Search results

  1. Msambichaka Mkinga

    Uongozi wa Rais Samia Usitiwe Najisi

    Kwa hakika, na bila mashaka, uongozi wa Rais Samia umeonesha ushupavu. Wakati viongozi waoga huwaogopa wapinzani wao wa kisiasa, Rais Samia, bila woga, anawaweka karibu. Tangu mfumo wa vyama vingi uanze, ni Rais Kikwete ndiye aliyekuwa anashikilia rekodi ya kukutana na viongozi wa vyama vya...
  2. Msambichaka Mkinga

    Mabadiliko Makubwa yanahitajika. Rais Samia 2025 apitishwe ili Kusimamia Mabadiliko

    Hakuna shaka hata kidogo kuwa Taifa letu hili linahitaji mabadiliko makubwa ya kutengeneza mifumo itakayoishi na kudumu, kwa kuanzia na katiba mpya. Kwa Katiba yetu ya sasa, mtu mmoja aitwaye Rais, kwa madaraka makubwa kupindukia aliyopewa na katiba, asipotaka, hakuna kinachoweza kufanyika...
  3. Msambichaka Mkinga

    Serikalini tuna Wachumi wasiojua Uchumi?

    Kwa namna tunavyoenda, hakika nchi hii tutaendelea kunung'unika na kulaumiana milele na kuwataja wenzetu wa mahali pengine Duniani wanavyosonga mbele. Sababu mojawapo kubwa ni kwamba hatutaki kuishi kwa kufuata kanuni za maendeleo ya uchumi. Ukitaka uchumi wa nchi au hata wa kwako binafsi...
  4. Msambichaka Mkinga

    Ujenzi wa Barabara tutumie Makampuni yenye teknolojia sahihi lakini ihusishe Technology Transfer

    Watanzania kwa kiasi kikubwa inaingizwa hasara kubwa na makampuni ya China. Kwa asilimia kubwa barabara nyingi zimejengwa na makampuni ya Kichina. Barabara hizi hazieleweki kama ujenzi wake haujakamilika au ulikwishakamilika, maana huku zinaendelea kujengwa, walikoanzia tayari zinakuwa kwenye...
  5. Msambichaka Mkinga

    Mfumo mzima wa uchaguzi wa Tanzania umelenga udanganyifu

    Tanzania, kiuhalisia, tumekuwa tukifanya demokrasia ya maigizo, demokrasia iliyokosa ingridients za demokrasia. Mfumo mzima unakosa uhalali wa demokrasia ya kweli: 1) Tume ya uchaguzi inateuliwa na kiongozi wa chama, yaani Tume ya uchaguzi inateuliwa na kiongozi wa chama kimojawapo...
  6. Msambichaka Mkinga

    Serikali kuongeza kodi na kuzipa majina tofauti ni kuuhadaa umma

    Kuna nchi zina kodi moja tu. Halafu kuna nchi zina sheria iliyoweka ukomo wa kodi. Bahati mbaya sana kwa Tanzania, tuna mfumo laghai wa kodi. Serikali huweza kuwadanfanya wananchi eti imepunguza kiwango fulani cha kodi wakati kiuhalisia inakuwa imeongeza kodi. Kwa mfano inaweza kutamka kuwa...
  7. Msambichaka Mkinga

    Mfumo Unaotumika Kwenye Sensa ni Uharibifu wa Fedha na Hauna Ufanisi

    Hakuna mtu anayeweza kuhoji umuhimu wa sensa. Wakristo wanakumbuka, kwa kadiri ya maandiko matakatifu ya Biblia, Mama Maria na Mt. Joseph walienda Betlehem kwaajili ya sensa, ni katika tukio hillo, Yesu Kristo Masihi ndiyo anazaliwa. Hivyo umuhimu wa sensa ulionekana hata kabla ya nyakati za...
  8. Msambichaka Mkinga

    Tozo zinaweza kugeuka na kuwa wizi wa dola dhidi ya Wananchi

    Msingi wa kodi, tozo au ushuru ni mapato. Kutokana na mapato uliyoyaingiza, sehemu ya hayo mapato, wewe uliyeingiza unastahili kutoa sehemu ya hayo mapato kama kodi, ushuru, tozo au jina jingine lolote utakalopenda kuita lenye lengo la makato yanayyoenda kwenye mamlaka za serikali. Hii ni kanuni...
  9. Msambichaka Mkinga

    Tanzania ya Maridhiano ni Ushindi wa Watanzania

    Tupo katika kipindi cha kuliponya Taifa, kutafuta maridhiano ya kitaifa, kuujenga na kuumirisha umoja wa kitaifa. Katika kufika hapo, wapo majemedari wa mstari wa mbele. Katika kufika hapo, wapo walioumia, walioteseka, waliotoa uhai, waliopotezwa, n.k. Lakini tukitaka kuwa washindi wa kweli...
  10. Msambichaka Mkinga

    Kuna nafasi nzuri zaidi ya kujenga Taifa linalozingatia haki na Rais Samia

    Ukiyatazama yaliyofanyika wakati wa Samia, ukiacha doa kubwa la kesi ya inayoaminika ni ya kumbambikia Mbowe na makomandoo, kuna nafasi nzuri zaidi ya kuijenga Tanzania ya haki na demokrasia, katika utawala huu wa Samia, pengine kuliko utawala wa mwingine yeyote. Kuna mengi positive yamefanyika...
  11. Msambichaka Mkinga

    Polepole, jambazi anapoweza kufundisha ustaarabu

    Hivi karibuni, hata bila ya kutumia ufahamu mkubwa, kuna mambo yaliyo dhahiri: 1) Polepole haamini kama Mama Samia ni mtu sahihi kwa nafasi yake kama Rais. Ukosoaji wake mkubwa ameuelekeza kwa Rais. 2) Polepole ana mashaka makubwa kuwa ama kuna siku atafikishwa kwenye vyombo vya sheria kujibu...
  12. Msambichaka Mkinga

    Rais Samia alifanya kosa la kiufundi

    Katiba yetu inasema wazi kuwa Rais atakoma kuwa Rais mara anapofariki. Dakika ile anapofariki tu, Urais wake umeishia pale. Hafi, akiwa umeubakiza Urais nyuma kiasi cha kuweza kukasimisha kwa mtu mwingine. Rais akifa, Katiba yetu inasema kuwa aliyekuwa Makamu wake, ataapishwa kuwa Rais. Atakuwa...
  13. Msambichaka Mkinga

    Tanganyika ya 1958 Ilikuwa na Demokrasia zaidi ya Tanzania ya leo

    Maendeleo ya nchi yoyote na hata mtu binafsi ni mabadiliko chanya ya wakati husika, ukilinganisha na ilivyokuwa kabla ya kipindi kinachofanyiwa tathmini. Maendeleo kwa Taifa, huangalia uchumi (wa nchi na wananchi wake), demokrasia, haki na uhuru (huangaliwa sheria, mifumo na utekelezaji wake)...
  14. Msambichaka Mkinga

    Rais Samia: Uchumi Hauwezi Kusimama kwa Kutegemea Ushauri wa Watu Wanafiki

    Mtu mnafiki amelaaniwa Duniani na Mbinguni. Na amtegemeaye mnafiki kamwe hawezi kufanikiwa. Kwa mujibu wa katiba, chombo cha kwanza cha kumshauri Rais ni Baraza la Mawaziri. Rais anatakiwa kujiuliza, hawa wanaounda Baraza la mawaziri ni watu wa namna gani? Rais ili afanikiwe katika uongozi...
  15. Msambichaka Mkinga

    Serikali Ina Wachumi wa Vyeti, Imekosa Wachumi Halisia?

    Katika ujenzi wa uchumi, ili uweze kufanikiwa na kusonga mbele kwa haraka ni lazima uzitambue: Sekta wezeshi Sekta muhimu Sekta kipaumbele Ukikosa uelewa huo, unaweza ukawa unapanga mipango yako, ukiamini umepanga ili kusonga mbele kumbe umepanga ili kurudi nyuma, kubakia mahali ulipo, au...
  16. Msambichaka Mkinga

    Samia Rais wa Ustawi

    Katika Taifa moja, kuna wakati watu waliambiwa, "Taifa hili ni tajiri. Ninyi ni matajiri". Wengi wakaamini. Wakaamini kuwa ghafla wamekuwa matajiri. Japo wengine hata kupata milo miwili ni shida, waliamini kuwa labda matajiri ndivyo wanavyoishi. Wengine japo kununua nguo mpya ni shida...
  17. Msambichaka Mkinga

    Rais saidia kuleta fikra mpya

    Umadhubuti wa Taifa unatokana na kukamilika kwa jamii. Ukamilifu wa Taifa unatokana na uwepo wa watu wenye fikra, uwezo, vipaji na weledi wa aina mbalimbali. Kila mmoja katika mchanganyiko huo wa wananchi, akitumika na kuchangia kikamilifu, mchango wake ndiyo huleta maendeleo katika Taifa. Na...
  18. Msambichaka Mkinga

    Mh. Rais Magufuli - Haya Ndiyo Tulikuwa Tunayataka

    Kuna hatua/kauli kadhaa ambazo Mh Rais Magufuli alizifanya/alizitamka, wengi zilitukwaza. Hazikutukwaza kwa sababu hatupendi kuzisikia bali tulijua athari zake katika uchumi wetu na maisha yetu kama wananchi tunaoipenda nchi yetu. Sina sababu ya kuzirejea hizo hatua au zile kauli ambazo...
  19. Msambichaka Mkinga

    Rais Jukumu lako la Msingi ni Kulinda Umoja wa Kitaifa

    Sikumbuki tarehe wala kikao gani cha chama lakini nakumbuka wakati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere akisisitiza dhana ya kukosoana ndani ya chama, aliwahi kutamka, 'Kukubali upungufu huu siyo kujidhalilisha bali ni kujiimarisha'. Mheshimiwa Rais ukitaka kuwa kiongozi mzuri, imarisha na kuikubali...
  20. Msambichaka Mkinga

    Serikali ya Tanzania Haiwezi Kuendesha Uchumi Wala Biashara

    Katika baadhi ya mataifa, serikali ndiyo huwa sababu ya biashara na uchumi kushamiri. Kwa Tanzania, serikali huwa ni chanzo cha biashara na uchumi kusinyaa. Na hayo husababishwa na sera, sheria na usimamizi usio rafiki wa uchumi na biashara. Tatizo ni nini? Huenda nisiwe sahihi kwa 100% lakini...
Back
Top Bottom