Hivi ni nchi gani nyingine duniani ambayo kila Mei mosi (siku ya wafanyakazi duniani) huongeza mishahara ya watumishi wake wa umma?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Katika miaka 10 ya awamu ya nne ya JK (2005 hadi 2015), kila mwaka ilikuwa ifikapo tarehe mosi Mei serikali ilikuwa ikitamgaza ongezeko la kiasi fulani kwenye mishahara ya watumishi wake wa serikali. Watumishi hawa walikuwa wakifurahi sana ifikapo Mei mosi kwa sababu hiyo.

Ukweli ni kuwa kitendo hicho kilikuwa ni danganya toto tu kwani ongezeko lililokuwa likitolewa lilikuwa sawa au chini ya annual increments za mishahara yao. Annual salary increments zao stahiki walikuwa hawazipati, badala yake walipata hiyo ongezeko la Mei mosi ya mishahara yao. Kibaya zaidi upandaji wa ngazi katika salary scales (aka promotion) ulikuwa wa nadra sana. Hivyo mtumishi wa serikali alijikuta kwenye ngazi moja ya mshahara kwa zaidi ya miaka 6 au 10. Kwa mjibu wa standing orders za utumishi wa umma, annual salary increment inapaswa kutolewa kila mwaka na mtumishi anapaswa kupanda ngazi moja kwenye salary scales zake kila baada ya miaka 2 au 3. Waliokuwa wakizidai walipewa visingizio mbali mbali - km taarifa zao za siri au opras zao kutokuwapo etc. Upandaji ngazi umekuwa wa upendeleo au kwa kutoa cho chote (rushwa) kwa maafisa utumishi etc. Watumishi wengi wamekuwa wakistaafu bila kufika mwisho wa salary scales zao.

Badala ya ongezeko la mishahara la kila Mei mosi serikali ingalifaa ifanye yafuatavyo:

1. Annual salary increments za mishahara ya watumishi wa umma zitolewe kila mwaka. Kusiwe na kisingizio cho chote.

2. Serikali ihakikishe mtumishi anapanda ngazi moja kwenye salary scale yake kila baada ya miaka 2 na isizidi miaka mitatu kama ambavyo standing orders zinavyoelekeza. Kusiwe na kisingizio cho chote. Mambo ya opras yafutwe. Kama mfanyakazi hafai ni wajibu wa mwajiri wake kujua hilo na kumchukulia hatua za kinidhamu ikiwamo kumwachisha au kumfukuza kazi. Kwa wale watumishi wengi ambao wamedumu kwenye ngazi moja kwa zaidi ya miaka mitatu warekebeshiwe ngazi zao za nyuma na kupata accelerated promotions zitakazowaweka walikostahili kuwa hadi sasa.

3. Posho ya usafiri wa kwenda na kurudi kazini: Watumishi hawa wanatumia kiasi kikubwa cha mishahara yao kwa gharama za usafiri wa kwenda na kurudi kazini. Waraka wa posho ya usafiri (transport allowance) urejeshwe kama ifuatavyo:
- Watumishi wa ngazi za chini stahiki yao ni daladala = Sh 40,000 kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi ya kati stahiki yao ni bodaboda = Sh 100,000/ kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi za juu stahiki yao ni mafuta ya gari = Sh 200,000/ kwa mwezi.
NB: Watumishi wa umma wa kisiasa wanapata posho hii tena kwa kiwango kikubwa sana eg wabunge. Ndiyo maana uchaguzi mkuu unapokuja kila mtumishi wa umma anatamani kwenda kugombea ubunge!

4. Posho ya kutoishi mijini (Out of town residential allowance): Watumishi wanaoishi mijini wana fursa nyingi za kutengeneza kipato halali cha ziada nje ya kazi zao za umma. Wanaoishi mbali na miji hawana fursa hizo na hivyo wengi wamekuwa wakikataa kwenda kufanya kazi huko au kutafuta visingizio vya kuhama maeneo hayo. Ikumbukwe kuwa huko mbali na miji (vijijini) ndiko asilimia 80% ya watanzania wanaishi. Posho hii itolewe kama ifuatavyo:
- Watumishi wa ngazi chini = Sh. 50,000/ kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi ya kati = Sh 100,000/ kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi ya juu = Sh 200,000/ kwa mwezi.

5. Kiwango cha pensheni inayolipwa kila mwezi kwa wastaafu waliokuwa watumishi wa umma: Hali ilivyo sasa licha ya kiwango hiki kuwa kidogo, kiko fixed na hivyo thamani yake hupungua kila mwaka. Kama ilivyofanyika kwa viongozi wakuu serikalini, ingalifaa kiwango hiki kikawa pegged kwa asilimia fulani ya incumbant salary ya existing equivalent officer. Ile ya mkupuo ndiyo iendelee kwa kikokotoo kilichopo cha denomator ya 540.

NB: Posho hizi zisikatwe kodi.

Haya yakifanyika watumishi wa umma watanufaika na hakutakuwa na haja ya kupandisha mishahara kila Mei mosi wala kubadilisha salary scales za mishahara ya watumishi hawa mara kwa mara au kubadilisha miundo ya mishahara ya watumishi hawa mara kwa mara. Miundo na salary scales za watumishi hawa ni mizuri sana (compared to most private sector), tatizo ni utekelezaji wake inapokuja kwenye promotions, annual increments, allowances and penssion.
 
Katika miaka 10 ya awamu ya nne ya JK (2005 hadi 2015), kila mwaka ilikuwa ifikapo tarehe mosi Mei serikalu ilikuwa ikitamgaza ongezeko la kiasi fulani kwenye mishahara ya watumishi wake wa serikali. Watumishi hawa walikuwa wakifurahi sana ifikapo Mei mosi kwa sababu hiyo.

Ukweli ni kuwa kitendo hicho kilikuwa ni danganya toto tu kwani ongezeko lililokuwa likitolewa lilikuwa sawa au chini ya annual increments zao. Annual salary increments zao stahiki walikuwa hawazipati, badala yake walipata hiyo ongezeko la Mei mosi ya mishahara yao. Kibaya zaidi upandaji wa ngazi katika salary scales (aka promotion) ulikuwa wa nadra sana. Hivyo mtumishi wa serikali alijikuta kwenye ngazi moja ya mshahara kwa zaidi ya miaka 6 au 10. Kwa mjibu wa standing orders za utumishi wa umma annual salary increment inapaswa kutolewa kila mwaka na mtumishi anapaswa kupanda ngazi moja kwenye salary scales zake kila baada ya miaka 2 au 3. Wamekuwa wakizidai wanapewa visingizio mbali mbali - km taarifa za siri hazipo mara Opras etc. Upandaji ngazi umekuwa wa upendeleo. Watumishi wengi wamekuwa wakistaafu bila kufika mwisho wa salary scales zao.

Badala ya ongezeko la mishahara la kila Mei mosi serikali ingalifaa ifanye yafuatavyo:

1. Annual salary increments za mishahara ya watumishi wa umma zitolewe kila mwaka. Kusiwe na kisingizio.
2. Ihakikishe mtumishi anapanda ngazi moja kwenye salary scale yake kila baada ya miaka 2 na isizidi miaka mitatu. Kusiwe na kisingizio cho chote. Mambo ya opras yafutwe. Kama mfanyakazi hafai ni wajibu wa mwajiri wake kujua hilo na kumchukulia hatua za kinidhamu ikiwamo kumwachisha au kumfukuza kazi. Kwa wale watumishi wengi ambao wamedumu kwenye ngazi moja kwa zaidi ya miaka mitatu warekebeshiwe ngazi zao za nyuma na kupata accelerated promotions zitakazowaweka walikostahili kuwa.
3. Posho ya usafiri wa kwenda na kurudi kazini: Watumishi hawa wanatumia kiasi kikubwa cha mishahara yao kwa gharama za usafiri wa kwenda na kurudi kazini. Waraka wa posho ya usafiri (transport allowance) urejeshwe kama ifuatavyo:
- Watumishi wa ngazi za chini stahiki yao ni daladala = Sh 40,000 kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi ya kati stahiki yao ni bodaboda = Sh 100,000/ kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi za juu stahiki yao ni mafuta ya gari = Sh 200,000/ kwa mwezi.
NB: Watumishi wa umma wa kisiasa wanapata posho hii tena kwa kiwango kikubwa sana eg wabunge.
4. Posho ya kutoishi mijini (Out of town residential allowance): Watumishi wanaoishi mijini wana fursa nyingi za kutengeneza kipato halali cha ziada nje ya kazi zao za umma. Wanaoishi mbali na miji hawana fursa hizo na hivyo wengi wamekuwa wakikataa kwenda kufanya kazi huko au kutafuta visingizio vya kuhama maeneo hayo. Ikumbukwe kuwa huko mbali na miji (vijijini) ndiko asilimia 80% ya watanzania wanaishi. Posho hii itolewe kama ifuatavyo:
- Watumishi wa ngazi chini = Sh. 50,000/ kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi ya kati = Sh 100,000/ kwa mwezi.
- Watumishi wa ngazi ya juu = Sh 200,000/ kwa mwezi.
5. Kiwango cha pensheni inayolipwa kwa mwezi kwa wastaafu waliokuwa watumishi wa umma: Hali ilivyo sasa licha ya kiwango hiki kuwa kidogo, kiko fixed na hivyo thamani yake hupungua kila mwaka. Kama ilivyofanyika kwa viongozi wakuu serikalini, ingalifaa kiwango hiki kikawa pegged kwa asilimia fulani ya incumbant salary ya existing equivalent officer. Ile ya mkupuo ndiyo iendelee kwa kikokotoo kilichopo cha denomator ya 540.

NB: Posho hizi zisikatwe kodi.
Haya yakifanyika watumishi wa umma watanufaika na hakutakuwa na haja ya kupandisha mishahara kila Mei mosi wala kubadilisha salary scales za mishahara ya watumishi hawa mara kwa mara au kubadilisha miundo ya mishahara ya watumishi hawa mara kwa mara. Miundo na salary scales za watumishi hawa ni mizuri sana (compared to most private sector), tatizo ni utekelezaji wake inapokuja kwenye promotions, annual increments, allowances and penshen.
Ngoja nikuulize swali jepesi tu

Hivi nchi gani duniani, ambayo imewahi shuhudia watumishi wake wa Umma, hawajaongezewa mishahara yao, ambayo ni kwa mujibu wa sheria, kwa miaka 5 mfululizo??
 
Maswali yatajibiwa kwa maawali humu, huu usimba na yanga ndo unaoifanya nchi kuwa kichwa cha mwendawazimu hata baada ya nchi kufikia umri wa kustaafu kwa lazima sasa.

Wafanyakazi wana vyama vyao, wanakatwa asilimia(2%) kadhaa ya mishahara yao kuchangia shughuli za vyama hivyo, kazi na umuhimu wa vyama hivyo ni nini? Au ndo kama vile kujenga jengo la waalimu pale Boma huku kilio kikiwa ni kile kile kwa miaka 60?

Kwa mujibu wa sheria, kwa mujibu wa sheria, sheria zipi sasa? Zile walizotumia wabobevu wakina Chengen kujilinda na madudu waliyofanya? Zile zinazowalinda wakina Ziton na Shimboni kuficha pesa nje ya nchi kwa msaada wa Jei?

Nchi iko umaskinini, kama kweli tunaonewa, tuweke kalamu chini mpaka tutakaposikilizwa, hamtaki! Basi tujikite jinsi ya kuiinua nchi kimaendeleo na teknolojia, tukiwabana akina symbion na songas wazawa waache kutuibia kwa mgongo wa wageni bila kujali ni mstaafu au jangili.
 
Haya...hyo ilikuwa kipind cha kikwete , alijikuna alipoweza, tupe takwimu za jiwe walilolikataa waashi
Miaka miwili ya kwanza ya awamu ya tano ilikuwa ni kufanya uhakiki wa idadi halisi ya watumishi hawa wa umma. Ikagundulika kuwa idadi kubwa ya watumishi hawa waliokuwa wanalipwa mishahara na serikali walikuwa ni aidha watumishi hewa au wenye vyeti vya kughushi aka vyeti feki. Hivyo zoezi la kwanza lilikuwa kuwaondoa watumishi hewa na wale feki kwenye payroll. Hivyo katika kipindi hiki cha uhakiki annual increments na upandaji wa madaraja ilibidi usimame.

Miaka 3 iliyofuata katika awamu hiyo ya tano watumishi halali wote wa umma walianza kupata nyongeza zao za misharahara kila mwaka (annual increment) bila kukosa. Pia upandaji wa madaraja (promotions) ulirejeshwa. Tatizo likawa upandaji wa madaraja mara nyingi ulikwamishwa na kile kinachoitwa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi au kwa kiingereza The Open Perfomance Review and Appraisal (OPRAS). Yaani kwa mfano kama wewe ni daktari bingwa wa upasuaji (surgeon) unapangiwa kwamba kwa mwaka ufanye 10 kwa siku, hivyo operesheni 3,600 kwa mwaka. Haizalishi quality ya hizo operesheni au wagonjwa utawapata wapi. Wanachotaka ni mesurable quantity. Hata kama operesheni hizo ni za mabusha tu (hydrocelectomies) au magovi tu (circumsicions). Usipofikisha idadi uliyopangiwa huwezi kupanda daraja la mshahara hata kama wagonjwa wote waliofika kwako uliwahudumia vizuri kabisa kibingwa.
Huu mfumo haufai - umewekwa pale ili watu wasipande mishahara yao. Ufutwe kwenye hii awamu ya sita.
 
Miaka miwili ya kwanza ya awamu ya tano ilikuwa ni kufanya uhakiki wa idadi halisi ya watumishi hawa wa umma. Ikagundulika kuwa idadi kubwa ya watumishi hawa waliokuwa wanalipwa mishahara na serikali walikuwa ni aidha watumishi hewa au wenye vyeti vya kughushi aka vyeti feki. Hivyo zoezi la kwanza lilikuwa kuwaondoa watumishi hewa na wale feki kwenye payroll. Hivyo katika kipindi hiki cha uhakiki annual increments na upandaji wa madaraja ilibidi usimame.

Miaka 3 iliyofuata katika awamu hiyo ya tano watumishi halali wote wa umma walianza kupata nyongeza zao za misharahara kila mwaka (annual increment) bila kukosa. Pia upandaji wa madaraja (promotions) ulirejeshwa.
Ni wapi huko mlipewa annual increment wakati wa JPM wew mnduku?
 
Umeharibu mwanzo tu😟😟,yaani umeanza tu kwa kumponda Kikwete!!
JKM ndiye aliyeleta heshima ya watumishi wa umma TANGANYIKA.
 
Kuna sehemu umepotosha, kipindi cha JK annual increments zilikuwa zinatolewa kila july, kutokana na kiwango chako cha mshahara. Mwendazake ndiye aliacha kutoa annual increments, kinyume kabisa na mikataba tuliyosaini. Hayo mambo ya ongezeko la mshahara mara nyingi ilikuwa ni kuongeza kima cha chini, wenye mishahara mikubwa walikuwa wanaguswa kidogo sana or hawaguswi kabisa.
 
Miaka miwili ya kwanza ya awamu ya tano ilikuwa ni kufanya uhakiki wa idadi halisi ya watumishi hawa wa umma. Ikagundulika kuwa idadi kubwa ya watumishi hawa waliokuwa wanalipwa mishahara na serikali walikuwa ni aidha watumishi hewa au wenye vyeti vya kughushi aka vyeti feki. Hivyo zoezi la kwanza lilikuwa kuwaondoa watumishi hewa na wale feki kwenye payroll. Hivyo katika kipindi hiki cha uhakiki annual increments na upandaji wa madaraja ilibidi usimame.

Miaka 3 iliyofuata katika awamu hiyo ya tano watumishi halali wote wa umma walianza kupata nyongeza zao za misharahara kila mwaka (annual increment) bila kukosa. Pia upandaji wa madaraja (promotions) ulirejeshwa. Tatizo likawa upandaji wa madaraja mara nyingi ulikwamishwa na kile kinachoitwa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi au kwa kiingereza The Open Perfomance Review and Appraisal (OPRAS). Yaani kwa mfano kama wewe ni daktari bingwa wa upasuaji (surgeon) unapangiwa kwamba kwa mwaka ufanye 10 kwa siku, hivyo operesheni 3,600 kwa mwaka. Haizalishi quality ya hizo operesheni au wagonjwa utawapata wapi. Wanachotaka ni mesurable quantity. Hata kama operesheni hizo ni za mabusha tu (hydrocelectomies) au magovi tu (circumsicions). Usipofikisha idadi uliyopangiwa huwezi kupanda daraja la mshahara hata kama wagonjwa wote waliofika kwako uliwahudumia vizuri kabisa kibingwa.
Huu mfumo haufai - umewekwa pale ili watu wasipande mishahara yao. Ufutwe kwenye hii awamu ya sita.
Nyamaza
 
Miaka miwili ya kwanza ya awamu ya tano ilikuwa ni kufanya uhakiki wa idadi halisi ya watumishi hawa wa umma. Ikagundulika kuwa idadi kubwa ya watumishi hawa waliokuwa wanalipwa mishahara na serikali walikuwa ni aidha watumishi hewa au wenye vyeti vya kughushi aka vyeti feki. Hivyo zoezi la kwanza lilikuwa kuwaondoa watumishi hewa na wale feki kwenye payroll. Hivyo katika kipindi hiki cha uhakiki annual increments na upandaji wa madaraja ilibidi usimame.

Miaka 3 iliyofuata katika awamu hiyo ya tano watumishi halali wote wa umma walianza kupata nyongeza zao za misharahara kila mwaka (annual increment) bila kukosa. Pia upandaji wa madaraja (promotions) ulirejeshwa. Tatizo likawa upandaji wa madaraja mara nyingi ulikwamishwa na kile kinachoitwa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi au kwa kiingereza The Open Perfomance Review and Appraisal (OPRAS). Yaani kwa mfano kama wewe ni daktari bingwa wa upasuaji (surgeon) unapangiwa kwamba kwa mwaka ufanye 10 kwa siku, hivyo operesheni 3,600 kwa mwaka. Haizalishi quality ya hizo operesheni au wagonjwa utawapata wapi. Wanachotaka ni mesurable quantity. Hata kama operesheni hizo ni za mabusha tu (hydrocelectomies) au magovi tu (circumsicions). Usipofikisha idadi uliyopangiwa huwezi kupanda daraja la mshahara hata kama wagonjwa wote waliofika kwako uliwahudumia vizuri kabisa kibingwa.
Huu mfumo haufai - umewekwa pale ili watu wasipande mishahara yao. Ufutwe kwenye hii awamu ya sita.
Mwendazake hajawahi toa annual increment, upotoshaji mwingine huu. Hizo statistics zako unatoa wapi?
 
Miaka miwili ya kwanza ya awamu ya tano ilikuwa ni kufanya uhakiki wa idadi halisi ya watumishi hawa wa umma. Ikagundulika kuwa idadi kubwa ya watumishi hawa waliokuwa wanalipwa mishahara na serikali walikuwa ni aidha watumishi hewa au wenye vyeti vya kughushi aka vyeti feki. Hivyo zoezi la kwanza lilikuwa kuwaondoa watumishi hewa na wale feki kwenye payroll. Hivyo katika kipindi hiki cha uhakiki annual increments na upandaji wa madaraja ilibidi usimame.

Miaka 3 iliyofuata katika awamu hiyo ya tano watumishi halali wote wa umma walianza kupata nyongeza zao za misharahara kila mwaka (annual increment) bila kukosa. Pia upandaji wa madaraja (promotions) ulirejeshwa. Tatizo likawa upandaji wa madaraja mara nyingi ulikwamishwa na kile kinachoitwa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi au kwa kiingereza The Open Perfomance Review and Appraisal (OPRAS). Yaani kwa mfano kama wewe ni daktari bingwa wa upasuaji (surgeon) unapangiwa kwamba kwa mwaka ufanye 10 kwa siku, hivyo operesheni 3,600 kwa mwaka. Haizalishi quality ya hizo operesheni au wagonjwa utawapata wapi. Wanachotaka ni mesurable quantity. Hata kama operesheni hizo ni za mabusha tu (hydrocelectomies) au magovi tu (circumsicions). Usipofikisha idadi uliyopangiwa huwezi kupanda daraja la mshahara hata kama wagonjwa wote waliofika kwako uliwahudumia vizuri kabisa kibingwa.
Huu mfumo haufai - umewekwa pale ili watu wasipande mishahara yao. Ufutwe kwenye hii awamu ya sita.
Acha Uongo. Ndani ya hii miaka Mitano wafanyakazi madalaja yamepanda lakini hakuna ongezeko la mshahara.
 
Ngoja nikuulize swali jepesi tu

Hivi nchi gani duniani, ambayo imewahi shuhudia watumishi wake wa Umma, hawajaongezewa mishahara yao, ambayo ni kwa mujibu wa sheria, kwa miaka 5 mfululizo?
Akikujibu nistue, nimeona Google ,Europa yote wameongezewa mishahara mwezi huu wa nne. Na ipo kisheria, kila mwaka mwezi wa nne wanaongezewa.

Kama kuna kitu ambacho misukule ya marehemu Inashangaza ni kumsifia mwenda zake rais alieshindwa kwa kila kitu.
 
Acha Uongo. Ndani ya hii miaka Mitano wafanyakazi madalaja yamepanda lakini hakuna ongezeko la mshahara.
Huwezi kupanda daraja bila ongezeko la mshahara. Daraja D halingani na daraja E na kadhalika. Kama ulipewa barua ya kukupandisha daraja ulitakiwa uwaone wahasibu wako wa salary section wakurekebeshee mshahara wako. Ilitakiwa iwe automatic lakini mambo yetu bado manual.
 
Mwendazake hajawahi toa annual increment, upotoshaji mwingine huu. Hizo statistics zako unatoa wapi?
Kama wewe hukupata annual increments itakuwa aidha mshahara wako ulishafikia cealing ya ngazi uliyonayo ie ulishamaliza increments zote za ngazi hiyo. Hivyo ulitakiwa uwe umeshapandishwa daraja linalofuata ili uweze kupata annual increments za daraja hilo jipya. Au wewe ngazi yako ya mshahara ni fixed kwa maana ya kuwa haina annual increments. Ngazi za mishahara kuanzia K hadi Z ni fixed hazina annual increments).
 
Kuna sehemu umepotosha, kipindi cha JK annual increments zilikuwa zinatolewa kila july
Kila mtumishi wa serikali ana tarehe na mwezi wake wa annual increment kutegemea tarehe na mwezi alioajiriwa. Siyo wote waliajiriwa Julai mosi. Ila zile nyongeza za mishahara zinazotangazwa siku ya Mei mosi, ndizo huanza kutolewa mwezi wa Julai.
 
Back
Top Bottom