingia kwenye nafasi za halmashauri, tulipokuja 2020... msema kweli lazima tuseme kweli"

"Hofu ya watanzania hofu ya wenzangu vyama vya siasa, asasi za kiraia, baadhi ya viongozi wa dini, msingi wa hofu yao ni yale yaliyotokea 2019/2020. Niwahakikishie Rais Samia Suluhu Hassan ameamua uchaguzi mwaka huu na mwakani mtaachwa wapiga uamuzi wao utoe tafsiri ya uchaguzi" - Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.

Chanzo: EATV
Aache uongo....
 
Yaani mimi kupiga kura tena kwa Tanzania hii sijui ...

Watu wengi wamekata tamaa kusimama kwenye foleni muda mrefu huku mnasikia viongozi wakubwa wakisema... 'Mpige kura msipige CCM ndiye mshindi'

Kinana bado sijaamini kauli yake
Jamaa lengo lao tukate tamaa, mimi big no nitapiga ili wajue kuwa sikuwachagua hata kidogo
 

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana amesema Rais Samia Suluhu Hassan amekusudia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kuwa huru na haki.

Kinana amesema hayo katika Mkutano Mkuu wa ACT- Wazalendo unaofanyika leo Machi 5, 2024 kwenye ukumbi wa mikutano wa Mlimani City.

Pia Soma:
- Rais Samia: Uchaguzi utakuwa huru na wa haki
 
Lakini si tutaiba kama kawaida, maana nilishapata hofu tusije tukapoteza majimbo
 
Kuna kamsemo ka kitoto kua mwanasiasa akikusalimia "habari ya asubuhi" basi toka nje kuhakiki kama kweli kumekucha.
Hawa jamaa ni waongo sijapata ona.

Hao mawaziri lukuki wapo tayari kupoteza nafasi zao, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya nk aisee sio rahisi kwa nchi hii.
 
Aache maneno matupu mbona amegomea Tume Huru na Katiba Mpya?
Si ndio hapo Sasa, yaani anategemea watu waamini kauli za mdomoni huku hawataki tume huru ya uchaguzi? Yaani bado anataka watu washiriki uchaguzi kisha watoe nafasi mbili tatu za hadaa kuonyesha kuwa Kuna uchaguzi huru. Wawape ACT maana hao ndio hiyo wanaamini kwenye mbeleko ya ccm.
 
Viongozi wavuta bange,ifikie hatua Bangi iharalishwe tu.
Watu wazima ovyo.
Ccm ndo adui wa maendeleo wa Nchi hii.
Akili ndogo kutaka kuongoza akili kubwa.
Kina Kasheku kwenda Dubai kusoma mkataba wa Bandari🐍.

Mpaka mda huu ilitakiwa mshtakiwe,Kwa vile wananchi wengi wa vijijini ni Majinga majinga ndo afueni yenu.
 
Sheria za Uchaguzi ndio za kubadili , hatuwezi kuingizwa kingi kwa kauli za Kinana , Mwenye Tuhuma za kuiba kura 2015 , Akiongoza ofisi ya Masaki .

Nani amesahau ?
kuzira na kususa hakutasaidia wala kubadili chochote....

ukiona hakuna haja kushiriki uchaguzu kaa kando na uwe mtulivu, acha watakaoshiriki wafanye hivyo kwa haki, uhuru na namani...

we watizame tu kwa tv...
 
View attachment 2925116

"Uchaguzi mwaka huu na mwaka ujao utakuwa wa huru na wa haki, wakati nazungumza hivi nina hakika wapo ambao wana mashaka na kauli hii, na hao wenye mashaka wanazo sababu, na sababu zao zinatokana na 2019 na 2020 huo ndio ukweli"

"Sheria tuliyokuwa nayo ya uchaguzi ambayo ilitupeleka kwenye uchaguzi wa 2015 iliwezesha wanachama kutoka upinzani 117 kuingia bungeni, sheria hiyo hiyo iliwezesha karibu asilimia 40 ya madiwani kuingia kwenye nafasi za halmashauri, tulipokuja 2020... msema kweli lazima tuseme kweli"

"Hofu ya watanzania hofu ya wenzangu vyama vya siasa, asasi za kiraia, baadhi ya viongozi wa dini, msingi wa hofu yao ni yale yaliyotokea 2019/2020. Niwahakikishie Rais Samia Suluhu Hassan ameamua uchaguzi mwaka huu na mwakani mtaachwa wapiga uamuzi wao utoe tafsiri ya uchaguzi" - Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.

Chanzo: EATV
CCM WAKIKUAMBIA KUMEKUCHA USIAMIMI TOKA KWANZA UKACHUNGULIE
MARIDHIANO HAWATAKI
KATIBA MPYA HAWATAKI
TUME HURU WAMEBADILISHA JINA TU TUME NI ILE ILE YA CCM
 
View attachment 2925116

"Uchaguzi mwaka huu na mwaka ujao utakuwa wa huru na wa haki, wakati nazungumza hivi nina hakika wapo ambao wana mashaka na kauli hii, na hao wenye mashaka wanazo sababu, na sababu zao zinatokana na 2019 na 2020 huo ndio ukweli"

"Sheria tuliyokuwa nayo ya uchaguzi ambayo ilitupeleka kwenye uchaguzi wa 2015 iliwezesha wanachama kutoka upinzani 117 kuingia bungeni, sheria hiyo hiyo iliwezesha karibu asilimia 40 ya madiwani kuingia kwenye nafasi za halmashauri, tulipokuja 2020... msema kweli lazima tuseme kweli"

"Hofu ya watanzania hofu ya wenzangu vyama vya siasa, asasi za kiraia, baadhi ya viongozi wa dini, msingi wa hofu yao ni yale yaliyotokea 2019/2020. Niwahakikishie Rais Samia Suluhu Hassan ameamua uchaguzi mwaka huu na mwakani mtaachwa wapiga uamuzi wao utoe tafsiri ya uchaguzi" - Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.

Chanzo: EATV
THIS IS NONSENSE!

Haya maelezo yalipaswa kutolewa na tume , tena tume HURU ya Uchaguzi, na waombe radhi kwa Watanzania kutokana na ukandamizwaji mkubwa wa HAKI na wizi wa kura wa kupindukia ambao haujawahi kutokea tangu mfumo wa vyama vingi kuasisiwa nchini,


Rais Samia ambaye ni mwanaCCM Pamoja na Kinana yeye kama Makamu Mwenyekiti wa chama kimojawapo cha SIASA Hana mamlaka ya kutupa au kututoa hofu maana yeye hayo mamlaka Hana Kwani naye kinandharia alipaswa kuwa muhanga wa huo ukandamizwaji, unless sasa tukubaliane kuwa CCM wao ndio wanaamua Uchaguzi uwe HURU au vinginevyo .


Hawa watu sijui wanatuonaje Watanzania, wanafikiri Sisi ni mazombi??
 
View attachment 2925116

"Uchaguzi mwaka huu na mwaka ujao utakuwa wa huru na wa haki, wakati nazungumza hivi nina hakika wapo ambao wana mashaka na kauli hii, na hao wenye mashaka wanazo sababu, na sababu zao zinatokana na 2019 na 2020 huo ndio ukweli"

"Sheria tuliyokuwa nayo ya uchaguzi ambayo ilitupeleka kwenye uchaguzi wa 2015 iliwezesha wanachama kutoka upinzani 117 kuingia bungeni, sheria hiyo hiyo iliwezesha karibu asilimia 40 ya madiwani kuingia kwenye nafasi za halmashauri, tulipokuja 2020... msema kweli lazima tuseme kweli"

"Hofu ya watanzania hofu ya wenzangu vyama vya siasa, asasi za kiraia, baadhi ya viongozi wa dini, msingi wa hofu yao ni yale yaliyotokea 2019/2020. Niwahakikishie Rais Samia Suluhu Hassan ameamua uchaguzi mwaka huu na mwakani mtaachwa wapiga uamuzi wao utoe tafsiri ya uchaguzi" - Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.

Chanzo: EATV
Makamu Mwenyekiti wa CCM yangu anakiri tulibaka uchaguzi 2019/2020.

Jasiri haachi asili
 
View attachment 2925116

"Uchaguzi mwaka huu na mwaka ujao utakuwa wa huru na wa haki, wakati nazungumza hivi nina hakika wapo ambao wana mashaka na kauli hii, na hao wenye mashaka wanazo sababu, na sababu zao zinatokana na 2019 na 2020 huo ndio ukweli"

"Sheria tuliyokuwa nayo ya uchaguzi ambayo ilitupeleka kwenye uchaguzi wa 2015 iliwezesha wanachama kutoka upinzani 117 kuingia bungeni, sheria hiyo hiyo iliwezesha karibu asilimia 40 ya madiwani kuingia kwenye nafasi za halmashauri, tulipokuja 2020... msema kweli lazima tuseme kweli"

"Hofu ya watanzania hofu ya wenzangu vyama vya siasa, asasi za kiraia, baadhi ya viongozi wa dini, msingi wa hofu yao ni yale yaliyotokea 2019/2020. Niwahakikishie Rais Samia Suluhu Hassan ameamua uchaguzi mwaka huu na mwakani mtaachwa wapiga uamuzi wao utoe tafsiri ya uchaguzi" - Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa.

Chanzo: EATV
Mheshimiwa askari Kinana mimi sina shida na kauli yako huo ni wajibu wala haitaki shukurani.Sisi tunataka iwepo sheria ya kuwepo uchaguzi ulio huru na haki bila mkono wa mtu kutumia cheo au wadhifa kufanya kinyume.Pia tumeshuhudia mtu wa kawaida sana anaapishwa kulinda na kutetea katiba lakini anaenda kinyume,ndio maana tunataka kuondoa Mungu watu anzia kwenye chama chako ndio mvunjaji mkuu wa katiba kwa kiwango kikubwa.Lakini kama mna mapungufu ya upeo jaribu AI kama msaada.
 
Kinana huwezi kuzungumzia ukosefu wa umeme kwenye viwanda, wewe ni uchaguzi tu? .kwa hiyo uchaguzi wa 2015 ulikuwa wa huru na haki mno?
Lowasa hakuibiwa kura?
Ukiambiwa CCM wanaiba kura unakomaza fuvu kisa buku 7, aliyeongea ukweli huu ni KM wa CCM, bisha tena.
 
Back
Top Bottom