umeme

  1. Mtu Asiyejulikana

    JamiiForums Tanzania TANESCO wameanza kutuandaa Kisaikolojia. Unakuja Mgao wa Umeme siku zijazo na Watu wanaanza kuingiza Nchini Majenereta

    Huu ni mwanzo... Tuanze kujiandaa na yale yajayo siku za usoni. Maji yameanza kupungua tena kwenye mabwawa. Tulicheleweshwa sana kimaendeleo. Sasa tutaweza kuifungua nchi vizuri na kurudisha uchumi uliokwama.
  2. M

    JamiiForums Tanzania SoC02 Ujenzi wa bwawa la Nyerere sio suluhisho la umeme kwani umeme wa maji sio chanzo sahihi cha nishati nchini Tanzania, itumike njia hii

    Umeme ni nishati muhimu sanaa katika maendeleo ya taifa la Tanzania kwani uzalishaji wa bidhaa nyingi viwandani, migodini, mashambani, wajasiriamali na nyumbani hutegemea nishati ya umeme ambayo kwa kiasi kikubwa unaotokana na maji ambao ndio unaosemekana kua nishati yenye gharama nafuu zaidi...
  3. Sildenafil Citrate

    JamiiForums Tanzania Taarifa ya kukosekana kwa umeme kwenye baadhi ya mikoa Nchini

    Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake kukosekana kwa huduma ya umeme kulikosababishwa na upungufu wa kina cha maji kwenye vyanzo vyetu vya Kihansi na Pangani pamoja na hitilafu iliyotokea kwenye vituo vya Kinyerezi I na Songas leo, Jumanne, Septemba 13, 2022. Hitilafu...
  4. Suzy Elias

    JamiiForums Tanzania DOKEZO Hapa wilaya ya Ngara umeme ni bidhaa ya anasa yapata miezi sasa

    Wilaya ya Ngara mkoani Kagera na viunga vyake hakika umeme umekuwa ni bidhaa ya anasa na aghari mno kuipata! Kuanzia Benaco, Ngara yenyewe hadi Rusumo umeme umekuwa ukiwaka kwa masaa yasiyozidi manne tena usiku tu na kosa kuche wenye umeme wao huuchukua. Mfano muda huu Benaco na Ngara yote...
  5. U

    JamiiForums Tanzania Umeme kukatika ovyo tatizo ni nini?

    TANESCO tujuzeni, kila mkoa ukiuliza nini shida mbona umeme unakatika sana kipindi hiki, wanasema "Lodi shedingi". Wizara toeni kauli tukanunue jenereta.
  6. Muwa mtamu

    JamiiForums Tanzania TANESCO: Arusha sasa ni rasmi mgao wa umeme?

    Tanesco Arusha, je sasa ni rasmi mgao wa umeme? Mbona hamjatangaza? Ndugu wanaJF, ni takriban wiki 3 sasa Tanesco Arusha wanakata umeme kila siku kuanzia saa 3 asubuhi na unarudi jioni sana. Maeneo mengi yanaathirika na kadhia hii hasa Meru na Arumeru kwa ujumla. Na maeneo kadhaa ndani ya...
  7. D

    JamiiForums Tanzania Mnatuchosha wanasiasa. Mtulipishe tu huo umeme wenu laki 8, Kila kitu tumejenga shule, afya mara barabara. Hizo V8 zenu mbona hamzitaji?

    Viongozi wa serikali Kila gharama serikali inayoingia kuhudumia jamii mnalalamika wakati Kodi mnazichukua kwetu. Kwani mnataka pesa ya serikali mfanyie nini? Mbona kama V8 zenu, maposho na mishahara mikubwa mnayolipana hatulalamiki? Juzi Waziri Afya eti NHIF inapata hasara Hadi kutamani...
  8. J

    JamiiForums Tanzania Waziri Makamba: Tutaweka mchanganyiko wa Umeme wa Maji, Gesi, Upepo, Jadidifu na hata Nyuklia kwenye Gridi ya Taifa

    Waziri wa Nishati January Makamba amesema wanakusudia kuweka mchanganyiko wa uhakika wa Umeme kwenye Gridi ya Taifa. Makamba amevitaja vyanzo mbalimbali vitakavyozalisha umeme huo kuwa ni Maji, Gesi, Jadidifu, Upepo na Just. Waziri Makamba amesema hata chanzo cha Nyuklia kinaweza kutumika kama...
  9. M

    JamiiForums Tanzania Wabunge Festo Sanga na Subira Mgalu mbona mnahangaika kumtetea Waziri Makamba kauli ya Umeme Laki 8?

    Siku ya leo mitandao yote ya kijamii inazunguka Clip ya Waziri wa Nishati, Januari Makamba ikisema kuanzia sasa gharama ya kuunganisha umeme iwe mjini iwe kijijini gharama ya kuletewa umeme ni laki 8. Clip hiyo imetokana na sehemu ya mahojiano ya ITV katika Kipindi cha Dakika 45 Makamba...
  10. gimmy's

    JamiiForums Tanzania Kama Makamba atatenda anayoyazungumza kuhusu umeme ni jambo la muda, tutarajie umeme bora siku za mbeleni

    Nianze kwakusema mimi ni muhanga wa huu umeme wa Tanzania kwani nilishawahi kupata hasara ya mamilioni mara kwa mara kwasababu ya low voltage. Mimi ni mjasiliamali mwenye kiwanda kidogo hivyo kutokana na umeme kuwa mdogo ilikua inalazimu kuwasha machine mojamoja kwani mbili kwa wakati mmoja...
  11. The Assassin

    JamiiForums Tanzania Kampuni ipi ina majiko imara ya umeme?

    Wakuu naomba kuuliza. Ni kampuni ipi ina majiko imara ya umeme/gas? Jiko linalohitajika la umeme, liwe na plate 2 za umeme na 2 za gas. Natanguliza shukurani.
  12. sky soldier

    JamiiForums Tanzania Maji ya kuchemsha na maji ya chupa yapi ni salama zaidi na yenye afya? Ni sawa kuchemsha maji ya kunywa kwenye birika ya umeme tofauti na sufuria?

    Habari yenu ndugu zangu, Maji ya kuchemsha na maji ya chupa yapi ni salama zaidi na yenye afya? Je, ni sawa kuchemsha maji ya kunywa kwenye birika ya umeme tofauti na kawaida tulivyozoea kuyachemsha kwenye sufuria kwa jiko la gesi au mkaa?
  13. Orketeemi

    JamiiForums Tanzania Pikipiki za umeme

    Habari. Naomba elimu kuhusu pikipiki za kuchaji [ za umeme]. Je, inatumia unit ngapi mpaka kuwa full charged? Bei zake ni kiasi gani ikiwa mpya? Na zinapatikana wapi hasa kwa Kanda ya ziwa. Uimara wake vip? Nitashukuru sana
  14. B

    JamiiForums Tanzania Serikali inajikosesha mapato yenyewe kwenye huduma za maji na umeme.

    Ili liko wako wazi wala situmii nguvu sana kudadavua. Nyumba nyingi kwenye miji na majiji hazina umeme wala maji hata kama huduma iyo imefika eneo hilo na ukiongea na mtu mmoja mmoja izo huduma anazihitaji isipokua ile hela ya mkupuo inakua mtihani kwake. Serikali inakwama wapi kumpelekea...
  15. Nyankurungu2020

    JamiiForums Tanzania January Makamba alituambia alifanya ukarabati wa miundo mbinu ya umeme iliyochakaa. Sasa hizi hitilafu na katikakatika ya umeme inatoka wapi?

    Tuliambiwa na January kuwa miundo mbinu ya umeme ilikuwa imechakaa sana. Hivyo ilihitaji ukarabati wa nguvu. Ukarabati ulifanyika na sasa tunaona hitilafu kibao. Mbaya zaidi umeme unakatika na kurudi ghafla kiasi cha kuharibu vifaa vya umeme vya watu.
  16. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Mitambo ya Bwawa la Mtera yapata hitilafu, mikoa 14 kukosa umeme

    Shirika la Umeme Tanzania TANESCO limethibitisha kutokea kwa hitilafu hiyo kwenye moja ya mitambo ya kuzalisha umeme ya Bwawa la Mtera na kusababisha upungufu wa Umeme. Mikoa 14 itakayokosa Umeme kwa muda usiofahamika ni pamoja na Ruvuma, Mbeya, Mwanza, Iringa, Manyara, Singida, Geita, Arusha...
  17. Replica

    JamiiForums Tanzania Mkurugenzi wa Shell: Mgogoro wa nishati utakuwa kipimo cha umoja wanachama EU. Bei yapanda mara 30(3,000%)

    Mkurugenzi wa Shell, Ben Van Beurden ameitahadharisha Ulaya inaweza kuhitaji kugawanya nishati kwa miaka kadhaa kwani mgogoro uliopo una kila dalili ya kudumu zaidi ya kipindi kimoja cha baridi. Maoni ya Mkurugenzi huyo anaeongoza kampuni kubwa zaidi barani Ulaya ya mafuta na gesi yanafatia...
  18. saidoo25

    JamiiForums Tanzania Mwekezaji afunga kiwanda kwa kukosa umeme

    Mwekezaji Mzawa wa Kiwanda cha kuzalisha nguzo za umeme cha TAWOODS, Peter Mwera amelazimika kufunga kiwanda chake baada ya kupata hasara ya zaidi ya shilingi bilioni moja kutokana na kukosa huduma ya umeme. Chanzo: Gazeti la Sauti ya Mara
  19. LUS0MYA

    JamiiForums Tanzania Kiwanda cha Cement Tanga chasimamisha uzalishaji kutokana na ukosefu wa umeme

    Taarifa ya habari ya UTV imeripoti leo magari ya kubeba cement yamekwama kwa zaidi ya siku saba kwa ukosefu wa mzigo wa cement kutokana na kusimama uzalishaji. TANESCO imeshindwa kutoa umeme wa kutosha kwa uzalishaji na meneja wa kiwanda amedai wanatumia zaidi ya milioni 500 kwa mwezi kununua...
  20. Marathon day

    JamiiForums Tanzania Tatizo la kukatika umeme mara kwa mara ifikapo saa moja usiku mpaka saa nne

    Ndugu wahusika, Mimi ninatatizo la hizi aina ya MITA za TANESCO Mpya, Yaani maeneo yangu IFIKAPO jioni ya saa 12 jioni mpaka saa 4 usiku ni shida Kila dakika Moja umeme unakatika na kuwaka mfululizo, cha ajabu majirani zangu umeme upo mda wote. Nilijaribu kuulizia Taneco wanasema aina ya MITA...
Back
Top Bottom