uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. Sam Gidori

    JamiiForums Tanzania, JamiiForums Uganda Facebook yafungia akaunti za viongozi wa serikali ya Uganda

    Zikiwa zimebaki siku chache kuelekea uchaguzi mkuu nchini Uganda, mtandao wa Facebook umefungia akaunti za viongozi wa serikali kwa tuhuma za kushawishi maamuzi ya umma, mtandao wa AFP umeripoti. Mkuu wa Mawasiliano wa Facebook wa Ukanda wa Nchi za Kusini mwa Sahara, Kezia Anim-Addo amesema...
  2. Kamanda Asiyechoka

    JamiiForums Tanzania Uchaguzi umeisha, tujitathmini upya

    Kichwa cha habari chajieleza. Ukweli ni kuwa hakuna tutachoambulia zaidi ya wabunge viti maalumu wapatao 19. Kubaki tunapiga kelele kuwa uchaguzi ulivurugwa haiwezi kutusaidia. Kilichobaki tujitathimini tutaweza kusimama tena? Nani alisababisha tukapoteza nanma hii? Atupishe haijalishi kama...
  3. Melubo Letema

    JamiiForums Tanzania Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Kufanyika tarehe 30/1/2021

    Uchaguzi Mkuu wa RT unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu wa kwanza, huku nafasi ambazo zitahitajika ni nafasi ya Rais na Makamu wake pamoja na Wajumbe 6, ikiwemo moja ya Viti Maalum Mwanamke. Fomu zitaanza kuchukuliwa Kesho (8 hadi 19, Januari), kwa ada ya shilingi laki mbili...
  4. Q

    JamiiForums Tanzania Uchaguzi wa Marekani umemalizika, tumeona umuhimu wa kujenga taasisi imara sio watu imara

    Uchaguzi wa Marekani umemalizika rasmi leo usiku kwa Rais mteule Joe Biden kuthibitishwa na mabunge yote mawili kuwa rais wa nchi hiyo baada ya rais Trump kwa kipindi cha miezi miwili kuhangaika kupinga matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika Novemba mwaka jana. Tulichojifunza zaidi ni jinsi...
  5. Replica

    JamiiForums Tanzania Asasi nne za kiraia zaishitaki Tanzania mahakama ya Afrika Mashariki kwa 'Ukiukwaji mkubwa' kutoka kwa polisi wake

    Asasi nne za kiraia zimeifikisha mahakamani Serikali ya Tanzania kwa ukiukwaji mkubwa kwenye uchaguzi mkuu wa karibuni ambao ulimrudisha madarakani Rais John Pombe Magufuli. Taasisi kutoka Kenya na Uganda zinaishtaki Tanzania kwenye Mahakama ya Afrika Mashariki, zikituhumu vyombo vya usalama...
  6. Miss Zomboko

    JamiiForums Tanzania Mbatia: Uchaguzi uliopita umetuacha uchi kama Taifa. Watanzania wamekata tamaa kwa Siasa zinazoendelea Nchini

    JAMES Mbatia, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi amesema, uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 2020, umelivua nguo Taifa. Anaandika Yusuph Katimba, Dar es Salaam…(endelea). Katika waraka wake wa Kheri ya Mwaka Mpya 2021, alioutoa kwa wanachama wa chama hicho na Watanzania amesema, Taifa limeingia...
  7. Erythrocyte

    JamiiForums Tanzania Salamu za Mwaka Mpya 2021 kwa Watanzania, Tundu Lissu atoa mwongozo wa kudai Tume Huru ya Uchaguzi

    Akitoa salamu za Mwaka mpya wa 2021 kwa wananchi wa Tanzania, Mh Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema , ametoa mwongozo wa kudai Tume huru ya uchaguzi kuanzia sasa, amesema kwa hali ilivyo nchini Tanzania ni vigumu kushiriki uchaguzi wowote bila Tume huru ya uchaguzi Amewaomba wadau...
  8. Queen Esther

    JamiiForums Tanzania Bima ya afya kwa wote imetajwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025

    Kwa unyenyekevu mkubwa naomba kuweka taarifa ikionesha Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020 hadi 2020 imeweka bayana kipengele cha Bima ya Afya kwa wote. Ilani hiyo chini ya Jemedari wetu mbeba maono Dr. John Pombe Magufuli inasomeka kama ifuatavyo:- 1. HUDUMA ZA JAMII Zimeanzia kutajwa kwenye...
  9. M

    JamiiForums Tanzania, JamiiForums Uganda Uchaguzi Uganda, kuna la kujifunza!

    Watanzania tumetoka katika uchaguzi siku chache zilizopita lakini jirani zetu wa Uganda wanaelekea katika uchaguzi siku chache zijazo. Mlio na nafasi jaribuni kufuatilia katika TV za Uganda hasa wale wachambuzi wa siasa kama mimi, kuna la kujifunza! Zingatieni usemi huu,"Nitajie rafiki yako...
  10. S

    JamiiForums Tanzania Nabii Suguye: Viongozi wa Serikali watubu kabla mwaka haujaisha kwa 'blunder' zilizofanywa kwenye Uchaguzi Mkuu 2020

    Katika mahubiri yanayoendelea WRM leo jumapili 27/12/2020, Nabii Nicolaus Suguye amewataka viongozi wa serikali wakatubu kwa blunder zilizofanyika ktk uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020. Ameongeza kwa kusema kuna watu wamekufa na wamesononeka kufuatia blunder hizo. Wakatubu kabla mwaka kabla mwaka...
  11. K

    JamiiForums Tanzania Siku 60 baada ya Uchaguzi: Ni wabunge wachache waliofanya cha maana jimboni, wengi wapo Dar

    Siku 60 baada ya uchaguzi mkuu hakuna Mbunge aliyeonekana kutambua kwamba uchaguzi ulishamalizika na Sasa ni muda wakutimiza ahadi walizoahidi. Wabunge wengi wamehamishia makazi yao Dar huku wakipanda mwewe kuelekea Dodoma pale inapolazimika kiratiba kufanya hivyo. Huku majimboni pia kwa kuwa...
  12. J

    JamiiForums Tanzania Waziri Jaffo hao Wakurugenzi walikuwa wanasimamia uchaguzi, huo ushuru wangekusanya muda gani? Usiwafute kazi tafadhali!

    Tunakumbushana tu waziri wa Tamisemi Mh Jaffo kwamba 2020 ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi na hao wakurugenzi ni wasimamizi wa uchaguzi. Kusema kwamba wasipofikisha 50% ya lengo la makusanyo ya mwaka ifikapo Devember 31 wajitathmini kama wanatosha kubaki ofisini ama uwatimue ni kuwaonea bure. Kwa...
  13. CUF Habari

    JamiiForums Tanzania Profesa Lipumba: Liwale hakupo shwari, Polisi wameua watu wawili sababu ule uchaguzi haukuwa huru na haki

    "Polisi wameua watu wawili Liwale kwa sababu ya uchaguzi haukuwa huru na haki sasa CCM kama hamtaki vyama vyingi mtuambie".-Prof. Lipumba. #UzinduziWaKongamanoLaKudaiTumeHuruNaKatibaMpya #OfisiKuuYaChamaBuguruni.
  14. Mystery

    JamiiForums Tanzania GE2020 Hivi kuna maana gani kuendelea kuyabakiza mabango ya Chagua Magufuli nchi nzima, wakati uchaguzi ushakwisha?

    Kuna kitu ambacho siyo cha kawaida, ambacho sijawahi kukiona katika miaka ya nyuma katika tawala zilizopita, kwa kuyabakiza mabango kwa maelfu yanaendelea kuwepo sehemu mbalimbali nchini, wakati uchaguzi ushakwisha! Mabango hayo yalitengenezwa maalum kwa ajili ya uchaguzi mkuu pekee na kwa...
  15. A

    JamiiForums Tanzania UCHAGUZI WA SHULE KWA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2021

    Majina ya waliopangiwa shule kuanza kidato cha kwanza, bonyeza link apo chini. http://196.192.73.4/allocations/
  16. CUF Habari

    JamiiForums Tanzania Taarifa kwa Umma: Polisi wavamia mkutano wa ndani wa Uchaguzi jumuiya CUF Handeni

    TAARIFA KWA UMMA: POLISI WAVAMIA MKUTANO WA NDANI WA UCHAGUZI WA JUMUIYA CUF HANDENI: Jeshi la Polisi limevamia Mkutano wa Uchaguzi wa Jumuiya za CUF- Chama Cha Wananchi- Jumuiya ya Wanawake (JUKECUF) na Jumuiya ya Vijana ( JUVICUF) Handeni Tanga. Kwa mujibu wa Maelezo ya Naibu Mkurugenzi...
  17. S

    JamiiForums Tanzania Hili kwa Polisi ni Jinai - Kuhusiana na Uchaguzi uliopita, tuseme tupime, labda Wanahabari wakikutana na wakuu watauliza

    Ni pale , kwa ujumla, ikiwemo uchaguzi Polisi wanapomkamata mtu kisha wakampeleka kwenye kituo cha polisi kisha mtu yule anapotolewa au kuachiwa anakutwa amepigwa sana kiasi ya kuhatarisha maisha yake na pengine akifikishwa hospitali hufariki kutokana na athari za mapigo aliyoyapata. Aina za...
  18. J

    JamiiForums Tanzania CHADEMA na ACT-Wazalendo wametuonesha Umuhimu wa ile sheria ya Ushirikiano wa vyama wakati wa Uchaguzi

    Kwa sasa kuna kutoaminiana kati ya vyama shirika katika uchaguzi mkuu wa 2020 nikimaanisha CHADEMA na ACT-Wazalendo. Kila kimoja kinalaumu kingine kwa maamuzi wanayochukua baada ya kufeli katika uchaguzi mkuu. Sheria ya ushirikiano wa vyama vya siasa inataka pawepo mkataba wa kisheria...
  19. Mystery

    JamiiForums Tanzania Jaji Warioba amethubutu kuukosoa Uchaguzi Mkuu uliopita. Je, viongozi wengine wastaafu mbona mpo kimya?

    Akiwa mwalikwa kwenye kongamano la haki za binadamu lililoandaliwa kwa ajili ya viongozi wa dini, lililofanyika jijini Dar tarehe 14 mwezi huu, Jaji Warioba alizitaja kasoro kuu 4 zilizojitokeza katika uchaguzi mkuu uliopita. Alizitaja kasoro hizo kama ifuatavyo:- 1. Wagombea wengi wa upinzani...
  20. TheDreamer Thebeliever

    JamiiForums Tanzania Maono yangu tunapoelekea 2025

    wenzetu wa CCM wanasema kuisha kwa uchaguzi ni mwanzo wa chaguzi nyingine. Ila kuelekea 2025 namuona mheshimiwa Majaliwa akikitwaa kijiti cha kuiongoza nchi kutoka kwa rais Magufuli. Namuona ndugu yangu Bernard Membe akirudi nyumbani CCM. Naliona anguko la CHADEMA na kuibuka kwa ACT kama...
Back
Top Bottom