Naomba radhi nimechelewa kwenye huu uzi maana MKOLONI WANGU KANIBANA SANA MWEZI HUU (Source:
Asprin)
Kuna watu watatu humu ambao kwa kweli walinisaidia sana kunishauri namna ya kuweka post na kuifanya iwe na changamoto mpaka sasa najivunia kuona kwamba wapo watu leo hii wanakiri kwamba kile ninachokifanya kimesaidia kubadili maisha yao.
Naomba niwalete kwenu Da'
AshaDii, kaka yangu
The Boss na dada yangu
gfsonwin.
Nakumbuka nilijiunga na Jamii forum mwaka 2008, wakati huo ikiitwa Jambo Forum, lakini nilipokuwa nikiweka post zangu watu wanalaumu kuwa ni ndefu na zikawa hazisomwi sana. Nikaacha kuweka post na kuendelea na maisha.
Siku moja nadhani mwaka 2011, nikajiambia hebu nijaribu tena, nakumbuka nilikuwa naweka post nyingi kwa siku tena ndefu tu kama zamani... Hali ikawa ni ile ile. Siku moja baada ya kusoma post ya AshaDii, nikavutiwa nayo na nikawasiliana na yeye kwa PM kwa ajili ya ushauri.
Alinisaidia sana kunielimisha namna ya kuweka post na kushiriki mjadala katika post niliyoweka na pia kushiriki mijadala mbalimbali katika majukwaa tofauti tofauti kwani itasaidia kutambuliwa kama mchangiaji mzuri wa JF... nashukuru kwamba ushauri huo umenisaidia sana.
The Boss na yeye alinisaidia sana namna ya ya kujenga hoja na kuitetea, pia alinisaidia sana kwenye maeneo ya IT.......... kwa mfano ku-quote, kuweka picha na vitu kana hivyo...
Dada yangu
gfsonwin sina la kusema, wewe mwenyewe unajua ni kiasi gani umekuwa msaada wangu kwa ushauri wa mambo ya kifamilia hususan kumjua Mungu na maombi. (SUGUA GOTI SANA...!)
Lakini pia yupo mama yangu
Mamndenyi, nilipopata ajali tarehe 25/10/2011, ulijitahidi sana kunitumia asali na mdalasini kama dawa, leo nimepona na nina bofya keyboard kama kawa, ubarikiwe mama.
Nitafanya kosa kubwa kama nisipowataja wanangu wawili ambao kupitia changamoto zao za ulinzi shirikishi zimenisaidia sana kuniepusha na kifo cha UKIMWI maana wamejitahidi sana kunibana kila kona mpaka nimesalimu amri...
Big up sana kwa mwanangu
Cantalisia popote ulipo na dada yako mkubwa
King'asti......
Naomba niwatambue wana MMU wooote jamani ngoja tu nitambue uwepo wa
SnowBall,
jouneGwalu,
Eiyer,
Mwita Maranya,
Asprin,
mwanjamiione,
BADILI TABIA na
nyumba kubwa .......
Mwisho ni wana CHIT CHAT, hapa naomba niwataje
Madame B,
lara 1,
cacico,
snowhite,
charminglady,
sweetlady 1, @Smail,
Kongosho na wengine ambao sikuwataja, lakini wamekuwa wakichagiza mijadala mbalimbali hapo chit chat kwa mipasho na kujishetua mpaka raha jamani.............. Loooooooh!!!!!!!!!!!