The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

Asante kwa taarif Mkuu, lets wait and see. Itakuwa poa mno kama Mrema akirejea alikotoka maana vitabaki vyama makini tu vya siasa.

Historia ya Mrema dhidi ya ufisadi ikiwekwa hapa nani wa kubishana ama kulinganishwa nayo?
Huyu mzee alipiga vita ufisadi kabla hata msamiati wa ufisadi haujaanza.
Chuki tu binafsi ambazo ni personal dhidi yake kwenye mchezo huu mchafu wa siasa ndizo zilipotufikisha hapa tulipo.
Ibra wewe unataka arudi ccm kwasababu hata msimamo wako hapa jamvini unaelemea upande wa ccm na kwa hivyo sishangai unapodai afanye hivyo ili vyama "Makini" vya upinzani vibaki.
 
Mzee wa KIlalacha na rafiki ya wa DP MTIKILA wameishiwa kabisa.Ni cheap Politicians
Aangalie asije akaishia kuwa na ngeu kama Mtikila kwa kukumbatia hizo siasa za njaa.
Umma siku hizi unajua kuwa LILA NA FILA HAZITANGAMANI
 
Mzee wa KIlalacha na rafiki ya wa DP MTIKILA wameishiwa kabisa.Ni cheap Politicians
Aangalie asije akaishia kuwa na ngeu kama Mtikila kwa kukumbatia hizo siasa za njaa.
Umma siku hizi unajua kuwa LILA NA FILA HAZITANGAMANI

Once again ushabiki tu...Humu ndani chadema wengi sana humu...Hivi Single D una guts za kumfananisha Mtikila na Mrema?
Unaweza kufanya hivyo kwa wale wageni wa siasa za bongo lakini si wote ndugu yangu...Wengine tuna memory safi sana kwenye issue kama hizi.
 
Once again ushabiki tu...Humu ndani chadema wengi sana humu...Hivi Steve D una guts za kumfananisha Mtikila na Mrema?
Unaweza kufanya hivyo kwa wale wageni wa siasa za bongo lakini si wote ndugu yangu...Wengine tuna memory safi sana kwenye issue kama hizi.

SteveD katoka wapi tena
 
Augustine Mrema kuwagawa CHADEMA na CUF na kuibukia CCM



Niliwahi kuandika huku nyuma kuhusu mafisadi kadhaa kujaribu kutumia makanisa wa wakristu, mkakati wao ukaja kuonekana wazi kupitia yale ya Rostam na KKKT. Na sasa mkakati huo unaendelea kwa kasi lakini kimya kimya bila vyombo vya habari kuandika ukiendelezwa na Lowassa. Baadaye nikaandika kuhusu Rostam na wenzake wakina Manji kutakana kuwatumia waislamu, hatimaye ikaja kujulikana wazi na ITV wakaanika kuhusu mikakati hiyo. Baada ya kuanikwa huko, kikundi hicho kidogo cha waislam kimeamua kujitokeza wazi wazi na kueleza bayana dhamaria yao ya kueneza udini na ukabila kupitia mihadhara. Tayari kikundi hicho kimeanza kazi katika mikoa kadhaa. Wakati Fulani nikawaeleza kuhusu mafisadi kumtumia Mbatia na ikaja kuonekana wazi katika uchaguzi Tarime. Na kiongozi mmoja wa NCCR alithibitisha kuwa fedha za kampeni walikuwa wakichukua kutoka kwa Makamba.


Sasa baada ya NCCR kuonekana imechafuka sana, sasa umepangwa mkakati mwingine wa kuitumia TLP hususani Mwenyekiti wake bwana Augustine Mrema. Mkakati huo utahusisha Mrema kupita katika mikoa mbalimbali kuisema CHADEMA, Mbowe na Reginald Mengi. Bwana Mrema atakuwa kuwa akikosoa ripoti ya jukwaa la wahariri ambayo iliweka wazi jinsi alivyotumia msiba wa Wangwe kutaka kujinufaisha kisiasa. Chini ya mkakati huo Bwana Mrema atajifanya kuwa rafiiki wa karibu na CUF ili kuwatenga na CHADEMA. Vyama hivi viwili vina ushirikiano wa karibu sana bungeni. Duru za uchunguzi zinaonyesha kwamba Bwana Mrema aliwahi kutembelea kiongozi mmoja mkuu wa nchi na kumuomba amuhakikishie kuwa ataendelea kuwa Mwenyekiti wa TLP dhidi ya anaowaita mamluki ambao wanataka mkutano mkuu wa chama hicho uitishwe ili waweze kumng’oa.


Chanzo cha habari kinaeleza kuwa Bwana Mrema alihakikishiwa kuendelea kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa masharti kwamba atumie chama hicho kuwapoteza maboya CUF katika mazungumzo yao ya mwafaka baina ya vyama hivyo na CCM. Mara baada ya kikao hicho, Mrema alifanya kikao kingine na watuhumiwa wawili wa ufisadi kwa lengo la kujadiliana kuhusu kupata fedha ya kuendesha chama hicho baada ya ruzuku ya chama hicho kupungua kutokana na aliyekuwa Mbunge wake Phares Kabuye kuondolewa. Watuhumiwa hao wawili walimpa sharti bwana Mrema kuwa chama chake na yeye mwenyewe wawe mstari wa mbele kumshambulia Mbowe, CHADEMA na Reginald Mengi. Mwandishi mmoja wa habari aliyepewa jukumu la kuratibu habari za Mrema ameeleza kuwa mkakati mzima kama ukifanikiwa unalengo la kuharibu na kupunguza imani ya upinzani kwa ujumla wake.

Baada ya kumaliza kuishambulia CHADEMA na Mbowe, Bwana Mrema atarejea CCM na kueleza kwamba anarejea CCM kwa sababu ushirikiano wa upinzani umekuvunjika na kwamba wapinzani ni wanafiki. Hata hivyo, Bwana Mrema anakibiliwa na upinzani mkali ndani ya chama chake kutoka kwa kundi la Vijana ambalo limejijenga chini ya aliyekuwa Mbunge bwana Benedict Ntungirehi ambaye analenga kumwondoa Mrema na kuleta mageuzi katika chama hicho. Hali si shwari ndani ya chama hicho baada ya hivi karibuni, chama hicho kukiandikia barua Kituo cha Demokrasia Tanzania(TCD) na nakala kupeleka kwa Rais Kikwete kikimlaumu Mkurugenzi wa Kituo hicho kushindwa kumtetea Kikwete kama Mwenyekiti wa CCM ambaye ni mwanachama wa kituo hicho alipotajwa kwenye orodha ya mafisadi. TLP imeilalamikia TCD kwa kumtetea Mbowe ambaye alikuwa Mkuu wa Msafara wa safari iliyoandaliwa na kituo hicho ya mjini Afrika Kusini ambayo Naibu Katibu Mkuu wa TLP aliyekuwa kwenye msafara huo aliwahi kumtuhumu Mbowe kuwa alifanya sherehe alipopokea Taarifa ya Kifo cha Chacha Wangwe.


Kati ya makombora ambayo Bwana Mrema amejiandaa kuirushia CHADEMA ni tuhuma kuwa chama hicho kinachukua wanachama na viongozi toka TLP na kuwahamaishia CHADEMA. Kati ya viongozi wanaotajwa ni pamoja na aliyekuwa Diwani wa Kata ya Sombetini Bwana Mawazo na aliyekuwa mgombea ubunge wa chama hicho Arusha mjini Bwana Godbless Lema. Habari kutoka Arusha zinaeleza kuwa wakati Bwana Mawazo alitoka TLP na kujiunga na CCM, bwana Lema si ametangaza kwa waandishi wa habari kwamba si mwanachama wa chama chochote cha siasa kwa sasa. Hata hivyo Bwana Mrema amesisitiza kuwa wanachama wake hao wasingeondoka chama hicho kama isingekuwa ushawishi kutoka CHADEMA. Mchambuzi mmoja anasema kwamba kama mkakati huo utafanikiwa basi unaweza kuwa mwanzo wa umaarufu wa CHADEMA kisiasa kuporomoka na ule wa Mrema kupanda na kumfanya apokelewe CCM kama shujaa aliyerejea baada ya kukamilisha kazi maalum.

PM
Sidhani kama utabiri wako utatimia.Bwana Godbless Lema alitimuliwa na TLP mkoa baada ya kumgudua alisuka deal ya kumhamishia Bwana Mawazo CCM.
CHADEMA wakimchukua Bwana Lema ni kufilisika kisiasa kwasababu hana tena thamani aliyokuwa nayo mwaka 2005.Bwana Lema alishiriki kichinichini kumpigia debemgombea wa CCM bwana Mawazo.
 
Once again ushabiki tu...Humu ndani chadema wengi sana humu...Hivi Single D una guts za kumfananisha Mtikila na Mrema?
Unaweza kufanya hivyo kwa wale wageni wa siasa za bongo lakini si wote ndugu yangu...Wengine tuna memory safi sana kwenye issue kama hizi.

JMushi asante sana kwa kuliweka hili sawa.
Kila binadamu ana mapungufu yake,historia itasimama Bwana Mrema kamwe hawezi kuwekwa fungu moja na Mch Mtikila.Kwa maoni yangu Tanzania bado inahitaji mchango wa Bwana Mrema hasa pale wizara ya mambo ya ndani.
 
Augustine Mrema kuwagawa CHADEMA na CUF na kuibukia CCM



Niliwahi kuandika huku nyuma kuhusu mafisadi kadhaa kujaribu kutumia makanisa wa wakristu, mkakati wao ukaja kuonekana wazi kupitia yale ya Rostam na KKKT. Na sasa mkakati huo unaendelea kwa kasi lakini kimya kimya bila vyombo vya habari kuandika ukiendelezwa na Lowassa. Baadaye nikaandika kuhusu Rostam na wenzake wakina Manji kutakana kuwatumia waislamu, hatimaye ikaja kujulikana wazi na ITV wakaanika kuhusu mikakati hiyo. Baada ya kuanikwa huko, kikundi hicho kidogo cha waislam kimeamua kujitokeza wazi wazi na kueleza bayana dhamaria yao ya kueneza udini na ukabila kupitia mihadhara. Tayari kikundi hicho kimeanza kazi katika mikoa kadhaa. Wakati Fulani nikawaeleza kuhusu mafisadi kumtumia Mbatia na ikaja kuonekana wazi katika uchaguzi Tarime. Na kiongozi mmoja wa NCCR alithibitisha kuwa fedha za kampeni walikuwa wakichukua kutoka kwa Makamba.


Sasa baada ya NCCR kuonekana imechafuka sana, sasa umepangwa mkakati mwingine wa kuitumia TLP hususani Mwenyekiti wake bwana Augustine Mrema. Mkakati huo utahusisha Mrema kupita katika mikoa mbalimbali kuisema CHADEMA, Mbowe na Reginald Mengi. Bwana Mrema atakuwa kuwa akikosoa ripoti ya jukwaa la wahariri ambayo iliweka wazi jinsi alivyotumia msiba wa Wangwe kutaka kujinufaisha kisiasa. Chini ya mkakati huo Bwana Mrema atajifanya kuwa rafiiki wa karibu na CUF ili kuwatenga na CHADEMA. Vyama hivi viwili vina ushirikiano wa karibu sana bungeni. Duru za uchunguzi zinaonyesha kwamba Bwana Mrema aliwahi kutembelea kiongozi mmoja mkuu wa nchi na kumuomba amuhakikishie kuwa ataendelea kuwa Mwenyekiti wa TLP dhidi ya anaowaita mamluki ambao wanataka mkutano mkuu wa chama hicho uitishwe ili waweze kumng’oa.


Chanzo cha habari kinaeleza kuwa Bwana Mrema alihakikishiwa kuendelea kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa masharti kwamba atumie chama hicho kuwapoteza maboya CUF katika mazungumzo yao ya mwafaka baina ya vyama hivyo na CCM. Mara baada ya kikao hicho, Mrema alifanya kikao kingine na watuhumiwa wawili wa ufisadi kwa lengo la kujadiliana kuhusu kupata fedha ya kuendesha chama hicho baada ya ruzuku ya chama hicho kupungua kutokana na aliyekuwa Mbunge wake Phares Kabuye kuondolewa. Watuhumiwa hao wawili walimpa sharti bwana Mrema kuwa chama chake na yeye mwenyewe wawe mstari wa mbele kumshambulia Mbowe, CHADEMA na Reginald Mengi. Mwandishi mmoja wa habari aliyepewa jukumu la kuratibu habari za Mrema ameeleza kuwa mkakati mzima kama ukifanikiwa unalengo la kuharibu na kupunguza imani ya upinzani kwa ujumla wake.

Baada ya kumaliza kuishambulia CHADEMA na Mbowe, Bwana Mrema atarejea CCM na kueleza kwamba anarejea CCM kwa sababu ushirikiano wa upinzani umekuvunjika na kwamba wapinzani ni wanafiki. Hata hivyo, Bwana Mrema anakibiliwa na upinzani mkali ndani ya chama chake kutoka kwa kundi la Vijana ambalo limejijenga chini ya aliyekuwa Mbunge bwana Benedict Ntungirehi ambaye analenga kumwondoa Mrema na kuleta mageuzi katika chama hicho. Hali si shwari ndani ya chama hicho baada ya hivi karibuni, chama hicho kukiandikia barua Kituo cha Demokrasia Tanzania(TCD) na nakala kupeleka kwa Rais Kikwete kikimlaumu Mkurugenzi wa Kituo hicho kushindwa kumtetea Kikwete kama Mwenyekiti wa CCM ambaye ni mwanachama wa kituo hicho alipotajwa kwenye orodha ya mafisadi. TLP imeilalamikia TCD kwa kumtetea Mbowe ambaye alikuwa Mkuu wa Msafara wa safari iliyoandaliwa na kituo hicho ya mjini Afrika Kusini ambayo Naibu Katibu Mkuu wa TLP aliyekuwa kwenye msafara huo aliwahi kumtuhumu Mbowe kuwa alifanya sherehe alipopokea Taarifa ya Kifo cha Chacha Wangwe.


Kati ya makombora ambayo Bwana Mrema amejiandaa kuirushia CHADEMA ni tuhuma kuwa chama hicho kinachukua wanachama na viongozi toka TLP na kuwahamaishia CHADEMA. Kati ya viongozi wanaotajwa ni pamoja na aliyekuwa Diwani wa Kata ya Sombetini Bwana Mawazo na aliyekuwa mgombea ubunge wa chama hicho Arusha mjini Bwana Godbless Lema. Habari kutoka Arusha zinaeleza kuwa wakati Bwana Mawazo alitoka TLP na kujiunga na CCM, bwana Lema si ametangaza kwa waandishi wa habari kwamba si mwanachama wa chama chochote cha siasa kwa sasa. Hata hivyo Bwana Mrema amesisitiza kuwa wanachama wake hao wasingeondoka chama hicho kama isingekuwa ushawishi kutoka CHADEMA. Mchambuzi mmoja anasema kwamba kama mkakati huo utafanikiwa basi unaweza kuwa mwanzo wa umaarufu wa CHADEMA kisiasa kuporomoka na ule wa Mrema kupanda na kumfanya apokelewe CCM kama shujaa aliyerejea baada ya kukamilisha kazi maalum.

PM


Leo nimesikia katika magazeti kwamba Mrema amejiandaa kuishambulia Chadema na hasa Mbowe .Mie nimeshangaa sana habari hii .Kama anataka kufa kwa heshima ya ki CCM yeye arudi tu kama wenzake na si kuleta mgororo.This time hatampata mtu watu wamesha amka na hawatampa nafasi hata kidogo.
 
Anything is possible under the sun. We cant deny what you are trying to convince us. Siasa za kibongo ni uchwara tu. To me that will come as no suprise. Leo mtu anapiga kelele jukwaani kwamba CCM mbaya, the next day yuko jukwaa la CCM anasema CCM nzuri na upinzani hovyo. Guys! We are not so stupid jamani. How's that possible? We cant be so stupid watanzania wote. You can only fool some people sometimes, but not all the people all the time. Kama mtu umeamua kuwa mpinzani, kuwa mpinzani mpaka kieleweke (mpaka kile unachokiamini kitimie). Lakini huu upinzani wa kibongo ni kama njaa flani hivi tu.
 
Leo nimesikia katika magazeti kwamba Mrema amejiandaa kuishambulia Chadema na hasa Mbowe .Mie nimeshangaa sana habari hii .Kama anataka kufa kwa heshima ya ki CCM yeye arudi tu kama wenzake na si kuleta mgororo.This time hatampata mtu watu wamesha amka na hawatampa nafasi hata kidogo.

Kama nilivyosema huko nyuma..Hawa watu wasipokuja pamoja basi mambo yataendelea kuwa yale yale.
Nilitowa ushauri similar kabla ya kifo cha Wangwe(RIP) Na bado ninasema tena...Kama kuna pandikizi ushahidi uwekwe...Lakini kama ni ugomvi kwasababu za nguvu za kisiasa then huo ni ubinafsi na kwa taafira zao hao Mbowe na Mrema...Tunafuatilia kwa karibu sana na kama data zikiletwa hapa sisi tutachambuwa tu na ukweli utajitenga...Hii JF hakuna litakaloharibika hapa.
 
Once again ushabiki tu...Humu ndani chadema wengi sana humu...Hivi Single D una guts za kumfananisha Mtikila na Mrema?
Unaweza kufanya hivyo kwa wale wageni wa siasa za bongo lakini si wote ndugu yangu...Wengine tuna memory safi sana kwenye issue kama hizi.

Ushabiki upi?kila mtu anatoa mtizamo wake.
Sina ubishi kwamba kama kuna mtu katika Tanzania ambaye alitegemewa kwamba angeweza kuiongoza nchi kutoka kambi ya upinzani, hasa mwaka 1995, angekuwa Augustine Lyatonga Mrema.

Lakini sasa hivi hafanyi siasa bali ni vituko,hivi kule marangu alikozaliwa uchaguzi wa 2005 alipata kura kiasi gani kulinganisha na miaka ya nyuma?is no more than playing foul games
 
Asante kwa taarifa.
Haya yakitimia, basi atakuwa hana tena nguvu kwani tayari yametabainishwa kabla. Yetu macho na masikio
 
Paparazi nakuunga mkono kwa bandiko lako. Ingawa sina hakika na mikakati hiyo ya Mreka kuvitenganisha Chadema na CUF, lakini taarifa nilizonazo ni kuwa Mrema anahaha kutaka kurejea CCM kwa masharti kuwa aachiwe jimbo moja katika mkoa wa Kilimanjaro. Lengo lake kubwa ni kutaka kuhakikisha anamalizia maisha yake kisiasa akiwa Mbunge. Lakini, ingawa mpango huu umekubaliwa kimsingi na baadhi ya viongozi wa juu, kumekuwa na upinzani mkali kutoka kwa wabunge wa CCM mkoani Kilimanjaro, kila mmoja akikataa kiliachia jimbo kwa ajili ya kumpisha mzee wa Kiraracha
 
Historia ya Mrema dhidi ya ufisadi ikiwekwa hapa nani wa kubishana ama kulinganishwa nayo?
Huyu mzee alipiga vita ufisadi kabla hata msamiati wa ufisadi haujaanza.
Chuki tu binafsi ambazo ni personal dhidi yake kwenye mchezo huu mchafu wa siasa ndizo zilipotufikisha hapa tulipo.
Ibra wewe unataka arudi ccm kwasababu hata msimamo wako hapa jamvini unaelemea upande wa ccm na kwa hivyo sishangai unapodai afanye hivyo ili vyama "Makini" vya upinzani vibaki.

Mkuu JMushi, ukizungumzia historia unaweza kuwaona watu wengi kama malaika. lakini ukirejea kwenye matukio ya sasa hivi, huyo Mrema unayemwlezea wa historia, si Mrema wa sasa, amebadilika sana Mkuu, amini usiamini.
 
Mrema alalamikia Chadema, Jukwaa la wahariri

2008-11-10 (Nipashe)
Na Muhibu Said


Ufa umezidi kudhihirika katika ushirikiano wa kisiasa wa vyama vya upinzani nchini, baada ya Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP), Augustine Mrema, kukituhumu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwamba kimekuwa kikiendesha kampeni nchi nzima kwa lengo la kumsambaratisha kisiasa yeye na chama chake.

Amedai kampeni hizo dhidi yake na chama chake, zimekuwa zikifanywa na Chadema kwa kutumia ripoti ya uchunguzi wa habari za msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe (Chadema), iliyotolewa hivi karibuni na Kamati ya Hiari ya Wahariri.


Kamati hiyo iliyoundwa na Jukwaa la Wahariri, ndiyo iliyofanya uchunguzi huo.


Ushirikiano wa vyama vya upinzani ulioanzishwa Oktoba 10, mwaka jana, hadi sasa unaundwa na vyama vya CUF, Chadema, TLP na NCCR-Mageuzi, kati ya vyama 15 vya kambi vyenye usajili wa kudumu.


Hivi karibuni, Baraza Kuu la Uongozi wa CUF Taifa, lilimuagiza Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad kuviandikia vyama vya Chadema, TLP na NCCR-Mageuzi kuvitaka vieleze kama bado vina nia ya dhati ya kuendelea na ushirikiano huo, baada ya baadhi ya viongozi wa vyama hivyo kutamka kwa nyakati tofauti kwamba, ushirikiano huo umekufa.


Mrema alitoa madai hayo dhidi ya Chadema alipozungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya TLP, Magomeni, jijini Dar es Salaam jana.


``Chadema kampeni wanayoifanya hivi sasa nchi nzima, wanaitumia ripoti hii, ambayo inalenga kuniangamiza mimi na chama changu kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.


Maana leo kuna watu wanasafishwa na wengine wanalindwa. Hivi sasa naambiwa Chadema wako Mwanza wanaendelea na kampeni hiyo,`` alidai Mrema.


Hata hivyo, Mrema alisema anatarajia leo kuweka bayana undani wa kampeni hizo za Chadema anazodai kwamba zinafanywa dhidi yake na chama chake, atakapozungumza na waandishi wa habari.


Alidai Kamati ya Hiari ya Wahariri licha ya wajumbe wake kufahamu anakoishi, iliko ofisi yake na namba yake ya simu, haikujishughulisha kumtafuta ili kumhoji, badala yake iliishia kutoa ripoti, ambayo imemtuhumu kuwa alihusika katika kutumia msiba wa Wangwe kama mradi wa kisiasa kwa kutamka kwamba, Chadema ndio waliomuua Wangwe na kuwashawishi baadhi ya wananchi wa Tarime washushe bendera yake na wapandishe bendera ya TLP.


Alisema kitendo hicho, mbali ya kudhihirisha nia mbaya, ajenda ya siri ya kamati dhidi yake na kutaka kumchonganisha na Chadema na Mbowe, kimemdhalilisha na kumvunjia hadhi na heshima aliyoijenga kwa muda mrefu.
 
Mrema alitisha Jukwaa la Wahariri

[Source Tanzania Daima]

na Mobini Sarya


MWENYEKITI wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema, anakusudia kulishitaki Jukwaa la Wahariri na magazeti kadhaa ikiwa hataombwa radhi kwa kuchafuliwa jina lake, kwa kuhusishwa kutoa maneno ya uchochezi kwenye msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mrema alisema anataka magazeti na wahariri waliotumika kumchafua wamuombe radhi kwenye ukurasa wa mbele sambamba na kuambatanisha fidia ya sh bilioni mbili kila mmoja, vingenevyo atawafikisha mahakamani.

“Nataka Jukwaa la Wahariri waniombe radhi ukurasa wa mbele pamoja na magazeti yaliyohusika kunikashfu bila kujali kuwa mimi Mrema nimewahi kuwa Naibu Waziri Mkuu wa nchi hii, Waziri wa Mambo ya Ndani na mbunge wa muda mrefu, kiongozi niliyefanya kazi hiyo kwa uaminifu mkubwa,” alisema Mrema.

Alisema Oktoba 14 mwaka huu, bila kufuata haki, Jukwaa la Wahariri lilitoa taarifa ya upande mmoja iliyokuwa inalenga kumchafua na kukisambaratisha chama chake huku ikisafisha baadhi ya wanasiasa baada ya kudaiwa aligeuza kifo cha Wangwe ‘mradi wa kisiasa’.

Alisema taarifa hiyo ilitolewa baada ya kamati iliyoundwa kuchunguza kama kwenye kifo kile palitokea vitendo vilivyoashiria vurugu, katika ripoti hiyo watu 18 walihojiwa lakini yeye hakuwahi kupewa nafasi ya kusikilizwa licha ya kwamba wahusika wanajua ofisini kwake na namba yake ya simu.

Alinukuu ripoti hiyo pale inaposema ‘kwa mfano Mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema, kamati ilielezwa kwamba alitumia msiba huo kuchonganisha familia ya Wangwe na CHADEMA kiasi cha kuwashawishi waishushe bendera ya CHADEMA na kupeperusha ya TLP. Alisema CHADEMA wamemuua Wangwe’.

Alidai licha ya taarifa hiyo kujionyesha kuwa ilikuwa na upungufu, ambayo hakidhi ripoti kamili, lakini viongozi wa jukwaa hilo waliisambaza kwenye vyombo vya habari kwa makusudi maalumu hata pale walipotahadharishwa kuwa inapendelea upande mmoja.

Aliongeza kuwa hata pale ilipofikishwa kwenye vyombo vya habari na ikaonekana kuwa taarifa hiyo inaegemea upande mmoja, wahariri wake walishindwa kujisumbua kuisoma zaidi ili wabaini upungufu wake kisha wamuulize, badala yake waliamua kuiandika hivyo hivyo.

Aidha, alisema katika kuonyesha kuwa ulikuwa mpango maalumu wa kuisambaratisha TLP, baada ya siku mbili alifanya mkutano na vyombo vya habari akaeleza athari za ripoti ile, lakini ni gazeti moja lililoandika habari yake na Jukwaa la Wahariri likishindwa kumuomba radhi hadharani na kumwalika kama walivyokuwa wamedai.

“Kwa kuwa wameamua kutumika kusambaratisha chama changu nimeamua kuwapa siku hadi Novemba 13 mwaka huu wakishindwa kuniomba radhi na kunipatia vibilioni mbili nitakwenda, tutakutana mahakamani wanieleza aliyewatuma wanichafue,” alisema.

Kwa mjibu wa malalamiko yake, tayari ameshampatia kazi wakili, Dk. Sengondo Mvungi kupitia Kampuni ya South Law Chamber kuhakikisha inawafungulia mashitaka wahariri hao.

Wahariri hao ni Mwenyekiti wa jukwaa hilo, Sakina Datoo, Mhariri wa gazeti la Nipashe, Jesse Kwayu, Mhariri wa Mwananchi, Theofil Makunga na Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda na Muhingo Rweyemamu, ambaye alikuwa mjumbe wa kamati iliyotoa ripoti hiyo.

Wengine ni mwandishi wa Sauti ya Amerika (VOA) aliyemtaja kama mdhamini wa jukwaa hilo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Saed Kubenea, Katibu wa Jukwaa, Jamila Abdallah na mjumbe, Neville Meena.


MT TAKE: Mrema muda wake umepita hata mwenyewe analitambua hilo. Anaelezea mambo aliyofanya enzi hizo lakini hana la maana la kuonyesha alilofanya siku za karibuni. Katika kila chaguzi anazoshiriki mzee wetu ndivyo anavyozidi kupata uchache wa kura. Sasa anadiriki kutaka kwenda mahakamani kudai vibilioni kadha kutaka kuua magazeti ambayo yamekuwa mwiba kwa mafisadi. Ingefaa ajiuzulu siasa wakati watu bado wanakumbuka mema aliyofanya.
 
JMushi asante sana kwa kuliweka hili sawa.
Kila binadamu ana mapungufu yake,historia itasimama Bwana Mrema kamwe hawezi kuwekwa fungu moja na Mch Mtikila.Kwa maoni yangu Tanzania bado inahitaji mchango wa Bwana Mrema hasa pale wizara ya mambo ya ndani.

Historia iliyo sahihi ni kuwa Mrema ni moja wa watu waliokuwa msitari wa mbele kuyapiga vita mageuzi. Wengine tulioshabikia upepo wa mageuzi bado hadi leo hii tunayo makovu ya harakati hizo yaliyosababishwa na Mrema akilitumia jeshi la polisi kupinga mabadiliko. Naye Mrema alikuja kuonja machungu hayo hayo yaliyotupata alipodandia meli ya wanamageuzi mwaka 1995 (kwa lengo la kugombea uraisi) na wanamageuzi wa kweli kwa ujinga wao wakampokea. Kati ya mwaka 1991 na mwaka 1995, Mrema atakumbukwa daima kwa kutumia virungu na mabomu ya machozi kujaribu kuzuia mageuzi. Hiyo ndiyo historia ya kweli hata kama itapingwa na hao wanaojiita mashabiki wa Mrema.
 
Mag3,
As a politician I believe Mrema is a man who's time has come and gone. Tanzania tunahitaji uongozi unao "inspire" si kupikapika majungu tu. We have so much to learn from the Obama phenomenon.
 
Back
Top Bottom