mahakama

Mahakama ni chombo kinachotafsiri na kutumia sheria katika kutoa haki. Ni moja wapo ya mihimili mitatu inayounda serikali, ambapo mihimili mingine ni Bunge na Serikali Kuu.
  1. ngoshwe

    JamiiForums Tanzania Mahakama ya Rufaa yabatilisha uamuzi wa Mahakama Kuu kesi ya dhamana ya makosa makubwa

    Katika hukumu iliyotolewa leo tarehe 5 Agosti, 2020, Jopo la Majaji watano wa Mahakama ya Rufani limekubaliana na Serikali kuwa kifungu cha 148(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai ,Sura ya 20 ya Sheria za Tanzania kinachozuia dhamana kwa makosa makubwa ya jinai yakiwemo mauaji...
  2. J

    JamiiForums Tanzania Tundu Lissu: Nina kesi 6 Mahakamani nikihusishwa na uchochezi lakini hazininyimi sifa ya kuwa Rais kwa mujibu wa Katiba

    Tundu Lissu mwenyewe amefafanua juu ya kesi zinazomkabili pale Mahakama ya Kisutu na kwamba kesi hizo hazimuondolei sifa ya kupigiwa kura na kuwa Rais wa JMT. Amebainisha kuwa hilo liko wazi kabisa katika katiba ya nchi yetu. Maendeleo hayana vyama!
  3. Japhet Karibu

    JamiiForums Tanzania Lissu kuidanganya Mahakama mpaka kesi kuahirishwa, Sheria itamuadhibu vipi?

    Kama mnakumbuka juzi Sheria ilimtaka Lisu kuhudhuria mahakamani kwa ajili ya kesi zake zilizopo Mahakamani lakini ulitolewa utetezi kutoka kwa wanasheria wake kuwa mteja wao ndugu Lisu asingeweza kuhudhuria mahakamani kwa sababu amejiweka karantini kwa siku 14 kwa kuhofia maambukizi ya Corona...
  4. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Kesi dhidi ya JamiiForums, namba 458: Jamhuri yafunga Ushahidi baada ya Tully Mwambapa kutoa Ushahidi. Kesi itaendelea 20 Agosti 2020

    Kesi namba 458 ya mwaka 2016 (Jamhuri dhidi ya Mkurugenzi wa Jamii Forums na Mwanahisa wa Jamii Media) inatajwa tena leo, Julai 30, 2020 majira ya saa 3 asubuhi mbele ya Hakimu Huruma Shaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar Mara ya mwisho iliposikilizwa Juni 25, 2020 Jamhuri...
  5. Erythrocyte

    JamiiForums Tanzania Kesi ya Tundu Lissu kuendelea kesho Mahakama ya Kisutu, maelfu watarajiwa kuhudhuria

    Hii ndio taarifa inayozunguka dunia nzima kwa sasa, kwamba Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Lissu, atatua Mahakamani kisutu kukabiliana na tuhuma zake . Vyombo mbalimbali vya kimataifa vinatarajiwa kuwepo na kurusha dunia nzima . Wote mnakaribishwa.
  6. Analogia Malenga

    JamiiForums Tanzania Mahakama ya Afrika, yaitaka Tanzania kubadili Katiba kuruhusu Wananchi kupinga matokeo ya Kura za Urais

    Mahakama ya Afrika yaitaka Tanzania kubadili Katiba kuruhusu Wananchi kupinga matokeo ya Kura za Urais Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu imetoa uamuzi kuwa Ibara ya 41(7) ya Katiba ya Tanzania inayokataza matokeo ya urais kupingwa Mahakamani inakiuka Ibara ya 1,2, 7(1)(a) ya Mkataba wa...
  7. Civilian Coin

    JamiiForums Tanzania Mashitaka yaliyosababisha Don Nalimison kufungwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza ni haya

    Deogratius Kisandu ambaye kwasasa anatambulika Kama DON NALIMISON kisheria, haya ndio yalikuwa mashitaka yaliyopelekea kufungwa japo alishinda kesi.
  8. FRANC THE GREAT

    JamiiForums Tanzania Mahakama nchini Brazil yamuamuru Rais Jair Bolsonaro kuvaa barakoa. Atakiwa kuheshimu sheria za nchi

    Habari! Kutokana na kushamiri ama kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya corona nchini Brazil, Mahakama nchini humo imemuamuru Rais wa nchi hiyo Jair Bolsonaro kuvaa barakoa ya kinga la sivyo 'kukiona cha mtema kuni'. Jair Messias Bolsonaro. Taarifa kamili: Katika uamuzi uliotolewa...
  9. Cannabis

    JamiiForums Tanzania Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu yafuta mashtaka ya kusafirisha dawa za kulevya kwa Mfanyabiashara Mussa Mohamed

    MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemfutia mashtaka Mfanyabiashara Mussa Mohamed aliyefikishwa mahakamani hapo leo Juni 23, 2020 akikabiliwa na mashtaka ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine. Hatua hiyo imekuja baada ya Wakili wa Serikali,Sylvia Mitanto kudai mbele ya Hakimu Mkazi...
  10. S

    JamiiForums Tanzania Namba 14: Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC), Jecha Salim Jecha achukua fomu ya urais Zanzibar. Arejesha fomu hiyo

    Jecha Salim Jecha amejitokeza kuchukua fomu za kuomba ridhaa ya kuteuliwa kuwa mgombea Urais visiwani humo kwa tiketi ya CCM. Jecha amewahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na vilevile aliwahi kugombea Ubunge wa Jimbo la Chumbuni. Maoni yangu: Vuta tafakuri hawa wasimamizi wa...
  11. Miss Zomboko

    JamiiForums Tanzania Wadhamini wa Lissu waiomba Mahakama kutoa hati ya kumkamata Tundu Lissu

    MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imetoa siku saba kwa upande wa Jamhuri kuwasilisha majibu ya kiapo kinzani na maombi ya wadhamini Ibrahim Ahmed na Robart Katula wa mbunge wa zamani wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, Julai 14, mwaka huu. Wadhamini hao amefungua maombi...
  12. Return Of Undertaker

    JamiiForums Tanzania Mahakama ya Afrika Mashariki yatupilia mbali pingamizi la Serikali juu ya sheria ya habari iliyofunguliwa na watetezi wa habari

    #HABARI Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ) imetupilia mbali rufaa iliyokatwa na Serikali, baada ya ushindi wa kesi ya kupinga baadhi ya vifungu vilivyoonekena kuwa kandamizi katika sheria ya huduma za vyombo vya habari ya mwaka 2016./ Serikali yabwagwa kesi sheria huduma vyombo vya habari ====...
  13. R

    JamiiForums Tanzania Mahakama Brazil yaamuru Serikali ifungue website ya Serikali na ichapishe taarifa za maambukizi ya Covid-19 kama yalivyokuwa yanatolewa

    Hii ni kutokana na serikali kuifunga website iliyokuwa ina report trend ya maambukizi ya coronavirus/covid-19. Mahakama imetoa hukumu kuwa kupata habari ni takwa la kikatiba na Rais asitumie ugonjwa wa covid-19 for political gain! Mh CJ Juma, umewasikia wenzako? ==== A Brazilian supreme...
  14. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Muswada wa Marekebisho Sheria-2020: Unajua watu hawataweza kudai haki kwa niaba ya Wanyonge? Viongozi wa juu Serikalini hawatashtakiwa moja kwa moja!

    Asasi za Kiraia 220 zimefanya uchambuzi wa muswada huo wa sheria na kuwasilisha mapendekezo ya mabadiliko ya muswada huo kwa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria. Taasisi hizo zimeeleza kuwa japo kuwa zinafahamu muswada huo una lengo wa kusasisha Sheria iliyopo sana huku ikibaki kuendana na...
  15. ngoshwe

    JamiiForums Tanzania Mahakama Kuu Dar, imetupilia mbali kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa dhidi ya Spika Ndugai kwa kumtambua Mwambe kama Mbunge baada ya Kujiuzulu

    Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetoa uamuzi na kutupilia mbali shauri la Kikatiba Na. 10 la mwaka 2020 lililofulinguliwa na Wakili wa Kujitegemea Revocatus Paul Kaunda kupinga Kauli ya Mhe. Spika aliyoitoa Bungeni kumtambua Mhe. Cecil Mwambe kuendelea kuwa Mbunge. Mahakama Kuu kupitia...
  16. Q

    JamiiForums Tanzania Spika Ndugai na Mwambe wapewa wito wa Mahakama, kesi kuanza Juni 3

    Kesi namba 12/2020 inayomkabili Spika wa Bunge, Job Ndugai imepangwa kuanza kusikilizwa Katika Mahakama Kuu ya Tanzania masijala ya Dar es salaam mnamo Juni 3 mwaka huu kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa Saba. Kesi hiyo ambayo imefunguliwa na Taasisi ya Haki za Kiraia na msaada wa...
  17. Analogia Malenga

    JamiiForums Tanzania Mahakama yamtia hatiani Zitto Kabwe katika kesi yake ya Uchochezi. Atakiwa kutotoa matamshi ya Uchochezi kwa mwaka 1. Asema kukata Rufaa

    Leo ikiwa ni siku ya Hukumu ya Mbunge wa Kigoma Mjini, Waandishi wenye Press Cards wamekataliwa kuingia kusikiliza hukumu ya Zitto kwa maelezo kwamba si waandishi wa Mahakama. UPDATE Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Ndugu Zitto ameachiwa huru kwa sharti kwamba asitoe matamshi ya uchochezi...
  18. Influenza

    JamiiForums Tanzania Idris Sultan afikishwa katika Mahakama ya Kisutu. Ashtakiwa kwa kumiliki laini ya simu isiyo na jina lake. Aachiwa kwa dhamana

    Mchekeshaji huyu alikuwa akishikiliwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay kwa takriban siku 8 akifanyiwa mahojiano. Haijajulikana ni mashtaka gani atasomewa lakini kwa wa mujibu wa Polisi, walikuwa wakimuhoji kwa tuhuma za kujaribu kuharibu ushahidi na makosa mengine ya Kimtandao. Endelea...
  19. R

    JamiiForums Tanzania Mahakama Kuu yatoa uamuzi kuwa kifungu kinachowanyima watuhumiwa dhanama ni batili

    Kifungu cha 148(5) cha CPA kinacho wanyima watuhumiwa wa makosa yaliyoainishwa na kifugu hicho ni batili na kifutwe kwa kuwa kinakiuka Katiba ya JMT na serikali. CHA AJABU: Mahakama imetoa muda wa miezi 18 kurekebisha /kufuta kifungu hicho. MAAJABU: Kitu batili unakiruhusu kiendelee kuwatesa...
  20. Influenza

    JamiiForums Tanzania Mbeya: Mpaluka Nyagali Mdude akamatwa na Heroine, apandishwa kizimbani akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi

    Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mdude Nyagali, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, kujibu shtaka linalomkabili ya uhujumu uchumi baada ya kukutwa na gramu 23.4 za dawa za kulevya aina ya Heroine. Pia soma: 1). Dar, Kinondoni: Yaliyojiri...
Back
Top Bottom