Jaji Warioba amethubutu kuukosoa Uchaguzi Mkuu uliopita. Je, viongozi wengine wastaafu mbona mpo kimya?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,477
30,130
Akiwa mwalikwa kwenye kongamano la haki za binadamu lililoandaliwa kwa ajili ya viongozi wa dini, lililofanyika jijini Dar tarehe 14 mwezi huu, Jaji Warioba alizitaja kasoro kuu 4 zilizojitokeza katika uchaguzi mkuu uliopita.

Alizitaja kasoro hizo kama ifuatavyo:-

1. Wagombea wengi wa upinzani kuenguliwa na Wasimamizi wa uchaguzi (maDED) pasipo sababu za msingi na Tume ya uchaguzi ya Taifa kujifanya kama hawaioni kasoro hiyo!

2. Mawakala wa vyama vya upinzani kuzuiliwa wasiingie kwenye vyumba vya kupigia kura.

3. Vyama vya siasa, hususani CCM kupuuza mapendekezo ya wajumbe waliyoyatoa kwenye kura za maoni kwenye majimbo yao na badala yake wao Kamati Kuu ya Chama kuwaletea watu "wao" ili wananchi hao wawapitishe bila ya kupingwa!

4. NEC kutosikiliza malalamiko ya wagombea wa uchaguzi, hususani wa vyama vya upinzani kwa wakati muafaka.

Alifafanua Waziri Mkuu huyo mstaafu Jaji Warioba kuwa chanzo cha kuvunjika amani katika nchi nyingi barani Afrika ni nchi hizo kupuuza Haki ya wananchi na kutoshughulikia kasoro kama hizo wakati wa chaguzi.

Akaendelea kusisitiza kuwa AMANI ni tunda la HAKI na mahali ambapo HAKI haipo ni vigumu sana kudumisha AMANI

Alisema kuwa nchi yetu inajivunia amani tuliyonayo ambayo tunapaswa kuienzi kwa kuondoa kasoro hizo za wazi kabisa zilizojitokeza kwenye uchaguzi uliopita

Jaji Warioba ni mmojawapo wa viongozi wastaafu wachache sana ambaye amediriki kuukosoa uchaguzi mkuu uliopita kwa namna ulivyoendeshwa

Swali langu ni kuwa, je viongozi wastaafu wengine hawakuziona kasoro hizo na kuamua kuwa "mabubu" bila kukemea kasoro hizo ambazo Jaji Warioba ametahadharisha kuwa kama zisipotafutiwa ufumbuzi wa haraka, basi zinaweza kutuondolea tunu hii adimu sana ya amani tuliyonayo kwenye nchi hii?

Au ndiyo tuseme kuwa viongozi wastaafu wengine pamoja na kuyaona hayo "madudu" ya uchaguzi wamejiamlia kujikakia kimya kwa kuogopa kuwa watakaripiwa na Jiwe na kuambiwa kuwa wanawashwawashwa?

Mungu ibariki Tanzania.
 
Na Siku zingine huyu huyu Jaji Mzee Warioba akiwasema au akiwashutumu Wapinzani nchini usiache pia kuja na Uzi hapa wa Kumshukuru mno tu.

Uchaguzi umekwisha,fanyeni kazi
Yaani nyiye maCCM mnategemea kuwa mfanye uharamia wa kupora kura, halafu mtegemee tukae kimya?

Hilo haliwezekani, tutaendelea kusema na kusema wee, hadi kilio chetu mtakapokisikia
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Huyo mzee ameamua kubaki na heshima yake mpaka kufa. Wengine wamepotoka
It's very true

Viongozi wengine wastaafu wameamua kulinda matumbo yao!

Isipokuwa Spika mstaafu Pius Msekwa, ambaye naye ameamua kumkalia kooni Spika Ndugai kwa namna anavyoikanyaga kanyaga Katiba ya nchi kwa kuendelea kuwatambua wale wabunge "wake" wa viti maalum, akina Halima Mdee, ambao chama cha Chadema kiliwavua uanachama wao, lakini Spika Ndugai akaamua kuendelea kuwakumbatia
 
Warioba siyo MUNGU muumba

Akijitokeza akaongea MUNGU kwa sauti tutauona ukweli,siyo binadamu aliye zaliwa na mwanamke ktk dunia
 
Kikwete anamke na mwanae wabunge na Mwinyi ana mwanae Rais na wengine wawili wabunge, jumla watatu halafu unataka waseme! Hata wewe haungesema.
 
Eu wamekubali mpaka wametoa msaada (sio mkopo)

China wamekubali tena wametutabiria makubwa!

Marekani ndo walianza mapema kabsa hadi wakatutolea mfano

Hayo ndo mataifa makubwa

Sasa je,tumaini la ufipa liko wapi kwa sasa?

Kumbuka Seif na zitto saivi wapo ofisini.

Who are u by the way?

Nawashauri nendeni mkashitaki INDIA😂😂😂😂😂
 
Asante Jaji na Waziri Mkuu Mtaafu Joseph SInde Warioba. Mungu akubariki kwa uthubutu wa kusema ukweli. Media zetu zote mbendembende, viongozi wengi wa dini wameacha kazi ya kubwa ya Unabii, Ukuhani na Ufalme, wamebakia nao kusema ndiyoooooo kwa watawala wadhalimu, waovu wasiotambua kuwa Mungu ndiye Mkuu wa yote (lakini uweza wake Mkuu unazuiliwa na Desturi yake nzuri sana ya Upole, Uvumilivu, Huruma, Upendo, Uwema na Ukarimu).
 
Bahati yake Makonda sio kiongozi kwa sasa.
Kuna Comred Magoti huyo ni noma,kama unewahi kusoma riwaya za James Hadley Chase, unaweza kumlinganisha na character mmoja anaitwa Vitto Ferrari, huyo akikukosa basi Israili malaika mtoa roho anasubiri.
 
Baada ya Makonda kuondoka sasa Mzee Warioba anathubutu kuongea, alikuwa kimya sana kipindi chote cha uongozi wa Bashite.

Je, alipewa tishio gani baada ya kile kipigo?
 
Hili la Warioba limezimwa, Vyombo vya habari vimefungwa mdomo wasijadili sana, Litapita.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom