Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,810
- 11,979
'MRADI WA UMEME WA RUSUMO HYDROPOWER PROJECT KUKAMILIKA MWEZI NOVEMBA 2022' - MAKAMBA
Siku ya sita ya Ziara ya Waziri wa Nishati January Makamba kwenye Mikoa 14 na Wilaya 38 imemfikisha kwenye mpaka wa Tanzania na Rwanda unapojengwa mradi mkubwa wa uzalishaji Umeme wa Maji wa Rusumo (Rusumo hydropower Project).
Mara baada ya kukagua mradi huo Waziri Makamba alipata nafasi ya kuongea na Wanahabari kuhusu hali ya mradi huo ulipofikia ambapo amesema>>' Kasi ya Ujenzi inaendelea vizuri na uko kwenye asilimia 95%, mradi ukikamilika Kampuni hii itauuzia umeme mashirika ya Umeme kwenye hizi nchi tatu (Rwanda, Burundi na Tanzania) umefadhiliwa na wafadhili wa Benki ya maendeleo ya Afrika na wafadhiri wengine wa Maendeleo' - Makamba.
Pamoja na hayo Waziri Makamba akaongeza kwa kusema >>'Tunautegemea mradi huu kuongeza uhakika wa umeme kwenye ukanda huu wa Ziwa Victoria, Jawabu la matatizo ya umeme kanda ya Ziwa ni mradi huu' - Makamba.
Mradi huu wa Rusumo Hydropower unategemewa kumalizika mwezi Novemba mwaka huu (2022) na utahusisha nchi 3 ambazo ni Tanzania, Rwanda na Burundi.
Siku ya sita ya Ziara ya Waziri wa Nishati January Makamba kwenye Mikoa 14 na Wilaya 38 imemfikisha kwenye mpaka wa Tanzania na Rwanda unapojengwa mradi mkubwa wa uzalishaji Umeme wa Maji wa Rusumo (Rusumo hydropower Project).
Mara baada ya kukagua mradi huo Waziri Makamba alipata nafasi ya kuongea na Wanahabari kuhusu hali ya mradi huo ulipofikia ambapo amesema>>' Kasi ya Ujenzi inaendelea vizuri na uko kwenye asilimia 95%, mradi ukikamilika Kampuni hii itauuzia umeme mashirika ya Umeme kwenye hizi nchi tatu (Rwanda, Burundi na Tanzania) umefadhiliwa na wafadhili wa Benki ya maendeleo ya Afrika na wafadhiri wengine wa Maendeleo' - Makamba.
Pamoja na hayo Waziri Makamba akaongeza kwa kusema >>'Tunautegemea mradi huu kuongeza uhakika wa umeme kwenye ukanda huu wa Ziwa Victoria, Jawabu la matatizo ya umeme kanda ya Ziwa ni mradi huu' - Makamba.
Mradi huu wa Rusumo Hydropower unategemewa kumalizika mwezi Novemba mwaka huu (2022) na utahusisha nchi 3 ambazo ni Tanzania, Rwanda na Burundi.