1- Ni Frws ngapi zinatosha kama mahari nikienda kuoa rwanda? nipe kiwango cha chin na juu.
2- Na taratibu zipi itatakiwa nifuate ili nioe mwanamke rwanda?
Asiri yang kwa mbali hiyo
1. Rwanda ukimpata mwanamke anaejielewa,mwenye malezi, huwezi kuset kiwango. Wewe mwenyewe unapanga kulingana na uwezo wako. Familia ya mwanamke, inakutambua kama mwanao na wewe pia, hivyo, ikiwa mnaanzisha familia, wanaamini majukumu yanaanza upya, hivyo hawawezi kuacha mende kuteseka. Kwa hiyo, wewe na uliemridhia, mnaweza ongea, yeye ujumbe atafikishia wazazi, then wewe, washenga wako wataongea kutokana na ulichokubaliana na mkeo mtarajiwa. Labda ukikutana na bishoo wa kisasa anaijiona amesoma, ndo atakwambia mi ni msomi ujue, na mahari yangu si chini ya milioni mbili(Tshs 5,000,000). Hapo ni wewe mwenyewe. Kama unataka mke bora, ni simple na huenda isivuke laki 5. Ila kama unataka bora mke, hata milioni 10.
2. Kama familia yoyote,inatakiwa ijue mtoto wao anaenda wapi. Je, aendako atakuwa salama? Hapo kulingana na uwezo ulio nao, unaweza fanyia taratibu za ndoa huko na ukamleta, kikubwa uelewe kwamba kuna watu kadhaa, yeye mwenyewe atakusaidia kujua idadi, kulingana pia na uwezo mlio nao, wawasindikize mpaka makao mapya yenu.
Taratibu za posa na vitu gani, Rwanda havipo. Kama mmeridhiana, mtatambulishana (hasa yeye atakutambulisha kwa wazazi na watu wake wa karibu). Huko hakunaga longo longo nyingi, ukiamuwa kama si muoga, unawaface wazazi mnaongea, au unamtafuta mtu mzima, kama zilivyo mila. Baada ya kumtolea mahari, ndoa ya kiserikali ndo mhimu sana kwa wengi. Ikiwa wewe unataka kukaa Rwanda, mtafunga ndoa na mtakaa. Ukitaka kumchukua kwenda kwenu, ni wewe tu. Ukitaka ndoa mkafungie TZ, ni wewe tu. Hapo ukifungia kule, documents unapeleka uhamiaji kutambulisha mgeni, rekodi zinawekwa unaingia.
Rwanda, unachotakiwa kama utataka kukaa, ni paspoti yako tu, wala huulizwi unaenda kufanya nini au kukaa muda gani, ukitaka, hamia mazima. Passport ikiisha muda, toka ukarenew.
Kama sijaeleweka popote niulize