Serikali ya Tanzania Haiwezi Kuendesha Uchumi Wala Biashara

Msambichaka Mkinga

JF-Expert Member
Oct 22, 2015
1,649
2,911
Katika baadhi ya mataifa, serikali ndiyo huwa sababu ya biashara na uchumi kushamiri. Kwa Tanzania, serikali huwa ni chanzo cha biashara na uchumi kusinyaa. Na hayo husababishwa na sera, sheria na usimamizi usio rafiki wa uchumi na biashara. Tatizo ni nini? Huenda nisiwe sahihi kwa 100% lakini ninaamini kwa kiasi kikubwa kuwa uchumi na biashara kwa tanzania unasimamiwa na watu wasioujua uchumi wala biashara.

Kwa Tanzania, anayeujua uchumi na biashara ni mtu mwenye vyeti vingi au hata PhD za kusomea uchumi na biashara. Hii inaweza pia kuwa ni sababu kubwa hata Rais wetu leo hii kuwajaza maprofesa na madaktari kwenye serikali yake akiamini kuwa atapata ufanisi. Kitu ambacho amesahau kuwa unaweza kuwa na maprofesa na madaktari wenye vyeti vingi vya biashara na uchumi lakini wasiojua uchumi wala biashara. Kuna watu wanaujua uchumi na biashara, kwa vile wanauishi uchumi na biashara, wanatenda/wanafanya shughuli za uchumi na biashara, wanauchunguza uchumi na biashara kila siku, na maisha yao yamejaa mafanikio katika uchumi na biashara. Ili kuyajua wanaoyajua hawa wanauchumi na wafanyabiashara halisi, wataalam nadharia wa uchumi na biashara (professors na PhD holders), wanalazimika kuingia darasanai kujifunza nadharia ambayo wachumi na wafanyabiashara halisi wanaishi na kuifanyia kazi.

Serikali ya Tanzania haijawahi kufanikiwa kwa lolote katika miradi ya uchumi na biashara lakini bado inaamini ina uwezo thabiti katika nyanja hizo. Serikali kwa kipindi kirefu imethibitisha pasipo hata chembe ya mashaka kuwa haiwezi kusimamia na kuendesha mradi wowote wa kibiashara na kiuchumi.

Serikali ya Tanzania inatakiwa iache masuala yote ya kibiashara na kiuchumi kwa sekta binafsi, na wasiingilie kama wanavyofanya hivi sasa. Hii inatokana na ukweli tuliopata kwa kipindi kirefu. Baadhi hapa chini ni mifano tu:

1) Migodi
Serikali ya Tanzania iliitafisha migodi ya madini yote toka kwa makampuni binafsi miaka ya sitini baada ya Azimio la Arusha. Baada ya hapo migodi ya dhahabu, Mica, Lead, Copper na Zinc, chini ya STAMICO, yote ilikufa. Mpaka miaka ya 1990, Tanzania ilikuwa inauza dhahabu inayochokonolewa na wachimbaji wadogo tu. Migodi ya serikali ilikuwa haizalishi hata kilo 1 ya dhahabu. Ni makampuni binafsi walioitoa Tanzania kutoka uzalishaji sifuri wa dhahabu mpaka kuwa nchi ya 3 kwa uzalishaji wa dhahabu barani Afrika mwanzoni mwa miaka 2000. Mgodi wa Bulyanhulu pekee, kwa wakati ule uliweza kutoa makusanyo ya kodi mbalimbali 98% ya makusanyo yote ya kodi katika mkoa. Ikumbukwe nyuma kidogo serikali ya Tanzania ilikuwa inashindwa hata kulipa mishahara ya wafanyakazi wake kwa wakati.

2) Kilimo
Kabla ya mashamba makubwa ya mkonge kutaifishwa, Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza kwa uzalishaji wa katani, na huku ikiwa mzalishaji mkubwa wa pamba, kahawa, chai, n.k. Utaifishaji wa mashamba hayo uliifanya Tanzania kupotea kabisa katika ramani ya Dunia katika uzalishaji wa mazao mbalimbali

3) Biashara za Bidhaa Muhimu
Miaka ya 1980 mwanzoni serikali iliamua kuendesha biashara ya maduka yenyewe, maduka ya RTC. Kwenye maduka haya, ukiritimba wa ajabu ulijengeka na kusababisha kushamiri kwa rushwa. Wenye kauli kwenye biashara hizi waligeuka kuwa ni mawaziri, wakuu wa mikoa, n.k. Wakazi wa maeneo, majina yao yaliandikwa kwenye daftari, na wewe kama siyo mkazi wa eneo husika, huwezi kupata bidhaa muhimu kama sukari, sabuni, sembe, bia, kanga, n.k. Na hata hao wakazi wa maeneo walipangiwa kiasi cha mwisho cha kuweza kununua. Ni sekta binafsi ndiyo iliyosababisha, siyo kupatikana kwa bidhaa hizo tu, bali kutoka kusukumwa kwenye foleni ya kununua sabuni mpaka hatua ya kushawishiwa ununue sababuni au nguo fulani kwa kuwa ina ubora, tena ukiwa nyumbani kwako ukitazama TV.

4) Huduma za Simu
Wakati biashara ya simu ikiendeshwa na serikali, ili kuunganishiwa tu simu upate kuongea, kuna wakati ilihitajika kufahamiana na operator au ilihitaji kumpa chochote. Kuna wakati pamoja na yote hayo, ilihitajika kukaa nje ya kiboksi cha TTCL zaidi ya masaa 12 kusubiria kuunganishiwa simu. Sekta binafsi ilipoingia, leo yamejaa matangazo tele ya kutushawishi wakati wote tutumie simu, na TTCL ikiendelea kufaidi uzoefu wa serikali katika kuendesha biashara ambao ni kuua biashara

5) Viwanda
Serikali hii iliwahi kutaka kufanya biashara ya viwanda. Tukawa na viwanda vya kuunganisha magari na matrekta, viwanda vya baiskeli, bia, sigara, soda, sukari, chumvi, viatu, matairi, nguo, zana za kilimo, sabuni, mafuta ya kupikia, majiko ya kupikia, maturubai, redio, n.k. Mafanikio ya viwanda hivyo yanafamika, lakini baadhi ni pamoja na watu kukamatwa na kusweka ndani kwa biashara ya magendo ya kuuza pakiti ya sigara au kreti la bia. Leo watu siyo tu wanaweza kupata sabuni, bia, sukari, kwa kiasi chochote, wakati wowote na mahali popote, lakini pia wametoka kutoka kwenye foleni za kugombania bidhaa mpaka kubembelezwa wanunue bidhaa. Nilishangaa sana niliposikia eti serikali inataka kuanza kufufua baadhi ya viwanda ili vijiendeshe. Nikasema kweli sikio la kufa halisikii dawa!

Nimeandika haya machache kuthibitisha tu kuwa serikali hii ya Tanzania haina uwezo hata chembe wa kuendesha uchumi wa kibiashara. Tunaposema serikali haina uwezo wa kuendesha biashara maana yake ni kuwa maofisa wa serikali kwa umoja wao hawana uwezo wa kuendesha uchumi wa kibiashara. Na ndiyo maana hata wengi wao wanapokoma kuwa maofisa wa serikali, wanapoanzisha biashara, hazifiki popote. Laiti kama maofisa wa serikali wangekuwa na uwezo wa kuendesha uchumi wa kibiashara, basi miradi inayosimamiwa na taasisi za serikali ndiyo ingekuwa miradi ya mfano kwa ustawi. Lakini ukweli ni kuwa miradi ya serikali ndiyo imekuwa mifano mizuri kwa ubovu wa uendeshaji na utengenezaji hasara. Tazama ufanisi wa kampuni kama:

1) TANESCO
Hawa wanapewa ruzuku, ni watoaji huduma pekee wa bidhaa muhimu ya nishati ya umeme, hawana mshindani. Shirika hili halijawahi kutengeneza faida wala halijawahi kuwa na ufanisi hata katika huduma yenyewe. Leo hii nchi nzima, TANESCO hawawezi kumuunganishia mteja mpya umeme hata angalao ndani ya mwezi mmoja tangu alipokamilisha malipo. Karibuni nimeongea na Meneja wa umeme Ilemela, Mwanza anasema wamesimama kuwaunganishia umeme wateja wapya kwa sababu hawana nguzo, na nguzo zikija wataanza kuunganisha wateja walioleta maombi mwezi wa nane, mwakajana. Ukienda katika uhalisia, watu wnaoshindwa hata kupata nguzo tu za miti, wanaweza kuendesha uchumi wa kibiashara? Hivi ingekuwa TANESCO ni kampuni binafsi, ingeweza kutokea hata siku moja ya kukosa nguzo? Mimi nina imani TANESCO ingekuwa ni kampuni binafsi, wanaojenga nyumba huenda wangekuwa wanafuatwa tangu nyumba ikiwa katika hatua ya msingi, na wasingelipia hata pesa ya nguzo. Kama serikali inashindwa kuisimamia tu TANESCO iliyoachiwa soko lote, itaweza kusimamia biashara mathalani ya anga ambako kuna washindani binafsi? Sitarajii kabisa.

2) TTCL
Hii kampuni kwa miaka mingi ilifurahia soko lisilo na ushindani lakini halina dalili ya kutembea. Ni shirika mfu. Serikali imeshindwa kuliendesha shirika hili kibiashara lakini serikali hiyo hiyo inaamini ina uwezo mkubwa sana wa kusimamia miradi ya wawekezaji.

UJUMBE KWA SERIKALI
1) Serikali kama inataka ifanikiwe kujenga uchumi wa Tanzania ni lazima iingie darasani kujifunza uchumi wa kibiashara. Na walimu wazuri siyo watu waliojaza makaratasi ya nadharia ya uchumi bali ijifunze kwa wanaouishi uchumi wa kibiashara, watu au taasisi zilizofanikiwa. Tuna wasomi wa nadharia wengi ambao hawawezi hata kuendesha biashara ya genge kwa faida. Ukitaka kuendesha biashara ya genge, mwalimu mzuri ni yule aliyefanikiwa kuanzisha genge, likapata faida, na baadaye likageuka kuwa duka au hoteli. Wataalam wa nadharia ya uchumi na biashara watumike tu kukusanya na kuyaweka pamoja mawazo na ushauri wa wanaouishi uchumi.

2) Serikali ikubali na itambue kuwa haina uwezo wa kusimamia uchumi. Kukosa uwezo huo ndio uliofanya miradi yote ya kibishara chini ya serikali kufa. Uliyeshindwa kuendesha miradi yako huwezi kuwa msimamizi mzuri wa miradi ya wengine, bali unaweza kuwa mwanafunzi mzuri maana unaujua uchungu wa kushindwa.

3) Serikali ijue namna ya kulinda mazingira ya uchumi wa kibiashara. Kauli tu ya serikali na hasa Rais ina uwezo wa kuua uchumi. Wanaofuatilia masuala ya uchumi wanafahamu. Siku ile tu Rais aliposema anazuia mchanga wa dhahabu wa kampuni ya Acacia kwenda nje, hisa za kampuni ya Acacia kwenye masoko ya fedha zilianguka kwa 20% (mamilioni ya dola yalipotea kwa usiku moja), makampuni yote ya madini yaliyowekeza Tanzania, hisa zao kwenye masoko ya fedha zilianguka. Makampuni yanayojenga miradi ya graphite, na yale yanayofanya utafiti wa madini ya Nickel, nayo yaliathirika sana maana na yenyewe yanategemea kusafirisha unfinished products yatakapoanza uzalishaji. Lakini pia kwa kiongozi mkuu kusema kampuni inaliibia Taifa, ni kauli nzito sana, na hasa inapotolewa wakati hakuna hata utafiti au uthibitisho maana kamati za kuchunguza zimeundwa baada ya kauli.

4) Uchumi ni Sayansi yenye miiko yake, ambayo kwa kiasi kikubwa serikali ya tanzania inaonekana kutokutambua lakini ikiamini kuwa inafahamu sana. Serikali ya Tanzania haijajua bado kuwa hela ya serikali (kodi) ni pesa ya wananchi, siyo ya serikali. Wananchi ndiyo walioitafuta, wakaigawia serikali kwa utaratibu/sheria zilizokubaliwa kwa njia ya kodi. Serikali ni lazima iitumie fedha hiyo kwa faida ya aliyeitoa ili aweze kuendelea kutoa zaidi. Ni loop ambayo haitakiwi kukatika. Mwananchi atoe kodi, kodi iende serikalini, serikali irudishe fedha kwa walipa kodi, walipa kodi wazalishe, sehemu ya faida waipatie serikali; mzunguko unaendelea. Kuchukua fedha kwa walipa kodi na kwenda kuifungia BOT, ni serikali kuamua kujinyonga yenyewe na kuwanyonga walipa kodi kiuchumi.

Serikali kila mara inaomba ushauri, huu ni sehemu ya ushauri, na kuonesha wanashaurika, wanastahili kutupa mrejesho ili tujue kuwa ushauri unapokelewa au hapana. Tunafanya hivi kwa kuamini kuwa kauli za Mh. Rais kuwa urais ni wa kwake, fomu alichukua mwenyewe bila ya kushauriwa na mtu, na hivyo halazimiki kufuata ushauri wa mtu, ilikuwa ni kauli ya kuteleza maana tukiizingatia hasa kauli hiyo kimantiki, ni kuwa hatuhitajiki kushauri lolote.
 
Unakuta serikali imesaini mkataba na mgodi wa kupeleka mchanga wa Dhahabu nje,mkataba haujavunjwa,ni halali,anatokea mtu ambaye hata hakuweka signature anausitisha tena bila kutumia mechanism za kutatua matatizo ambazo ziko kwenye mkataba.


Anajua kuwa yeye ndio katoa leseni za kuzalisha viroba,anajua viwanda vinaendelea na uzalishaji na wana stock kubwa kwenye maghala,anajua wafanyabiashara mitaani pia wana stock kubwa,anaamka huko alikolala,anapiga marufuku bila kujali kuna watu tayari wana mzigo,hajui kwamba ilihitajika notisi ya muda wa kutosha.


Anaamka mtu anaondoa hela zote benki za mtaani na kupeleka benki kuu ambako hazina mzunguko,zimekaa tu.

Anaamka mtu badala ya kutoa formula ya jinsi gani wananchi watapata fedha,yeye anawaahidi kwamba hawatapata fedha,na zitakauka mfukoni.


Anaamka mtu hajui hili wala lile kuhusu biashara ya sukari,anaenda anaivurugaaaaaaa,mwishowe mpaka leo sokoni bei juu.

Anaibuka mtu anaenda na vurugu zake bandarini......mpaka jamii ya wafanyabiashara inapata hofu wanakimbia.

Anaibuka mtu akishangilia na kucheka baada ya kusikia biashara ya usafirishaji kwa malori inaelekea kufa eti kaokoa barabara.

Anaibuka mtu anasema anajenga viwanda wakati sekta ya Kilimo iko hoi,na bajeti haina mwelekeo wa nini kifanywe wapi
 
Katika baadhi ya mataifa, serikali ndiyo huwa sababu ya biashara na uchumi kushamiri. Kwa Tanzania, serikali huwa ni chanzo cha biashara na uchumi kusinyaa. Na hayo husababishwa na sera, sheria na usimamizi usio rafiki wa uchumi na biashara. Tatizo ni nini? Huenda nisiwe sahihi kwa 100% lakini ninaamini kwa kiasi kikubwa kuwa uchumi na biashara kwa tanzania unasimamiwa na watu wasioujua uchumi wala biashara.

Kwa Tanzania, anayeujua uchumi na biashara ni mtu mwenye vyeti vingi au hata PhD za kusomea uchumi na biashara. Hii inaweza pia kuwa ni sababu kubwa hata Rais wetu leo hii kuwajaza maprofesa na madaktari kwenye serikali yake akiamini kuwa atapata ufanisi. Kitu ambacho amesahau kuwa unaweza kuwa na maprofesa na madaktari wenye vyeti vingi vya biashara na uchumi lakini wasiojua uchumi wala biashara. Kuna watu wanaujua uchumi na biashara, kwa vile wanauishi uchumi na biashara, wanatenda/wanafanya shughuli za uchumi na biashara, wanauchunguza uchumi na biashara kila siku, na maisha yao yamejaa mafanikio katika uchumi na biashara. Ili kuyajua wanaoyajua hawa wanauchumi na wafanyabiashara halisi, wataalam nadharia wa uchumi na biashara (professors na PhD holders), wanalazimika kuingia darasanai kujifunza nadharia ambayo wachumi na wafanyabiashara halisi wanaishi na kuifanyia kazi.

Serikali ya Tanzania haijawahi kufanikiwa kwa lolote katika miradi ya uchumi na biashara lakini bado inaamini ina uwezo thabiti katika nyanja hizo. Serikali kwa kipindi kirefu imethibitisha pasipo hata chembe ya mashaka kuwa haiwezi kusimamia na kuendesha mradi wowote wa kibiashara na kiuchumi.

Serikali ya Tanzania inatakiwa iache masuala yote ya kibiashara na kiuchumi kwa sekta binafsi, na wasiingilie kama wanavyofanya hivi sasa. Hii inatokana na ukweli tuliopata kwa kipindi kirefu. Baadhi hapa chini ni mifano tu:

1) Migodi
Serikali ya Tanzania iliitafisha migodi ya madini yote toka kwa makampuni binafsi miaka ya sitini baada ya Azimio la Arusha. Baada ya hapo migodi ya dhahabu, Mica, Lead, Copper na Zinc, chini ya STAMICO, yote ilikufa. Mpaka miaka ya 1990, Tanzania ilikuwa inauza dhahabu inayochokonolewa na wachimbaji wadogo tu. Migodi ya serikali ilikuwa haizalishi hata kilo 1 ya dhahabu. Ni makampuni binafsi walioitoa Tanzania kutoka uzalishaji sifuri wa dhahabu mpaka kuwa nchi ya 3 kwa uzalishaji wa dhahabu barani Afrika mwanzoni mwa miaka 2000. Mgodi wa Bulyanhulu pekee, kwa wakati ule uliweza kutoa makusanyo ya kodi mbalimbali 98% ya makusanyo yote ya kodi katika mkoa. Ikumbukwe nyuma kidogo serikali ya Tanzania ilikuwa inashindwa hata kulipa mishahara ya wafanyakazi wake kwa wakati.

2) Kilimo
Kabla ya mashamba makubwa ya mkonge kutaifishwa, Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza kwa uzalishaji wa katani, na huku ikiwa mzalishaji mkubwa wa pamba, kahawa, chai, n.k. Utaifishaji wa mashamba hayo uliifanya Tanzania kupotea kabisa katika ramani ya Dunia katika uzalishaji wa mazao mbalimbali

3) Biashara za Bidhaa Muhimu
Miaka ya 1980 mwanzoni serikali iliamua kuendesha biashara ya maduka yenyewe, maduka ya RTC. Kwenye maduka haya, ukiritimba wa ajabu ulijengeka na kusababisha kushamiri kwa rushwa. Wenye kauli kwenye biashara hizi waligeuka kuwa ni mawaziri, wakuu wa mikoa, n.k. Wakazi wa maeneo, majina yao yaliandikwa kwenye daftari, na wewe kama siyo mkazi wa eneo husika, huwezi kupata bidhaa muhimu kama sukari, sabuni, sembe, bia, kanga, n.k. Na hata hao wakazi wa maeneo walipangiwa kiasi cha mwisho cha kuweza kununua. Ni sekta binafsi ndiyo iliyosababisha, siyo kupatikana kwa bidhaa hizo tu, bali kutoka kusukumwa kwenye foleni ya kununua sabuni mpaka hatua ya kushawishiwa ununue sababuni au nguo fulani kwa kuwa ina ubora, tena ukiwa nyumbani kwako ukitazama TV.

4) Huduma za Simu
Wakati biashara ya simu ikiendeshwa na serikali, ili kuunganishiwa tu simu upate kuongea, kuna wakati ilihitajika kufahamiana na operator au ilihitaji kumpa chochote. Kuna wakati pamoja na yote hayo, ilihitajika kukaa nje ya kiboksi cha TTCL zaidi ya masaa 12 kusubiria kuunganishiwa simu. Sekta binafsi ilipoingia, leo yamejaa matangazo tele ya kutushawishi wakati wote tutumie simu, na TTCL ikiendelea kufaidi uzoefu wa serikali katika kuendesha biashara ambao ni kuua biashara

5) Viwanda
Serikali hii iliwahi kutaka kufanya biashara ya viwanda. Tukawa na viwanda vya kuunganisha magari na matrekta, viwanda vya baiskeli, bia, sigara, soda, sukari, chumvi, viatu, matairi, nguo, zana za kilimo, sabuni, mafuta ya kupikia, majiko ya kupikia, maturubai, redio, n.k. Mafanikio ya viwanda hivyo yanafamika, lakini baadhi ni pamoja na watu kukamatwa na kusweka ndani kwa biashara ya magendo ya kuuza pakiti ya sigara au kreti la bia. Leo watu siyo tu wanaweza kupata sabuni, bia, sukari, kwa kiasi chochote, wakati wowote na mahali popote, lakini pia wametoka kutoka kwenye foleni za kugombania bidhaa mpaka kubembelezwa wanunue bidhaa. Nilishangaa sana niliposikia eti serikali inataka kuanza kufufua baadhi ya viwanda ili vijiendeshe. Nikasema kweli sikio la kufa halisikii dawa!

Nimeandika haya machache kuthibitisha tu kuwa serikali hii ya Tanzania haina uwezo hata chembe wa kuendesha uchumi wa kibiashara. Tunaposema serikali haina uwezo wa kuendesha biashara maana yake ni kuwa maofisa wa serikali kwa umoja wao hawana uwezo wa kuendesha uchumi wa kibiashara. Na ndiyo maana hata wengi wao wanapokoma kuwa maofisa wa serikali, wanapoanzisha biashara, hazifiki popote. Laiti kama maofisa wa serikali wangekuwa na uwezo wa kuendesha uchumi wa kibiashara, basi miradi inayosimamiwa na taasisi za serikali ndiyo ingekuwa miradi ya mfano kwa ustawi. Lakini ukweli ni kuwa miradi ya serikali ndiyo imekuwa mifano mizuri kwa ubovu wa uendeshaji na utengenezaji hasara. Tazama ufanisi wa kampuni kama:

1) TANESCO
Hawa wanapewa ruzuku, ni watoaji huduma pekee wa bidhaa muhimu ya nishati ya umeme, hawana mshindani. Shirika hili halijawahi kutengeneza faida wala halijawahi kuwa na ufanisi hata katika huduma yenyewe. Leo hii nchi nzima, TANESCO hawawezi kumuunganishia mteja mpya umeme hata angalao ndani ya mwezi mmoja tangu alipokamilisha malipo. Karibuni nimeongea na Meneja wa umeme Ilemela, Mwanza anasema wamesimama kuwaunganishia umeme wateja wapya kwa sababu hawana nguzo, na nguzo zikija wataanza kuunganisha wateja walioleta maombi mwezi wa nane, mwakajana. Ukienda katika uhalisia, watu wnaoshindwa hata kupata nguzo tu za miti, wanaweza kuendesha uchumi wa kibiashara? Hivi ingekuwa TANESCO ni kampuni binafsi, ingeweza kutokea hata siku moja ya kukosa nguzo? Mimi nina imani TANESCO ingekuwa ni kampuni binafsi, wanaojenga nyumba huenda wangekuwa wanafuatwa tangu nyumba ikiwa katika hatua ya msingi, na wasingelipia hata pesa ya nguzo. Kama serikali inashindwa kuisimamia tu TANESCO iliyoachiwa soko lote, itaweza kusimamia biashara mathalani ya anga ambako kuna washindani binafsi? Sitarajii kabisa.

2) TTCL
Hii kampuni kwa miaka mingi ilifurahia soko lisilo na ushindani lakini halina dalili ya kutembea. Ni shirika mfu. Serikali imeshindwa kuliendesha shirika hili kibiashara lakini serikali hiyo hiyo inaamini ina uwezo mkubwa sana wa kusimamia miradi ya wawekezaji.

UJUMBE KWA SERIKALI
1) Serikali kama inataka ifanikiwe kujenga uchumi wa Tanzania ni lazima iingie darasani kujifunza uchumi wa kibiashara. Na walimu wazuri siyo watu waliojaza makaratasi ya nadharia ya uchumi bali ijifunze kwa wanaouishi uchumi wa kibiashara, watu au taasisi zilizofanikiwa. Tuna wasomi wa nadharia wengi ambao hawawezi hata kuendesha biashara ya genge kwa faida. Ukitaka kuendesha biashara ya genge, mwalimu mzuri ni yule aliyefanikiwa kuanzisha genge, likapata faida, na baadaye likageuka kuwa duka au hoteli. Wataalam wa nadharia ya uchumi na biashara watumike tu kukusanya na kuyaweka pamoja mawazo na ushauri wa wanaouishi uchumi.

2) Serikali ikubali na itambue kuwa haina uwezo wa kusimamia uchumi. Kukosa uwezo huo ndio uliofanya miradi yote ya kibishara chini ya serikali kufa. Uliyeshindwa kuendesha miradi yako huwezi kuwa msimamizi mzuri wa miradi ya wengine, bali unaweza kuwa mwanafunzi mzuri maana unaujua uchungu wa kushindwa.

3) Serikali ijue namna ya kulinda mazingira ya uchumi wa kibiashara. Kauli tu ya serikali na hasa Rais ina uwezo wa kuua uchumi. Wanaofuatilia masuala ya uchumi wanafahamu. Siku ile tu Rais aliposema anazuia mchanga wa dhahabu wa kampuni ya Acacia kwenda nje, hisa za kampuni ya Acacia kwenye masoko ya fedha zilianguka kwa 20% (mamilioni ya dola yalipotea kwa usiku moja), makampuni yote ya madini yaliyowekeza Tanzania, hisa zao kwenye masoko ya fedha zilianguka. Makampuni yanayojenga miradi ya graphite, na yale yanayofanya utafiti wa madini ya Nickel, nayo yaliathirika sana maana na yenyewe yanategemea kusafirisha unfinished products yatakapoanza uzalishaji. Lakini pia kwa kiongozi mkuu kusema kampuni inaliibia Taifa, ni kauli nzito sana, na hasa inapotolewa wakati hakuna hata utafiti au uthibitisho maana kamati za kuchunguza zimeundwa baada ya kauli.

4) Uchumi ni Sayansi yenye miiko yake, ambayo kwa kiasi kikubwa serikali ya tanzania inaonekana kutokutambua lakini ikiamini kuwa inafahamu sana. Serikali ya Tanzania haijajua bado kuwa hela ya serikali (kodi) ni pesa ya wananchi, siyo ya serikali. Wananchi ndiyo walioitafuta, wakaigawia serikali kwa utaratibu/sheria zilizokubaliwa kwa njia ya kodi. Serikali ni lazima iitumie fedha hiyo kwa faida ya aliyeitoa ili aweze kuendelea kutoa zaidi. Ni loop ambayo haitakiwi kukatika. Mwananchi atoe kodi, kodi iende serikalini, serikali irudishe fedha kwa walipa kodi, walipa kodi wazalishe, sehemu ya faida waipatie serikali; mzunguko unaendelea. Kuchukua fedha kwa walipa kodi na kwenda kuifungia BOT, ni serikali kuamua kujinyonga yenyewe na kuwanyonga walipa kodi kiuchumi.

Serikali kila mara inaomba ushauri, huu ni sehemu ya ushauri, na kuonesha wanashaurika, wanastahili kutupa mrejesho ili tujue kuwa ushauri unapokelewa au hapana. Tunafanya hivi kwa kuamini kuwa kauli za Mh. Rais kuwa urais ni wa kwake, fomu alichukua mwenyewe bila ya kushauriwa na mtu, na hivyo halazimiki kufuata ushauri wa mtu, ilikuwa ni kauli ya kuteleza maana tukiizingatia hasa kauli hiyo kimantiki, ni kuwa hatuhitajiki kushauri lolote.
Ni awamu ya tano ambayo mfanyabiashara wa dodoma alijipiga risasi kutokana na serikali kuingilia biashara na kuzivuruga
 
Umenena vema sana mkuu, ila sasa unaowaeleza ndio shida tupu. Serikali ya Tanzania ni sawa na kichwa cha mwendawazimu...

Nchi hii bila vyeti hata kama unaujua uchumi namna gani, unakuwa hufai hata kuigwa wala kuchangia mawazo binafsi...
 
Bwana Mkubwa anawaona wafanyabiashara wote ni wapiga dili tuu,haamini mtu anaweza tajirika kwa ubunifu,juhudi na uthubutu pekee
Kasumba ya ujenzi,ukipunguza inchi moja ya lami mkandarasi anakujaza mihela kibao.
 
Mkuu umechambua vizuri sana, ila nina wasi wasi kama umejiandaa vya kutosha kukabiliana na mke wangu Lizaboni na wenzake! Nchi yetu sasa hivi tunaongozwa na akili ya kunguni!! Na ninaposikia mtu anajitapa eti tnaelekea uchumi wa viwanda huwa nashangaa sana, huwa najiuliza hii akili ya viwanda wataitoa wapi?
 
Serikali kila mara inaomba ushauri, huu ni sehemu ya ushauri, na kuonesha wanashaurika, wanastahili kutupa mrejesho ili tujue kuwa ushauri unapokelewa au hapana. Tunafanya hivi kwa kuamini kuwa kauli za Mh. Rais kuwa urais ni wa kwake, fomu alichukua mwenyewe bila ya kushauriwa na mtu, na hivyo halazimiki kufuata ushauri wa mtu, ilikuwa ni kauli ya kuteleza maana tukiizingatia hasa kauli hiyo kimantiki, ni kuwa hatuhitajiki kushauri lolote.
Mkuu Msambichaka Mkinga, kwanza asante kwa bandiko hili. Sijui kama litachangiwa sana na wengi humu kufuatia Watanzania wengi kumkubali sana rais Magufuli kuwa kila anachofanya he is right, hivyo pia wanafuata ushauri wa rais mfano kipindi bora kabisa cha TV rais wetu anachoangalia ni Shilawadu, hivyo wengi kupenda kuchangia kwa wingi topic za kishilawadu Shilawadu halafu mambo kama haya ambayo ni very serious, sidhani kama utaona wachangiaji wengi.

Niliwahi kushauri huko nyuma kuwa

Japo Beggars Can Not Be Choosers, Tuache Siasa Kwenye Uchumi. We Have to Choose Or. ..

Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT

Utumbuaji: Tuache Siasa Kwenye Professionalism, Sio Kila Mtumbuliwa ni Jipu!.

Paskali
 
Unakuta serikali imesaini mkataba na mgodi wa kupeleka mchanga wa Dhahabu nje,mkataba haujavunjwa,ni halali,anatokea mtu ambaye hata hakuweka signature anausitisha tena bila kutumia mechanism za kutatua matatizo ambazo ziko kwenye mkataba.


Anajua kuwa yeye ndio katoa leseni za kuzalisha viroba,anajua viwanda vinaendelea na uzalishaji na wana stock kubwa kwenye maghala,anajua wafanyabiashara mitaani pia wana stock kubwa,anaamka huko alikolala,anapiga marufuku bila kujali kuna watu tayari wana mzigo,hajui kwamba ilihitajika notisi ya muda wa kutosha.


Anaamka mtu anaondoa hela zote benki za mtaani na kupeleka benki kuu ambako hazina mzunguko,zimekaa tu.

Anaamka mtu badala ya kutoa formula ya jinsi gani wananchi watapata fedha,yeye anawaahidi kwamba hawatapata fedha,na zitakauka mfukoni.


Anaamka mtu hajui hili wala lile kuhusu biashara ya sukari,anaenda anaivurugaaaaaaa,mwishowe mpaka leo sokoni bei juu.

Anaibuka mtu anaenda na vurugu zake bandarini......mpaka jamii ya wafanyabiashara inapata hofu wanakimbia.

Anaibuka mtu akishangilia na kucheka baada ya kusikia biashara ya usafirishaji kwa malori inaelekea kufa eti kaokoa barabara.

Anaibuka mtu anasema anajenga viwanda wakati sekta ya Kilimo iko hoi,na bajeti haina mwelekeo wa nini kifanywe wapi
zamani jeshini kulikuwa na wimbo wa tarumbeta ukipigwa (pamparara papaaapa, chungulia pipaa...) ikiitwa bigula ukiisikia unajua saa ya kusanyiko la chakula tayari.... Siku hizi tunatwaliwa na kauli za mihemko bila kujua taratibu wala alama za nyakati!

Mkuu ungemalizia na "kisha wanajitokeza watu badala ya kuona jahazi tulilomo linatobolewa wao wanashangilia kwa vifijo na oyeee nyingiii!!! bila kujali kuwa likizama na wao hawana maboya ya kuelea.... wala hawakujiandaa"

Hakika shangwe zao ndio mauti yetu na kizazi chao!
 
The guy is taking us back 35 years. Kidumu cha Mapinduzi na Idumu fikra za Mwenyekiti
 
1:NIMEKUELEWA VIZURI MKUU, Na huo ndio uzalendo wenyewe...
Hapo kwenye KATANI(Sasa duniani inaitwa WHITEGOLD) kuna maelezo kidogo, HAdi Kesho Tanzania ni ya Pili nyuma ya Brazil kwa uzalishaji duniani japo Asilimia kama sabini Mzalishaji na Exporter ni MoDewji
Sisal: The most useful plant you've never heard of - CNN.com. Bado lakini tunarudi kwenye hoja yako Sekta binafsi ndio kila kitu...

Mhutasari Wa maelezo yako kwa maoni yangu ni kwamba serikali ijikite kwenye kusimamia biashara na wafanya biashara/viwanda sio kufanya biashara.

2:MADINI
Nilichojifunza kuhusu suala la madini, ilibidi kabla ya kauli, wapitie utaratibu mzima wa operation za madini, Waende TMAA wajifunze, Wafuatilia Production chain ya GOLD(Bullion) na Cupper/Gold Concentrate ndio wangeweza kuidentify Abdnormal from normal. Nimewafuatilia kwa karibu sana acacia na operation zao, kwanza hata watanzania wengi wanaofanya kazi /proffesionals migodini wanasikitishwa sana na maneno ya kisiasa. Acacia wanafanya Exploration ya Dhahabu Kenya, Wanaweza kwenda kujikita huko badala ya kufanya expansion kwa sababu zisizo za lazima. Ndio maana binasi nasubiri kujua wanaibaje kama process zote ni transparent. Kukosea kupo ila wakae waongee ili wapate hitimisho based on ushauri wako.

3:KUHUSU WASOMI AU PHDS KUWA HAWANA MSAADA SIO KWELI
Vile wanavyosoma wasomi wetu, vingi ni grobally accepted and tested principles zinazofanya kazi.Wananafasi kubwa sana kubadilisha kabisa uchumi wa nchi yetu kama wakisikilizwa.
Mfano FUATILIA ECONOMIC MIRACLE chile chini ya Pinochet, Kazi na Mipango yote ilipangwa na WASOMI Unaowapinga sio WAFANYA BIASHARA, Walikuwa economists wanafunzi kutoka Chicago university chini ya Lecture wao. Ninakubaliana na wewe kuwa hawa hawana uwezo wa Kuendesha biashara ndio maana sikubaliani na mkuu wa TTCL kuwa Prof(Muadhili wa telecom) tofautisha na MCHECHE NHC. Wao kama wasomi wabaki kama policy maker, watu wa planning, Kusimamia hawa wanaofanya kazi/biashara nchini.

4:Kuhusu Pesa kurudishwa BOT, naona sio sawa Pesa ziwekwe kwenye banks binafsi bila utaratibu wenye faida. Bali kuziweka BOT zikae bila kutumika sio sawa sana. Zirudi kwenye mizunguko kwa utaratibu wenye faida kwa serikali na bank na wananchi pia, lakini priolity iwe ni mipango na malengo makubwa ya hizo pesa.

TANZANIA INAWZA KUENDESHA UCHUMI KUPITIA WASOMI WAKE ILA KUENDESHA BIASHARA HAIWEZI BADALA YAKE ISIMAMIE BIASHARA.

Pia Wanasiasa wanataka kugawa katika makundi mawili yaani wenda useme WATAWALA NI PERFECT 100% au WABAYA 100%. Ila ukweli ni kwamba wote wanamazuri na mabaya na wanakosoleka CONSTRUCTIVELY KAMA ULIVYOFANYA MKULU...
 
zamani jeshini kulikuwa na wimbo wa tarumbeta ukipigwa (pamparara papaaapa, chungulia pipaa...) ikiitwa bigula ukiisikia unajua saa ya kusanyiko la chakula tayari.... Siku hizi tunatwaliwa na kauli za mihemko bila kujua taratibu wala alama za nyakati!

Mkuu ungemalizia na "kisha wanajitokeza watu badala ya kuona jahazi tulilomo linatobolewa wao wanashangilia kwa vifijo na oyeee nyingiii!!! bila kujali kuwa likizama na wao hawana maboya ya kuelea.... wala hawakujiandaa"

Hakika shangwe zao ndio mauti yetu na kizazi chao!
Yaani watu wamelalia macho na masikio. Wanadai wafanyakazi na wafanyabiashara wote ni wapiga dili.. Akili za kichawi kabisa za tukose wote. Ipo siku watajitambua kama mfalme juha... Lkn ni baada ya kuaibika.
 
Mkuu Msambichaka Mkinga, kwanza asante kwa bandiko hili. Sijui kama litachangiwa sana na wengi humu kufuatia Watanzania wengi kumkubali sana rais Magufuli kuwa kila anachofanya he is right, hivyo pia wanafuata ushauri wa rais mfano kipindi bora kabisa cha TV rais wetu anachoangalia ni Shilawadu, hivyo wengi kupenda kuchangia kwa wingi topic za kishilawadu Shilawadu halafu mambo kama haya ambayo ni very serious, sidhani kama utaona wachangiaji wengi.

Niliwahi kushauri huko nyuma kuwa

Japo Beggars Can Not Be Choosers, Tuache Siasa Kwenye Uchumi. We Have to Choose Or. ..

Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT

Utumbuaji: Tuache Siasa Kwenye Professionalism, Sio Kila Mtumbuliwa ni Jipu!.

Paskali
Msimdanganye mchana kweupe magufail kuwa anapendwa!!!!!
pascal, magu anachukiwa saaaaaaana!!!
Anachukiwa nakosa mfano wa ulinganifu.
 
Serikali ya Tanzania haina uelekeo.Haijui inakotoka wala unakoenda , Ni kama vile mwenawazimu.Mwendawazimu hajui anakoenda wala anakotoka ukimuonya umekosea njia ataokota mawe akutwange nayo.Hivyo ndivyo ilivyokuwa serikali ya Ccm.Halafu kuna watu wanajiga va eti chama changu ni chama bora.Chama bora!!!!!! Nini umewafanyia watanzania tangu uwe madarakani ili nao waweze kujivuba popote wanapokwenda??????Nafikiri mnajuwa nani aliyetoa hiyo kauli.
 
Asante sana kwa kutoa hoja za msingi nafikiria hao makada waliopo Lumumba wameipata hiyo message.
 
Msimdanganye mchana kweupe magufail kuwa anapendwa!!!!!
pascal, magu anachukiwa saaaaaaana!!!
Anachukiwa nakosa mfano wa ulinganifu.
labda kama ni kuchukiwa mitandaoni na watu ambao sio wapiga kura na hawamati kwenye mustakabali wa taifa letu lakini kwa wananchi wa kawaida, huwaambii kitu kuhusu Magufuli na 2020 utashuhudia.

Paskali
 
zamani jeshini kulikuwa na wimbo wa tarumbeta ukipigwa (pamparara papaaapa, chungulia pipaa...) ikiitwa bigula ukiisikia unajua saa ya kusanyiko la chakula tayari.... Siku hizi tunatwaliwa na kauli za mihemko bila kujua taratibu wala alama za nyakati!

Mkuu ungemalizia na "kisha wanajitokeza watu badala ya kuona jahazi tulilomo linatobolewa wao wanashangilia kwa vifijo na oyeee nyingiii!!! bila kujali kuwa likizama na wao hawana maboya ya kuelea.... wala hawakujiandaa"

Hakika shangwe zao ndio mauti yetu na kizazi chao!
Hahahaaa
 
Yaani watu wamelalia macho na masikio. Wanadai wafanyakazi na wafanyabiashara wote ni wapiga dili.. Akili za kichawi kabisa za tukose wote. Ipo siku watajitambua kama mfalme ****... Lkn ni baada ya kuaibika.
Hao wanaojiita sio wapiga dili wametekeleza bajeti kwa asilimia 30, Lissu anasema "ni bajeti iliyotekelezwa kwa kiwango cha chini kuliko zote"

Tulitaraji baada ya kuzuia safari za nje,semina,masomo kwa watumishi,kuzuia ajira basi bajeti ijitosheleze.

Sasa hata walioruhusu semina,safari za nje,waliofanya Private Public Partnership,waliopeleka watumishi na wanafunzi nje za nchi kusoma walitekeleza bajeti kwa kiwango kikubwa kuliko hawa

Je hawa wanapeleka fedha wapi?
 
Back
Top Bottom