Anamaanisha master's degree itambulike kwenye mifumo ya ajira, Yani iwe na general impact Kama ambavyo mtu mwenye diploma akienda kusoma degree akirudi anafanyiwa recategorization..ambapo kwasasa master's degree haina impact.
Ndio..ikiwezekana na PhD kabisa..itambulike.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shime shime shime watumishi wenzangu ...asiye na mwana aeleke jiwe.

Tunapoelekea Mei Mosi ya kwanza ya Rais Samia S. Hassan akiwa katimiza mwaka mmoja kazini si vibaya tukatanguliza yale tunayotarajia kusikia toka kwake.

Kama alivyotuahidi nyongeza ya mshahara mwaka huu bila shaka hilo limeisha ila ni wazi haki za watumishi zimekandamizwa kwa muda mrefu sana.

Basi si vibaya tukimueleza Mama nini hasa tungependa toka kwake. Ningependa kusema machache.

1. Haki ya Mtumishi kuhama kituo cha kazi
Hili limekuwa ni tatizo sugu na la muda mrefu sana. Watumishi wa serikali hasa walimu wamekuwa wakipokwa haki yao ya kuhama kwa hiyari. Serikali imekuwa ikitoa kigezo kuwa itasababisha upungufu wa watumishi huko watokako. Sijui hoja hii ina mashiko gani maana wengine wakitoka wengine wanakuja.

Lakini hata sababu ya msingi kabisa ya kwenda unganisha familia watumishi hawasikilizwi hii hupelekea kuibuka kwa matapeli na watumishi wanapigwa sana pesa wanapopigania uhamisho.

Tungependa Mama alitizame hili kwa uzito wake.

2. Fao la uzazi
Nyinyi ni mashahidi nafikiri wengi hapa mnafahamu haki hii ambayo watumishi wamepunjwa. Tungependa Mama alitizame hili pia kwa macho yake mazuri kabisaa.

3. Annual increment
Hapa wala hakuna maneno mengi nafikiri ninyi ni mashahidi Awamu ya tano ilichofanya...ilifutilia mbalii.. hili nalo litizamwe kwa macho yake yootee

... Endeleeni na mapendekezo ni nini Tumwambie Mama.
Warudishe fao la kujitoa hifadhi za jamii kila mtu afe na chake kwanini wapangie matumizi hela isiyokua ya kwao?? Huu ni wizi wa mchana kweupe
 
Tunakupenda sana Mama, tunaomba nyongeza ya mishahara uifanye awamu inayokuja!
 
Inawezekana sijui kweli sasa usiniache na kutokujua kwangu na kunidhihaki na kunikejeli kwa uswahili na domo langu…just eleza tu kama ni maelekezo ya standing order au Waraka upi ili usaidie na wengine wasiojua kama mimi
Ni udhaifu wa Sheria ya ajira na mahusiano kazini. Watu walishapambana sana bila mafanikio. Watu walishafikishana mpaka kwa msuluhishi, CMA bila mafanikio.

Zaidi ya 90% ya Watumishi wanaokatwa mishahara ya hivi vyama siyo wanachama wao.

Na wanakata kwa kushirikiana na serikali, maana Hakuna mtu anaweza kukatwa mshahara bila kumhusisha Mwajiri.

IMG_20220405_144945.jpg
 
Warudishe fao la kujitoa hifadhi za jamii kila mtu afe na chake kwanini wapangie matumizi hela isiyokua ya kwao?? Huu ni wizi wa mchana kweupe
Hii ni sherehe ya Watumishi wa Umma ndo maana hutasikia TUGHE wala nn wakiongelea fao la kujitoa. mfano mzuri hata kwa aliyeanzisha uzi hajazungumzia. Hii sherehe siku hiyo itakua imesheheni pongezi za mama
 
Tafadhali, mwenye uwezo atuwekee hicho kifungu tukisome neno kwa neno
Ni udhaifu wa Sheria ya ajira na mahusiano kazini. Watu walishapambana sana bila mafanikio. Watu walishafikishana mpaka kwa msuluhishi, CMA bila mafanikio.

Zaidi ya 90% ya Watumishi wanaokatwa mishahara ya hivi vyama siyo wanachama wao.

Na wanakata kwa kushirikiana na serikali, maana Hakuna mtu anaweza kukatwa mshahara bila kumhusisha Mwajiri.

View attachment 2176630
 
Hii ni sherehe ya Watumishi wa Umma ndo maana hutasikia TUGHE wala nn wakiongelea fao la kujitoa. mfano mzuri hata kwa aliyeanzisha uzi hajazungumzia. Hii sherehe siku hiyo itakua imesheheni pongezi za mama
Hahahaa yaaan siku hiyo jina litatajwa hadi tutajificha chini ya meza
 
Hii ni sherehe ya Watumishi wa Umma ndo maana hutasikia TUGHE wala nn wakiongelea fao la kujitoa. mfano mzuri hata kwa aliyeanzisha uzi hajazungumzia. Hii sherehe siku hiyo itakua imesheheni pongezi za mama
Jitahidi tuliza kichwa ili uelewe
 
Sababu zitakazotolewa pale mtakapoambiwa mwaka huu mambo sio mazuri tuvumilie..
1. Vita vya Russia na Ukraine
2. Bank ya Dunia imetutoa uchumi wa kati
3. Mfumuko wa Bei nk
Hivyo ndugu watumishi tuendelee kuupiga mwingi kwa pamoja..
Meimosi oyeeeeeeee
 
Ni udhaifu wa Sheria ya ajira na mahusiano kazini. Watu walishapambana sana bila mafanikio. Watu walishafikishana mpaka kwa msuluhishi, CMA bila mafanikio.

Zaidi ya 90% ya Watumishi wanaokatwa mishahara ya hivi vyama siyo wanachama wao.

Na wanakata kwa kushirikiana na serikali, maana Hakuna mtu anaweza kukatwa mshahara bila kumhusisha Mwajiri.

View attachment 2176630

Mkuu mm hapa n mfano mzuri,nimejitoa huko na wala sikatwi hiyo sjui ada ya uwakala.
 
Bango la mwaka huu la watumishi liwe na kauli fupi tu,,AHADI NI DENI,,, c mnakumbuka aliahidi mwaka huu atawaongeza mshahara
 
Mkuu mm hapa n mfano mzuri,nimejitoa huko na wala sikatwi hiyo sjui ada ya uwakala.
Of course, Kuna watu hawakatwi. Lakini as long as hiyo Sheria ipo Ni siku yoyote wakiamua unaweza kuanza kukatwa.

IMG_20220405_144945.jpg
 
Mengine yote sawa lakini namba moja hapana kwa sababu hata ingekuwa wewe usingehamisha wafanyakazi kiholela bila kujali uhitaji.Pili ukiruhusu mtu ahamie anapopataka nani? atafanya kazi maeneo ya kijijini kwani wengi wanaomba kuhamia mjini kwa visingizio anamfuata mwenzi na vingine vingi ila issue kubwa wanataka kuhamia mjini.Wengine hawataki tu kufanyia kazi mkoa au wilaya fulani nao wanaomba uhamisho bila kuwa makini Kuna sehemu kutakuwa na upungufu wa wafanya kazi.
Binafisi nashauri uhamisho wa wafanyakazi uzingatie uhitaji na msawazo wa wafanyakazi.
Shime shime shime watumishi wenzangu ...asiye na mwana aeleke jiwe.

Tunapoelekea Mei Mosi ya kwanza ya Rais Samia S. Hassan akiwa katimiza mwaka mmoja kazini si vibaya tukatanguliza yale tunayotarajia kusikia toka kwake.

Kama alivyotuahidi nyongeza ya mshahara mwaka huu bila shaka hilo limeisha ila ni wazi haki za watumishi zimekandamizwa kwa muda mrefu sana.

Basi si vibaya tukimueleza Mama nini hasa tungependa toka kwake. Ningependa kusema machache.

1. Haki ya Mtumishi kuhama kituo cha kazi
Hili limekuwa ni tatizo sugu na la muda mrefu sana. Watumishi wa serikali hasa walimu wamekuwa wakipokwa haki yao ya kuhama kwa hiyari. Serikali imekuwa ikitoa kigezo kuwa itasababisha upungufu wa watumishi huko watokako. Sijui hoja hii ina mashiko gani maana wengine wakitoka wengine wanakuja.

Lakini hata sababu ya msingi kabisa ya kwenda unganisha familia watumishi hawasikilizwi hii hupelekea kuibuka kwa matapeli na watumishi wanapigwa sana pesa wanapopigania uhamisho.

Tungependa Mama alitizame hili kwa uzito wake.

2. Fao la uzazi
Nyinyi ni mashahidi nafikiri wengi hapa mnafahamu haki hii ambayo watumishi wamepunjwa. Tungependa Mama alitizame hili pia kwa macho yake mazuri kabisaa.

3. Annual increment
Hapa wala hakuna maneno mengi nafikiri ninyi ni mashahidi Awamu ya tano ilichofanya...ilifutilia mbalii.. hili nalo litizamwe kwa macho yake yootee

... Endeleeni na mapendekezo ni nini Tumwambie Mama
 
Mengine yote sawa lakini namba moja hapana kwa sababu hata ingekuwa wewe usingehamisha wafanyakazi kiholela bila kujali uhitaji.Pili ukiruhusu mtu ahamie anapopataka nani? atafanya kazi maeneo ya kijijini kwani wengi wanaomba kuhamia mjini kwa visingizio anamfuata mwenzi na vingine vingi ila issue kubwa wanataka kuhamia mjini.Wengine hawataki tu kufanyia kazi mkoa au wilaya fulani nao wanaomba uhamisho bila kuwa makini Kuna sehemu kutakuwa na upungufu wa wafanya kazi.
Binafisi nashauri uhamisho wa wafanyakazi uzingatie uhitaji na msawazo wa wafanyakazi.
Suala la upungufu wa watumishi si la mtumishi , ni la serikali kwa maana ndio yenye kuajiri. Mimi nimeshatumikia zaidi ya miaka 7 kituo fulani. Kuhama kwenda mahala ninapostahili ni haki yangu.
 
Afanye uhakiki wa watumishi tena maana ripoti ya CAG inaonesha bado Kuna watumishi hewa
 
Back
Top Bottom