Msambichaka Mkinga
JF-Expert Member
- Oct 22, 2015
- 1,649
- 2,911
Tupo katika kipindi cha kuliponya Taifa, kutafuta maridhiano ya kitaifa, kuujenga na kuumirisha umoja wa kitaifa. Katika kufika hapo, wapo majemedari wa mstari wa mbele. Katika kufika hapo, wapo walioumia, walioteseka, waliotoa uhai, waliopotezwa, n.k.
Lakini tukitaka kuwa washindi wa kweli, tusamehe bila kusahau, tuaminiane, kuna wakati pande zilizokuwa zinasigana, kila upande ujishushe ili kuwa katika level nzuri. Najua kuna hardliners pande zote - CCM na CHADEMA. Lakini ukweli ni kwamba, kama kila upande ukishikilia msimamo wake katika mambo inayoyataka, na kutaka kupata yote kwa 100% kwa muda unaotaka, kwa wakati unaotaka, na kwa namna uunavyotaka, hatushindi.
Nchi imefika katika hatua nzuri. Watanzania, kila siku tunazidi kupata points 3, na katika haya mapambano, tuna majemedari waliokaa mbele kutuongoza, ni Rais wetu Mh. Rais Samia na Mh. Freeman Mbowe (pole sana kwa mateso, lakini ufurahi kwa kuwa umeteseka kwaajili ya watanzania. Ni sawa na mama anayelia kwa uchungu wa operation ya uzazi, lakini umwonapo mtoto, huyasahau mateso yake, na kufurahia ujio wa mwanae. Mungu akujalie ujasiri ya kuyapokea uliyoyapitia kwa moyo wa hekima).
Mh. Rais Samia na Mh. Freeman Mbowe, ninyi ni dira. Mkisimama pamoja kwaajili ya lengo moja la kutaka kuijenga Tanzania ya ushindani lakini inayozingatia umoja, upendo, na uzalendo kwa Taifa na watu wake, walio nyuma yenu, nao hakika watatembea katika njia yenu.
Watanzania tumechoshwa na siasa zisizo na tija, siasa za kukomoana, siasa za hila, siasa za chuki, tunataka mawazo kinzani lakini yasiyoondoa upendo miongoni mwetu, umoja miongoni mwetu, na uzalendo kwa Taifa letu. Kwa upande wa Rais Samia na CCM,
nahitaji sana hekima kwa sababu mna dola. Ni rahisi sana kwenu kukosa hekima na kutumia nguvu za dola, kwa sababu mamlaka, hupofushwa, lakini mkiwa na hekima, dola itawapa nafasi nzuri zaidi ya kuyapata mawazo chanya ya kulijenga Taifa la mfano, na ndicho tunachokitaka tulio wengi.
Mungu aliye chanzo cha kila jema, tunakuomba uwajaze hekima waliopata nafasi ya kuwa viongozi ili walitazame zaidi Taifa kuliko vyama na nafsi zao. Viongozi wetu wanaposimama kwaajili ya yaliyo mema kwa Taifa letu, uwajaze ujasiri wa kutokubali kuyumbishwa na mawakala wa ibilisi, wanaofurahia Tanzania ya uonevu na utengano.
Lakini tukitaka kuwa washindi wa kweli, tusamehe bila kusahau, tuaminiane, kuna wakati pande zilizokuwa zinasigana, kila upande ujishushe ili kuwa katika level nzuri. Najua kuna hardliners pande zote - CCM na CHADEMA. Lakini ukweli ni kwamba, kama kila upande ukishikilia msimamo wake katika mambo inayoyataka, na kutaka kupata yote kwa 100% kwa muda unaotaka, kwa wakati unaotaka, na kwa namna uunavyotaka, hatushindi.
Nchi imefika katika hatua nzuri. Watanzania, kila siku tunazidi kupata points 3, na katika haya mapambano, tuna majemedari waliokaa mbele kutuongoza, ni Rais wetu Mh. Rais Samia na Mh. Freeman Mbowe (pole sana kwa mateso, lakini ufurahi kwa kuwa umeteseka kwaajili ya watanzania. Ni sawa na mama anayelia kwa uchungu wa operation ya uzazi, lakini umwonapo mtoto, huyasahau mateso yake, na kufurahia ujio wa mwanae. Mungu akujalie ujasiri ya kuyapokea uliyoyapitia kwa moyo wa hekima).
Mh. Rais Samia na Mh. Freeman Mbowe, ninyi ni dira. Mkisimama pamoja kwaajili ya lengo moja la kutaka kuijenga Tanzania ya ushindani lakini inayozingatia umoja, upendo, na uzalendo kwa Taifa na watu wake, walio nyuma yenu, nao hakika watatembea katika njia yenu.
Watanzania tumechoshwa na siasa zisizo na tija, siasa za kukomoana, siasa za hila, siasa za chuki, tunataka mawazo kinzani lakini yasiyoondoa upendo miongoni mwetu, umoja miongoni mwetu, na uzalendo kwa Taifa letu. Kwa upande wa Rais Samia na CCM,
nahitaji sana hekima kwa sababu mna dola. Ni rahisi sana kwenu kukosa hekima na kutumia nguvu za dola, kwa sababu mamlaka, hupofushwa, lakini mkiwa na hekima, dola itawapa nafasi nzuri zaidi ya kuyapata mawazo chanya ya kulijenga Taifa la mfano, na ndicho tunachokitaka tulio wengi.
Mungu aliye chanzo cha kila jema, tunakuomba uwajaze hekima waliopata nafasi ya kuwa viongozi ili walitazame zaidi Taifa kuliko vyama na nafsi zao. Viongozi wetu wanaposimama kwaajili ya yaliyo mema kwa Taifa letu, uwajaze ujasiri wa kutokubali kuyumbishwa na mawakala wa ibilisi, wanaofurahia Tanzania ya uonevu na utengano.