Wanawake wenzangu wenye vitanzi (IUD), mnaendeleaje?

Wanawake wenzangu wenye vitanzi (IUD), mnaendeleaje?

Mimi mwanaume, nilijifunza kuhusu hii njia tangu nikiwa miaka 17 kupitia kitabu fulani.
Kwa uzoefu wangu hakuna njia ngumu kufuata kama hii. Afadhali withdrawal method.
Mwanaume ukae na mwanamke chumba kimoja, hauumwi kitu, rijali kamili, umri kuanzia 42 kushuka chini 18 ujizuie ngono siku 5 mpaka 7 huo mtihani mgumu sana.
Withdrawal wakati wa ovulation mkuu? The way sex inavyokuwa sweet kwenye siku za joto?. Kama uko serious kuzuia mimba hii ni hatari. Kama abstaining haiwezekani bora hata kutumia kondomu. Ila withdrawal wakati mtu anaovulate mmmmh,lakini kwa wanaoweza wafanye. Halafu kama huwezi kujizuia sex kwa siku chache, hizo njia za kisasa ndo mbaya zaidi,zinamuondolea mwanamke au kumpunguzia ile hamu ya kusex kabisa, yaani wewe mume unakuwa unataka yeye hataki,kama mnabakana vile. Halafu kuna wanawake wakitumia hizo njia wanatoka damu mfululizo hata mwezi au miezi,sasa kujizuia siku 6-10 huwezi,mke wako akichoma sindano atoke damu siku 30 mfululizo utaweza kuvumilia kukaa bila kusex siku 30 mfululizo ? Sio kwamba wote wanakutwa na hali hii ila kuna wanaokutwa. Pia kingine hizo njia zinafanya sex inakuwa na ladha sio nzuri sana,mwanamke anakuwa hana joto na wengine wanakuwa wakavuuu. Sex inakuwepo,lakini ladha au ule utamu unapungua. Hamna njia rahisi isiyo na changamoto.
 
Mkuu mchezo mtamu ila matokea ya ule mchezo sio matamu naogopa sana mimba alooh 😭
Situation kama hizi nawaonea sana wivu wanawake wa kizungu wenzetu wanaeleweka kiurahisi na wenza wao, shughuli iko huku sht holes countries
Kwa sisi waafrika mwanamke bado anachukuliwa kama " chombo cha starehe" na kazi yake ni kutimiza matamanio ya mwanaume bila kujali hisia au afya ya mwanamke huyo. Ni hivi punda afe mzigo ufike. Wanaume wanakuzwa na fikra hizo na wanawake wanakuzwa na fikra kwamba wao ni vyombo vya starehe na wanapaswa kutimiza haja za wanaume wao hata kama wao wataathirika. Ndio maana inatakiwa watu wazungumzie masuala haya kabla hata ya kufunga ndoa,matarajio yajulikane. Mimi binafsi pamoja na baba mjengo tuliongea hili suala kwa undani kabla ya kuoana,mimi nilikuwa nafahamu kwahiyo nilianzisha mada . Halafu tukajifunza wote kwa pamoja ( tulipata mwalimu online) alikuwa mwanamke na tuliomba nafasi ya kusikia kutoka kwa mume wa huyo mwalimu jinsi gani yeye kama mwanaume analichukulia hilo swala na anakabiliana na changamoto zinazojitokeza. Pia wao binafsi walipata fursa ya kuongea kivyao( man to man). Ilisaidia kwa kweli. So tulifunga ndoa tushajua what to expect.
 
Plus inaleta ile hali ya ukaribu kati yako na mumeo. That feeling unaipata wakati wa kudiscuss your cycle with your husband is so sweet 😋😋😋❤️❤️. Then mkianza countdown kusubiria safe days,hadi raha yaani kama mnaisubiria siku ya harusi.

Hata research zinaonesha couples wanaotumia Natural Family Planning Methods kama BOM divorce rate yao ipo chini sana compared to couples wanaotumia hizi njia za kisasa.
Sawa
 
Habari,

Hii ni kwa wanawake wenzangu ambao wanatumia uzazi wa mpango aina ya IUD (Intra-uterine Device) au Kitanzi.

How are you guys? Vinawapa maudhi kama kilivyoninyoosha mimi au mmetulia?

I have to say nili-opt kutumia IUD sababu niliambiwa haina maudhi, na niliweka a copper IUD nikiambiwa ni non-hormonal yaani hakiingilii mifumo ya homoni. Miaka miwili ya mwanzo naona niliishi nacho tu poa.

Kuanzia around February 2025, nikaanza kupata periods zinazodumu siku 8 hadi 10, tumbo likawa linauma Mungu hapendi, nikipona yeast infection napata BV na mzunguko unaendelea hivyo.

Nimetoa IUD tangu November 2025. Kila kitu kimetulia! Yaani periods zangu zimerudi kuwa normal, sipati infections anymore na wala siumwi tumbo.

Tatizo ni kwamba; NIMEKIMISS. Namiss maisha yangu ya kuwa siwazi kupata ujauzito. Maana huku kwenye ndoa muda wowote unamwagiwa ndani, sipendi kukaa roho juu kabisaa. Niweke tena nikitumaini nitatulia miaka miwili mingine?
Naskia kuna njia za asili jaribu tumia izo
 
Kitanzi cha Copper ni kweli hakina hormone za uzazi lakini usichoambiwa ni kwamba Copper ina uwezo wa kuathiri hormone za uzazi hasa estrogen ndio maana kuna hayo maudhi unayapata.

Hiyo sentensi kwamba " hakina homoni ni maneno tu ya kutia watu moyo ili waone kina uafadhali".

Mbaya zaidi kitanzi cha copper kinatoa kiwango kikubwa cha copper mwilini kuliko kiwango kinachoruhusiwa kwahiyo kinaleta " copper toxicity". So unaepuka hormones unapambana na copper toxicity.

Kuna group Facebook la wanawake kutoka sehemu mbalimbali duniani wanaotumia hizo Copper IUD, simulizi wanazotoa hao wamama sio poa. Ukipata nafasi kalitafute usome,utaona hayo mambo wanayopambana nayo.Hayo majitu ni masumu.

Bora njia za asili kama Billings Ovulation Method au kujipima joto mdomoni au homoni kwenye mkojo. Unazuia mimba kiuhakika bila madhara yoyote.
Tunaoomba tuelezee vizur hiz methods za asili ulizotutajia
 
UTI ni maambukizi kwenye mfumo wa mkoji na IUD inawekwa kwenye mfumo wa uzazi
Sasa vinaingilianaje
Kitanzi hakisababishi UTI moja kwa moja bila kinaongeza hatari kwa sababu bacteria wanaweza kuweka makazi pale ya kudumu kisha bakteria hao wakawa wanahama mara kwa mara na kusogea kwenye njia ya mkojo na kuleta maambukizi. Katika hili kitanzi kinakuwa kama makazi ya bacteria kitaalamu wanaita " biofilm".
 
My dear hazizuiliki,hiyo ni kawaida. Mwili wako unakuwa unataka mtoto kwa kipindi hicho kwa lazima, kwahiyo usumbufu kwa baba mjengo muhimu. Ni hivi zile homoni zinakufanya unakuwa kama chizi fulani hivi. Ndio maana mawasiliano ni muhimu na yeye awe anakusapoti. Ni kukabiliana nazo tu kwa kujiwekea taratibu fulani za kufuata kwa kipindi hicho cha usumbufu. Ovulation ni kiashiria kwamba wewe ni mwanamke uliyekamilika na mwili wako unafanya kazi vizuri. Binafsi ukitoa ule usumbufu kwa baba mjengo, ovulation naipenda kwa sababu ndo kipindi ambacho ninakuwa na furaha muda wote,ngozi inakuwa nzuriii pia nakuwa na nguvu nyingi za kufanya kazi kwahiyo kazi zote zinazochukua muda mrefu hapo nyumbani nazifanya nikiwa ovulation. Ovulation ikikata tu nakuwaga na hasira hasira na pia nakuwa mvivu wa kazi si kazini wala si nyumbani na usingizi debe. Nakuwa binadamu mwingine kabisaaa. Nikiwa kwenye Ovulation huwa naishi, ovulation ikikata nakuwa
Ivi ni kweli kutoshiriki muda mrefu kunapelekea maumiv ya mgongo na kiuno hasa ukiwa period
 
Tunaoomba tuelezee vizur hiz methods za asili ulizotutajia
Mimi nayotumia inaitwa Billings Ovulation Method au BOM kwa kifupi,kwa njia hii unachunguza ule ute unaotoka kwenye via vya uzazi kwa kuhisi tu " unajiskiaje" mfano unyevu, ukavu,utelezii, etc. Pia unaweza kuuchunguza kwa macho au hata kuushika kama bado hujawa mzoefu wa kuchunguza unajiskiaje. Ukishajichunguza na kujua kama uko kwenye siku za kushika mimba au siku salama then unaepuka tendo la ndoa kama hautaki kushika ujauzito kwa wakati huo. Njia nyingine zinahusisha teknolojia kama vile kupima homoni kwenye mkojo kwa vipimo unavyoweza kuwa navyo nyumbani au kupima joto la mwili kwa themometa maalum inawekwa mdomoni. Teknolojia hizi hurahisisha mwanamke kujua kama yuko kwenye siku za kushika ujauzito au lah kisha yeye mwenyewe atafanya maamuzi kulingana na anataka kushika ujauzito au kuzuia ujauzito.
 
Ivi ni kweli kutoshiriki muda mrefu kunapelekea maumiv ya mgongo na kiuno hasa ukiwa period
Self control sio rahisi kipenzi ila inahitajika maana kuna kipindi mume ataumwa,atasafiri kutafutia familia n.k. Kama huna self control huku mume ameenda kuhangaikia familia labda kasafiri mwezi au miezi miwli utafanyaje?
 
Wana pesa za kutosha kulea,wewe unazo?
Hujanielewa hoja yangu.
Nimemkatalia jamaa kwamba kuwa na watoto wengi kunapoteza muda wa kufanya biashara. Hivyo akimaanisha wafanyabiashara waliofanikiwa hawataki au hawawezi kuwa na watoto wengi.
Personally nilihitaji watoto wawili tu.
 
Mkuu mchezo mtamu ila matokea ya ule mchezo sio matamu naogopa sana mimba alooh 😭
Situation kama hizi nawaonea sana wivu wanawake wa kizungu wenzetu wanaeleweka kiurahisi na wenza wao, shughuli iko huku sht holes countries
Watu sikuhizi mnaogopa mimba kuliko ukimwi😅

Hapo dawa ni kuolewa na mwanaume mkae mbalimbali! Tofauti na hapo atakubaka kwa lazima😆
 
Kitanzi hakisababishi UTI moja kwa moja bila kinaongeza hatari kwa sababu bacteria wanaweza kuweka makazi pale ya kudumu kisha bakteria hao wakawa wanahama mara kwa mara na kusogea kwenye njia ya mkojo na kuleta maambukizi. Katika hili kitanzi kinakuwa kama makazi ya bacteria kitaalamu wanaita " biofilm".
Sawasawa
 
Back
Top Bottom