Qur'aan inaihitajia sana Sunnah kuliko Sunnah inavyoihitajia Sunnah. Qur'aan pekee yake haitoshelezi nila Sunnah, ndiyo maana Allah akasema :
2. Yeye ndiye aliye mpeleka Mtume kwenye watu wasio jua kusoma, awasomee Aya zake na awatakase, na awafunze Kitabu na hikima, ijapo kuwa kabla ya haya walikuwa katika upotofu ulio dhaahiri. (al-Jumu'a : 2)
Hapo katika aya hekima ni Sunnah. Maana Uislamu ndiyo Sunnah na Sunnah ndiyo Uislamu haviachani viwili hivyo. Kama alivyo sema Imamu al-Bahbahari katika Sharhu Sunnah.
Allah aliye juu anasema :
43. Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na inameni pamoja na wanao inama. (al-Baqarah : 43)
Naomba utuonyeshe namna ya kusali katika Qur'aan kuanzia mwanzo mpaka mwisho na utonyeshe namna ya kutoa zaka katika Qur'aan.
Hakuna sehemu ambayo sijaelewa, ndiyo maana nakukosoa. Huwezi kuwa Muislamu ukiwa unafata Qur'aan tu, kwanza unapingana na Qur'aan yenyewe, vipi una unaabudu ?
Unatakiwa usome dini yako kama unataka kuujua Uislamu.
Ukamuulize msomi wa dini siyo daktari wala mshona viatu, na huenda huyo mshona viatu akawa na elimu ya dini kumzidi huyo daktari na akajibu swali hilo, na kama huyo daktari bingwa akiwa mjuzi wa tafsiri ya Qur'aan hapo sawa, ila mtu wa kwanza kumuuliza ni msomi wa dini, akueleze aya husika Mtume aliifasiri vipi na maswahaba zake walielewa vipi na kuifanyia kazi vipi.
Watu sampuli(mnao jiita watetezi wa Uislamu na hamjausoma Uislamu) yako ndiyo mmepotosha maana nyingi sana za aya kwa kuleta maana ambazo sizo sahihi ili kuendana na mambo yenu ya Kisayansi na msahau ya kuwa Qur'aan ni muongozo na si kitabu cha Sayansi wala historia.