1. Ni nani ambaye pengine anaandaliwa kumrithi Mr. Tall, akiondoka madarakani?
2. Mfumo wa elimu ya Rwanda ukoje? Kuanzia msingi mpaka vyuo.
3. Mfumo wa matibabu ukoje, huduma za afya zinapatikana kwa urahisi?
Watu wengi wanatumia bima ya afya?
Je serikali inagharamia matibabu kwa baadhi ya makundi ya watu?
4. Rwanda mnachimba madini gani hasa?
5. Kwa nini unasema Rwanda ni masikini wakati mmewekeza mpaka kwenye baadhi ya vilabu vya mpira ulaya (Arsenal, PSG nk..)?
6. Vipi huko Rwanda umeme ni tatizo kubwa? Kuna mgao wa umeme? Vijiji vyote vina umeme?
7. Je huko pia kuna machawa? 😂
Ahsante sana!
1. Sijui
2. Rwanda shule ya msingi ni miaka 6, sekondali miaka 6(O level miaka 3 na A level miaka 3) Kwa sasa kuna kitu kinaitwa 9 years Basic Education. Unasoma shule ya msingi miaka 6, na 3 ya O level sehemu moja.
Kwingine ni 12 years Basic Education. Yaani miaka yote 12 unasomea sehemu moja.
Elimu kwa ujumla imekumbwa na changamoto ya mfumo. Zamani, kulikuwa na mfumo wa kifaransa, badae ukageuzwa kuwa wa kiingeleza. Hivyo, waliokuwa wakisoma mfumo wa kifaransa, walipata changamoto ya kuadapt lugha.
Mbali na hilo, uongozi wa Wizara unaokuja, unakuja na mapya yake. Labda vyuo vikuu, na kwenyewe badhi ya sections furani, kama sheria, nursing,ICT, ndo unakuta wameiva sana.
Ila wasomi wengi, wapo chini ya kiwango
3. Mfumo wa matibabu, wanywarwanda wamegawanywa katika makundi 4 kulingana na uwezo wao. Kundi la kwanza, linasaidiwa na serikali kulipiwa.
Kundi la pili na la tatu, kila kichwa cha familia ni Faranga elfu 3(karibia elfu 6 ya Tanzania). Kundi la 4 ambalo ni la watu wenye uwezo wa juu, kila kichwa cha familia ni elfu 7(Karibia 14 ya kitanzania).
Kwa ujumnla, upatikanaji ni rahisi, kwa sababu kila raia ana access kwa daktari. Na kabla hujafika huko, nchi nzima kuna wahudumu wa afya, kila kitongoji, ukijisikia vibaya unamuona. Huduma za kwanza wanatoa, na dose kama za malaria na magomnjwa madogo madogo unapata hapo hapo. Ikiwa ni kesi iliyo nje ya uwezo wao, kuna zahanati za kata. Hapo wakiferi, unaenda kituo cha afya. Kesi yako ikiwa kubwa, unapewa referal kuelekea Hospitali ya wilaya.
Kwa hiyo kuna bima ya afya ya Pamoja(CBHI Community Based Health Insurance), na bima za mashirika. So, ukienda kwa ajili ya matibabu, unalipia 10% ya gharama zote, hata ulazwe miaka 10.
uongozi wa wilaya ukibainisha mtu hana uwezo, serikali inaghalamia 100%
4. Rwanda, madini yapo. Kuhusu labda tetesi za wanaossema ya DRC. Hilo sitoliingilia, lakini inawezekanaje mashariki ya Congo yote iwe na hizo ressources, then zisivuke mpaka! Sema tu kwa kuwa ni nchi ndogo, na technologia labda isiwe kubwa kama ya migodi ya kifahari, na uchimbaji wake ni wa masharti, lakini madini yote yapo. Labda nitafute majina.
5. Umasikini naouongelea, ni hatua ya maendeleo ukilinganisha na nchi jilani zilizotangulia, au na maisha kwa ujumla. Uwekezaji kwa timu za nje, ni kwa ajili ya kuhamasisha watu kuja kuwekeza ndani na kutengeneza ajira. Jambo hilo linasaidia kupunguza ukosefu wa ajira. Pia, ukilinganisha na nchi jirani,fursa za kimaisha ni tofauti na za nchi hizo. Hivyo,niseme ni nchi ambayo inajijenga, miaka 30 ni muda mfupi sana kuweza kufikia hatua za waliokutangulia.
6. Rwanda mgao wa umeme hakuna. Inaweza tokea labda kama kuna marekebisho. Vijini umeme unasambazwa, nadhani kwa sasa wanyarwanda 70% au zaidi kidogo wana umeme. Kukatika ni kama 5%
7. Nahisi uchawa unamaanisha kujipendekeza: Rwanda unalipwa kwa kile ulichokifanya na chenye manufaa kwa jamii.
Ukizingatia, ni nchi cganga,chama tawala cha RPF ndo kimekuwepo kuhakikisha kila jambo linatekelezwa. Vyama vya upinzani, vingi vilionekana kutaka kurudisha mfumo wa kikabila,havikupewa nafasi.
Hata vilivyopo, ni kwa misingi ya chama tawala. Upinzani utakuwepo kuhakikisha wanaikosoa serikali kwa yale yasiyokuwa sahihi, na sera zenye mashiko. Sasa, wenye sera hizo, utakuta ni mtu anaehitaji kujenga jina kisiasa au kujipatia chochote tu.
Kama sijajibu vizuri uliza