Hiki kisa kukiweka nlikua naona noma sana.
Anyway, ntajaribu kuweka codes kwa usalama.
Kipindi nipi Form 5 miaka hiyo nasoma boarding boys tulipata mualiko kwenda shule ya boarding ya girls. Officially ilikua ni kwa ajili ya debate lakini uhalisia ilikua ni kucheza mziki na kufamamiana.
Kuna manzi nlikutana nae siku hiyo alikua ni mkali kinoma. Kapanda hewani, rangi ya mtume, slim na figure moja matata. Alikua na jicho yule manzi akikuangalia unahisi upo ndotoni. Kama bahati tukaanza kuongea tukaelewana na ile siku nzima nka spend nae na hata mziki hatukucheza. Tulikaa tu nje kwenye viti, story kwa sana. Wakati tunaondoka kanipa namba yake njia nzima tunachat. Kipindi hicho ni mwendo wa Nokia Obama tu. Zinafichwa hatari sizikamatwe. Siku ile ile tukaanza kudate lakini kula tunda ilichukua miezi karibia sita.
Katika wanawake wote nliowahi kuwa nao hakuna nliewahi kumpenda kama huyu. Kipindi hicho nlikuawaga nacheza Basketball sana, ile likizo nlikuaga nadundia kikapu pale UDSM, kwao alipokua anafikiawakati wa likizo ilikua kwa baba mdogo wake maeneo ya Kimara. Alikua anakuja uwanjani anakaa nje wakati tunacheza, anatucheki halafu jioni muda wa kuondoka tunatembea hadi Ubungo pale pembeni ya Tanesco, kipindi hicho kuna stand ya daladala. Tukifika hapo anapanda daladala ya Kimara na mimi naenda home. Yale mapenzi yalidumu mpaka tunamaliza Form 6.
Tulimaliza alikaa Dar hadi mwezi wa 7, kuonana karibia kila wiki, ratiba ni kukutana kwa ajili ya show au kwenye kikapu, kipindi hicho nacheza ligi na team moja jina kapuni. Mwezi wa 7 akaenda kwao kabisa Moshi. Mapenzi ya kwenye simu yakaanza. Vyuo vikafata. Mikoa tofauti. Kuonana ikawa shida. Mambo yakawa mengi, akaanza kunipotezea, na mimi nlikua nshajua huyu sio wangu tena. Kwa ule uzuri, plus umbali na life la chuo. Siku akaniambia tuachane, ile ile semester ya kwanza, mimi nkawa muelewa sana hakuamini. Maisha yakaendelea.
Ikawa baada ya muda kama miezi au mwaka ananicheki tunaongea au tunaweza chat af anapotea, sikuona point yoyote kuhangaika kurudiana nae, so akinitafuta najibu fresh tu akipotea na mimi nakausha lakini sijawahi kugombana nae wala kumjibu vibaya, mimi ni full vibes tu. Now ni mwalimu wa secomdary, alishaolewaga kitambo tu na ana watoto anaishi mkoani huko kaskazini.
March mwaka huu siku kancheki instagram anaomba namba yangu, nikampa akanipigia. Akaniambia mdogo wake wa mwisho anasoma chuo hapa Dar, degree ya mambo ya ICT, wamepewa barua za kuombea field lakini hana connection yoyote. Akaniomba nimsaidie kumtafutia field na kumpa ABCs za jinsi kuendana na hii taalumu coz mimi ndo taaluma yangu na nafanya kazi na watu wengi wa hii taaluma. Mi sina shida kabisa, nkamuambia ampe namba yangu anicheki.
Kweli siki hiyo hiyo jioni yule dogo kanipigia, nmeongea nae vizuri kajitambulisha na shikamoo kibao. Nkamuambia baada ya kama siku 3 hivi ntakua na kazi karibia na chuoni kwao ataniletea hiyo barua.
Hiyo siku anaileta ndo nkamuona, ni version ya dada yake copy and paste kipindi naanza nae mapenzi miaka hiyo. Alikuja na mwenzie kibonge bonge. Nkachukua barua wakasepa. Akawa anantafuta sana whatsapp kuomba ushauri na kuulizia nimefikia wapi, namjibu tu kawaida inaisha. Sijawahi waza kumla, nna majanga yangu kibao ya michepuko. Kuongeza mwanamke haikua in my favour kabisa. Kuna siku kama two weeks zimepita now siku Madrid kamtoa Chelsea UEFA nlikua na wanangu tunakunywa bia huku tunacheki game, katika kuperuzi status za watu nkaona amejipost status, zile za manzi anaangalia camera tu na kubetua midomo. Nkacomment pale tukaanza kuchat, sasa na zile bia kichwani nkawa kama namuonesha namtaka na yeye anakuja tu, nkamuomba pics zake katuma kama 20. Nkajua hapa tayari.
Kesho yake nlikua naingia job mchana. Mambo ya support tu hamna ishu. Asubuhi nikamcheki jamaa alieingia asubuhi nkamuomba amalize siku nzima na mimi siku tunaingia wote ntamaliza siku nzima na yeye apumzike mwamba kakubali. Midaa ya saa 3 hivi nkatext kale katoto whatsapp nkakaambia nataka kukaona, kakauliza saa ngapi na wapi, nkaaambia mchana maeneo ya External kakasema kakitoka class saa 6 katakuja.
Sikutaka kutumia nguvu nyingi, nkaenda kununua Wine ya Four Cousins chupa mbili na icecream ile kubwa nkaziweka kwa fridge nkaenda kupata supu halafu nkaenda maeneo ya External, nkaaagiza kuku nusu na chips ya kufunga nkawa nakasubiri. By saa 8 hivi kakawa kamefika, kamevaa zile suruali zao wanaziita high waist, kanaita balaa. Kalivosema kamefika mimi nkaita bolt ya gari ki IST halafu nkamuambia dereva kuna mtu tunamfata kituo cha daladala, tumefika nkampigia simu na maelekezo kaja kaingia kwenye gari tumesepa. Home moja kwa moja.
Tumeingia ndani ananiuliza why umenileta kwako nkamjibu mchana huu na hili jua unataka twende wapi, subiri jion ntakutoa out halafu ntakurudidha hostel. Nkakaandalia msosi kakala fresh tukawa tunapiga story. Nkaweka movie muda unasogea. Baada ya kama nusu saa nkafata wine chupa moja na glass mbili, kauliza vimaswali pale nkamtoa hofu tukaanza kunywa.
Nimejilia mema ya nchi mchana kutwa, baada ya bao la kwanza nkakaletea icecream tunakula kwa bed full mahaba na usiku hakajaondoka kakalala. Usiku nkampeleka kucheki game ya Liverpool na Benfica full burudani.
Now kanataka kuja karibia kila siku, shule haijachanganya bado, tatizo mapopo yangu ya kila siku nayapeleka wapi.
Naona sikatendei haki coz najua sitakuja kuweza kukatreat au kukapenda kama ilivokuaga kwa dada yake. Kama atamwambia dada yake au vipi atajua mwenyewe.