The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 746
- 2,106
Habari Wakuu,
Leo tena shahidi wa 12 Denis Urio anaendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi ya Mbowe na wenzake: Kesi imeahirishwa hadi 28/01/2022, Luteni Denis Urio kuendelea na ushahidi wake
Fuatana nami kupata yatakayojiri
UPDATES:
Jaji ameingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Robert Kidando nipo pamoja na wakili
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji ikikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na wakili
Jaji anaita Washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na tupo Tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Nasisi pia tupo tayari Kuendelea
Shahidi anapanda Kizimbani
Jaji: Shahidi Jana Ulikuwa Unatoa Ushahidi Wako, Unaulizwa Maswali Chini ya Kiapo na Leo Utaendelea Kuulizwa Maswali Chini ya Kiapo
Wakili John Mallya: Shahidi tunaendelea tulipo Ishia Jana, Mheshimiwa Jaji Naomba Jibu lake la Mwisho
Jaji: ni Kwamba Asipotumia Jina Namba zake Jina lake halitoonekana...
Malya: hivi kazi ya VIP PROTECTION Inafanyikaje
Shahidi: Mheshimiwa Jaji kazi ya VIP PROTECTION Inafanyika kwa mtu yoyote, Kwa Kufuata Sheria na Kanuni za Nchi
Malya: Ni sahihi Kwamba kazi Wanazofanya VIP protection Ni lazima wawe naye Kwa Wajibu wa Kum' protect
Shahidi: Ni sahihi Malya: hawa VIP protection Ni sawa na Body guard?
Shahidi: Sijawahi Kusikia Body Guard mimi
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 26
Malya: Umesema kuwa hawa VIP protection Wanakuwa pamoja na Wanayem' protect, sasa ni somee Meseji ya Tarehe 20 July 2020, Ya Saa Mbili Asubuhi
Shahidi: Hawa wawili Kuanzia Siyo Mbaya Hawawezi Kutelekezwa, Nitakuwa nao Full time
Malya: Kwa Kazi gani
Shahidi: Ulinzi Ndiyo
Malya: Je, kuna meseji nyingine yoyote kwamba kuna mahali Mbowe anasema nitawatuma Kufanya kazi nyingine au uhalifu?
Shahidi: kwenye meseji hazipo
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo Namba 35
Malya: Tumeletewa report kule ulikopeleka simu , Je hii namba ina Jina gani?
Shahidi: Imeandikwa FREE... Ambayo ni namba ya Freeman Aikael Mbowe
Malya: Very Good shahidi umeniongezea information nilikuwa sijui, sasa washa simu yako
Shahidi anabonyeza simu, anasema tayari
Malya: Unasema Ulikuwa Unawasiliana na Mbowe Kupitia Mtandao Wa Telegram
Shahidi: Ndiyo Mtandao Wa Telegram
Malya: Naomba usogee kwa Mheshimiwa Jaji pale kamuonyeshe namba unayosema ume-chat na Mbowe. Je, hapa kuna Jina FREE linaonekana, ukiwa umefungua meseji?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji HAKI YA MUNGU hii ni akaunti ya Mbowe siyo Group, nafungua
Malya: Jina Free Ukifungua Meseji linaonekana au halionekani?
Shahidi: Halionekani lakini ni Akaunti ya Mbowe
Malya: Je, ulitoa Ufafanuzi/Maelezo kuwa Jina FREE halionekani?
Shahidi: Si nilimjibu mimi Bwana, Mimi siyo Mtaalamu Wa IT, Sasa nitoe Maelezo Ya nini
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba atoe jibu
Jaji: Umeelewa Swali? Kwamba Wakati Unasoma Ulitoa Ufafanuzi? Kuwa jina halionekani
Shahidi: Ufafanuzi huo sikutoa
Mahakama: (Kicheko)
Malya: Haya Ulisema Kwamba Mbowe alikuwa nakupa Wishes za Christmas na Mwaka Mpya, je Meseji zimeanza lini
Shahidi: Tarehe 20 July 2020
Malya: Alikuwa anakutakia Heri ya Mwaka Mpya Kupitia nini
Shahidi: alikuwa ananipigia Simu
Malya: Alikuwa anakupigia simu kwa njia ipi
Shahidi: Kwa Telegram
Malya: Je, unafahamu kwamba ukipiga Simu Telegram unabakia na Calls Record
Shahidi: Sina Utaalamu huo
Malya: Je Jana Wakati wa Ushahidi Wako Kama Ulituonyesha WhatsApp Calls na Meseji za Mbowe
Shahidi: aliyechunguza ndiye anafahamu
Malya: Kwa hiyo Mtaalamu anaweza Kuwa amepunguza au ameongeza?
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi hajasema hivyo
Malya: Nitauliza Upya Kuokoa muda, Kilichokufanya Jana usitoe Calls za WhatsApp
Shahidi: nilisema kwamba Mimi Nilikuwa na wasiliana na Mbowe Kwa WhatsApp, Meseji na Telegram
Malya: Sawa Jana Ulionyesha WhatsApp Call wakati wa Ushahidi Wako?
Shahidi: Sikuonyesha
Malya: Ulionyesha namba zingine ambazo Ulikuwa Mbowe alikuwa anakupigia Simu
Shahidi: Sikuonyesha
Shahidi: (Ghafla) Sikuonyesha Kwa sababu..
Malya: sitaki sababu hapa
Shahidi: Sikuonyesha Kwa sababu
Malya: Sijakuuliza kuhusu sababu
Jaji: Shahidi sikiliza swali ndiyo ujibu
Malya: Naomba Kielelezo Namba 28
Malya anamkabidhi shahidi
Malya: Jana ulishindwa Kuiwasha hii simu
Shahidi: Sikushindwa, haikuwaka
Malya: Ulitoa Explanation Kwanini ilishindwa Kuwaka
Shahidi: Nilieza Kwamba simu ina ibovu wa Display, Ukiwasha Hai Display Kitu chochote
Malya: Kama kuna Taarifa ya Muhimu ambayo Mbowe anataka Kujitetea Kutumia hiyo Simu atafanyeje, Utampa akatengeneze
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Wakati natoa Ushahidi Wangu Kuhusu Kukabidhi Simu, Nilisema, Nilienda na Simu moja, Sikujua Kama Nilitakiwa Kukabidhi Simu, Nikauliza kwa sababu gani wakasema sababu ya Uchunguzi, Tarehe 10 nilipeleka simu zingine, na Mimi nilipeleka Simu Ikiwa imedondoka haifanyi kazi
Malya: Aliyechunguza hajasema Kwamba Simu Mbovu, Isipokuwa wewe unaogopa kwa sababu unajua Kilichopo humo hutaki kionekane
Shahidi: Washa wewe
Malya: Mimi siwezi Kuwasha Simu yako
Shahidi: basi awashe hata Mheshimiwa Jaji
Malya: wewe Ndiyo Mwenye Simu Shahidi: basi hayo Mengine ni Maoni
Malya: Kuna report ya hii Simu, Je Jana Ulionyesha Call Logs za mbowe
Shahidi: Sikuonyesha
Malya: Calls za Khalfani Bwire Jana Ulionyesha
Shahidi: Sikuonyesha, Sababu sikuulizwa
Malya: Je, jana Ulionyesha Meseji za Ling'wenya Kuhusu Kuwasiliana nao wasikengeuke
Shahidi: Sikuonyesha sababu sikuziona
Malya: Ni sahihi unasema Kwamba a baada ya kuwapeleka Vijana Wanne Kwa Mbowe Mwisho wa Kuwasiliana naye ilikuwa Tarehe 24
Shahidi: Ndiyo
Malya: Wakati Mbowe anaacha Kupokea Simu yako alikuwa tayari na Vijana Wanne
Shahidi: Ndiyo
Malya: Soma hapa
Shahidi: Kaka Wale Mtu 3 au 4 Ni Muhimu
Malya: Sasa kama Umeshampa Mtu Nne ukitaka uwasiliane naye nini
Shahidi: Nilichokitaka Kwake baada ya kukikosa nikakipata kwa Bwire
Malya: Kwa hiyo Wakati anaacha Kuwasiliana na wewe Hitaji lake alikuwa ameshalimaliza
Shahidi: Ndiyo
Malya: Miji ya Arusha, Dar es Salaam, Mbeya na Mwanza ina masoko mangapi?
Shahidi: Mimi sifahamu anafahamu Mbowe
Malya: Miji niliyotaja ina vituo vya mafuta vingapi?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji najibu swali kama Ifuatavyo anayejua idadi ya vituo vya mafuta ambavyo alipanga kulipua ni Freeman Mbowe
Malya: Shahidi Miji hiyo ina Mikusanyiko Mingapi
Shahidi: Mheshimiwa Jaji mimi sijui ina mikusanyiko mingapi, Ila Mheshimiwa Mbowe ndiye anajua kwa sababu alipanga kulipua
Malya: Ulifika Ofisi za DCI Je Ulifika ukiwa na Simu zako
Shahidi: Ndiyo
Malya: Je, ulieleza Jana Kama Ulikuwa na Simu zako
Shahidi: Mheshimiwa Jaji nilifika kwa DCI nikampa Taarifa, akasema endelea nao
Malya: Maelezo Yako Mazuri ila siyahitaji, Swali langu Ulieleza Kama Ulimuonyesha DCI Simu zako na Mawasiliano ya Mbowe?
Shahidi: Sikueleza
Malya: Unafahamu kwamba DCI ana vifaa Vya Kurekodi?
Shahidi: Mimi sifahamu
Malya: Je, unafahamu kwamba DCI ana vifaa Vya Upelelezi
Shahidi: Mimi sifahamu Kwa sababu, Kazi yangu haikuwa Kufanya Upelelezi Bali Kutafuta Watu wa Kufanya Kazi
Malya: Wakati Khalfani Bwire, Je alikwambia Vifaa wanavyokwenda Kuvitumia
Shahidi: Hakuniambia
Malya: Wakati Unaingia Jeshini ulikuwa na Certificate ya Form Four na Certificate Ya Ufundi
Shahidi: Ni sahihi ya Diesel Engine
Malya: Bwire alikuja Nyuma yako
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Ulikwenda South Africa Kufanya Mafunzo lini
Shahidi: 2010
Malya: Ukawa Mwanafunzi Bora
Shahidi: Hapana
Malya: Kwanini ulipewa zawadi ya Bunduki
Shahidi: Mheshimiwa Jaji, Inaonyesha Jinsi gani Wakili anataka Kuniweka Maneno Mdomoni, Labda yeye ndiyo alipewa Bunduki baada ya kufuzu Law School, anataka Kuficha Uhalifu
Malya: Ulipewa award gani
Shahidi: Sikupewa Award
Malya: Lakini wewe Ulifuzu
Shahidi: Ndiyo
Malya: Wakati Unakwenda Darfur Mara ya kwanza ulikuwa koplo?
Shahidi: Ni sahihi
Malya: na kwenye Jeshi koplo siyo Afisa
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Wakili ananitaka nieleze Kamisheni ya Kijeshi
Jaji: amekuuliza koplo ni Afisa siyo Afisa
Shahidi: Ni Afisa
Malya: Wakati Unakwenda Darfur ulikuwa na Ling'wenya kinachokufanya umkane Ni Kitu gani
Shahidi: Sijamkana, Siwezi Kukumbuka kama Nilikuwa naye
Malya: Shahidi Wewe ni Luteni Wa Jeshi, Je una Degree?
Shahidi: Hapana
Malya: Huna Digrii lakini ni Luteni wa Jeshi
Shahidi: Ndiyo
Malya: Adamoo na Ling'wenya Mlipoachana Morogoro alikwenda Wapi
Shahidi: Walikwenda Dar es Salaam
Malya: Naomba Kielelezo D1, Maelezo aliyo andika Kingai ambapo anasema alimuhoji Ling'wenya akakiri, Soma hapa
Shahidi: Luteni Urio alitupa nauli TSh 87,000 nauli ya kwenda Moshi
Malya: na wewe Umesema Walitoka Kwako Walikwenda Wapi
Shahidi: Nimekwambia Dar es Salaam Siyo Moshi
Malya: Kwenye Nauli uliwapa TSh ngapi
Shahidi: TSh 199,000
Malya: hapo Wao Wameamdika uliwapa TSh Ngapi
Shahidi: Nauli TSh 87,000, Ndivyo walivyo andika wao
Malya: Ulielezea Shahidi Kwenye Ushahidi Wako namba Uliyotumia Kuwasiliana na Bwire ni Namba gani
Shahidi: Sikueleza
Malya: Wakati Mnaenda Kuonana na Swila Mara ya Kwanza Ilikuwa lini
Shahidi: Tarehe 11 August 2020
Malya: Ndiyo Siku hiyo ulitoa Maelezo Yako
Shahidi: Ndiyo
Malya: Nimesikia Siku Unakutana na DCI Mlikutana baadae akaja Kingai
Shahidi: sahihi
Malya: Ulielezea Kuna mtu Yoyote alikuja Kuwa Join Baadae
Shahidi: Kuwa Join wapi?
Malya: Kwenye Kikao cha Siku hiyo na DCI na Kingai
Shahidi: Hakuna Mtu yoyote alikuja Kutujoin Siku hiyo
Malya: Kwenye Meseji ya Mwisho ambayo Mbowe alikutumia, Ukasema Hukueleza, ni kwanini hukutuma Meseji Nyingine Kuuliza Una maana gani
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Baada ya Kupita Muda Hakuna Mawasiliano, Nilimuuliza Bwire Boss wako anajua, Sasa ningejibu Meseji ya Nini
Malya: Na ni Ushahidi Wako Kwamba Ofisi za Swila ni Ghorofa ya Nane Makao Makuu
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Mheshimiwa nafikiri Sina Swali la Ziada kwa Shahidi huyu
Anasimama Adv. Dickson Matata
Matata: Nikumbushe Ulionana na Mbowe Tarehe ngapi
Shahidi: Mwezi Wa Saba, 2020 Sikumbuki Tarehe gani
Matata: Na Ulipo Onana naye ndiyo alikwambia anahitaji Vijana Wa Kuambatana naye wa Kuchukua dola
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kwa Maelezo yako Ndiyo alikwambia anahitaji Vijana hao Vijana Kwa ajili ya Kumsaidia Kuwashambulia Viongozi ambao hawaupendi Upinzani
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Ndipo alipokwambia Kwamba anataka Kuhakikisha anachoma Masoko na Vituo Vya Mafuta
Shahidi: Naomba Ni'refresh alisema Kwamba ataleta Taharuki Kwa Kufanya hayo Uliyo niambia
Matata: juzi Ulisema Kwamba Ulifanya Kitu kinaitwa Tactical appreciation, na Mimi Leo nataka tufanye Tactical appreciation ya Kisheria, Wakati anakwambia Mlikuwa Wawili
Shahidi: Ndiyo
Matata: Kwa Lugha Nyingine Hapakwepo na Watu wengine
Shahidi: Sahihi
Matata: tofauti na Siku hiyo, Kuna Siku yoyote aliwahi Kukwambia Jambo hilo au kukuandikia Barua
Shahidi: Hakuna
Matata: Kwa hiyo kwa tafsiri nyingine hatutopata ushahidi wa maandishi au wa sauti au meseji unaoweza kuthibitisha kuwa alikwambia hayo maneno?
Shahidi: Hakuna sauti
Matata: Baada ya Kukwambia Ukaona Inafaa ukatoe Taarifa, Ukaenda kwa DCI, Kwanza Ulimpigia Simu halafu akakupa appointment
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Kwamba Baada ya Kumueleza akamuita Kingai
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Utakubaliana na Mimi Kwamba DCI ni Mtu Mwenye Ujuzi Katika Upelelezi
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kingai alikuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Unafahamu Kwamba anakuwa na uzoefu wa Upelelezi
Shahidi: Kwanza Nilikuwa sijui kuwa ni Mpelelezi
Matata: Mtu akiwa Mpelelezi Wa Mkoa ana uzoefu au hana Uzoefu
Shahidi: anakuwa na Uzoefu
Matata: Wewe Kama Komandoo, Katika Kikao hicho na Baada ya Hapo, Hukuona wewe au DCI na Kingai, Hukuona Kuwa Kuna Umuhimu kuwa Msiridhike Kile ambacho umesema, Je Hukuona Kuwa Kuna Umuhimu Wa Kurekodi Voice Notes
Shahidi: Mamlaka labda Ndiyo haikuona Umuhimu
Matata: Wewe Uliona Kuna Umuhimu au Hakuna Umuhimu, Kwamba Usiridhike na Maneno Utengeneze Voice Record
Shahidi: Niliona Kuna Umuhimu
Matata: kwenye huo Umuhimu hukuona Kuna Umuhimu Wa Vinasa Sauti na Meseji ambao Vitasema Exactly Kuwa anataka Kulipua
Masoko
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Mbowe alikuwa alishaniambia Kwa Meneno, asingerudia
Matata: Narudia Swali langu, kwenye huo Umuhimu hukuona Kuna Umuhimu Wa Vinasa Sauti na Meseji ambao Vita, sema Exactly Kuwa anataka Kulipua Masoko
Shahidi: Sikuwa na Vifaa Vya kunasa Sauti
Matata: Freeman Mbowe akikataa leo hakusema, ni ushahidi gani unao mbele ya Mahakama Kwamba Mbowe alisema hayo maneno uliyosema?
Shahidi: Ni ushahidi wa meseji ya kusema "muda umeisha"
Matata: hiyo meseji inayosema muda umeisha ina sehemu inasema kulipua masoko
Shahidi: Hakuna mahali inasema
Matata: hiyo Meseji ina sehemu inasema kushambulia viongozi ambao hawapendi upinzani?
Shahidi: Hakuna mahali inasema hivyo
Matata: Hiyo meseji kuna sehemu inasema kulipua vituo vya mafuta
Shahidi: hakuna mahali inasema hivyo
Matata: Tutoke hapo, Unasema Ulienda Kwa DCI na Kabla ya kwenda Ulimpigia Simu,
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Ulielezea Mahakama Kwamba Ulikuwa Unafahamiana na DCI
Shahidi: Nilieleza, Kuna Mtu aliuliza Kama Nilienda Ofisi ya DCI Mara ngapi
Matata: Mimi Sitaki Habari ya Kwenda Ofisini, DCI Anabadirika, nakuuliza Kama Ulielezea Kwamba Unafahamiana na DCI
Shahidi: Sikueleza
Matata: Ulieleza Mahakamani hapa Kwamba Namba yake Ulipata Wapi
Shahidi: Sikueleza
Matata: Hata hiyo namba yenyewe Ulitaja
Shahidi: Sikutaja
Matata: Ushahidi gani Unathibitisha Kwamba Ulimpigia Simu
Shahidi: Ushahidi ninao kwa sababu nina namba zake na Nilifika Ofisini Kwake
Shahidi: Je ulivitaja hivyo Vitu Wakati Unahojiwa na Upande wa Mashitaka
Shahidi: Sikuvitaja
Matata: Unasema Kwamba Ulienda Kesho Ukasema Una Appointment naye Ukakutana na Secretary Wake
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kwa Maana hiyo Ulifuata Utaratibu wa Umma Wa Jinsi ya Kuingia Ofisi Fulani
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Ulisema Kwamba Ulipofika Ulifuata taratibu za Ofisi za Umma
Shahidi: Nilieleza Kwamba, Nilionyesha Kitambulisho kama Askari
Matata: Ulisema Kwamba Askari apaswi Kufuata Utaratibu Wa Kuingia Ofisi Za Umma
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Mimi Nilieleza Kuwa ni Askari, yeye Ndiye alitakiwa aniambie Kufuata Utaratibu
Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili wa Serikali Abdallah Chavula, Ulisema Kwamba Nyie Askari hamfuati Utaratibu
Shahidi: Sikueleza
Matata: Ulileta Visitors Book Kuonyesha Kweli Ulienda Ofisi Za DCI
Shahidi: Hapana Sikuleta
Matata: Shahidi Wewe ni Mwanajeshi, Ulitakiwa Kufuata Taratibu zote za Kijeshi
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Unapotoka Mkoa Mmoja Kwenda Mkoa Mwingine, unatakiwa Kuwa na Movement Order
Shahidi: Inategemea na Siku Ngapi, Kama Chini ya Siku Tatu unaweza Kwenda bila Movement Order kama zaidi ya Siku Nne Unatakiwa Kuwa na Movement Orde
Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili Abdallah Chavula Uliyasema hayo
Shahidi: sikuyasema
Matata: Unapokuwa Askari Unapoenda Ofisi za Umma si lazima Uwe na Pass
Shahidi: Ni kwenye Kitabu Unachotaka,
Matata: Si lazima uonyeshe Pass
Shahidi: Ndiyo ni lazima
Matata: Umeleta Mahakamani hapa Pass Kwamba Umeruhusiwa Kutoka kazini Kwako
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Sijaleta Sikujua I nahitajika Mahakamani
Matata: Tarehe 11 ulienda kwa Inspector Swila na Tarehe 12 Ulimpelekea Simu
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Ulileta Mahakamani Hapa Pass za Umeruhusiwa
Shahidi: Sikuleta, Sikupewa Maelezo
Matata: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo Namba 20
Matata: Naomba Nikuonyesha Kielelezo namba 20 ambacho Kina Miamala yako ya namba ya Airtel
Matata: Jana Wakati Unahojiwa ulisema Freeman Mbowe alikurushia Kwa Mara ya Kwanza TSh 500,000
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Ukatoa TSh 499,000
Shahidi: Kweli
Jaji: Umeelewa Swali? Anasema Umetumiwa TSh 500,000, Swali Ukatoa kwenye hiyo Fedha kiasi gani?
Shahidi: Ni TSh 499,000
Matata: Kwa Mantiki Nyingine Hukutoa yote Kwa sababu Kuna Makato kidogo
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kwa hiyo Ulichukua TSh 500,000 Ukatoa TSh 499,000 Je Makato TSh ngapi?
Shahidi: TSh 1000
Matata: Naomba Nikuonyeshe Kwa Siku hiyo, Mheshimiwa Jaji Namuonyesha Muamala Wa Siku hiyo ambapo anasema alitoa Muamala Wa TSh 499,000
Matata: Sasa Shahidi angalia Tarehe 20 July 2020, Kwenye Miamala sehemu ambayo Umeenda Kwa Wakala Ukatoa TSh 499,000
Jaji: anakuuliza Hapo Hapo hapo Kwenye hiyo Nyaraka
Shahidi: Hapa Kwenye Miamala Haipo hiyo 499,000
Matata: Mheshimiwa Jaji naomba ni Muonyeshe Hapo hapo, Kuna Majedwali ambayo Yanaonyesha Receiver Balance kabla ya kutumiwa TSh 500,000 kutoka Kwa Mbowe.. Utakubaliana na Mimi Kwenye akaunti yako palikuwa na TSh 49,646
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Baada ya Kuweka TSh 500,000 balance Ikawa TSh 549,646
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Tarehe hiyo hiyo Ukatoa TSh 300,000
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Balance Yako Ikabakia 243,646
Shahidi: Ni sahihi
Matata: hebu chukua salio uliokuwa nalo la 549,646 Kutoa 300,000 ukabaki na 243,646 tuone Makato ni TSh ngapi
Amesimama Mmoja Wakili wa Serikali Robert Kidando
Wakili wa Serikali Robert Kidando: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Naona Hajajengewa Misingi Kwamba wakili anauliza ikiwa hayo Makato yapo au hayapo..
Matata: Mheshimiwa Jaji Mimi lengo langu nikutaka kujua kwanini Shahidi atoe TSh 499,000 akatwe TSh 1,000 na atoe TSh 300,000 akatwe Elfu Sita na usheeee..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hicho ndicho alichopaswa Kuulizwa
Matata: Je Shahidi Utakubaliana na Mimi Kwamba Ukitoa TSh 300,000 ikibakia TSh 243,646 Je Elfu 6 inaenda Wapi?
Shahidi: Siwezi Kujua Kama ni Makato au imeenda wapi
Matata: Kwani hiyo Tsh 1000 Mwanzo Ulijuaje Kama ni Makato
Shahidi: (Kimya)
Jaji: Swali lako la Mwisho liasema Kuhusu Elfu 6 nimesharekodi
Mallya anasaidia kufafanua kidogo
Matata: Shahidi Ulitoa maelezo hii TSh 1,000 Ilienda wapi
Shahidi: Sijawahi Kutoa
Matata: Shahidi sasa ulitoa...sorry Mheshimiwa Jaji Kidogo
Matata anapekua Nyaraka hapa
Matata: Shahidi Umesema Freeman Aikael Mbowe alikuwa na Mpango Wa Kulipua Vituo Vya Mafuta, Je Wakati Unahojiwa ulitaja Majina ya Vituo Vya Mafuta
Shahidi: Hakuniambia Vituo Vya mafuta anavyoenda Kulipua Bali alitaja Mikoa tu
Matata: Kwa hiyo ukiulizwa Alitaka Kulipua Vituo gani Morogoro hutakuwa na Majibu
Shahidi: Sitokuwa na Majibu kwa kweli
Matata: Tukisema Utaje Vituo Vya Mafuta alivyo taka Kulipua Mkoa wa Mwanza Utakuwa na Majibu au hutakuwa na Majibu
Shahidi: Mimi sina Majibu, Majibu atakuwa nayo Freeman Mbowe
Matata: Ukiulizwa pia Kuhusu Mkoa wa Dar es Salaam Vituo Vipi Vya Mafuta alitaka Kulipua
Shahidi: Mimi sina Majibu, Majibu anayo Freeman Mbowe, Mimi alinificha
Matata: Ukiulizwa ni eneo gani alipanga Kukata Miti kati ya Mkoa wa Morogoro na Iringa
Shahidi: Hakuniambia ni Eneo gani
Matata: Ukiulizwa, Ukiachana Na Sabaya ni Viongozi gani wengine Walipanga Kuwashambulia
Shahidi: Sikutaja Jina la Kiongozi Yoyote, Hakuniambia Kiongozi Yupi
Matata: Mpaka anakushirikisha bila Shaka alikuwa anakuamini
Shahidi: Ndiyo
Matata: Ukiachana na suala la Kumtafutia Vijana, Je alikueleza kuhusu kumtafutia vilipuzi
Shahidi: Hakunieleza
Matata: Kuhusu kumtafutia silaha za kuwashambulia viongozi
Shahidi: Hakunieleza
Matata: Naomba Kurejesha Kielelezo cha simu .. Ahsante
Mallya: Mheshimiwa Jaji, hata hivyo haiwaki.
Matata anaketi..
Anasimama Wakili Peter Kibatala
Kibatala: Shahidi Nikikuita baba Careen ni sawa?
Shahidi: Ni sawa
Kibatala: Baba Junior
Shahidi: Ni Sawa
Kibatala: Baba Jackson
Shahidi: Ni sawa
Kibatala: Jackson amezaliwa Lini
Shahidi: 17 December 2020
Kibatala: Hospitali gani
Shahidi: Hospitali Ya Mkoa Morogoro
Kibatala: Nani na nani alikwepo
Shahidi: Mke wangu na Jirani
Kibatala: Wewe ni Mkristo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: unasali Kanisa lipi
Shahidi: Parokia Ya Ngerengere, Kigango cha Kizuka
Kibatala: Paroko wako Unamfahamu
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Kwani Kanisani Umeenda Mara ya Mwisho lini?
Shahidi: Juzi juzi
Kibatala: Paroko anayehudumu Ngerengere Unamfahamu
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Katekista anayemsadia Paroko
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: narudia tena Mara ya Mwisho Kanisani Umeenda Lini
Shahidi: Sikumbuki Kusema Kweli
Kibatala: Una Gari ya silver
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Aina gani
Shahidi: Rav 4
Kibatala: Namba zake zipi
Shahidi: T 114 DHL
Kibatala: Toka Mwaka 16 August 2020 hiyo Gari ipo Wapi
Shahidi: Kazini Kwangu Ngerengere
Kibatala: Toka Tarehe 16 August 2020 Gari hii ilikuwa parked Wapi
Shahidi: Nilikuwa natumia, Kila Nilipo ipo
Kibatala: Baada Tarehe 16 August 2020 Gari hii umeitumia
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umekuja kutoka Morogoro kutoa ushahidi kwenye hii Kesi, na kwamba siyo kutoka kambi fulani ya Jeshi ulikokuwa umetekwa?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji (Shahidi kamuita Jaji hapa ana jambo gani?)
Kibatala: Ndugu shahidi RELAX..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mawakili Uliwakataza Kutoa Mawazo yao Bali Kuulizwa maswali
Kibatala: Shahidi hiyo Gari Ipo wapi
Shahidi: Kambini Kizuka
Kibatala: Umepeleka lini hiyo Gari
Shahidi: Ijumaa Wiki Iliyopita
Kibatala: Utaratibu gani Umetumika kupark hiyo gari
Shahidi: Park at Your Own Risk
Kibatala: Kwa hiyo wewe Kama afisa wa Jeshi unataka Kuniambia Kuwa Una park Gari at Owner's Risk Kambini, Upo serious kweli wewe?
Shahidi: Lipo Katika Parking ya Staff
Kibatala: Bado Kwamba Unaendelea Kusema Gari ipo Parking Owner's Risk?
Shahidi: Hapana Nimeliondoa jibu la Owner's Risk
Kibatala: Jibu lako la Kwanza kwamba Uli park Chini ya Owner's Risk Ulilitoa Chini ya Kiapo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: haya, Turudi tena Kwamba Gari Umei' park Kwa Utaratibu gani
Shahidi: Pale Hakuna Ku'Register, Nilitoka Kwenye Oparation Nikaambiwa Nije kutoa Ushahidi
Kibatala: hapo Maana yake ni Owner's Risk
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: si Ndiyo umeliondoa hilo Jibu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Naiachia Mahakama Twende Eneo Lingine
Kibatala: Mwanzo Ulisema Ulikuwa unapanda Tax huna Gari
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Basi Ujue kwanini Nimekuuliza Kuhusu Gari
Kibatala: Shahidi Fungua Yohana Sura ya 8, Mstari wa 31 Mpaka 39
Shahidi anasoma biblia hapa..
Amemaliza..
Kibatala: Unafahamu Maan ya hilo Neno
Shahidi: Ndiyo Nafahamu
Kibatala: Maana yake ni nini
Shahidi: Tusiogope, Tuseme Kweli
Kibatala: Soma pia Waefeso Sura ya 4 Mstari Wa 25 Mpaka 32
Shahidi anasomeshwa Biblia tena
Kibatala: Je, unafahamu Maana ya hilo Neno
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Maana Yake ni nini
Shahidi: Tusiseme Uongo na tupendane
Kibatala: Kwa Hiyo Unafahamu Kwamba Maisha ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya yapo Mikononi Mwako
Shahidi: Ndiyo najua
Kibatala: na Ulisema Kwamba Mara Ya Kwanza Ulikutana na Mbowe Lini
Shahidi: JULY 2020
Kibatala: Tarehe Ngapi
Shahidi: Sikumbuki ni Tarehe za Kati kati
Kibatala: zipi hizo
Shahidi: Tarehe 10 Mpaka 15
Kibatala: Hizo ndiyo Tarehe za Katikati
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na wewe ni Luten wa Jeshi la Wananchi Tanzania tunalolipenda wote
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Elimu yako ni Form Four
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulipata Divisheni Ngapi
Shahidi: Three ya Point 25
Kibatala: unajua Division Four Inaanza point ngapi
Shahidi: Point 28 ila Sikumbuki Vizuri
Kibatala: Kwa hiyo Unakumbuka au hukumbuki
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Umesoma wapi.?
Shahidi: King'ori Sekondari
Kibatala: Headmaster Wako ni nani
Shahidi: Simkumbuki
Kibatala: Graduation Mlifanya lini
Shahidi: Hatukufanya Graduation
Kibatala: Ukimaliza Form Four lini
Shahidi: Mwaka 1999
Kibatala: Yule Mchungaji Wako anayefundisha Mzumbe Mara ya Mwisho Kuwasiliana naye ni Lini
Shahidi: Sina Mchungaji
Kibatala: Na Nabii Tito anayefundisha Mzumbe Umeacha Kusali Kwake lini
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Habari Nzito ya Mbowe Ulimshirikisha Paroko au Mchungaji
Shahidi: Sikumshirikisha Mtu
Kibatala: lakini Ulishindwa kulala
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: lakini Ukaenda Kumshirikisha nani
Shahidi: DCI na Kingai
Kibatala: Mwingine Je?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Msemo wa Kwamba Askari hawezi Kuwa Raia ila Raia anaweza Kuwa Askari Maana yake nini
Shahidi: Kwamba Ukishakuwa Askari huwezi kuwa Raia, Ila Raia anaweza Kwenda kujifunza Kuwa Askari
Kibatala: Jeshi la Wananchi Tanzania Mnafundishwa Kuwa Jeshi la Polisi ni Jeshi Kweli au si Kweli
Shahidi: Kweli
Kibatala: Raia Akiona Uhalifu unatendeka anaweza Kuzuia Uhalifu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwamba Mwajeshi Akiona Uhalifu Unatendeka anaweza Kuzuia au anaacha utokee alafu ana report Taarifa Polisi
Shahidi: Anazuia Uhalifu
Kibatala: ila wewe Ulikuwa na Mbowe anakwambia Mambo ya Kigaidi ukamuacha
Shahidi: Ndiyo Maana Nilienda Ku report Polisi
Kibatala: Kwani Jeshini si Kuna sehemu ya kwenda Kutoa Taarifa za Kihalifu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Jeshi la Wananchi Tanzania Kuna Kitengo Kina shughulika na Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kuna Jeshi la Navy ambalo kazi yao Ni Kushughulika na Ugaidi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: na bado wewe ni Luteni wa Jeshi kabisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwani kwa ufahamu wako wewe Jeshi halishirikiani na Jeshi la Polisi
Shahidi: Kama ikihitajika
Kibatala: Kwani Shahidi Kwa Mfano Mbowe angelipua Kituo cha Mafuta Puma pale Mwenge, Jeshi Pale Jirani Wangedhurika au Wasingedhurika
Shahidi: Wangedhurika
Kibatala: Bado Ukaona Usiwaambie Jeshi
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: unasema Kwamba Mbowe alikwambia Kukata Miti wapi
Shahidi: Kukata Miti Kwenye Barabara zote zinazo ingia Mjini
Kibatala: pale Kambi ya Jeshi Lugalo Kuna Barabara ya Kuingia Mjini au Hakuna
Shahidi: Ipo
Kibatala: Kama Wangekata Miti pale Barabara ya Lugalo Jeshi lingedhurika au lisingedhurika
Shahidi: Lingedhurika
Kibatala: Lakini Bado wewe Ukaona Usiwaambie Jeshi
Shahidi: Nilipeleka Taarifa Polisi Kwa sababu wao Wana husika na Uchunguzi
Kibatala: Kati ya Wewe Ulipo pale Mgulani Kambini na Ofisi za DCI, Wapi Ilikuwa Rahisi Kwako Ku report?
Shahidi: Kambini Mgulani
Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa Logic na Common sense
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: haya pale kwa DCI umesema Kwamba Kuna Scanner, Umejitambulisha Kuwa wewe ni Luteni na ukafanyeje
Shahidi: Nikatoa Kitambulisho
Kibatala: Baada ya Pale Ulimwambia Jaji Kwamba Jina lako liliingizwa Kwenye Register
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba sisi tumefika Kwa DCI Mara ngapi
Shahidi: Hapana, Sijui
Kibatala: Nikikukwambia Kwamba pale kwa DCI Nilifika Kumsindikiza Edward Lowassa Mwaka 2017
Shahidi: Ndiyo nitakubali
Kibatala: Unafahamu Kuwa DCI ni Mwanajeshi
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Kuna Mtu alipiga Simu Kwanza Kuhakiki appointment Yako
Shahidi: Hapana Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Wanajeshi hasa DCI ambaye ndiye Kama WAZIRI Mkuu wa Jeshi la Polisi ni watu wa tahadhari kwa sababu ni Watu wana deal na Uhalifu Nchi Nzima?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, Umemwambia Jaji Kwamba Kuna Kitambulisho Ulipewa cha Kuvaa
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kwa DCI Kuna Askari Kwa ajili ya Kimsindikiza Wanaenda Kwa DCI
Shahidi: Sikumwambia Jaji
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kuna Askari Wa Kukusindikiza Mpaka Kwa PS wa DCI
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Waiting Area ya Ofisi za DCI Makochi ni Rangi gani
Shahidi: Ya Brown
Kibatala: Unauhakika Kwamba Siyo Mekundu
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: Ukifika kwenye Ofisi za DCI PS anakuwa Upande Upi
Shahidi: Upande huu, (anaonyesha Kushoto)
Kibatala: Umebadilsha Sasa hivi eeh?
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba niilipokuwa Ulipokuwa wait Area Kwa DCI iwapo Body Guard Wake Ukiwa Una subiri Kuingia
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je Jana wakati wa Ushahidi Ulizungumzia Meza na Viti, Je Ulizungumzia DCI kuwa Ni Mnene, Mfupi, Mwembamba au Lah
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je Ukaona ni Muhimu tufahamu Viti na Meza na siyo DCI ambaye Ulimfuata
Shahidi: DCI SI anajulikana
Kibatala: anajulikana na nani
Shahidi: Watanzania wote
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kwamba Utaratibu gani Ulitumia Kutoka
Shahidi: Sijamwambia
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kuwa Ulipokuwa Unatoka Ulisaini Out
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unasema Ulifika Ofisi ya DCI Saa ngapi
Shahidi: Nimefika Majira ya Saa Mbili au Saa Tatu
Kibatala: Je Unafahamu Kwamba Huo Ndiyo Muda wa Kufika DCI
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Kwamba Chini ya Kiapo hapo Luteni Kwamba Siku hiyo DCI alipanda Ngazi Kwa Mguu Mpaka Ghorofa Ya Saba
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo ufahamu Kwamba DCI alikuwa na Umri Miaka zaidi ya 50 na Sasa amestaafu Kwamba alipanda Ngazi
Shahidi: Sifahamu alifikaje Juu
Kibatala: kwa hiyo Wewe Unasema Kwamba DCI Kiongozi Wao Kama. Waziri Mkuu, Kuwa Lift yake Ilikuwa bovu
Shahidi: Hapana, Sifahamu
Kibatala: Jana Ulionyeshwa Simu zako, na Moja ilikuwa na Display ya Mke Wako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Simu zako zote Nne Umepewa, Je Ni wakati gani Uliomba nafasi ya Kungalia Simu yako Namba ya Kingai Kama Kweli uliwasiliana naye?
Shahidi: Hapana Sikumwambia jaji
Kibatala: Je Kwa DCI pia ulimuomba Jaji nafasi ya Kungalia namba ya DCI Kwenye Simu yako?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Sasa Ni saa Saba Kamili, Kama Wenzetu wataridhia Twende Health Break na naomba Niependekeza Kwako Dakika 45
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: Kwa Maana hiyo tuta' break Kwa Muda wa Dakika 45 na Saa Saba na Dakika 45 tutarudi
Jaji amerejea
Kesi imetajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kwa Upande wa Jamhuri tumetimia Kama Ilivyo kuwa Mwanzoni tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Kama Mwanzo, Wakili John Mallya amepata Udhuru atarejea Baada ya Dakika 10 badala yake naomba Wakili Michael Lugina awakilishe Ingawa ni wakili wa Mshtakiwa Wa Nne
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Naona italeta Shida, Kwa sababu Wakili Michael Lugina Tayari ameshaingia Kwenye Quorum, Mshtakiwa Wa Pili anahitaji Kupata Full representation..
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa Maoni yangu Mimi, Mimi Ndiyo Nina Cross Exermine, Ila Ooohh Kwa Bahati Nzuri ndiyo anaingia... Huyu hapo.. Ikupendeze Kurekodi kuwa Sote Tupo na tupo tayari Kuendelea
Jaji anaandika Kidogo, Mahakama ipo Kimya wakati huu
Jaji: Shahidi nakukumbusha kuwa Ulikuwa Chini ya Kiapo wakati Unatoa Ushahidi Na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo Wakati Unatoa Ushahidi
Jaji: Shahidi nakukumbusha kuwa Ulikuwa Chini ya Kiapo wakati Unatoa Ushahidi Na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo Wakati Unatoa Ushahidi Wakili
Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kwa Hisani ya Mwisho Nikumbushwe Swali lake
Jaji: Kama Iwapo Alikuwa na Simu zake na Kama Aliomba Mahakama atoe humo namba za DCI Akasema Hapana
Kibatala: Unafahamu Kwamba Utambulisho Wa su Moja dhidi ya Nyingine ni IMEI, Je unafahamu
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Mawakili Wenzetu wa Somi waliluomhoza Kutoa Nyaraka fulani hivi
Shahidi: Ndiyo Nakumbuka
Kibatala: Kwahiyo Nyaraka Ile Ilikuwa ni Kuthibitisha Kuwa palikuwa na Makabidhiano kati yako wewe na Inspector Swila
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Inaitwa Techno nini Vile
Shahidi: Tecno CAMMO
Kibatala: Niambie Kama wakati Unaonyeshwa Simu zako zote Nne, Je ulitambua Simu Moja Moja Kwa kutumia IMEI namba Shahidi Hapana, Nilitambua Moja tu
Kibatala: Kwahiyo Kama tuna Simu Nne, Tatu hukuzitambua kwa IMEI namba ya Simu Moja Moja
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: kwa hiyo hii Tecno CAMMO ulitambua Kwa IMEI namba
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa Ushahidi Wako wote hapa umesema Kwamba Unaishi Ngerengere, Je Kuna sehemu Umesema Kwamba unaishi kihonda
Shahidi: Nina Makazi Mawili Ngerengere na Kihonda
Kibatala: Je Ulisema Jana na Leo Kabla Sijakuuliza
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je Kuna Mahala Popote Ulitambua Maneno CAMMO Kama Yapo
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Kuna Maneno gani badala yake
Shahidi: Tecno tu
Kibatala: Je, Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Abdallah Chavula Ulimfafanulia Mheshimiwa Jaji Kwamba hiyo Tecno ndiyo Tecno CAMMO
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Wakati Wa Ushahidi Wako Wote Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Abdallah Chavula, Uliongozwa kutoa Betri na Kusoma IMEI namba na Kumwambia Mheshimiwa Jaji Kama IMEI zinafafana na Inspector Swila Wakati wa Makabidhiano?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Soma Hapa Pameandikwa Kwamba wewe Luteni Urio unaishi Wapi
Shahidi: Kihonda
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwenye Kielelezo Kuwa wewe Luteni Urio Unaishi Kihonda Shahidi anatikisa kichwa hapa, namna gani..
Kibatala: Mahakamani, Usijibu kwa Kichwa
Shahidi: Sikumwambia Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Soma Hapa
Shahidi: CD/IR/2097/2020
Kibatala: Ni nini hiyo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Ulifafanua ni nini hicho
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Kuna IMEI namba Ngapi hapo
Shahidi ameshika Kielelezo cha karatasi moja
Shahidi: Sijui ni IMEI namba ngapi
Kibatala: Unafahamu Inspector Swila alikozitoa hizi IMEI namba au hufahamu
Shahidi: Kwenye Simu yangu
Kibatala: Je, Zipo ngapi hizo IMEI namba zipo ngapi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Hiyo ni Standard Form Document
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Soma hapo chini
Shahidi: Jina na Sahihi ya anayekabidhiwa
Kibatala: Wakati unatoa Ushahidi Jana Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba hiyo ni sahihi yako
Shahidi: Nilimwambia
Kibatala: Soma Hapo Chini ya Mstari Uliochapwa
Shahidi: 11 August 2020 Imeandaliwa Chini ya
Kibatala: ulifafanua Kuwa Kwanini hayo Maelezo Yapo Chini ya Nyaraka
Shahidi: Siku fafanua
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Nyaraka inasema Mimi Luteni Denis Urio Wa Kihonda Morogoro, Na mkabidhi Vitu ambavyo Vimekamatiwa Tarehe Deshi, Kutoka Kwa Mtuhumiwa Deshi, Vitu aina ya Deshi, Ushahidi Wako wewe Tukiangalia Kwenye Deshi tunaweza Kujua ni nini
Shahidi: Sijui ni nini
Kibatala: Mkumbushe Mheshimiwa Jaji Ulisema Simu yako wewe Ulikabidhi sababu ya
Shahidi: Uchunguzi
Kibatala: ambapo Wewe Unaamini ilikuwa Mawasiliano ya wewe na nani
Shahidi: Mheshimiwa Mbowe
Kibatala: Tuache Simu, Turudi Ofisini Kwa DCI
Kibatala: Lengo la Kutaja Meza na Viti Kwa DCI Lengo ilikuwa Kuonyesha Kwamba Ulifika kwa DCI, Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Ulimwambia kuwa Meza ni ya Rangi gani
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Kwakuwa Lengo lako lilikuwa Kuonyesha Unaifahamu Ofisi ya DCI Je Ulisema Juu Palikuwa na nakshi gani
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Kwa kuwa Lengo lako lilikuwa Kuonyesha Unaifahamu Ofisini ya DCI Je Ulisema Juu ya Rangi ya Viti
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je Umwambia Jaji Details zingine Kuhusu ile Ofisi
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kama Ofisi Ya DCI Kuna Bendera ya Taifa
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Sasa Ulimwambia Detail hiyo Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Ofisini Kwa DCI kuwa Kuna Picha ambazo zinaonyesha Matukio Mbalimbali ya Utejelezaji Wa Majukumu Yake
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuhusu hilo
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je, ofisini kwa DCI kuna kalenda zaidi ya Tatu
Shahidi: Niliona moja
Kibatala: Ulimwambia kuhusu hiyo kalenda moja
Shahidi: Sikumwambia, na pembeni ya Kiti chake kuna kiti kingine pia sikumwambia Mhe Jaji
Mahakama: (Kicheko)
Kibatala: ahsante kwa taarifa
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Ofisini Kuna Beseni la Kunawa Mikono
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ofisini Kwa DCI palikuwa na Askari Wangapi Wa zamu
Shahidi: Walikuwa wawili Ila Sikumwambia
Kibatala: Kwamba Pale Reception Kuna Magari ya Viongozi Mazuri Mazuri, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana Sikumwambia
Kibatala: Pale Nje Kuna Gari ya Rapid Response, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Umeliona
Shahidi: Sikumwambia, Ila siku hiyo halikuwepo
Kibatala: Unakumbuka Juu ya somo letu la TRUTH SHALL SET YOU FREE?
Shahidi: Ndiyo nalikumbuka
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwanini ulishindwa Kumweka Mheshimiwa Mbowe Chini ya Ulinzi?
Shahidi: Hapana Sikumwambia
Kibatala: Ni nini cha Ziada Kilichoongezeka kutoka Tarehe July 2020 Mpaka Leo hapa Mahakamani
Shahidi: Tuna Amani tu Tanzania
Kibatala: Tarehe ya Katikati ya July 2020, Toka Kipindi Kile Mpaka Leo ni zaidi Ya Mwaka sasa, Je Kuna Kitu cha Ziada ambacho wewe Binafsi Moyoni Mwako ulipata Taarifa ya ziada
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Swali hilo lime Ulizwa na kujibiwa, Amani.
Kibatala: Twende Eneo Lingine, Unasema Baada ya Kupata Taarifa za Freeman Mbowe Kupanga Uhalifu, Bado Unasema hukumbuki Tarehe?
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Swila anasemw alifungua Faili lake Tarehe 18 July 2020, Unaweza Kukumbuka Siku Uliyoenda Kwa DCI
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: sisi shida yetu ilikuwa ni Kutaka Kujua Kama Ulifika kwa DCI lini Tujue kuwa Faili lilitungwa au la
Shahidi: Siwezi Kukumbuka Tarehe
Kibatala: Kwa Mujibu wa Bando Kitita la Commital hata DCI hajui Wewe Ulifika Lini Ofisini Kwake
Shahidi: Siwezi Kumsemea
Kibatala: Je Unakumbuka Tarehe Uliyokutana na Khalfani Bwire
Shahidi: Sikumbuki ila ilikuwa Mwenzi Wa Saba
Kibatala: Je, Khalfani Bwire Uliwasiliana naye lini akiwa Tunduma
Shahidi: Sikumbuki ila Katikakati ya Mwezi Wa saba
Kibatala: Na Adam Kasekwa Uliwasiliana naye lini
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Kwa Mujibu Wa Mohammed Ling'wenya katika Maelezo Yake anasema Kwamba Tarehe 24 July 2020 Mkakutana Morogoro Shahidi Ndiyo
Kibatala: Siku Sita Tangu Inspector Swila aseme alifungua Faili Tarehe 18
Shahidi: Sijui
Kibatala: Si upige Hesabu Kutoka Tarehe 18 July 2020 Mpaka 24 July 2020 ni Siku ngapi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Umeanza Kuwakusanya hawa baada ya Tarehe 20 July 2020
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Na wewe ndiyo Ulikuwa Unawafahamu hawa wala Siyo Mbowe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaweza Kutuisaidia Kuwa Kwanini Inspector Swila alifungua Faili la Kula Njama Tarehe 18 July 2020 Wakati Wakati Umekutana hawa Vijana Tarehe 20 Mpaka 24
Shahidi: Sijui sasa
Kibatala: Je wewe Ulikula Njama na Mbowe.
Shahidi: Sijala Njama na Mbowe
Kibatala: Kwani Shahidi suala hili Kuna Mtu Zaidi Yako alienda Kutoa Taarifa Kwa DCI
Shahidi: Ni Mimi Pekee Yangu ndiye niliye Mwambia DCI Kibatala Kwani wewe Ulimueleza Jaji Kwamba Mbowe alikuwa tayari ana vijana Wengine
Shahidi: Sikumwambia Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Baada ya Kutoka Kwa DCI ulienda Wapi
Shahidi: Morogoro
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulitumia Usafiri gani Kurudi Morogoro
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je, baada ya Kutoka Kwa DCI Ulifika Nyumbani Kwako Usiku
Shahidi: Nilifika Jioni Jioni
Kibatala: Tuambie nani alikwepo Nyumbani Kwako ulimkuta Siku hiyo
Shahidi: Mke wangu
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba alikwepo Mtoto wako Careen Nyumbani kwako
Shahidi: Alikwepo Mke wangu na Watoto
Kibatala: Unabadilisha Enheeeee
Kibatala: haya Ulitumia Basi gani Kurudi Morogoro
Shahidi: Abood bus Service
Kibatala: Je Unayo ticket
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mimi na Malya tunafahamu CASA Motel, na Kila Gari Inayoingia pale inasajiliwa
Shahidi: Sijui
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Gari yako Tax ile Ilisajiliwa pale Mlangoni
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba CASA Motel ni Nyumba ya Chini au Ghorofa
Shahidi: Ni Ghorofa
Kibatala: Ndiyo hiyo si Taarifa Muhimu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji sasa
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba mlilaa sehemu gani, Nje au Ndani
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba mlikaa kwenye Makochi ya namna gani
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ushahidi Wako Kuwa Mbowe Mwenyekiti Wa Chadema Taifa, alikuwa CASA Motel Bila Dereva wala Mlinzi
Shahidi: Nilisema Alitupokea Kijana Mmoja akasema Chairman Yule Pale
Kibatala: Sasa Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba aliyekuwa anaye wahudumia ni Mwanamke au Mwanaume
Shahidi: Hapa Sikumwambia
Kibatala: Je wewe Luteni Wa Jeshi Moja ya ulichojifunza ni Kufanya kazi Katika High Pressure, Si Ndiyo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Moja ya Ulichojifunza ni Kuongeza umakini
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa Afisa wa JWTZ nimesoma tangu Wakati wa Willy Gamba, Luteni Unaitwa sehemu na Mtu ambaye humjui unaenda tu?
Shahidi: Nilikuwa namsikia kwenye TV tu
Kibatala: Mtu akakupigia yeye ni Peter Kibatala akakuita Goba Unakuja tu
Shahidi: Alikuwa anawasiliana Siku nyingi
Kibatala: Ulipokuwa Pale Kwa Mhe Freeman Mbowe, Nani alilipa Chakula
Shahidi: Freeman Mbowe
Kibatala: Nani alilipa Tax Yako
Shahidi: Freeman Mbowe
Kibatala: Pamoja na Kukwambia Taarifa za Ugaidi bado Ukapokea Fadhila zake
Shahidi: Siyo Taarifa za Ugaidi, Ni Uhalifu tu
Kibatala: Kwa hiyo Baada ya Kukwambia Mipango hiyo ya Uhalifu, Bado alilipia Tax Yako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, wewe Kama Luten wa Jeshi, Ulimwambia Mtu yoyote Kuhusu Swala hilo
Shahidi: Nilimwambia CEO wangu
Kibatala: Ulimwambia lini
Shahidi: Tarehe 05 August 2020
Kibatala: hayo Mambo Uliyo enda Kumwambia CEO wako, Yapo Katika Maelezo Yako Uliyo andika Kwa Inspector Swila
Shahidi: Hayapo Katika Maelezo yangu
Kibatala: hayo Unayosema Kwamba Ulienda Ku report Kwa CEO wako, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Sikumbuki Kama nilimwambia
Kibatala: Mimi Nikikwambia hujamwambia?
Shahidi: No, Sikumbuki nilitamka Kwenye situation gani
Kibatala: Mlikaa na Mbowe pale CASA Motel akakwambia Masuala Kadhaa wa Kadhaa
Shahidi: CASA Motel Siyo Wakati wa hiyo Mipango, CASA Motel ni Wakati wa 2012
Kibatala: Baada ya Kujua Mbowe ana mipango ya Kigaidi Uliendelea Kuwasiliana naye
Shahidi: Ndiyo nilikuwa naendelea Kuwasiliana naye ili Kumtafutia Watu wa Kutekeleza Mipango yake
Kibatala: Ni kweli Kwamba Ulishiriki Mipango ya Kigaidi
Shahidi: Sikushiriki
Kibatala: Nani aliyemuwezesha Mbowe Kupata hao Vijana Kutekeleza Mipango ya Kigaidi
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Wewe ni Afisa Wa Jeshi, Je Unafahamu Sheria yoyote Inayoruhusu wewe Kutafuta Vijana Kutekeleza Mipango ya Kigaidi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wewe si Ulikuwa Darfur
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kilichokufanya Mpaka Muende Darfur ni Janja Weed na SPLM
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Ingewezekana Wewe Askari Umeenda Darfur Chini ya Chapter Seven Ukawa Unafanya Mawasiliano ya Simu na Kiongozi wa Janja Weed?
Shahidi: Nisingeeleweka
Kibatala: Ni Kwa Sababu Yule alikuwa Mhalifu wa Amani?
Shahidi: Ndiyo alikuwa Mhalifu Wa Amani
Kibatala: lakini huku Tanzania ulikuwa Unawasiliana na Freeman Mbowe
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Je Kule Darfur Ungemuita Kiongozi Wa Janja Weed "Bro" Ungeeleweka?
Shahidi: Nisingeeleweka
Kibatala: Kwani Kule Darfur Si palikuwa na Askari Wengine Wa Chapter Six Wanaofanya Peace Keeping wapo armed na wanafanya Demining?
Kibatala: na Kwamba Wewe Kabla ya Tarehe 05 August 2020 Hakuna Uliyekuwa Umempa Taarifa Ndani ya Jeshi Kuwa Umepewa Kazi na DCI na Kingai
Shahidi: Sikumwambia Mtu
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba huyo Dogo Adam Kasekwa anajina lingine anaitwa Adamoo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mohammed Ling'wenya anajina Lingine anaitwa DOYI
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Moses Lijenje Yupo wapi
Shahidi: Nilimkabidhi Kwa Freeman Mbowe
Kibatala: Moses Lijenje Yupo Hai au amekufa
Shahidi: Nilimkabidhi Freeman Mbowe
Kibatala: ulimkabidhi Wapi
Shahidi: Nilimpigia Simu akasema Kwamba ameshafika
Kibatala: Nikuonyeshe Meseji zako utanionyesha sehemu ambayo ina meseji Kuwa Mbowe anasema Umemkabidhi?
Shahidi: Hakuna. Alinipigia Simu
Kibatala: Jana Ulionyesha Sauti zako za Kukabidhiana Kwa Mbowe Moses Lijenje
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wewe Mpaka Unaonana na Moses Lijenje, alikuwa anafahamu Masuala ya Ugaidi
Shahidi: Hapana, Masuala ya Ulinzi
Kibatala: Wewe Ulionana Lini tena na Moses Lijenje Baada ya Tarehe 21 August 2020
Shahidi: Sikuonana naye tena
Kibatala: Walicho ongea Na Mbowe Huko Hai au Popote unakifahamu
Shahidi: Sikifahamu
Kibatala: Unaweza kuonyesha chochote kile au sauti ukionyeshe kwa mheshimiwa Jaji kwamba Freeman Mbowe alimwambia Lijenje wakafanye ugaidi?
Shahidi: Sijawahi kusikia mimi
Kibatala: Ni sahihi kwamba hakuna Pesa iliyotoka Moja Kwa Moja kutoka kwa Mbowe Kwenda Kwa Moses Lijenje
Shahidi: Hakuna
Kibatala: badala yake Shahidi Unasema Mbowe alituma Laki Tano ambayo iingia Kwenye Simu yako, halafu wewe Ukatoa ya kwako
Mfukoni
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Nakuuliza tena, Kuna Pesa unazo Mfukoni Mwako, na Mbowe katima. Pesa za Kwenye Simu, Je pesa uliyompa Moses Lijenje, ulitoa Kwa Wakala Ukampa au Ulitoa za Kwako Mfukoni
Shahidi: Nilitoa Laki 3 kwenye muamala, Nikachanganya na za Kwangu Mfukoni
Kibatala: Unasema Kwamba Moses Lijenje Ulikutana naye Morogoro Tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 21 August 2020
Kibatala: na hiyo Fedha Ulipokea Lini Kwenye Miamala
Shahidi: Tarehe 20 August 2020
Kibatala: Na hiyo 500,000 ulipokea Kutoka Mbowe Moja kwa Moja?
Shahidi: Hapana Kwa Wakala
Kibatala: Wewe Ulitumiwa TSh ngapi
Shahidi: 500,000
Kibatala: Kwa Wakala Ulitoa TSh Ngapi
Shahidi: TSh 300,000, na Mfukoni nilikuwa na 199,000
Kibatala: Lijenje na Khalfani Bwire Uliwapa TSh ngapi
Shahidi: Niliwapa hiyo Tsh 300,000, Wagawane
Kibatala: Ile Laki 499,000 sasa Ilitoka Wapi
Shahidi: Siwezi Kutoa Pesa yote, Nilikata TSh 1000 la Makato
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Ulimkata Mbowe TSh 1000 katika ile TSh 500,000
Shahidi: Ndiyo Mbowe alikatwa Juu Kwa Juu, TSh 1000 nilijikata Mimi
Kibatala: Ulijikata wewe Kwa Sababu ipi
Shahidi: Ilienda Katika Deposit Ya Kampuni
Kibatala: Kwa hiyo Ile TSh 1000 hujui Imeenda Wapi?
Shahidi: (Kimya)
Jaji: Kuna sehemu Mnashindwa Kuelewana, Wewe Ulitumiwa TSh 500,000, Ukaenda Kutoa 300,000, na Mfukoni Kwako Ukatoa 199,000, Anzieni hapo.
Kibatala: Swali langu hiyo 499,000 Imetoka Wapi, ambayo Ulimwambia Malya.. Na assume Kuwa ile Laki 5 haiwezi Kutoka Yote, Laki 3 nilitoa Kwa sababu Nilikuwa na Balance Yangu
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Mfukoni Kwako Ulikuwa na Laki 2 ni nani aliyekata TSh 1000, Ni wewe au Wakala?
Shahidi: Ni Wakala
Kibatala: Ile Laki 2 Iliyobakia katika Simu yako Ulitoa lini?
Shahidi: Nilitoa Walipo Kuja...... Sikumbuki
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Nipewe Kielelezo namba 20
Kibatala: Shahidi Tafuta Ile Laki Mbili ambayo ilibakia katika simu yako Ulitoa Tarehe Ngapi, Ukipata wewe tuambie..
Shahidi aanaendelea kutafuta Miamala...
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Shahidi ile Nyaraka siyo yake, na Shahidi hajajengewa uwezo Wa Kusoma Ile Nyaraka, Kuokoa Muda, Shahidi aelekezwe Maeneo hayo na wakili..
Kibatala: Sawa Fair enough, Wacha Twende Kwa namna Nyingine
Kibatala: Shahidi Kwani Wewe Unakumbuka ulitoa lini hiyo pesa Kibatala anamfuata Shahidi, Na Kumueleza Kwenye Nyaraka ya Airtel, Ili Kuokoa muda Shahidi ANATUTA TENA..
Shahidi: Kuna Laki Mbili na Nusu
Kibatala: Miye Nimekuuliza Laki Mbili
Shahidi: Laki 2 Hakuna
Kibatala: Baadae Unasema Freeman alikutumia Laki 2 na Tisini na Tisa Je Ilikuwa Tarehe Ngapi
Shahidi: Ilikuwa Tarehe 22 july 2020
Kibatala: Namba Iliyo Ingiza ni 0780900244 Hiyo namba ya nani
Shahidi: Sijui ya nani
Kibatala: Siyo namba ya Mbowe?
Shahidi: Siyo Namba ya Mbowe
Kibatala: Pesa Uliyompatia Ling'wenya na Adamoo ulitoa Mfukoni na yenyewe au Ulitoa kwa Wakala
Shahidi: Nilitoa Kwa Wakala
Kibatala: Ulitoa TSh Ngapi
Shahidi: TSh 170, 000
Kibatala: Tafuta Tarehe 24 July 2020 Mahala ambapo unasa Ulitoa TSh 170,000
Shahidi: Haipo Katika Kielelezo Namba 20
Kibatala: lakini wewe Unasisitiza ulitoa Kwa Wakala
Shahidi: Ndiyo Kwa sababu nilitoa Kwa Serial Namba
Kibatala: Lakini Haipo Katika Kielelezo namba 20
Kibatala: Hiyo namba hapo 0782 237913 ni Namba ya nani
Shahidi: Siwezi Kukumbuka Mpaka niangalie Kwenye Note Book
Kibatala: Hiyo Notebook ipo wapi
Shahidi: Hotelini Kwangu
Kibatala: Hotel Yako Inaitwa Je Vile
Jaji: Kuna ulazima Wa Kutaja Hotel aliyofikia?
Kibatala: Ndiyo Kwasababu Tangu Mwanzo Case Theory Yetu ni Kwamba Hatokei Nyumbani Wala Hotelini sababu amewekwa sehemu
Jaji: Ndiyo Nauliza Kuna Ulazima Wa Kutaja Hotel ambayo anatoka Kuja Kutoa Ushahidi
Kibatala: Sawa Mheshimiwa Jaji Wacha Niendelee
Kibatala: hiyo Namba 0787 555200 ilituma TSh 190,000 Kwenda 0782 237913
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Huo Mhamala unafahamu
Shahidi: Ndiyo lakini Sikumbuki
Kibatala: Hiyo namba Iliyotuma ni Ya Kwako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namba Unaye Mtumia Unaifahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji, Je ni maJukumu gani Moses Lijenje alipewa Kutekeleza Majukumu ya ugaidi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Wewe Binafsi Exactly ni wapi Moses Lijenje alikuwa anaishi Moshi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Tunakweda Kwa Bwire Mheshimiwa Wa Kwanza, Wakati anatoka Tunduma Kuja Morogoro alikuwa anajua anakuja Kufanya Ugaidi
Shahidi: alikuwa Hajui
Kibatala: Na Yeye huyu Khalfani Bwire Una Ushahidi Wowote Wa Kimaandishi Ambao Ulimsainisha Bwire
Shahidi: Sina Ushahidi Wowote
Kibatala: Unayo Meseji ambayo Khalfani Bwire ana acknowledge Brother Asante kwa TSh 150,000 nimepata?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Kuna Majukumu Yoyote Mahususi ambayo unayafahu Kuwa alipewa na Freeman Mbowe Kwenda Kufanya Ugaidi
Shahidi: Khalfani Bwire aliniambia Kwenye simu Tarehe 04 kuwa Bro Samahani tumesha Kengeuka, Wakati huo anasema Yupo Moshi
Kibatala: Khalfani Bwire alipewa Jukumu gani Mahususi la Kutekeleza Ugaidi
Shahidi: alisema Kwamba tumepewa Jukumu la kwenda Kumdhuru Sabaya
Kibatala: alikwambia Kwamba wanaenda Kumdhuru Sabaya Tarehe Ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: namna Mahususi ambayo Bwire alikuwa anaenda Kumdhuru Sabaya Unaifahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Bwire Alikwambia Chochote Kuhusu chochote Kuhusu Bastola aina ya Luger A5340
Shahidi: hajawahi Kuniambia
Kibatala: Bwire aliwahi Kukwambia lolote Kuhusu na Madawa ya Kulevya
Shahidi: hajawahi Kuniambia
Kibatala: Bwire alishawahi Kukwambia Kwamba walikutana Popote Kupanga Mipango Ya Ugaidi
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Bwire alikuwa informer Wako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulimwambia Taarifa hiyo DCI Shahidi: Hapana nilimwambia Kingai
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Bwire Ali confess Kwako
Shahidi: Ndiyo Kibatala Je Ulimwambia Kingai Kwamba Bwire ka' Confess Kwako
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: DCI alikwambia Umwambie Kingai Kila Kitu au Vingine Umfiche
Shahidi: Nimwambie Vyote
Kibatala: Taarifa Muhimu Ka hizo kwanini Hukumwambia Kingai
Shahidi: Taarifa za Muhimu Nilimwambia Kingai
Kibatala: Tarehe 11 August 2020 Ulikutana na Inspector Swila
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Jeshini Kule Kuna Mtu yoyote Ulimwambia Kuwa Bwire ame Confess
Shahidi: Sikumwambia Mtu , Sababu siyo Mahala Sahihi
Kibatala: Kwa hiyo wewe ulimruhusu Bwire Waendelee na Mipango yao, Mipango ipi
Shahidi: Waendelee na Mipango yao ya Kumdhuru Sabaya, Kama Wakiweza
Kibatala: kwa hiyo Baada ya Kumdhuru Sabaya Walitakiwa Kuriport Kwako tena
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Luteni Wa Jeshi la Wananchi Tanzania, uliwaruhusu Kwamba wakatekeleze Mpango wa Kumdhuru Sabaya Kwa sababu wapo Ground?
Shahidi: Ningefanyaje sasa na Watu wapo Ground
Kibatala: Kwani Wakati huo walikuwa weshamdhuru au Bado
Shahidi: Walikuwa Bado, Ndiyo Wapo Kwenye Mpango
Kibatala: Je Baada ya Bwire Ku Confess Kwako, Ulimwambia Afande Kingai
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Kwani Shahidi Wakati wa Tarehe 11 August 2020 ulipoenda kwa Inspector Swila alikwambia Kuwa Bwire alikamatwa
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Je Kingai alikwambia Kuwa Bwire amekamatwa
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Je Maelezo yako si Uliandika Tarehe 12 August 2020
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Maelezo Yako Uliandika Kwamba Bwire Ali Confess
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: Mimi bado nipo Tarehe 11 na Tarehe 12 August 2020
Kibatala: Wakili alikwambia Wakatinakabidhiana Simu mlisainiana Makaratasi Ma ngapi
Shahidi: Makaratasi Manne
Kibatala: Jana Ulitoa Makaratasi Mangapi
Shahidi: Nilitoa Karatasi Moja
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi Kuhusu Makaratasi Matatu
Shahidi: Siku toa kwa sababu Sikupewa
Kibatala: hukupewa na nani
Shahidi: Na Wakili ambaye alikuwa akiniongoza
Kibatala: Unakumbuka ulikuwa Unafanya Mawasiliano na Simu ipi Mara kwa Mara kwa Mara Shahidi: Kwa Samsung ya Torch
Kibatala: Hiyo Samsung ya Torch ndiyo Sumsumg Duo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna Mahala Popote ambapo Umefafanua kwa Jaji Kuwa hiyo Samsung Duo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mara ya Mwisho Kufanya Mawasiliano na Kingai Ulifanya Mara ya Mwisho ni lini
Shahidi: 10 August 2020
Kibatala: Nikukuombea Upewe Samsung DUO utaweza Kuonyesha Call Record zako na Kingai
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namba ya Kingai Unaifahamu
Shahidi: Mpaka Nisome Kwenye Notebook Yangu
Kibatala: Mbayo Ipo wapi
Shahidi: Ipo Hotelini
Kibatala: Sawa Nitakuombea Mahakamani Ruhusa Ya Kufuata Notebook yako
Kibatala: Je Unafahamu hata Basic za Intelligence Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je Wakati Mbowe amajiachia Kuongea na wewe Kwenye simu Kuhusu Mipango hiyo ya Ugaidi
Shahidi: Hakunipigia Simu alisema Kwamba Tuonane
Kibatala: Na Ni simu ipi pia itaonyesha Call Record za Simu Ya Bwire Tarehe 04 August 2020
Shahidi: Ni hiyo Simu ya Samsung Duo
Kibatala: Hivi Ile simu Yako ya Jana Ulikabidhi Simu Lini
Shahidi: Tarehe 11 August 2020
Kibatala: Ulimfafanulia Jaji Kwamba Simu yako inauwezo Wa Kukaa na Chaji zaidi Ya Mwaka Mmoja na Nusu
Shahidi: Hapana
Kibatala: Simu Yako Ilikuwa na Kiasi gani Cha charge Wakati Unamkabidhi
Shahidi: Ilikuwa Chini Kidogo ya Nusu
Kibatala: Ulimfafanulia Jaji Kwanini Simu hii ni tofauti na zile Tatu Kwamba Ina Kaa Na Chaji Mwaka Mmoja na Nusu
Shahidi: Siku fafanua
Kibatala: Ulisema Kwamba Pia Mbowe alikuomba Makampuni yanayo Install Mawasiliano Ya Jeshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulisema Kwamba Pia Mbowe alikuomba Makampuni yanayo Install Mawasiliano Ya Jeshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Hilo Ombi ni kwamba wewe Ulilichukuliaje, La Kawaida au?
Shahidi: Niliona la kawaida tu
Kibatala: na wewe ni Afisa wa Juu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ni sahihi Kwa wewe Afisa Kuwa na Mahusiano na Mawasiliano na Watu Waliofukuzwa Jeshi Kwa Utovu Wa Nidhamu
Shahidi: Kuna Maisha Nje ya Jeshi, Siyo Hawa tu wapo wengine Wengi tunaishi nao Mtaani
Kibatala: Kanuni za Kijeshi Inaruhusiwa Kuwa na Mahusiano na Junior officer kupeana pesa na Kutafutiana kazi
Shahidi: Uraiani inaruhusiwa
Kibatala: Hawa Wangekuwa Watu wabaya au Majambazi usingekiwa na Mahusiano au Mawasiliano nao?
Shahidi: Hawa siyo Majambazi, Ni watu Wazuri
Kibatala: Baada ya Kubadilishana Pesa na Ma' junior Wako wewe Kama Prudent Officer, Ulikuwa na Jukumu la Kijeshi ku' report hilo Jambo
Shahidi: Siku report Ila Kuna sehemu lilikuwa linafanyiwa Uchunguzi
Kibatala: Nilisikia Kuwa umefahamiana na Mbowe tangu 2008
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba wewe Ulishawahi Kutumiwa Pesa na Mbowe
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je ilikuwa Muhimu Kwa Jaji Kujua Kama Alikutumia au Hakukutumia
Shahidi: Haikuwa Muhimu
Kibatala: Hii Namba ya 0754612525 ni Namba ya nani
Shahidi: Ya kwangu
Kibatala: Walikwambia Upande wa Mashitaka Kwamba report inaonyesha Namba hii Katika Taarifa Ya Chunguzi
Shahidi: Sikuambiwa
Kibatala: Unasema Bwire Unamfahamu Vizuri, unajua Bwire alishawahi Kuwa Body Guard Wa Kiongozi Fulani Jeshini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: unasema Ulionana na MBOWE sehemu Nyingine zaidi ya CASA Motel, Ulimwambia Jaji sehemu nyingine inaitwaje
Shahidi: Nilimwambia ni Mikocheni
Kibatala: Ni kweli Ulikuwa, hujui Identity ya Viongozi waliokuwa wanaenda kudhuriwa
Shahidi: Nilikuwa siwajui
Kibatala: Hata Sabaya ulikuwa humjui?
Shahidi: Nilikuwa simjui
Kibatala: Shahidi CDF ni Kiongozi Wa Kitaifa au Siyo Kiongozi Wa Kitaifa
Shahidi: Kiongozi wa Kitaifa
Kibatala: lakini wewe Hukuona sababu Ya Ku report Jeshini
Shahidi: Kimya
Kibatala: Chief of staff Wa Jeshi ni Kiongozi Wa Kitaifa au siyo Kiongozi Wa Kitaifa
Shahidi: Ni Kiongozi Wa Kitaifa
Kibatala: Waziri Wa Ulinzi ni Kiongozi wa Kitaifa au Siyo
Shahidi: Ni Kiongozi Wa Kitaifa
Kibatala: Na Swala lake linaweza Kushughulikiwa Jeshi?
Shahidi: Linaweza Kushughulikiwa na Jeshi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kuhairisha Cross Examination Sababu Ya muda Nitaendelea Jumatatu Kama Wenzangu Wataridhia..
WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: Kufuatia Muda na Ombi la Wakili Kiongozi Wa Jopo LA Utetezi, Nahairisha Mpaka Jumatatu Tarehe 31 January ambapo Shahidi Namba 12 ataendelea Kuwa Kizimbani Kutoa Ushahidi Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi
Jaji anatoka
Leo tena shahidi wa 12 Denis Urio anaendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi ya Mbowe na wenzake: Kesi imeahirishwa hadi 28/01/2022, Luteni Denis Urio kuendelea na ushahidi wake
Fuatana nami kupata yatakayojiri
UPDATES:
Jaji ameingia
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Robert Kidando nipo pamoja na wakili
- Pius Hilla
- Abdallah Chavula
- Jenitreza Kitali
- Nassoro Katuga
- Esther Martin
- Ignasi Mwinuka
- Mawakili wa Serikali Waandamizi na Tulimanywa Majige, Wakili wa Serikali
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji ikikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na wakili
- Seleman Matauka
- Alex Massaba
- Paul Kisabo
- Sisty Aloyce
- Maria Mushi
- Khadija Aron
- Michael Lugina
- Evaresta Kisanga
- John Mallya
- Nashon Nkungu
- Dickson Matata
Jaji anaita Washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na tupo Tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Nasisi pia tupo tayari Kuendelea
Shahidi anapanda Kizimbani
Jaji: Shahidi Jana Ulikuwa Unatoa Ushahidi Wako, Unaulizwa Maswali Chini ya Kiapo na Leo Utaendelea Kuulizwa Maswali Chini ya Kiapo
Wakili John Mallya: Shahidi tunaendelea tulipo Ishia Jana, Mheshimiwa Jaji Naomba Jibu lake la Mwisho
Jaji: ni Kwamba Asipotumia Jina Namba zake Jina lake halitoonekana...
Malya: hivi kazi ya VIP PROTECTION Inafanyikaje
Shahidi: Mheshimiwa Jaji kazi ya VIP PROTECTION Inafanyika kwa mtu yoyote, Kwa Kufuata Sheria na Kanuni za Nchi
Malya: Ni sahihi Kwamba kazi Wanazofanya VIP protection Ni lazima wawe naye Kwa Wajibu wa Kum' protect
Shahidi: Ni sahihi Malya: hawa VIP protection Ni sawa na Body guard?
Shahidi: Sijawahi Kusikia Body Guard mimi
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 26
Malya: Umesema kuwa hawa VIP protection Wanakuwa pamoja na Wanayem' protect, sasa ni somee Meseji ya Tarehe 20 July 2020, Ya Saa Mbili Asubuhi
Shahidi: Hawa wawili Kuanzia Siyo Mbaya Hawawezi Kutelekezwa, Nitakuwa nao Full time
Malya: Kwa Kazi gani
Shahidi: Ulinzi Ndiyo
Malya: Je, kuna meseji nyingine yoyote kwamba kuna mahali Mbowe anasema nitawatuma Kufanya kazi nyingine au uhalifu?
Shahidi: kwenye meseji hazipo
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo Namba 35
Malya: Tumeletewa report kule ulikopeleka simu , Je hii namba ina Jina gani?
Shahidi: Imeandikwa FREE... Ambayo ni namba ya Freeman Aikael Mbowe
Malya: Very Good shahidi umeniongezea information nilikuwa sijui, sasa washa simu yako
Shahidi anabonyeza simu, anasema tayari
Malya: Unasema Ulikuwa Unawasiliana na Mbowe Kupitia Mtandao Wa Telegram
Shahidi: Ndiyo Mtandao Wa Telegram
Malya: Naomba usogee kwa Mheshimiwa Jaji pale kamuonyeshe namba unayosema ume-chat na Mbowe. Je, hapa kuna Jina FREE linaonekana, ukiwa umefungua meseji?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji HAKI YA MUNGU hii ni akaunti ya Mbowe siyo Group, nafungua
Malya: Jina Free Ukifungua Meseji linaonekana au halionekani?
Shahidi: Halionekani lakini ni Akaunti ya Mbowe
Malya: Je, ulitoa Ufafanuzi/Maelezo kuwa Jina FREE halionekani?
Shahidi: Si nilimjibu mimi Bwana, Mimi siyo Mtaalamu Wa IT, Sasa nitoe Maelezo Ya nini
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba atoe jibu
Jaji: Umeelewa Swali? Kwamba Wakati Unasoma Ulitoa Ufafanuzi? Kuwa jina halionekani
Shahidi: Ufafanuzi huo sikutoa
Mahakama: (Kicheko)
Malya: Haya Ulisema Kwamba Mbowe alikuwa nakupa Wishes za Christmas na Mwaka Mpya, je Meseji zimeanza lini
Shahidi: Tarehe 20 July 2020
Malya: Alikuwa anakutakia Heri ya Mwaka Mpya Kupitia nini
Shahidi: alikuwa ananipigia Simu
Malya: Alikuwa anakupigia simu kwa njia ipi
Shahidi: Kwa Telegram
Malya: Je, unafahamu kwamba ukipiga Simu Telegram unabakia na Calls Record
Shahidi: Sina Utaalamu huo
Malya: Je Jana Wakati wa Ushahidi Wako Kama Ulituonyesha WhatsApp Calls na Meseji za Mbowe
Shahidi: aliyechunguza ndiye anafahamu
Malya: Kwa hiyo Mtaalamu anaweza Kuwa amepunguza au ameongeza?
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi hajasema hivyo
Malya: Nitauliza Upya Kuokoa muda, Kilichokufanya Jana usitoe Calls za WhatsApp
Shahidi: nilisema kwamba Mimi Nilikuwa na wasiliana na Mbowe Kwa WhatsApp, Meseji na Telegram
Malya: Sawa Jana Ulionyesha WhatsApp Call wakati wa Ushahidi Wako?
Shahidi: Sikuonyesha
Malya: Ulionyesha namba zingine ambazo Ulikuwa Mbowe alikuwa anakupigia Simu
Shahidi: Sikuonyesha
Shahidi: (Ghafla) Sikuonyesha Kwa sababu..
Malya: sitaki sababu hapa
Shahidi: Sikuonyesha Kwa sababu
Malya: Sijakuuliza kuhusu sababu
Jaji: Shahidi sikiliza swali ndiyo ujibu
Malya: Naomba Kielelezo Namba 28
Malya anamkabidhi shahidi
Malya: Jana ulishindwa Kuiwasha hii simu
Shahidi: Sikushindwa, haikuwaka
Malya: Ulitoa Explanation Kwanini ilishindwa Kuwaka
Shahidi: Nilieza Kwamba simu ina ibovu wa Display, Ukiwasha Hai Display Kitu chochote
Malya: Kama kuna Taarifa ya Muhimu ambayo Mbowe anataka Kujitetea Kutumia hiyo Simu atafanyeje, Utampa akatengeneze
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Wakati natoa Ushahidi Wangu Kuhusu Kukabidhi Simu, Nilisema, Nilienda na Simu moja, Sikujua Kama Nilitakiwa Kukabidhi Simu, Nikauliza kwa sababu gani wakasema sababu ya Uchunguzi, Tarehe 10 nilipeleka simu zingine, na Mimi nilipeleka Simu Ikiwa imedondoka haifanyi kazi
Malya: Aliyechunguza hajasema Kwamba Simu Mbovu, Isipokuwa wewe unaogopa kwa sababu unajua Kilichopo humo hutaki kionekane
Shahidi: Washa wewe
Malya: Mimi siwezi Kuwasha Simu yako
Shahidi: basi awashe hata Mheshimiwa Jaji
Malya: wewe Ndiyo Mwenye Simu Shahidi: basi hayo Mengine ni Maoni
Malya: Kuna report ya hii Simu, Je Jana Ulionyesha Call Logs za mbowe
Shahidi: Sikuonyesha
Malya: Calls za Khalfani Bwire Jana Ulionyesha
Shahidi: Sikuonyesha, Sababu sikuulizwa
Malya: Je, jana Ulionyesha Meseji za Ling'wenya Kuhusu Kuwasiliana nao wasikengeuke
Shahidi: Sikuonyesha sababu sikuziona
Malya: Ni sahihi unasema Kwamba a baada ya kuwapeleka Vijana Wanne Kwa Mbowe Mwisho wa Kuwasiliana naye ilikuwa Tarehe 24
Shahidi: Ndiyo
Malya: Wakati Mbowe anaacha Kupokea Simu yako alikuwa tayari na Vijana Wanne
Shahidi: Ndiyo
Malya: Soma hapa
Shahidi: Kaka Wale Mtu 3 au 4 Ni Muhimu
Malya: Sasa kama Umeshampa Mtu Nne ukitaka uwasiliane naye nini
Shahidi: Nilichokitaka Kwake baada ya kukikosa nikakipata kwa Bwire
Malya: Kwa hiyo Wakati anaacha Kuwasiliana na wewe Hitaji lake alikuwa ameshalimaliza
Shahidi: Ndiyo
Malya: Miji ya Arusha, Dar es Salaam, Mbeya na Mwanza ina masoko mangapi?
Shahidi: Mimi sifahamu anafahamu Mbowe
Malya: Miji niliyotaja ina vituo vya mafuta vingapi?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji najibu swali kama Ifuatavyo anayejua idadi ya vituo vya mafuta ambavyo alipanga kulipua ni Freeman Mbowe
Malya: Shahidi Miji hiyo ina Mikusanyiko Mingapi
Shahidi: Mheshimiwa Jaji mimi sijui ina mikusanyiko mingapi, Ila Mheshimiwa Mbowe ndiye anajua kwa sababu alipanga kulipua
Malya: Ulifika Ofisi za DCI Je Ulifika ukiwa na Simu zako
Shahidi: Ndiyo
Malya: Je, ulieleza Jana Kama Ulikuwa na Simu zako
Shahidi: Mheshimiwa Jaji nilifika kwa DCI nikampa Taarifa, akasema endelea nao
Malya: Maelezo Yako Mazuri ila siyahitaji, Swali langu Ulieleza Kama Ulimuonyesha DCI Simu zako na Mawasiliano ya Mbowe?
Shahidi: Sikueleza
Malya: Unafahamu kwamba DCI ana vifaa Vya Kurekodi?
Shahidi: Mimi sifahamu
Malya: Je, unafahamu kwamba DCI ana vifaa Vya Upelelezi
Shahidi: Mimi sifahamu Kwa sababu, Kazi yangu haikuwa Kufanya Upelelezi Bali Kutafuta Watu wa Kufanya Kazi
Malya: Wakati Khalfani Bwire, Je alikwambia Vifaa wanavyokwenda Kuvitumia
Shahidi: Hakuniambia
Malya: Wakati Unaingia Jeshini ulikuwa na Certificate ya Form Four na Certificate Ya Ufundi
Shahidi: Ni sahihi ya Diesel Engine
Malya: Bwire alikuja Nyuma yako
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Ulikwenda South Africa Kufanya Mafunzo lini
Shahidi: 2010
Malya: Ukawa Mwanafunzi Bora
Shahidi: Hapana
Malya: Kwanini ulipewa zawadi ya Bunduki
Shahidi: Mheshimiwa Jaji, Inaonyesha Jinsi gani Wakili anataka Kuniweka Maneno Mdomoni, Labda yeye ndiyo alipewa Bunduki baada ya kufuzu Law School, anataka Kuficha Uhalifu
Malya: Ulipewa award gani
Shahidi: Sikupewa Award
Malya: Lakini wewe Ulifuzu
Shahidi: Ndiyo
Malya: Wakati Unakwenda Darfur Mara ya kwanza ulikuwa koplo?
Shahidi: Ni sahihi
Malya: na kwenye Jeshi koplo siyo Afisa
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Wakili ananitaka nieleze Kamisheni ya Kijeshi
Jaji: amekuuliza koplo ni Afisa siyo Afisa
Shahidi: Ni Afisa
Malya: Wakati Unakwenda Darfur ulikuwa na Ling'wenya kinachokufanya umkane Ni Kitu gani
Shahidi: Sijamkana, Siwezi Kukumbuka kama Nilikuwa naye
Malya: Shahidi Wewe ni Luteni Wa Jeshi, Je una Degree?
Shahidi: Hapana
Malya: Huna Digrii lakini ni Luteni wa Jeshi
Shahidi: Ndiyo
Malya: Adamoo na Ling'wenya Mlipoachana Morogoro alikwenda Wapi
Shahidi: Walikwenda Dar es Salaam
Malya: Naomba Kielelezo D1, Maelezo aliyo andika Kingai ambapo anasema alimuhoji Ling'wenya akakiri, Soma hapa
Shahidi: Luteni Urio alitupa nauli TSh 87,000 nauli ya kwenda Moshi
Malya: na wewe Umesema Walitoka Kwako Walikwenda Wapi
Shahidi: Nimekwambia Dar es Salaam Siyo Moshi
Malya: Kwenye Nauli uliwapa TSh ngapi
Shahidi: TSh 199,000
Malya: hapo Wao Wameamdika uliwapa TSh Ngapi
Shahidi: Nauli TSh 87,000, Ndivyo walivyo andika wao
Malya: Ulielezea Shahidi Kwenye Ushahidi Wako namba Uliyotumia Kuwasiliana na Bwire ni Namba gani
Shahidi: Sikueleza
Malya: Wakati Mnaenda Kuonana na Swila Mara ya Kwanza Ilikuwa lini
Shahidi: Tarehe 11 August 2020
Malya: Ndiyo Siku hiyo ulitoa Maelezo Yako
Shahidi: Ndiyo
Malya: Nimesikia Siku Unakutana na DCI Mlikutana baadae akaja Kingai
Shahidi: sahihi
Malya: Ulielezea Kuna mtu Yoyote alikuja Kuwa Join Baadae
Shahidi: Kuwa Join wapi?
Malya: Kwenye Kikao cha Siku hiyo na DCI na Kingai
Shahidi: Hakuna Mtu yoyote alikuja Kutujoin Siku hiyo
Malya: Kwenye Meseji ya Mwisho ambayo Mbowe alikutumia, Ukasema Hukueleza, ni kwanini hukutuma Meseji Nyingine Kuuliza Una maana gani
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Baada ya Kupita Muda Hakuna Mawasiliano, Nilimuuliza Bwire Boss wako anajua, Sasa ningejibu Meseji ya Nini
Malya: Na ni Ushahidi Wako Kwamba Ofisi za Swila ni Ghorofa ya Nane Makao Makuu
Shahidi: Ni sahihi
Malya: Mheshimiwa nafikiri Sina Swali la Ziada kwa Shahidi huyu
Anasimama Adv. Dickson Matata
Matata: Nikumbushe Ulionana na Mbowe Tarehe ngapi
Shahidi: Mwezi Wa Saba, 2020 Sikumbuki Tarehe gani
Matata: Na Ulipo Onana naye ndiyo alikwambia anahitaji Vijana Wa Kuambatana naye wa Kuchukua dola
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kwa Maelezo yako Ndiyo alikwambia anahitaji Vijana hao Vijana Kwa ajili ya Kumsaidia Kuwashambulia Viongozi ambao hawaupendi Upinzani
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Ndipo alipokwambia Kwamba anataka Kuhakikisha anachoma Masoko na Vituo Vya Mafuta
Shahidi: Naomba Ni'refresh alisema Kwamba ataleta Taharuki Kwa Kufanya hayo Uliyo niambia
Matata: juzi Ulisema Kwamba Ulifanya Kitu kinaitwa Tactical appreciation, na Mimi Leo nataka tufanye Tactical appreciation ya Kisheria, Wakati anakwambia Mlikuwa Wawili
Shahidi: Ndiyo
Matata: Kwa Lugha Nyingine Hapakwepo na Watu wengine
Shahidi: Sahihi
Matata: tofauti na Siku hiyo, Kuna Siku yoyote aliwahi Kukwambia Jambo hilo au kukuandikia Barua
Shahidi: Hakuna
Matata: Kwa hiyo kwa tafsiri nyingine hatutopata ushahidi wa maandishi au wa sauti au meseji unaoweza kuthibitisha kuwa alikwambia hayo maneno?
Shahidi: Hakuna sauti
Matata: Baada ya Kukwambia Ukaona Inafaa ukatoe Taarifa, Ukaenda kwa DCI, Kwanza Ulimpigia Simu halafu akakupa appointment
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Kwamba Baada ya Kumueleza akamuita Kingai
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Utakubaliana na Mimi Kwamba DCI ni Mtu Mwenye Ujuzi Katika Upelelezi
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kingai alikuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha, Unafahamu Kwamba anakuwa na uzoefu wa Upelelezi
Shahidi: Kwanza Nilikuwa sijui kuwa ni Mpelelezi
Matata: Mtu akiwa Mpelelezi Wa Mkoa ana uzoefu au hana Uzoefu
Shahidi: anakuwa na Uzoefu
Matata: Wewe Kama Komandoo, Katika Kikao hicho na Baada ya Hapo, Hukuona wewe au DCI na Kingai, Hukuona Kuwa Kuna Umuhimu kuwa Msiridhike Kile ambacho umesema, Je Hukuona Kuwa Kuna Umuhimu Wa Kurekodi Voice Notes
Shahidi: Mamlaka labda Ndiyo haikuona Umuhimu
Matata: Wewe Uliona Kuna Umuhimu au Hakuna Umuhimu, Kwamba Usiridhike na Maneno Utengeneze Voice Record
Shahidi: Niliona Kuna Umuhimu
Matata: kwenye huo Umuhimu hukuona Kuna Umuhimu Wa Vinasa Sauti na Meseji ambao Vitasema Exactly Kuwa anataka Kulipua
Masoko
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Mbowe alikuwa alishaniambia Kwa Meneno, asingerudia
Matata: Narudia Swali langu, kwenye huo Umuhimu hukuona Kuna Umuhimu Wa Vinasa Sauti na Meseji ambao Vita, sema Exactly Kuwa anataka Kulipua Masoko
Shahidi: Sikuwa na Vifaa Vya kunasa Sauti
Matata: Freeman Mbowe akikataa leo hakusema, ni ushahidi gani unao mbele ya Mahakama Kwamba Mbowe alisema hayo maneno uliyosema?
Shahidi: Ni ushahidi wa meseji ya kusema "muda umeisha"
Matata: hiyo meseji inayosema muda umeisha ina sehemu inasema kulipua masoko
Shahidi: Hakuna mahali inasema
Matata: hiyo Meseji ina sehemu inasema kushambulia viongozi ambao hawapendi upinzani?
Shahidi: Hakuna mahali inasema hivyo
Matata: Hiyo meseji kuna sehemu inasema kulipua vituo vya mafuta
Shahidi: hakuna mahali inasema hivyo
Matata: Tutoke hapo, Unasema Ulienda Kwa DCI na Kabla ya kwenda Ulimpigia Simu,
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Ulielezea Mahakama Kwamba Ulikuwa Unafahamiana na DCI
Shahidi: Nilieleza, Kuna Mtu aliuliza Kama Nilienda Ofisi ya DCI Mara ngapi
Matata: Mimi Sitaki Habari ya Kwenda Ofisini, DCI Anabadirika, nakuuliza Kama Ulielezea Kwamba Unafahamiana na DCI
Shahidi: Sikueleza
Matata: Ulieleza Mahakamani hapa Kwamba Namba yake Ulipata Wapi
Shahidi: Sikueleza
Matata: Hata hiyo namba yenyewe Ulitaja
Shahidi: Sikutaja
Matata: Ushahidi gani Unathibitisha Kwamba Ulimpigia Simu
Shahidi: Ushahidi ninao kwa sababu nina namba zake na Nilifika Ofisini Kwake
Shahidi: Je ulivitaja hivyo Vitu Wakati Unahojiwa na Upande wa Mashitaka
Shahidi: Sikuvitaja
Matata: Unasema Kwamba Ulienda Kesho Ukasema Una Appointment naye Ukakutana na Secretary Wake
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kwa Maana hiyo Ulifuata Utaratibu wa Umma Wa Jinsi ya Kuingia Ofisi Fulani
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Ulisema Kwamba Ulipofika Ulifuata taratibu za Ofisi za Umma
Shahidi: Nilieleza Kwamba, Nilionyesha Kitambulisho kama Askari
Matata: Ulisema Kwamba Askari apaswi Kufuata Utaratibu Wa Kuingia Ofisi Za Umma
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Mimi Nilieleza Kuwa ni Askari, yeye Ndiye alitakiwa aniambie Kufuata Utaratibu
Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili wa Serikali Abdallah Chavula, Ulisema Kwamba Nyie Askari hamfuati Utaratibu
Shahidi: Sikueleza
Matata: Ulileta Visitors Book Kuonyesha Kweli Ulienda Ofisi Za DCI
Shahidi: Hapana Sikuleta
Matata: Shahidi Wewe ni Mwanajeshi, Ulitakiwa Kufuata Taratibu zote za Kijeshi
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Unapotoka Mkoa Mmoja Kwenda Mkoa Mwingine, unatakiwa Kuwa na Movement Order
Shahidi: Inategemea na Siku Ngapi, Kama Chini ya Siku Tatu unaweza Kwenda bila Movement Order kama zaidi ya Siku Nne Unatakiwa Kuwa na Movement Orde
Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili Abdallah Chavula Uliyasema hayo
Shahidi: sikuyasema
Matata: Unapokuwa Askari Unapoenda Ofisi za Umma si lazima Uwe na Pass
Shahidi: Ni kwenye Kitabu Unachotaka,
Matata: Si lazima uonyeshe Pass
Shahidi: Ndiyo ni lazima
Matata: Umeleta Mahakamani hapa Pass Kwamba Umeruhusiwa Kutoka kazini Kwako
Shahidi: Mheshimiwa Jaji Sijaleta Sikujua I nahitajika Mahakamani
Matata: Tarehe 11 ulienda kwa Inspector Swila na Tarehe 12 Ulimpelekea Simu
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Ulileta Mahakamani Hapa Pass za Umeruhusiwa
Shahidi: Sikuleta, Sikupewa Maelezo
Matata: Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo Namba 20
Matata: Naomba Nikuonyesha Kielelezo namba 20 ambacho Kina Miamala yako ya namba ya Airtel
Matata: Jana Wakati Unahojiwa ulisema Freeman Mbowe alikurushia Kwa Mara ya Kwanza TSh 500,000
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Ukatoa TSh 499,000
Shahidi: Kweli
Jaji: Umeelewa Swali? Anasema Umetumiwa TSh 500,000, Swali Ukatoa kwenye hiyo Fedha kiasi gani?
Shahidi: Ni TSh 499,000
Matata: Kwa Mantiki Nyingine Hukutoa yote Kwa sababu Kuna Makato kidogo
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Kwa hiyo Ulichukua TSh 500,000 Ukatoa TSh 499,000 Je Makato TSh ngapi?
Shahidi: TSh 1000
Matata: Naomba Nikuonyeshe Kwa Siku hiyo, Mheshimiwa Jaji Namuonyesha Muamala Wa Siku hiyo ambapo anasema alitoa Muamala Wa TSh 499,000
Matata: Sasa Shahidi angalia Tarehe 20 July 2020, Kwenye Miamala sehemu ambayo Umeenda Kwa Wakala Ukatoa TSh 499,000
Jaji: anakuuliza Hapo Hapo hapo Kwenye hiyo Nyaraka
Shahidi: Hapa Kwenye Miamala Haipo hiyo 499,000
Matata: Mheshimiwa Jaji naomba ni Muonyeshe Hapo hapo, Kuna Majedwali ambayo Yanaonyesha Receiver Balance kabla ya kutumiwa TSh 500,000 kutoka Kwa Mbowe.. Utakubaliana na Mimi Kwenye akaunti yako palikuwa na TSh 49,646
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Baada ya Kuweka TSh 500,000 balance Ikawa TSh 549,646
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Tarehe hiyo hiyo Ukatoa TSh 300,000
Shahidi: Ni sahihi
Matata: Na Balance Yako Ikabakia 243,646
Shahidi: Ni sahihi
Matata: hebu chukua salio uliokuwa nalo la 549,646 Kutoa 300,000 ukabaki na 243,646 tuone Makato ni TSh ngapi
Amesimama Mmoja Wakili wa Serikali Robert Kidando
Wakili wa Serikali Robert Kidando: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Naona Hajajengewa Misingi Kwamba wakili anauliza ikiwa hayo Makato yapo au hayapo..
Matata: Mheshimiwa Jaji Mimi lengo langu nikutaka kujua kwanini Shahidi atoe TSh 499,000 akatwe TSh 1,000 na atoe TSh 300,000 akatwe Elfu Sita na usheeee..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hicho ndicho alichopaswa Kuulizwa
Matata: Je Shahidi Utakubaliana na Mimi Kwamba Ukitoa TSh 300,000 ikibakia TSh 243,646 Je Elfu 6 inaenda Wapi?
Shahidi: Siwezi Kujua Kama ni Makato au imeenda wapi
Matata: Kwani hiyo Tsh 1000 Mwanzo Ulijuaje Kama ni Makato
Shahidi: (Kimya)
Jaji: Swali lako la Mwisho liasema Kuhusu Elfu 6 nimesharekodi
Mallya anasaidia kufafanua kidogo
Matata: Shahidi Ulitoa maelezo hii TSh 1,000 Ilienda wapi
Shahidi: Sijawahi Kutoa
Matata: Shahidi sasa ulitoa...sorry Mheshimiwa Jaji Kidogo
Matata anapekua Nyaraka hapa
Matata: Shahidi Umesema Freeman Aikael Mbowe alikuwa na Mpango Wa Kulipua Vituo Vya Mafuta, Je Wakati Unahojiwa ulitaja Majina ya Vituo Vya Mafuta
Shahidi: Hakuniambia Vituo Vya mafuta anavyoenda Kulipua Bali alitaja Mikoa tu
Matata: Kwa hiyo ukiulizwa Alitaka Kulipua Vituo gani Morogoro hutakuwa na Majibu
Shahidi: Sitokuwa na Majibu kwa kweli
Matata: Tukisema Utaje Vituo Vya Mafuta alivyo taka Kulipua Mkoa wa Mwanza Utakuwa na Majibu au hutakuwa na Majibu
Shahidi: Mimi sina Majibu, Majibu atakuwa nayo Freeman Mbowe
Matata: Ukiulizwa pia Kuhusu Mkoa wa Dar es Salaam Vituo Vipi Vya Mafuta alitaka Kulipua
Shahidi: Mimi sina Majibu, Majibu anayo Freeman Mbowe, Mimi alinificha
Matata: Ukiulizwa ni eneo gani alipanga Kukata Miti kati ya Mkoa wa Morogoro na Iringa
Shahidi: Hakuniambia ni Eneo gani
Matata: Ukiulizwa, Ukiachana Na Sabaya ni Viongozi gani wengine Walipanga Kuwashambulia
Shahidi: Sikutaja Jina la Kiongozi Yoyote, Hakuniambia Kiongozi Yupi
Matata: Mpaka anakushirikisha bila Shaka alikuwa anakuamini
Shahidi: Ndiyo
Matata: Ukiachana na suala la Kumtafutia Vijana, Je alikueleza kuhusu kumtafutia vilipuzi
Shahidi: Hakunieleza
Matata: Kuhusu kumtafutia silaha za kuwashambulia viongozi
Shahidi: Hakunieleza
Matata: Naomba Kurejesha Kielelezo cha simu .. Ahsante
Mallya: Mheshimiwa Jaji, hata hivyo haiwaki.
Matata anaketi..
Anasimama Wakili Peter Kibatala
Kibatala: Shahidi Nikikuita baba Careen ni sawa?
Shahidi: Ni sawa
Kibatala: Baba Junior
Shahidi: Ni Sawa
Kibatala: Baba Jackson
Shahidi: Ni sawa
Kibatala: Jackson amezaliwa Lini
Shahidi: 17 December 2020
Kibatala: Hospitali gani
Shahidi: Hospitali Ya Mkoa Morogoro
Kibatala: Nani na nani alikwepo
Shahidi: Mke wangu na Jirani
Kibatala: Wewe ni Mkristo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: unasali Kanisa lipi
Shahidi: Parokia Ya Ngerengere, Kigango cha Kizuka
Kibatala: Paroko wako Unamfahamu
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Kwani Kanisani Umeenda Mara ya Mwisho lini?
Shahidi: Juzi juzi
Kibatala: Paroko anayehudumu Ngerengere Unamfahamu
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Katekista anayemsadia Paroko
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: narudia tena Mara ya Mwisho Kanisani Umeenda Lini
Shahidi: Sikumbuki Kusema Kweli
Kibatala: Una Gari ya silver
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Aina gani
Shahidi: Rav 4
Kibatala: Namba zake zipi
Shahidi: T 114 DHL
Kibatala: Toka Mwaka 16 August 2020 hiyo Gari ipo Wapi
Shahidi: Kazini Kwangu Ngerengere
Kibatala: Toka Tarehe 16 August 2020 Gari hii ilikuwa parked Wapi
Shahidi: Nilikuwa natumia, Kila Nilipo ipo
Kibatala: Baada Tarehe 16 August 2020 Gari hii umeitumia
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Umekuja kutoka Morogoro kutoa ushahidi kwenye hii Kesi, na kwamba siyo kutoka kambi fulani ya Jeshi ulikokuwa umetekwa?
Shahidi: Mheshimiwa Jaji (Shahidi kamuita Jaji hapa ana jambo gani?)
Kibatala: Ndugu shahidi RELAX..
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mawakili Uliwakataza Kutoa Mawazo yao Bali Kuulizwa maswali
Kibatala: Shahidi hiyo Gari Ipo wapi
Shahidi: Kambini Kizuka
Kibatala: Umepeleka lini hiyo Gari
Shahidi: Ijumaa Wiki Iliyopita
Kibatala: Utaratibu gani Umetumika kupark hiyo gari
Shahidi: Park at Your Own Risk
Kibatala: Kwa hiyo wewe Kama afisa wa Jeshi unataka Kuniambia Kuwa Una park Gari at Owner's Risk Kambini, Upo serious kweli wewe?
Shahidi: Lipo Katika Parking ya Staff
Kibatala: Bado Kwamba Unaendelea Kusema Gari ipo Parking Owner's Risk?
Shahidi: Hapana Nimeliondoa jibu la Owner's Risk
Kibatala: Jibu lako la Kwanza kwamba Uli park Chini ya Owner's Risk Ulilitoa Chini ya Kiapo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: haya, Turudi tena Kwamba Gari Umei' park Kwa Utaratibu gani
Shahidi: Pale Hakuna Ku'Register, Nilitoka Kwenye Oparation Nikaambiwa Nije kutoa Ushahidi
Kibatala: hapo Maana yake ni Owner's Risk
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: si Ndiyo umeliondoa hilo Jibu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Naiachia Mahakama Twende Eneo Lingine
Kibatala: Mwanzo Ulisema Ulikuwa unapanda Tax huna Gari
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Basi Ujue kwanini Nimekuuliza Kuhusu Gari
Kibatala: Shahidi Fungua Yohana Sura ya 8, Mstari wa 31 Mpaka 39
Shahidi anasoma biblia hapa..
Amemaliza..
Kibatala: Unafahamu Maan ya hilo Neno
Shahidi: Ndiyo Nafahamu
Kibatala: Maana yake ni nini
Shahidi: Tusiogope, Tuseme Kweli
Kibatala: Soma pia Waefeso Sura ya 4 Mstari Wa 25 Mpaka 32
Shahidi anasomeshwa Biblia tena
Kibatala: Je, unafahamu Maana ya hilo Neno
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Maana Yake ni nini
Shahidi: Tusiseme Uongo na tupendane
Kibatala: Kwa Hiyo Unafahamu Kwamba Maisha ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya yapo Mikononi Mwako
Shahidi: Ndiyo najua
Kibatala: na Ulisema Kwamba Mara Ya Kwanza Ulikutana na Mbowe Lini
Shahidi: JULY 2020
Kibatala: Tarehe Ngapi
Shahidi: Sikumbuki ni Tarehe za Kati kati
Kibatala: zipi hizo
Shahidi: Tarehe 10 Mpaka 15
Kibatala: Hizo ndiyo Tarehe za Katikati
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na wewe ni Luten wa Jeshi la Wananchi Tanzania tunalolipenda wote
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Elimu yako ni Form Four
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulipata Divisheni Ngapi
Shahidi: Three ya Point 25
Kibatala: unajua Division Four Inaanza point ngapi
Shahidi: Point 28 ila Sikumbuki Vizuri
Kibatala: Kwa hiyo Unakumbuka au hukumbuki
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Umesoma wapi.?
Shahidi: King'ori Sekondari
Kibatala: Headmaster Wako ni nani
Shahidi: Simkumbuki
Kibatala: Graduation Mlifanya lini
Shahidi: Hatukufanya Graduation
Kibatala: Ukimaliza Form Four lini
Shahidi: Mwaka 1999
Kibatala: Yule Mchungaji Wako anayefundisha Mzumbe Mara ya Mwisho Kuwasiliana naye ni Lini
Shahidi: Sina Mchungaji
Kibatala: Na Nabii Tito anayefundisha Mzumbe Umeacha Kusali Kwake lini
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Habari Nzito ya Mbowe Ulimshirikisha Paroko au Mchungaji
Shahidi: Sikumshirikisha Mtu
Kibatala: lakini Ulishindwa kulala
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: lakini Ukaenda Kumshirikisha nani
Shahidi: DCI na Kingai
Kibatala: Mwingine Je?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Msemo wa Kwamba Askari hawezi Kuwa Raia ila Raia anaweza Kuwa Askari Maana yake nini
Shahidi: Kwamba Ukishakuwa Askari huwezi kuwa Raia, Ila Raia anaweza Kwenda kujifunza Kuwa Askari
Kibatala: Jeshi la Wananchi Tanzania Mnafundishwa Kuwa Jeshi la Polisi ni Jeshi Kweli au si Kweli
Shahidi: Kweli
Kibatala: Raia Akiona Uhalifu unatendeka anaweza Kuzuia Uhalifu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwamba Mwajeshi Akiona Uhalifu Unatendeka anaweza Kuzuia au anaacha utokee alafu ana report Taarifa Polisi
Shahidi: Anazuia Uhalifu
Kibatala: ila wewe Ulikuwa na Mbowe anakwambia Mambo ya Kigaidi ukamuacha
Shahidi: Ndiyo Maana Nilienda Ku report Polisi
Kibatala: Kwani Jeshini si Kuna sehemu ya kwenda Kutoa Taarifa za Kihalifu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Jeshi la Wananchi Tanzania Kuna Kitengo Kina shughulika na Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kuna Jeshi la Navy ambalo kazi yao Ni Kushughulika na Ugaidi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: na bado wewe ni Luteni wa Jeshi kabisa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwani kwa ufahamu wako wewe Jeshi halishirikiani na Jeshi la Polisi
Shahidi: Kama ikihitajika
Kibatala: Kwani Shahidi Kwa Mfano Mbowe angelipua Kituo cha Mafuta Puma pale Mwenge, Jeshi Pale Jirani Wangedhurika au Wasingedhurika
Shahidi: Wangedhurika
Kibatala: Bado Ukaona Usiwaambie Jeshi
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: unasema Kwamba Mbowe alikwambia Kukata Miti wapi
Shahidi: Kukata Miti Kwenye Barabara zote zinazo ingia Mjini
Kibatala: pale Kambi ya Jeshi Lugalo Kuna Barabara ya Kuingia Mjini au Hakuna
Shahidi: Ipo
Kibatala: Kama Wangekata Miti pale Barabara ya Lugalo Jeshi lingedhurika au lisingedhurika
Shahidi: Lingedhurika
Kibatala: Lakini Bado wewe Ukaona Usiwaambie Jeshi
Shahidi: Nilipeleka Taarifa Polisi Kwa sababu wao Wana husika na Uchunguzi
Kibatala: Kati ya Wewe Ulipo pale Mgulani Kambini na Ofisi za DCI, Wapi Ilikuwa Rahisi Kwako Ku report?
Shahidi: Kambini Mgulani
Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa Logic na Common sense
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: haya pale kwa DCI umesema Kwamba Kuna Scanner, Umejitambulisha Kuwa wewe ni Luteni na ukafanyeje
Shahidi: Nikatoa Kitambulisho
Kibatala: Baada ya Pale Ulimwambia Jaji Kwamba Jina lako liliingizwa Kwenye Register
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba sisi tumefika Kwa DCI Mara ngapi
Shahidi: Hapana, Sijui
Kibatala: Nikikukwambia Kwamba pale kwa DCI Nilifika Kumsindikiza Edward Lowassa Mwaka 2017
Shahidi: Ndiyo nitakubali
Kibatala: Unafahamu Kuwa DCI ni Mwanajeshi
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Kuna Mtu alipiga Simu Kwanza Kuhakiki appointment Yako
Shahidi: Hapana Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Wanajeshi hasa DCI ambaye ndiye Kama WAZIRI Mkuu wa Jeshi la Polisi ni watu wa tahadhari kwa sababu ni Watu wana deal na Uhalifu Nchi Nzima?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, Umemwambia Jaji Kwamba Kuna Kitambulisho Ulipewa cha Kuvaa
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Kwa DCI Kuna Askari Kwa ajili ya Kimsindikiza Wanaenda Kwa DCI
Shahidi: Sikumwambia Jaji
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kuna Askari Wa Kukusindikiza Mpaka Kwa PS wa DCI
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Waiting Area ya Ofisi za DCI Makochi ni Rangi gani
Shahidi: Ya Brown
Kibatala: Unauhakika Kwamba Siyo Mekundu
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: Ukifika kwenye Ofisi za DCI PS anakuwa Upande Upi
Shahidi: Upande huu, (anaonyesha Kushoto)
Kibatala: Umebadilsha Sasa hivi eeh?
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba niilipokuwa Ulipokuwa wait Area Kwa DCI iwapo Body Guard Wake Ukiwa Una subiri Kuingia
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je Jana wakati wa Ushahidi Ulizungumzia Meza na Viti, Je Ulizungumzia DCI kuwa Ni Mnene, Mfupi, Mwembamba au Lah
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je Ukaona ni Muhimu tufahamu Viti na Meza na siyo DCI ambaye Ulimfuata
Shahidi: DCI SI anajulikana
Kibatala: anajulikana na nani
Shahidi: Watanzania wote
Kibatala: Je Ulimwambia Jaji Kwamba Utaratibu gani Ulitumia Kutoka
Shahidi: Sijamwambia
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kuwa Ulipokuwa Unatoka Ulisaini Out
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unasema Ulifika Ofisi ya DCI Saa ngapi
Shahidi: Nimefika Majira ya Saa Mbili au Saa Tatu
Kibatala: Je Unafahamu Kwamba Huo Ndiyo Muda wa Kufika DCI
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Kwamba Chini ya Kiapo hapo Luteni Kwamba Siku hiyo DCI alipanda Ngazi Kwa Mguu Mpaka Ghorofa Ya Saba
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo ufahamu Kwamba DCI alikuwa na Umri Miaka zaidi ya 50 na Sasa amestaafu Kwamba alipanda Ngazi
Shahidi: Sifahamu alifikaje Juu
Kibatala: kwa hiyo Wewe Unasema Kwamba DCI Kiongozi Wao Kama. Waziri Mkuu, Kuwa Lift yake Ilikuwa bovu
Shahidi: Hapana, Sifahamu
Kibatala: Jana Ulionyeshwa Simu zako, na Moja ilikuwa na Display ya Mke Wako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Simu zako zote Nne Umepewa, Je Ni wakati gani Uliomba nafasi ya Kungalia Simu yako Namba ya Kingai Kama Kweli uliwasiliana naye?
Shahidi: Hapana Sikumwambia jaji
Kibatala: Je Kwa DCI pia ulimuomba Jaji nafasi ya Kungalia namba ya DCI Kwenye Simu yako?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Sasa Ni saa Saba Kamili, Kama Wenzetu wataridhia Twende Health Break na naomba Niependekeza Kwako Dakika 45
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: Kwa Maana hiyo tuta' break Kwa Muda wa Dakika 45 na Saa Saba na Dakika 45 tutarudi
Jaji amerejea
Kesi imetajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Kwa Upande wa Jamhuri tumetimia Kama Ilivyo kuwa Mwanzoni tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Kama Mwanzo, Wakili John Mallya amepata Udhuru atarejea Baada ya Dakika 10 badala yake naomba Wakili Michael Lugina awakilishe Ingawa ni wakili wa Mshtakiwa Wa Nne
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Naona italeta Shida, Kwa sababu Wakili Michael Lugina Tayari ameshaingia Kwenye Quorum, Mshtakiwa Wa Pili anahitaji Kupata Full representation..
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa Maoni yangu Mimi, Mimi Ndiyo Nina Cross Exermine, Ila Ooohh Kwa Bahati Nzuri ndiyo anaingia... Huyu hapo.. Ikupendeze Kurekodi kuwa Sote Tupo na tupo tayari Kuendelea
Jaji anaandika Kidogo, Mahakama ipo Kimya wakati huu
Jaji: Shahidi nakukumbusha kuwa Ulikuwa Chini ya Kiapo wakati Unatoa Ushahidi Na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo Wakati Unatoa Ushahidi
Jaji: Shahidi nakukumbusha kuwa Ulikuwa Chini ya Kiapo wakati Unatoa Ushahidi Na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo Wakati Unatoa Ushahidi Wakili
Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kwa Hisani ya Mwisho Nikumbushwe Swali lake
Jaji: Kama Iwapo Alikuwa na Simu zake na Kama Aliomba Mahakama atoe humo namba za DCI Akasema Hapana
Kibatala: Unafahamu Kwamba Utambulisho Wa su Moja dhidi ya Nyingine ni IMEI, Je unafahamu
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Mawakili Wenzetu wa Somi waliluomhoza Kutoa Nyaraka fulani hivi
Shahidi: Ndiyo Nakumbuka
Kibatala: Kwahiyo Nyaraka Ile Ilikuwa ni Kuthibitisha Kuwa palikuwa na Makabidhiano kati yako wewe na Inspector Swila
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Inaitwa Techno nini Vile
Shahidi: Tecno CAMMO
Kibatala: Niambie Kama wakati Unaonyeshwa Simu zako zote Nne, Je ulitambua Simu Moja Moja Kwa kutumia IMEI namba Shahidi Hapana, Nilitambua Moja tu
Kibatala: Kwahiyo Kama tuna Simu Nne, Tatu hukuzitambua kwa IMEI namba ya Simu Moja Moja
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: kwa hiyo hii Tecno CAMMO ulitambua Kwa IMEI namba
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa Ushahidi Wako wote hapa umesema Kwamba Unaishi Ngerengere, Je Kuna sehemu Umesema Kwamba unaishi kihonda
Shahidi: Nina Makazi Mawili Ngerengere na Kihonda
Kibatala: Je Ulisema Jana na Leo Kabla Sijakuuliza
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je Kuna Mahala Popote Ulitambua Maneno CAMMO Kama Yapo
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Kuna Maneno gani badala yake
Shahidi: Tecno tu
Kibatala: Je, Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Abdallah Chavula Ulimfafanulia Mheshimiwa Jaji Kwamba hiyo Tecno ndiyo Tecno CAMMO
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Wakati Wa Ushahidi Wako Wote Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Abdallah Chavula, Uliongozwa kutoa Betri na Kusoma IMEI namba na Kumwambia Mheshimiwa Jaji Kama IMEI zinafafana na Inspector Swila Wakati wa Makabidhiano?
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Soma Hapa Pameandikwa Kwamba wewe Luteni Urio unaishi Wapi
Shahidi: Kihonda
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwenye Kielelezo Kuwa wewe Luteni Urio Unaishi Kihonda Shahidi anatikisa kichwa hapa, namna gani..
Kibatala: Mahakamani, Usijibu kwa Kichwa
Shahidi: Sikumwambia Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Soma Hapa
Shahidi: CD/IR/2097/2020
Kibatala: Ni nini hiyo
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Ulifafanua ni nini hicho
Shahidi: Sikufafanua
Kibatala: Kuna IMEI namba Ngapi hapo
Shahidi ameshika Kielelezo cha karatasi moja
Shahidi: Sijui ni IMEI namba ngapi
Kibatala: Unafahamu Inspector Swila alikozitoa hizi IMEI namba au hufahamu
Shahidi: Kwenye Simu yangu
Kibatala: Je, Zipo ngapi hizo IMEI namba zipo ngapi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Hiyo ni Standard Form Document
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Soma hapo chini
Shahidi: Jina na Sahihi ya anayekabidhiwa
Kibatala: Wakati unatoa Ushahidi Jana Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba hiyo ni sahihi yako
Shahidi: Nilimwambia
Kibatala: Soma Hapo Chini ya Mstari Uliochapwa
Shahidi: 11 August 2020 Imeandaliwa Chini ya
Kibatala: ulifafanua Kuwa Kwanini hayo Maelezo Yapo Chini ya Nyaraka
Shahidi: Siku fafanua
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Nyaraka inasema Mimi Luteni Denis Urio Wa Kihonda Morogoro, Na mkabidhi Vitu ambavyo Vimekamatiwa Tarehe Deshi, Kutoka Kwa Mtuhumiwa Deshi, Vitu aina ya Deshi, Ushahidi Wako wewe Tukiangalia Kwenye Deshi tunaweza Kujua ni nini
Shahidi: Sijui ni nini
Kibatala: Mkumbushe Mheshimiwa Jaji Ulisema Simu yako wewe Ulikabidhi sababu ya
Shahidi: Uchunguzi
Kibatala: ambapo Wewe Unaamini ilikuwa Mawasiliano ya wewe na nani
Shahidi: Mheshimiwa Mbowe
Kibatala: Tuache Simu, Turudi Ofisini Kwa DCI
Kibatala: Lengo la Kutaja Meza na Viti Kwa DCI Lengo ilikuwa Kuonyesha Kwamba Ulifika kwa DCI, Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Ulimwambia kuwa Meza ni ya Rangi gani
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Kwakuwa Lengo lako lilikuwa Kuonyesha Unaifahamu Ofisi ya DCI Je Ulisema Juu Palikuwa na nakshi gani
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Kwa kuwa Lengo lako lilikuwa Kuonyesha Unaifahamu Ofisini ya DCI Je Ulisema Juu ya Rangi ya Viti
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je Umwambia Jaji Details zingine Kuhusu ile Ofisi
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kama Ofisi Ya DCI Kuna Bendera ya Taifa
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Sasa Ulimwambia Detail hiyo Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Kwamba Ofisini Kwa DCI kuwa Kuna Picha ambazo zinaonyesha Matukio Mbalimbali ya Utejelezaji Wa Majukumu Yake
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuhusu hilo
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je, ofisini kwa DCI kuna kalenda zaidi ya Tatu
Shahidi: Niliona moja
Kibatala: Ulimwambia kuhusu hiyo kalenda moja
Shahidi: Sikumwambia, na pembeni ya Kiti chake kuna kiti kingine pia sikumwambia Mhe Jaji
Mahakama: (Kicheko)
Kibatala: ahsante kwa taarifa
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Ofisini Kuna Beseni la Kunawa Mikono
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ofisini Kwa DCI palikuwa na Askari Wangapi Wa zamu
Shahidi: Walikuwa wawili Ila Sikumwambia
Kibatala: Kwamba Pale Reception Kuna Magari ya Viongozi Mazuri Mazuri, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana Sikumwambia
Kibatala: Pale Nje Kuna Gari ya Rapid Response, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Umeliona
Shahidi: Sikumwambia, Ila siku hiyo halikuwepo
Kibatala: Unakumbuka Juu ya somo letu la TRUTH SHALL SET YOU FREE?
Shahidi: Ndiyo nalikumbuka
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwanini ulishindwa Kumweka Mheshimiwa Mbowe Chini ya Ulinzi?
Shahidi: Hapana Sikumwambia
Kibatala: Ni nini cha Ziada Kilichoongezeka kutoka Tarehe July 2020 Mpaka Leo hapa Mahakamani
Shahidi: Tuna Amani tu Tanzania
Kibatala: Tarehe ya Katikati ya July 2020, Toka Kipindi Kile Mpaka Leo ni zaidi Ya Mwaka sasa, Je Kuna Kitu cha Ziada ambacho wewe Binafsi Moyoni Mwako ulipata Taarifa ya ziada
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Swali hilo lime Ulizwa na kujibiwa, Amani.
Kibatala: Twende Eneo Lingine, Unasema Baada ya Kupata Taarifa za Freeman Mbowe Kupanga Uhalifu, Bado Unasema hukumbuki Tarehe?
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Swila anasemw alifungua Faili lake Tarehe 18 July 2020, Unaweza Kukumbuka Siku Uliyoenda Kwa DCI
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: sisi shida yetu ilikuwa ni Kutaka Kujua Kama Ulifika kwa DCI lini Tujue kuwa Faili lilitungwa au la
Shahidi: Siwezi Kukumbuka Tarehe
Kibatala: Kwa Mujibu wa Bando Kitita la Commital hata DCI hajui Wewe Ulifika Lini Ofisini Kwake
Shahidi: Siwezi Kumsemea
Kibatala: Je Unakumbuka Tarehe Uliyokutana na Khalfani Bwire
Shahidi: Sikumbuki ila ilikuwa Mwenzi Wa Saba
Kibatala: Je, Khalfani Bwire Uliwasiliana naye lini akiwa Tunduma
Shahidi: Sikumbuki ila Katikakati ya Mwezi Wa saba
Kibatala: Na Adam Kasekwa Uliwasiliana naye lini
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Kwa Mujibu Wa Mohammed Ling'wenya katika Maelezo Yake anasema Kwamba Tarehe 24 July 2020 Mkakutana Morogoro Shahidi Ndiyo
Kibatala: Siku Sita Tangu Inspector Swila aseme alifungua Faili Tarehe 18
Shahidi: Sijui
Kibatala: Si upige Hesabu Kutoka Tarehe 18 July 2020 Mpaka 24 July 2020 ni Siku ngapi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Umeanza Kuwakusanya hawa baada ya Tarehe 20 July 2020
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Na wewe ndiyo Ulikuwa Unawafahamu hawa wala Siyo Mbowe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaweza Kutuisaidia Kuwa Kwanini Inspector Swila alifungua Faili la Kula Njama Tarehe 18 July 2020 Wakati Wakati Umekutana hawa Vijana Tarehe 20 Mpaka 24
Shahidi: Sijui sasa
Kibatala: Je wewe Ulikula Njama na Mbowe.
Shahidi: Sijala Njama na Mbowe
Kibatala: Kwani Shahidi suala hili Kuna Mtu Zaidi Yako alienda Kutoa Taarifa Kwa DCI
Shahidi: Ni Mimi Pekee Yangu ndiye niliye Mwambia DCI Kibatala Kwani wewe Ulimueleza Jaji Kwamba Mbowe alikuwa tayari ana vijana Wengine
Shahidi: Sikumwambia Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Baada ya Kutoka Kwa DCI ulienda Wapi
Shahidi: Morogoro
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Ulitumia Usafiri gani Kurudi Morogoro
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je, baada ya Kutoka Kwa DCI Ulifika Nyumbani Kwako Usiku
Shahidi: Nilifika Jioni Jioni
Kibatala: Tuambie nani alikwepo Nyumbani Kwako ulimkuta Siku hiyo
Shahidi: Mke wangu
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba alikwepo Mtoto wako Careen Nyumbani kwako
Shahidi: Alikwepo Mke wangu na Watoto
Kibatala: Unabadilisha Enheeeee
Kibatala: haya Ulitumia Basi gani Kurudi Morogoro
Shahidi: Abood bus Service
Kibatala: Je Unayo ticket
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mimi na Malya tunafahamu CASA Motel, na Kila Gari Inayoingia pale inasajiliwa
Shahidi: Sijui
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Gari yako Tax ile Ilisajiliwa pale Mlangoni
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba CASA Motel ni Nyumba ya Chini au Ghorofa
Shahidi: Ni Ghorofa
Kibatala: Ndiyo hiyo si Taarifa Muhimu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji sasa
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba mlilaa sehemu gani, Nje au Ndani
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba mlikaa kwenye Makochi ya namna gani
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Ushahidi Wako Kuwa Mbowe Mwenyekiti Wa Chadema Taifa, alikuwa CASA Motel Bila Dereva wala Mlinzi
Shahidi: Nilisema Alitupokea Kijana Mmoja akasema Chairman Yule Pale
Kibatala: Sasa Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Hapana Siku Mwambia
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba aliyekuwa anaye wahudumia ni Mwanamke au Mwanaume
Shahidi: Hapa Sikumwambia
Kibatala: Je wewe Luteni Wa Jeshi Moja ya ulichojifunza ni Kufanya kazi Katika High Pressure, Si Ndiyo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Moja ya Ulichojifunza ni Kuongeza umakini
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa Afisa wa JWTZ nimesoma tangu Wakati wa Willy Gamba, Luteni Unaitwa sehemu na Mtu ambaye humjui unaenda tu?
Shahidi: Nilikuwa namsikia kwenye TV tu
Kibatala: Mtu akakupigia yeye ni Peter Kibatala akakuita Goba Unakuja tu
Shahidi: Alikuwa anawasiliana Siku nyingi
Kibatala: Ulipokuwa Pale Kwa Mhe Freeman Mbowe, Nani alilipa Chakula
Shahidi: Freeman Mbowe
Kibatala: Nani alilipa Tax Yako
Shahidi: Freeman Mbowe
Kibatala: Pamoja na Kukwambia Taarifa za Ugaidi bado Ukapokea Fadhila zake
Shahidi: Siyo Taarifa za Ugaidi, Ni Uhalifu tu
Kibatala: Kwa hiyo Baada ya Kukwambia Mipango hiyo ya Uhalifu, Bado alilipia Tax Yako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, wewe Kama Luten wa Jeshi, Ulimwambia Mtu yoyote Kuhusu Swala hilo
Shahidi: Nilimwambia CEO wangu
Kibatala: Ulimwambia lini
Shahidi: Tarehe 05 August 2020
Kibatala: hayo Mambo Uliyo enda Kumwambia CEO wako, Yapo Katika Maelezo Yako Uliyo andika Kwa Inspector Swila
Shahidi: Hayapo Katika Maelezo yangu
Kibatala: hayo Unayosema Kwamba Ulienda Ku report Kwa CEO wako, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Sikumbuki Kama nilimwambia
Kibatala: Mimi Nikikwambia hujamwambia?
Shahidi: No, Sikumbuki nilitamka Kwenye situation gani
Kibatala: Mlikaa na Mbowe pale CASA Motel akakwambia Masuala Kadhaa wa Kadhaa
Shahidi: CASA Motel Siyo Wakati wa hiyo Mipango, CASA Motel ni Wakati wa 2012
Kibatala: Baada ya Kujua Mbowe ana mipango ya Kigaidi Uliendelea Kuwasiliana naye
Shahidi: Ndiyo nilikuwa naendelea Kuwasiliana naye ili Kumtafutia Watu wa Kutekeleza Mipango yake
Kibatala: Ni kweli Kwamba Ulishiriki Mipango ya Kigaidi
Shahidi: Sikushiriki
Kibatala: Nani aliyemuwezesha Mbowe Kupata hao Vijana Kutekeleza Mipango ya Kigaidi
Shahidi: Ni Mimi
Kibatala: Wewe ni Afisa Wa Jeshi, Je Unafahamu Sheria yoyote Inayoruhusu wewe Kutafuta Vijana Kutekeleza Mipango ya Kigaidi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wewe si Ulikuwa Darfur
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kilichokufanya Mpaka Muende Darfur ni Janja Weed na SPLM
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Ingewezekana Wewe Askari Umeenda Darfur Chini ya Chapter Seven Ukawa Unafanya Mawasiliano ya Simu na Kiongozi wa Janja Weed?
Shahidi: Nisingeeleweka
Kibatala: Ni Kwa Sababu Yule alikuwa Mhalifu wa Amani?
Shahidi: Ndiyo alikuwa Mhalifu Wa Amani
Kibatala: lakini huku Tanzania ulikuwa Unawasiliana na Freeman Mbowe
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Je Kule Darfur Ungemuita Kiongozi Wa Janja Weed "Bro" Ungeeleweka?
Shahidi: Nisingeeleweka
Kibatala: Kwani Kule Darfur Si palikuwa na Askari Wengine Wa Chapter Six Wanaofanya Peace Keeping wapo armed na wanafanya Demining?
Kibatala: na Kwamba Wewe Kabla ya Tarehe 05 August 2020 Hakuna Uliyekuwa Umempa Taarifa Ndani ya Jeshi Kuwa Umepewa Kazi na DCI na Kingai
Shahidi: Sikumwambia Mtu
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba huyo Dogo Adam Kasekwa anajina lingine anaitwa Adamoo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mohammed Ling'wenya anajina Lingine anaitwa DOYI
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Unafahamu Moses Lijenje Yupo wapi
Shahidi: Nilimkabidhi Kwa Freeman Mbowe
Kibatala: Moses Lijenje Yupo Hai au amekufa
Shahidi: Nilimkabidhi Freeman Mbowe
Kibatala: ulimkabidhi Wapi
Shahidi: Nilimpigia Simu akasema Kwamba ameshafika
Kibatala: Nikuonyeshe Meseji zako utanionyesha sehemu ambayo ina meseji Kuwa Mbowe anasema Umemkabidhi?
Shahidi: Hakuna. Alinipigia Simu
Kibatala: Jana Ulionyesha Sauti zako za Kukabidhiana Kwa Mbowe Moses Lijenje
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wewe Mpaka Unaonana na Moses Lijenje, alikuwa anafahamu Masuala ya Ugaidi
Shahidi: Hapana, Masuala ya Ulinzi
Kibatala: Wewe Ulionana Lini tena na Moses Lijenje Baada ya Tarehe 21 August 2020
Shahidi: Sikuonana naye tena
Kibatala: Walicho ongea Na Mbowe Huko Hai au Popote unakifahamu
Shahidi: Sikifahamu
Kibatala: Unaweza kuonyesha chochote kile au sauti ukionyeshe kwa mheshimiwa Jaji kwamba Freeman Mbowe alimwambia Lijenje wakafanye ugaidi?
Shahidi: Sijawahi kusikia mimi
Kibatala: Ni sahihi kwamba hakuna Pesa iliyotoka Moja Kwa Moja kutoka kwa Mbowe Kwenda Kwa Moses Lijenje
Shahidi: Hakuna
Kibatala: badala yake Shahidi Unasema Mbowe alituma Laki Tano ambayo iingia Kwenye Simu yako, halafu wewe Ukatoa ya kwako
Mfukoni
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Nakuuliza tena, Kuna Pesa unazo Mfukoni Mwako, na Mbowe katima. Pesa za Kwenye Simu, Je pesa uliyompa Moses Lijenje, ulitoa Kwa Wakala Ukampa au Ulitoa za Kwako Mfukoni
Shahidi: Nilitoa Laki 3 kwenye muamala, Nikachanganya na za Kwangu Mfukoni
Kibatala: Unasema Kwamba Moses Lijenje Ulikutana naye Morogoro Tarehe ngapi
Shahidi: Tarehe 21 August 2020
Kibatala: na hiyo Fedha Ulipokea Lini Kwenye Miamala
Shahidi: Tarehe 20 August 2020
Kibatala: Na hiyo 500,000 ulipokea Kutoka Mbowe Moja kwa Moja?
Shahidi: Hapana Kwa Wakala
Kibatala: Wewe Ulitumiwa TSh ngapi
Shahidi: 500,000
Kibatala: Kwa Wakala Ulitoa TSh Ngapi
Shahidi: TSh 300,000, na Mfukoni nilikuwa na 199,000
Kibatala: Lijenje na Khalfani Bwire Uliwapa TSh ngapi
Shahidi: Niliwapa hiyo Tsh 300,000, Wagawane
Kibatala: Ile Laki 499,000 sasa Ilitoka Wapi
Shahidi: Siwezi Kutoa Pesa yote, Nilikata TSh 1000 la Makato
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Ulimkata Mbowe TSh 1000 katika ile TSh 500,000
Shahidi: Ndiyo Mbowe alikatwa Juu Kwa Juu, TSh 1000 nilijikata Mimi
Kibatala: Ulijikata wewe Kwa Sababu ipi
Shahidi: Ilienda Katika Deposit Ya Kampuni
Kibatala: Kwa hiyo Ile TSh 1000 hujui Imeenda Wapi?
Shahidi: (Kimya)
Jaji: Kuna sehemu Mnashindwa Kuelewana, Wewe Ulitumiwa TSh 500,000, Ukaenda Kutoa 300,000, na Mfukoni Kwako Ukatoa 199,000, Anzieni hapo.
Kibatala: Swali langu hiyo 499,000 Imetoka Wapi, ambayo Ulimwambia Malya.. Na assume Kuwa ile Laki 5 haiwezi Kutoka Yote, Laki 3 nilitoa Kwa sababu Nilikuwa na Balance Yangu
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Mfukoni Kwako Ulikuwa na Laki 2 ni nani aliyekata TSh 1000, Ni wewe au Wakala?
Shahidi: Ni Wakala
Kibatala: Ile Laki 2 Iliyobakia katika Simu yako Ulitoa lini?
Shahidi: Nilitoa Walipo Kuja...... Sikumbuki
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba Nipewe Kielelezo namba 20
Kibatala: Shahidi Tafuta Ile Laki Mbili ambayo ilibakia katika simu yako Ulitoa Tarehe Ngapi, Ukipata wewe tuambie..
Shahidi aanaendelea kutafuta Miamala...
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Shahidi ile Nyaraka siyo yake, na Shahidi hajajengewa uwezo Wa Kusoma Ile Nyaraka, Kuokoa Muda, Shahidi aelekezwe Maeneo hayo na wakili..
Kibatala: Sawa Fair enough, Wacha Twende Kwa namna Nyingine
Kibatala: Shahidi Kwani Wewe Unakumbuka ulitoa lini hiyo pesa Kibatala anamfuata Shahidi, Na Kumueleza Kwenye Nyaraka ya Airtel, Ili Kuokoa muda Shahidi ANATUTA TENA..
Shahidi: Kuna Laki Mbili na Nusu
Kibatala: Miye Nimekuuliza Laki Mbili
Shahidi: Laki 2 Hakuna
Kibatala: Baadae Unasema Freeman alikutumia Laki 2 na Tisini na Tisa Je Ilikuwa Tarehe Ngapi
Shahidi: Ilikuwa Tarehe 22 july 2020
Kibatala: Namba Iliyo Ingiza ni 0780900244 Hiyo namba ya nani
Shahidi: Sijui ya nani
Kibatala: Siyo namba ya Mbowe?
Shahidi: Siyo Namba ya Mbowe
Kibatala: Pesa Uliyompatia Ling'wenya na Adamoo ulitoa Mfukoni na yenyewe au Ulitoa kwa Wakala
Shahidi: Nilitoa Kwa Wakala
Kibatala: Ulitoa TSh Ngapi
Shahidi: TSh 170, 000
Kibatala: Tafuta Tarehe 24 July 2020 Mahala ambapo unasa Ulitoa TSh 170,000
Shahidi: Haipo Katika Kielelezo Namba 20
Kibatala: lakini wewe Unasisitiza ulitoa Kwa Wakala
Shahidi: Ndiyo Kwa sababu nilitoa Kwa Serial Namba
Kibatala: Lakini Haipo Katika Kielelezo namba 20
Kibatala: Hiyo namba hapo 0782 237913 ni Namba ya nani
Shahidi: Siwezi Kukumbuka Mpaka niangalie Kwenye Note Book
Kibatala: Hiyo Notebook ipo wapi
Shahidi: Hotelini Kwangu
Kibatala: Hotel Yako Inaitwa Je Vile
Jaji: Kuna ulazima Wa Kutaja Hotel aliyofikia?
Kibatala: Ndiyo Kwasababu Tangu Mwanzo Case Theory Yetu ni Kwamba Hatokei Nyumbani Wala Hotelini sababu amewekwa sehemu
Jaji: Ndiyo Nauliza Kuna Ulazima Wa Kutaja Hotel ambayo anatoka Kuja Kutoa Ushahidi
Kibatala: Sawa Mheshimiwa Jaji Wacha Niendelee
Kibatala: hiyo Namba 0787 555200 ilituma TSh 190,000 Kwenda 0782 237913
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Huo Mhamala unafahamu
Shahidi: Ndiyo lakini Sikumbuki
Kibatala: Hiyo namba Iliyotuma ni Ya Kwako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namba Unaye Mtumia Unaifahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji, Je ni maJukumu gani Moses Lijenje alipewa Kutekeleza Majukumu ya ugaidi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Wewe Binafsi Exactly ni wapi Moses Lijenje alikuwa anaishi Moshi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Tunakweda Kwa Bwire Mheshimiwa Wa Kwanza, Wakati anatoka Tunduma Kuja Morogoro alikuwa anajua anakuja Kufanya Ugaidi
Shahidi: alikuwa Hajui
Kibatala: Na Yeye huyu Khalfani Bwire Una Ushahidi Wowote Wa Kimaandishi Ambao Ulimsainisha Bwire
Shahidi: Sina Ushahidi Wowote
Kibatala: Unayo Meseji ambayo Khalfani Bwire ana acknowledge Brother Asante kwa TSh 150,000 nimepata?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Kuna Majukumu Yoyote Mahususi ambayo unayafahu Kuwa alipewa na Freeman Mbowe Kwenda Kufanya Ugaidi
Shahidi: Khalfani Bwire aliniambia Kwenye simu Tarehe 04 kuwa Bro Samahani tumesha Kengeuka, Wakati huo anasema Yupo Moshi
Kibatala: Khalfani Bwire alipewa Jukumu gani Mahususi la Kutekeleza Ugaidi
Shahidi: alisema Kwamba tumepewa Jukumu la kwenda Kumdhuru Sabaya
Kibatala: alikwambia Kwamba wanaenda Kumdhuru Sabaya Tarehe Ngapi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: namna Mahususi ambayo Bwire alikuwa anaenda Kumdhuru Sabaya Unaifahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Bwire Alikwambia Chochote Kuhusu chochote Kuhusu Bastola aina ya Luger A5340
Shahidi: hajawahi Kuniambia
Kibatala: Bwire aliwahi Kukwambia lolote Kuhusu na Madawa ya Kulevya
Shahidi: hajawahi Kuniambia
Kibatala: Bwire alishawahi Kukwambia Kwamba walikutana Popote Kupanga Mipango Ya Ugaidi
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Bwire alikuwa informer Wako
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulimwambia Taarifa hiyo DCI Shahidi: Hapana nilimwambia Kingai
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Bwire Ali confess Kwako
Shahidi: Ndiyo Kibatala Je Ulimwambia Kingai Kwamba Bwire ka' Confess Kwako
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: DCI alikwambia Umwambie Kingai Kila Kitu au Vingine Umfiche
Shahidi: Nimwambie Vyote
Kibatala: Taarifa Muhimu Ka hizo kwanini Hukumwambia Kingai
Shahidi: Taarifa za Muhimu Nilimwambia Kingai
Kibatala: Tarehe 11 August 2020 Ulikutana na Inspector Swila
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Jeshini Kule Kuna Mtu yoyote Ulimwambia Kuwa Bwire ame Confess
Shahidi: Sikumwambia Mtu , Sababu siyo Mahala Sahihi
Kibatala: Kwa hiyo wewe ulimruhusu Bwire Waendelee na Mipango yao, Mipango ipi
Shahidi: Waendelee na Mipango yao ya Kumdhuru Sabaya, Kama Wakiweza
Kibatala: kwa hiyo Baada ya Kumdhuru Sabaya Walitakiwa Kuriport Kwako tena
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Luteni Wa Jeshi la Wananchi Tanzania, uliwaruhusu Kwamba wakatekeleze Mpango wa Kumdhuru Sabaya Kwa sababu wapo Ground?
Shahidi: Ningefanyaje sasa na Watu wapo Ground
Kibatala: Kwani Wakati huo walikuwa weshamdhuru au Bado
Shahidi: Walikuwa Bado, Ndiyo Wapo Kwenye Mpango
Kibatala: Je Baada ya Bwire Ku Confess Kwako, Ulimwambia Afande Kingai
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Kwani Shahidi Wakati wa Tarehe 11 August 2020 ulipoenda kwa Inspector Swila alikwambia Kuwa Bwire alikamatwa
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Je Kingai alikwambia Kuwa Bwire amekamatwa
Shahidi: Hakuniambia
Kibatala: Je Maelezo yako si Uliandika Tarehe 12 August 2020
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Maelezo Yako Uliandika Kwamba Bwire Ali Confess
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: Mimi bado nipo Tarehe 11 na Tarehe 12 August 2020
Kibatala: Wakili alikwambia Wakatinakabidhiana Simu mlisainiana Makaratasi Ma ngapi
Shahidi: Makaratasi Manne
Kibatala: Jana Ulitoa Makaratasi Mangapi
Shahidi: Nilitoa Karatasi Moja
Kibatala: Ulitoa Ufafanuzi Kuhusu Makaratasi Matatu
Shahidi: Siku toa kwa sababu Sikupewa
Kibatala: hukupewa na nani
Shahidi: Na Wakili ambaye alikuwa akiniongoza
Kibatala: Unakumbuka ulikuwa Unafanya Mawasiliano na Simu ipi Mara kwa Mara kwa Mara Shahidi: Kwa Samsung ya Torch
Kibatala: Hiyo Samsung ya Torch ndiyo Sumsumg Duo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna Mahala Popote ambapo Umefafanua kwa Jaji Kuwa hiyo Samsung Duo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mara ya Mwisho Kufanya Mawasiliano na Kingai Ulifanya Mara ya Mwisho ni lini
Shahidi: 10 August 2020
Kibatala: Nikukuombea Upewe Samsung DUO utaweza Kuonyesha Call Record zako na Kingai
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Namba ya Kingai Unaifahamu
Shahidi: Mpaka Nisome Kwenye Notebook Yangu
Kibatala: Mbayo Ipo wapi
Shahidi: Ipo Hotelini
Kibatala: Sawa Nitakuombea Mahakamani Ruhusa Ya Kufuata Notebook yako
Kibatala: Je Unafahamu hata Basic za Intelligence Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Je Wakati Mbowe amajiachia Kuongea na wewe Kwenye simu Kuhusu Mipango hiyo ya Ugaidi
Shahidi: Hakunipigia Simu alisema Kwamba Tuonane
Kibatala: Na Ni simu ipi pia itaonyesha Call Record za Simu Ya Bwire Tarehe 04 August 2020
Shahidi: Ni hiyo Simu ya Samsung Duo
Kibatala: Hivi Ile simu Yako ya Jana Ulikabidhi Simu Lini
Shahidi: Tarehe 11 August 2020
Kibatala: Ulimfafanulia Jaji Kwamba Simu yako inauwezo Wa Kukaa na Chaji zaidi Ya Mwaka Mmoja na Nusu
Shahidi: Hapana
Kibatala: Simu Yako Ilikuwa na Kiasi gani Cha charge Wakati Unamkabidhi
Shahidi: Ilikuwa Chini Kidogo ya Nusu
Kibatala: Ulimfafanulia Jaji Kwanini Simu hii ni tofauti na zile Tatu Kwamba Ina Kaa Na Chaji Mwaka Mmoja na Nusu
Shahidi: Siku fafanua
Kibatala: Ulisema Kwamba Pia Mbowe alikuomba Makampuni yanayo Install Mawasiliano Ya Jeshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulisema Kwamba Pia Mbowe alikuomba Makampuni yanayo Install Mawasiliano Ya Jeshi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Hilo Ombi ni kwamba wewe Ulilichukuliaje, La Kawaida au?
Shahidi: Niliona la kawaida tu
Kibatala: na wewe ni Afisa wa Juu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ni sahihi Kwa wewe Afisa Kuwa na Mahusiano na Mawasiliano na Watu Waliofukuzwa Jeshi Kwa Utovu Wa Nidhamu
Shahidi: Kuna Maisha Nje ya Jeshi, Siyo Hawa tu wapo wengine Wengi tunaishi nao Mtaani
Kibatala: Kanuni za Kijeshi Inaruhusiwa Kuwa na Mahusiano na Junior officer kupeana pesa na Kutafutiana kazi
Shahidi: Uraiani inaruhusiwa
Kibatala: Hawa Wangekuwa Watu wabaya au Majambazi usingekiwa na Mahusiano au Mawasiliano nao?
Shahidi: Hawa siyo Majambazi, Ni watu Wazuri
Kibatala: Baada ya Kubadilishana Pesa na Ma' junior Wako wewe Kama Prudent Officer, Ulikuwa na Jukumu la Kijeshi ku' report hilo Jambo
Shahidi: Siku report Ila Kuna sehemu lilikuwa linafanyiwa Uchunguzi
Kibatala: Nilisikia Kuwa umefahamiana na Mbowe tangu 2008
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba wewe Ulishawahi Kutumiwa Pesa na Mbowe
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Je ilikuwa Muhimu Kwa Jaji Kujua Kama Alikutumia au Hakukutumia
Shahidi: Haikuwa Muhimu
Kibatala: Hii Namba ya 0754612525 ni Namba ya nani
Shahidi: Ya kwangu
Kibatala: Walikwambia Upande wa Mashitaka Kwamba report inaonyesha Namba hii Katika Taarifa Ya Chunguzi
Shahidi: Sikuambiwa
Kibatala: Unasema Bwire Unamfahamu Vizuri, unajua Bwire alishawahi Kuwa Body Guard Wa Kiongozi Fulani Jeshini
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: unasema Ulionana na MBOWE sehemu Nyingine zaidi ya CASA Motel, Ulimwambia Jaji sehemu nyingine inaitwaje
Shahidi: Nilimwambia ni Mikocheni
Kibatala: Ni kweli Ulikuwa, hujui Identity ya Viongozi waliokuwa wanaenda kudhuriwa
Shahidi: Nilikuwa siwajui
Kibatala: Hata Sabaya ulikuwa humjui?
Shahidi: Nilikuwa simjui
Kibatala: Shahidi CDF ni Kiongozi Wa Kitaifa au Siyo Kiongozi Wa Kitaifa
Shahidi: Kiongozi wa Kitaifa
Kibatala: lakini wewe Hukuona sababu Ya Ku report Jeshini
Shahidi: Kimya
Kibatala: Chief of staff Wa Jeshi ni Kiongozi Wa Kitaifa au siyo Kiongozi Wa Kitaifa
Shahidi: Ni Kiongozi Wa Kitaifa
Kibatala: Waziri Wa Ulinzi ni Kiongozi wa Kitaifa au Siyo
Shahidi: Ni Kiongozi Wa Kitaifa
Kibatala: Na Swala lake linaweza Kushughulikiwa Jeshi?
Shahidi: Linaweza Kushughulikiwa na Jeshi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kuhairisha Cross Examination Sababu Ya muda Nitaendelea Jumatatu Kama Wenzangu Wataridhia..
WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: Kufuatia Muda na Ombi la Wakili Kiongozi Wa Jopo LA Utetezi, Nahairisha Mpaka Jumatatu Tarehe 31 January ambapo Shahidi Namba 12 ataendelea Kuwa Kizimbani Kutoa Ushahidi Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi
Jaji anatoka