Wananchi wanaotaka kuanza mazoezi wajue kupunguza mwili na kuondoa kitambi/tumbo ni vitu viwili tofauti. Six packs ni kwa wito maalum.

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,239
22,318
Wakuu kwa mara nyingine nipo hapa kwenye jukwaa la michezo kushea mawili matatu kuhusu mambo ya michezo na mazoezi. Kuna mwamko mkubwa sana wa wananchi kupenda michezo na kujihusisha na matukio yote ya kuweka mwili fit. Ni jambo la kujipongeza kwa kweli. Vikundi vya jogging vinazidi kuongezeka.

Binafsi siku za karibuni nimeanza mazoezi ya kukimbia kivyangu na kwa sasa nimefikia uwezo wa kukimbia 2.3km kwa dakika 15. Hakika hiki ni kishindo cha awamu ya 6. Changamoto niliyopata ni ile ya kisaikolojia kuona vibonge wakikata 13km huku mimi nikishindwa kufika hata 3km kwa kukimbia. Ila tayari nimepata jibu kuwa suala la mazoezi ni pana sana. Mtu anaweza kuonekana ana mwili mkubwa ila akawa fit kuanzia mwilini hadi pumzi.

Ila kama kichwa cha uzi kinavyosema ni kuwa wananchi waelewe kupunguza mwili kuna uhusiano mdogo na kuondoa kitambi au kitumbo flani hivi kisichoeleweka. Mchakato wa kuondoa tumbo na kupata six packs sio mdogo. Ni mchakato unaohitaji uvumilivu kwasababu inabidi ufanye mazoezi makali ya kuondoa kitambi na kupata six packs. Kupunguza mwili ni rahisi kwa sababu waweza tu kufanya jogging na ku-control misosi. Vijana wa umri mdogo wana nafasi kubwa ya kuondoa vitambi na kupata six packs ila wale wakubwa shughuli ni pevu.

Kama huwezi kupitia kwenye maumivu makali ya kutafuta six packs hata wajiunge kukuombea kina Mwamposa, Kakobe, Kadinali Pengo, Sheikh Kipozeo, Zumaridi, Dokta Manyaunyau, wazee wa kimila na viongozi wengine wa kiimani hutaweza kuondoa kitambi.

Nawatakia kila la heri.
 
Ukiwa na nidhamu ya mazoezi tumbo unalikata

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kweli.
Jibu sahihi ni;
Ukiwa na Nidhamu ya kupangilia Vyakula na Ukaacha ULAFI, KITAMBI UTAISHIA KUKIONA KWA WALE KULA KULA.
Unaweza kuwa na Nidhamu ya Mazoezi mnoooo lkn ukitoka hapo unakula SUPU YA ULIMI NA CHAPATI 8, UKASHUSHIA NA CASTLE LITE 4 so what is next na mazoezi yako...
Anyway naamini upo uhusiano wa Karibu sana kati ya Kitambi na Ulafi wa kufakamia vyakula bila mpangilio.
 
130? Umri wako! Urefu wako!

Ukitembea kutoka posta hadi mbezi kwa wiki mara tatu

Ndani ya miezi mitatu utaona mabadiliko makubwa
Ni kweli, mazoezi yanahitaji discipline pamoja na utaratibu mzuri wa chakula. Unapungua. Nami naanza rasmi kesho asubuhiiii. Nataka nipunguze hizo kilo 130 nilizo nazo zije kwenye 100 zinatosha. Niombeeni wana JF.
 
Mimi nilikuwa mfanya mazoezi sana, nikayaacha na ndambi imerudi aisee....nina kllikizo mshenzi nataka niifanyie kazi chaap.nakimbia km 3-4 kwa dk 25, baada ya hapo nafanya aerobic nusu saa...nina mwili mkubwa lkn nina pumzi, wik end nafanya na vijana nawatoa jasho...tufanye mazoezi wakuu...
 
Wakuu kwa mara nyingine nipo hapa kwenye jukwaa la michezo kushea mawili matatu kuhusu mambo ya michezo na mazoezi. Kuna mwamko mkubwa sana wa wananchi kupenda michezo na kujihusisha na matukio yote ya kuweka mwili fit. Ni jambo la kujipongeza kwa kweli. Vikundi vya jogging vinazidi kuongezeka.

Binafsi siku za karibuni nimeanza mazoezi ya kukimbia kivyangu na kwa sasa nimefikia uwezo wa kukimbia 2.3km kwa dakika 15. Hakika hiki ni kishindo cha awamu ya 6. Changamoto niliyopata ni ile ya kisaikolojia kuona vibonge wakikata 13km huku mimi nikishindwa kufika hata 3km kwa kukimbia. Ila tayari nimepata jibu kuwa suala la mazoezi ni pana sana. Mtu anaweza kuonekana ana mwili mkubwa ila akawa fit kuanzia mwilini hadi pumzi.

Ila kama kichwa cha uzi kinavyosema ni kuwa wananchi waelewe kupunguza mwili kuna uhusiano mdogo na kuondoa kitambi au kitumbo flani hivi kisichoeleweka. Mchakato wa kuondoa tumbo na kupata six packs sio mdogo. Ni mchakato unaohitaji uvumilivu kwasababu inabidi ufanye mazoezi makali ya kuondoa kitambi na kupata six packs. Kupunguza mwili ni rahisi kwa sababu waweza tu kufanya jogging na ku-control misosi. Vijana wa umri mdogo wana nafasi kubwa ya kuondoa vitambi na kupata six packs ila wale wakubwa shughuli ni pevu.

Kama huwezi kupitia kwenye maumivu makali ya kutafuta six packs hata wajiunge kina Mwamposa, Kakobe, Kadinali Pengo, Sheikh Kipozeo, Zumaridi, Dokta Manyaunyau, wazee wa kimila na viongozi wengine wa kiimani hutaweza kuondoa kitambi.

Nawatakia kila la heri.
Kuna vitu lazima uvijue kwanza, kuna tofauti ya mtu kuwa na mwili mkubwa na mtu kuwa mnene. Kuna mtu anaweza kuonekana mwembamba ila kumbe mwilini ana mafuta mengi.
Mtu aliye na mwili mkubwa ndio akifanya mazoezi anakuwa na packs. Hii miili ya kg 40 wale washibe na wafanye mazoezi ya kawaida tu inatosha. Hawa wakisema wapunguze lishe na kuongeza mazoezi hubakia na vifua kama vya panzi huku vimbavu vikijichora kama vya mbwa.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Kuna vitu lazima uvijue kwanza, kuna tofauti ya mtu kuwa na mwili mkubwa na mtu kuwa mnene. Kuna mtu anaweza kuonekana mwembamba ila kumbe mwilini ana mafuta mengi.
Mtu aliye na mwili mkubwa ndio akifanya mazoezi anakuwa na packs. Hii miili ya kg 40 wale washibe na wafanye mazoezi ya kawaida tu inatosha. Hawa wakisema wapunguze lishe na kuongeza mazoezi hubakia na vifua kama vya panzi huku vimbavu vikijichora kama vya mbwa.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
Umetoa ufafanuzi mzuri sana. Watu wanajichanganya kudhani mazoezi ni kupunguza tu mwili. Miaka kadhaa iliyopita nilikuwa mwembamba sana nikaamua kwenda gym. Yule mwalimu wa Gym aliniambia niwe nakula sana pia. Yaani hata ule muda niko kitandani nakaribia kulala niwe natafuna chochote kinachotafunika. Pia alinipunguzia mazoezi ya kukimbia kwenye treadmill na kuweka nguvu kwenye vyuma na mazoezi mengine
 
Kwenu kama mna asili ya miili mikubwa ni kujisumbua buree la muhimu kula kwa utaratibu.

Kuna familiya nyingi nazijua yaani wanakula mavyakula meeeengi chochote chakula wanakula ila ukoo mzima hakuna mtu mnene, ukoo mzima wamekauka.

N.b mazoezi ni muhimu.
 
Kwenu kama mna asili ya miili mikubwa ni kujisumbua buree la muhimu kula kwa utaratibu.

Kuna familiya nyingi nazijua yaani wanakula mavyakula meeeengi chochote chakula wanakula ila ukoo mzima hakuna mtu mnene, ukoo mzima wamekauka.

N.b mazoezi ni muhimu.
Umefunga uzi mkuu, kuna familia nyingine matukunyema karibia wote yan miili ya kurithi mibaya sana waweza kesha unafanya mazoezi lakini wapi
 
Kwenu kama mna asili ya miili mikubwa ni kujisumbua buree la muhimu kula kwa utaratibu.

Kuna familiya nyingi nazijua yaani wanakula mavyakula meeeengi chochote chakula wanakula ila ukoo mzima hakuna mtu mnene, ukoo mzima wamekauka.

N.b mazoezi ni muhimu.
Nakazia, wengine mtatusema bure tu, tuwe na shida, tukose pesa, hata tushindie mihogo daily bado miili haipungui. Nimeamua tu kumaintain mwili wangu usizidi hapa ulipo basi.
 
Back
Top Bottom