Ni kweli naelewa unatakiwa uchanganye kwa mashine, unaweza nunua kila kitu na vikorokoro vingine ukaongezewa kwenye mashine zinazosaga wakakusagia ukapaki mifuko yako, saizi ya punje itakuwa ngumu kama unatumia kinu na sio mashine. Namsoma amesema alinunua kinu.... alternatively kuna maduka ya vyakula huwa yanauza mahindi yaliyoparazwa na vikorokoro vingine vingi, vifaranga wanahitaji vitu vyote muhimu kwani wanakua haraka. Kuna formula zinataja damu, mabaki ya samaki, majani yaliokaushwa, premix, kwa v iwango tofauti sasa kama vikizidi au kupungua.... mimi nina vifaranga chotara hapa wiki 2 nawalisha starter bado ila watakaototolewa na hawa najiandaa kuchanganya mwenyewe nitaleta feedback hapa

Mama Joe vifaranga walishatotolewa tayari? Yaani kujitengenezea chakula cha vifaranga hiki ni kitendawili tunatakiwa tukitegue tuweze kupata faida kubwa, tunakusikilizia Mkuu.
 
Mama Joe vifaranga walishatotolewa tayari? yaani kujitengenezea chakula cha vifaranga hiki ni kitendawili tunatakiwa tukitegue tuweze kupata faida kubwa, tunakusikilizia Mkuu.

Mkuu ishu ya Utenegnezaji wa Chakula ni Ngumu kwa sababu tu, ni vigumu kujua DCP, Hapa ndo kwenye kazi ngumu sana, Naugumu unakuja kwa sababu ni laizima ujue CP inayopo kwa kila aina ya Chakula cha kuku,

Natatizo hilo linasababibishwana ukweli kwamba zile nafaka za kuchanganya unakuta zina tofautiana CP, unaweza kuta Mahindi ya Rukwa na ya kutoka My be Tangayakawa na CP tofauti na wewe usha ambiwa unapimb kilo 10 za mahindi so hapo ndo tatizo lilipo

Ila nimesema kwa anaye taka kutengeneza nitampatia contct za hao jamaa wa Keny na unaweza tuma sample wewe mwenyewe ili wakuambie kama CP iliyopo inatosheleza au la, matokea hutoka siku hiyo hiyo na unaweza tuma kwa njia ya DHL au hata Mabasi ya Kenya kama Kampala Coach

Na CP hiwezi pimwa kwa Kilo au Macho ni lazima utumie kifaa maalumu cha kupimia
 
Mwezi Ujao Mwishoni au May nitaenda Kenya kufuatilia wale Kuku wa Israeli pamoja na ile mbegu yao mpya ya kuku wa Kienyeji inayo taga kuliko wa kisasa, jamaa nimewasiliana nao na inabidi niende kwa sababu wao hawawezi tuma vifaranga kwa sabau ya sheria za maswala ya mifugo, na kama kuna mtu yuko wizara ya kilimo na mifugo hebu atupe utaratibu wa kuingiza mifugo unakuwa vipi, make Nasikia boda huwa wanasumbua sana.

Ingawa huku Arusha kuna watu huwa wanaletewa vifaranga kutoka Nairobi kenya na vinatumwa kwa Ndege sijajua sheria zinasema vipi, Ila ikishindikana nitapita nao tu pale Namanga Boda
 
Ukitak kutuma Sample Kenya kwaajili ya kupima DCP basi contct ni hizo hapo KARI Naivasha P.O. Box 25, 20117 Naivasha, Tel. 0726 264 032.

Na ni bora kila mtu akajaribu kutenegeneza kw kufuata zile formula and then utume na jamaa kama haijafikia viwango watakuambia ni kitu gani cha kuongeza au kupunguza
 
Mkuu kubota nakushuru kwa elim kubwa unayotupatia, mi niliwahi kufuga kuku ambapo nilianza na kuku wakubwa 30, na nilikuwa na bahati ya kuku wangu kutotoa vifaranga wengi, ila mpaka mradi unakufa kwa sababu ya kuibiwa kuku sikuwahi kukuza vifaranga, walikuwa wakifikisha wiki mbili walikuwa wanapatwa na nundu nundu hasa maeneo ya kichwani, kitu kilichokuwa kinasababisha wafe. Kwa uzoef wako km umewahi kukutana na tatizo hilo ulilitatua namna gani? Tupo pamoja
 
Safi sana mkuu Kubota nimeipenda sana hii ya kutumia mbwa kama mlinzi na mimi ngoja niitumie maaana hawa wanyama mwitu dawa ni kuwapambanisha na mnyama mwenzao.

Vipi kuhusu PANYA unweza kuwadhibiti kwa njia gani maana huwezi kufuga PAKA akakaa na MBWA sehemu moja...na ukisema utumie SUMU YA PANYA kuna uwezekano wa kuua kuku woote.
 
Ukitak kutuma Sample Kenya kwaajili ya kupima DCP basi contct ni hizo hapo KARI Naivasha P.O. Box 25, 20117 Naivasha, Tel. 0726 264 032.

Na ni bora kila mtu akajaribu kutenegeneza kw kufuata zile formula and then utume na jamaa kama haijafikia viwango watakuambia ni kitu gani cha kuongeza au kupunguza

Mkuu nipo arusha maeneo ya porin kidogo. Please ni PM namba yako ya simu please!
 
Mkuu kubota nakushuru kwa elim kubwa unayotupatia, mi niliwahi kufuga kuku ambapo nilianza na kuku wakubwa 30, na nilikuwa na bahati ya kuku wangu kutotoa vifaranga wengi, ila mpaka mradi unakufa kwa sababu ya kuibiwa kuku sikuwahi kukuza vifaranga, walikuwa wakifikisha wiki mbili walikuwa wanapatwa na nundu nundu hasa maeneo ya kichwani, kitu kilichokuwa kinasababisha wafe. Kwa uzoef wako km umewahi kukutana na tatizo hilo ulilitatua namna gani? Tupo pamoja

Mkubwa wangu Lutayega, mimi pia yaliwahi kunikuta hayo matatizo ya kuku kota manundu, tatizo hilo nimelielezea kwa kirefu sana kwenye post yangu inayohusu magonjwa huko nyuma, ukipata nafasi ndugu yangu pitia usome post zote za thread hii utaokota vingi zaidi. Mimi tatizo la manundu halikuwa linanikosesha usingizi baada ya kufanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuwatibu vifaranga kwa kuwapaka mafuta ya alizeti kwenye manundu yao. Sielewi ni jinsi gani mafuta ya alizeti yanavyotibu ugonjwa lakini hata kama kichwa kilikuwa kimevimba uvimbe unanyauka, ni miujiza!
 
Safi sana mkuu Kubota nimeipenda sana hii ya kutumia mbwa kama mlinzi na mimi ngoja niitumie maaana hawa wanyama mwitu dawa ni kuwapambanisha na mnyama mwenzao...

Vipi kuhusu PANYA unweza kuwadhibiti kwa njia gani maana huwezi kufuga PAKA akakaa na MBWA sehemu moja...na ukisema utumie SUMU YA PANYA kuna uwezekano wa kuua kuku woote...

Mkubwa Asigwa, panya wanadhibitiwa kwa sumu na mitego isipokuwa ni kama ulivyohisi usipokuwa makini unaweza kuta umenasa kuku badala ya panya. Njia ya sumu haifai kwa vile ni rahisi sana kudhuru kuku. Kwa vile mara myingi panya husumbua zaidi wakati wa usiku unapaswa kuchunguza wanakoijia panya na kuweka mitego yako huko huko ili iwanase kabla hawajaingia ndani. Kinachowapeleka panya ndani ya banda la kuku huwa ni kufuata chakula kwa hiyo ukitega mtego wako nje kwenye mapito yao utawanasa tu isipokuwa kumbuka asubuhi na mapema kuondoa mitego hiyo ili kusalimisha kuku.

Njia nyingine ambayo nimefanikiwa sana ni kuchimbia ndoo hizi za lita 10. Unachimba shimo nje ya nyumba kwa panya wanaotokea nje. Ndoo moja inatosha kwa panya wa majumbani. Ukishachimba shimo unaizamisha ndoo yote na kufukia kando kando ya shimo na kuta za ndoo. Ndoo ifukiwe vizuri kiasi kwamba ndoo inazamishwa yote.

Baada ya hapo unaijaza maji nusu ndoo! Halafu unanyunyizia pumba kuzunguka kingo ya ndoo kwa juu. Panya wanapenda sana pumba na wanapokula huwa wanatabia ya kutokuwa na utulivu hivyo fujo fujo zao hujikuta wamedumbukia na hawawezi kutoka nje. Hakikisha kila asubuhi unadamka kuondoa panya waliozama na kufunika mtego huo kwa kitu kizito ili kuzuia vifaranga wasidumbukie wakati wa mchana.

Ukifanya hivi kwa wiki nzima ukoo wa panya uliokuwa unakusumbua hutoweka. Elewa panya huishi kwa koo. Ukiangamiza koo nzima huchukua muda mrefu sana hadi ukoo mpya uje toka mbali. Njia hii imekuwa ikitumika kwa mafanikio makubwa sana kuangamiza panya mashambani, unahitaji kutega ndoo kama nne hadi nane kwa ekari moja kutegemea na wingi wa points ambazo panya wanaingilia shamba.

Wadau wengine wataboresha zaidi kama kuna nyongeza, karibuni.
 
Mkuu Kuku wa Kizungu labda Parent, lakini haa wa Mayai hawafai na hata kiutalaamu haishauriwiingawa yanaweza totolewa lakini hivyo vifaranga watakua dhaifi na wanaweza kufa,

Kwa kuku wa kizungu ni lazima ununue Parents, Vifaranga au Kuku wazima na Vifaranga parents wanaagizwa kutoka South Africa, Uholanzi na Ugeruman, Ila kwa Africa mashariki Kenya ndo pekee kwenye kampuni inayo zalisha Vifaranga Parents wa kuku nyama na kuk mayai,

Asante sana Mkuu Chasha. Mimi Ninafuga kuku wa mayai wa kizungu ambao watatu wamekua majogoo. Haya majogoo yanamuonekano kama machotara (weupe na kama kahawia mgongoni na njanonjano) hawa huwapanda wa mayai kwa kwenda mbele. Kwa majibu yako ina maansha hata hawa majogoo si riziki? kwa mfano nikawatoa nikawa cross na kuku wa kienyeji pure hawataweza toa vifaranga na kukua? na kama wakitoa vifaranga ni watakua cross au ndio iyo chotara? Asante sana
 
Mkubwa Asigwa, panya wanadhibitiwa kwa sumu na mitego isipokuwa ni kama ulivyohisi usipokuwa makini unaweza kuta umenasa kuku badala ya panya. Njia ya sumu haifai kwa vile ni rahisi sana kudhuru kuku. Kwa vile mara myingi panya husumbua zaidi wakati wa usiku unapaswa kuchunguza wanakoijia panya na kuweka mitego yako huko huko ili iwanase kabla hawajaingia ndani. Kinachowapeleka panya ndani ya banda la kuku huwa ni kufuata chakula kwa hiyo ukitega mtego wako nje kwenye mapito yao utawanasa tu isipokuwa kumbuka asubuhi na mapema kuondoa mitego hiyo ili kusalimisha kuku.

Njia nyingine ambayo nimefanikiwa sana ni kuchimbia ndoo hizi za lita 10. Unachimba shimo nje ya nyumba kwa panya wanaotokea nje. Ndoo moja inatosha kwa panya wa majumbani. Ukishachimba shimo unaizamisha ndoo yote na kufukia kando kando ya shimo na kuta za ndoo. Ndoo ifukiwe vizuri kiasi kwamba ndoo inazamishwa yote. Baada ya hapo unaijaza maji nusu ndoo! Halafu unanyunyizia pumba kuzunguka kingo ya ndoo kwa juu.

Panya wanapenda sana pumba na wanapokula huwa wanatabia ya kutokuwa na utulivu hivyo fujo fujo zao hujikuta wamedumbukia na hawawezi kutoka nje. Hakikisha kila asubuhi unadamka kuondoa panya waliozama na kufunika mtego huo kwa kitu kizito ili kuzuia vifaranga wasidumbukie wakati wa mchana. Ukifanya hivi kwa wiki nzima ukoo wa panya uliokuwa unakusumbua hutoweka.

Elewa panya huishi kwa koo. Ukiangamiza koo nzima huchukua muda mrefu sana hadi ukoo mpya uje toka mbali. Njia hii imekuwa ikitumika kwa mafanikio makubwa sana kuangamiza panya mashambani, unahitaji kutega ndoo kama nne hadi nane kwa ekari moja kutegemea na wingi wa points ambazo panya wanaingilia shamba. Wadau wengine wataboresha zaidi kama kuna nyongeza, karibuni.
Asante sana mkuu...hii ya kutumia ndoo nimeipenda sana ni bora kuliko kuua kwa kutumia SUMU.. Safi sana mkuu.
 
Mkuu Kubota naomba kukuuliza swali ambalo litakua linarudi nyuma kidogo.

Mfano nikiamua kuwalaza kuku wakubwa kwenye banda moja na wakawa wanatumia banda hilo hilo katika utagaji, wakimaliza kutaga nakusanya mayai na kuyahifadhi sehemu tofauti na yalipotagiwa na nikigundua kuku ameanza kuatamia namwekea mayai kwenye kiota cha kuatamia halafu namuhamisha banda na kumuweka kwenye banda la pili maalumu kwa kuatamishia je huyo kuku muatamiaji hawezi kuyasusia mayai kama akikuta alipozoea kutagia mayai yake yamehamishiwa kwenye banda jingine?

Au anaweza kuvamia viota vingine vya kuku wengine ambao bado wanataga na kuanza kuyatia joto mayai ya kuku wengine??

Thanks in advance
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom