Salamu za Mwaka Mpya 2021 kwa Watanzania, Tundu Lissu atoa mwongozo wa kudai Tume Huru ya Uchaguzi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,703
218,231
Akitoa salamu za Mwaka mpya wa 2021 kwa wananchi wa Tanzania, Mh Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema , ametoa mwongozo wa kudai Tume huru ya uchaguzi kuanzia sasa, amesema kwa hali ilivyo nchini Tanzania ni vigumu kushiriki uchaguzi wowote bila Tume huru ya uchaguzi

Amewaomba wadau wote kuhakikisha wanadai Tume huru ya uchaguzi bila kuchoka, ndani ya nchi na kwenye majukwaa yote ya kimataifa , huku akitoa mifano ya nchi za Ghana, Kenya na Malawi kama kielelezo cha mafanikio ya upatikanaji wa Tume huru kutokana na juhudi za wananchi wa nchi hizo.

Mimi binafsi naunga mkono madai ya Tume huru ya Uchaguzi nchini Tanzania, natoa wito kwa Watanzania kupigania Tume huru ya uchaguzi kwa udi na uvumba ili kuwezesha mchakato huru na wa haki wa kupata viongozi na hatimaye kuondoa manung'uniko, laana na mikosi kwenye nchi, kupigania Tume huru halijawahi kuwa kosa mahali popote kwenye dunia hii wala Ahera, Haki huinua Taifa.
 
Oyooooooo! Rais wa nchi hii kaongea Sasa. Yule kashindwa hata kutoa salaam za mwaka mpya.

Ukiwa hupendwi bwana inakuwa taabu sana.

Ni kweli mpakwa mafuta TAML, tuko mdogo mdogo na askofu Mwamakula tunapanga mikakati ya kuandamana (hata kimoyomoyo) ili kuipata tume huru. Tutaipata tu!
 
Akitoa salamu za Mwaka mpya wa 2021 kwa wananchi wa Tanzania , Mh Lissu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema , ametoa mwongozo wa kudai Tume huru ya uchaguzi kuanzia sasa , amesema kwa hali ilivyo nchini Tanzania ni vigumu kushiriki uchaguzi wowote bila Tume huru ya uchaguzi...
Aje tudai nae huku bongo
 
Eti akitoa salamu za mwaka mpya kwa watanzania.., lini?,na wapi?. Yule status yake ya ukimbizi haimuhusu kuongelea Siasa akiwa huko aliko Kama unabisha kuwa wewe sio muongo weka ushahidi wa video.
Uko nyuma sana !
 
  • Thanks
Reactions: BAK
So tunatakiwa kufanya nini kupata hiyo Tume huru ya uchaguzi?
 
Back
Top Bottom