Kwanini Kagame amemitumua Karusisi na kumuweka Gashugi ambaye hana uzoefu mkubwa ???
Kwanini Rwanda, nchi ambayo ni tajiri inaogopa kuwekewa vikwazo vya misaada (Aids and Grants) kutoka EU na G7 ???
Hivi kima cha kipato cha kila raia wa Rwanda (GDP Per Capita) ni kikubwa kiasi gani ???
. Karusisi: Hakuna mnyarwanda kwenye cheo chake ni mungu-mtu. Amekuwepo, ametekeleza majukumu yake, na wengine wanahitaji kupata uzoefu.
Sijui kitu gani unachokiita kutimua: Je, kama anakopelekwa kunahitaji mwenye uzoefu alio nao, au anatakiwa pia na yeye ajifunze mengine, atakuwaje ametimuliwa!!! Gashugi nae ana haki ya kuwa na madaraka kwenye nchi yake, kama amekidhi vigezo. Katoka sehemu moja, kahamishiwa kwingine, na baada ya muda atakabidhiwa mwingine.
Rwanda haiogopi kuwekewa vikwazo. Ni kweli msaada kama upo, ni msaada. Ila usipokuwepo, maisha yataendelea.
Mwaka 1994 Rwanda iliishi kwa msaada wa nani? Mara mia Tanzania iliyopokea wakimbizi, ikawapa hifadhi na mahitaji mhimu,itaheshimika miaka mia kuliko hao wa mbali, ambao misaada yao ina masharti.
Hivi, hao mnawaona wajinga,ndo wana hela za kuchezea kutoa misaada? Kodi za raia ndo ziende kuchezewa?
Marekani imeisaidia Ukraine kwenye vita vyake. Kilichofuata ni mfano hai wa hiyo misaada.
Missada hiyo unayoisema, chunguza imekaeje kwanza.
Shilika likija na hela, na kukuelekeza namna ya kuzitumia, na wanaozitumia wametoka nao kwao, ndo wanunulie magari, ndo walipwe mishahara, ndo matumizi yao kila siku, kwenye milioni 100, msaada kwako ni kiasi gani?
Nchi tajiri labda unaipima kwa vigezo gani!! Rwanda ni nchi inayojitafuta, siyo nchi tajiri. Japo pia si masikini kihivyo.
GDP ipo kwenye Dola elfu moja na kitu