The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

OK. Lakini tusisahau kwamba hakuna mtu mbaya asiyekuwa na uzuri, and the converse is also true.

Si ni mrema aliyelifanya jiji la DSM lipambwe na vivuli vya miti tunavyoviona sasa? Vipi veranda za wahindi jijini ambazo zilijaa tope na wahindi wakalazimishwa na mrema kujengea concrete pavements? Mmesahau majumba yaliyokuwa yanaonekana kama magofu mijini kwa kupauka lakini amri ya siku saba ya mrema ikayageuza peponi kwa usafi baada ya kukarabatiwa na kupakwa rangi? Ni nani aliyeanzisha police posts kila mtaa kama sio mrema akiwa mambo ya ndani? Au tusemeje sijui, makonda kuvaa sare sio mrema aliyeanzisha kwa zilezile amri za siku saba? Wanawake kufunguka akili kwamba wawapeleke waume zao vituo vya polisi kama wanadundwa sio mrema ambaye alikuwa kipenzi cha wanawake isipokuwa mkewe tu?

Nakumbuka wakati fulani madaktari wa Muhimbili waliandamana kwenda ikulu kupitia wizara ya mambo ya ndani, mapolisi wakataka kuwapiga mabomu ya machozi na kuwazuia, lakini mrema aliwauliza kama waandamanaji hao wameshika silaha yoyote au wanafanya fujo, akaambiwa wanatembea tu na hawafanyi fujo yoyote ila kuyabana magari yanayopita. Mrema akawaambia mapolisi wawaache madaktari waeleze hisia zao kwa amani wasibughudhiwe, akaonekana dirishani kwake akiyafuatilia maandamano hayo yakipita pale kwake, tena baadaye alikwenda mwenyewe tena kwa mguu ikulu kuhakikisha anachoambiwa na wasaidizi wake ni sahihi. Nilishangaa maafisa wa polisi wakiwapanga na kuwaongoza waandamanaji sehemu ya kukaa kwenye lango la kuingilia kwa waziri mkuu na kuwaruhusu viongozi wa waandamanaji kuingia ndani wengine wakilindwa pale langoni kwa amani, raha mustarehe. Pamoja na maneno ya kiuchokozi waandamanaji wengine waliyokuwa wanamrushia afisa wa polisi, yeye aliziba masikio kwa pamba akitazama tu ingawa angeweza kufanya kitu mbaya kama angetaka. Hiyo yote ilikuwa ni amri ya mrema ambaye alimonitor yeye mwenyewe binafsi na tena alichanganyika nao na kuchat au kuwapungia mkono. Je, kuna waziri gani kabla na baada ya mrema kaonyesha ushirikiano huo? Tena wakati ule bosi wake Rais alikuwa Zimbabwe kikazi, ambapo maandamano hayo mapolisi wangegeuza tafsiri kuwa ni uhaini ili wajihalalishie vipigo.

Acha bwana, kweli mrema ana hasi nyingi sana, lakini historia itamkumbuka katika chanya nyingi sana, baadhi yake hizo hapo juu. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Watanzania wa leo ni waelewa sana sio kama enzi zile. Humdanganyi mtu isipokuwa kama mtu huyo naye anatafuta kukudanganya, kazi ikawa kutafuta nani mdanganyaji zaidi. Nani kakwambia kuna mwanasiasa anayeheshimu haki 100% Ukitaka kuwa mwanasiasa mwenye mafanikio makubwa ni lazima uwe msanii uliyebobea. Jibu unaloliita ni sahihi kwa leo sio jibu sahihi la jana na hatujui kesho itakuwaje.

Ndiyo maana naichukia siasa upeo. Sina hakika kama hata huko akhera mwanasiasa anayo nafasi kama inatokea akiwa ndani ya uanasiasa, ni kama na ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia mbinguni au tuseme ngamia kupita tundu la sindano. Ni sawa na makaburi meupe kwa kupakwa chokaa nje lakini ndani kumejaa mifupa. I hate politics! Lazima uwe mbinafsi kwa sababu vinginevyo siasa sio mahali pako. Unapotoa khanga unategemea kukubaliwa na hao unaowapatia khanga. Huo uchungu wanaodai wanao kwa wanachi na maumivu yao sio kweli, wanao uchungu na matumbo yao. Kwani uchungu huo una tija kwa kupewa nafasi ya uongozi wa siasa tu, mbona hawafanyi lolote msipowachagua?

A good politician - relatively though - ni yule anayejitoa kufanya kazi bega kwa bega na wananchi katika jitihada ya kuikwamua jamii kuondokana na matatizo yanayowakabili, pasipo kujiwekea matumaini ya kulipwa fadhila kwa kupewa returns za kuchaguliwa tena na kujitafutia sifa kwa kutumia migongo ya wasio na hatia. Nene mvifile hilo.
 
Ni kweli Mrema ana tabia fulani ambazo huwashangaza watu. hatuwezi kusema moja kwa moja kuwa Mrema hafai au hakufaa wakati wake. kusema hivo ni sawa na kusema kuwa wale waliomuweka kwenye nafasi alizoshika walikuwa hawafai pia au hata wapiga kura wa wakati huo walikuwa hawafai jambo ambalo si kweli. Ubovu WA Mrema na ufinyu wa mawazo yake ni mtizamo wa watu lakini angepewa nafasi ajieleze angeweza kufafanua vizuri. Sasa ikiwa ameona kuwa Kikwete na CCM yake wanafanya vizuri asemeje na yeye ndivo anavoona? Labda ana siri yake pengine ni maandalizi ya kurudi CCM. hiyo ndo staili yake ya kuishi kisiasa ameitumia na amefanikiwa wewe unadhani ataiacha?
 
Huyu mzee alivuma sana. Sina zinakwenda. Akiwa vunjo kwenye mchakato wa uchaguzi 2010, Alikuwa na haya ya kusema.[video=youtube_share;JKNESoyV-i0]http://youtu.be/JKNESoyV-i0[/video]
 
wakati ukuta,,kila enzi na kitabu chake, Mrema ni jembe la enzi, huwezi kuandika historia iwayo yote ya mageuzi tz bila kumtaja mrema,,,,,ni mtu wa kwanza jasiri kutuambia kuwa tunaibiwa,,,,,

Amekuwa mbunge majimbo matatu tofauti na kwa vyama vitatu tofauti na kiongozi wa juu wa vyama vitatu tofauti,,,viwili akiwa mwenyekiti. Amehimili na kushinda hila nyingi za mapinduzi,,walio pambana naye kisiasa wamejikuta wakifa kisiasa yeye anadunda. Amebambikwa kesi nyingi na kushinda,,,,hata sasa ni mtumishi wa watu,,naam umri unasonga ila anajua political timing sana kushinda wengi.

Juzi alisain kutokuwa na iman na waziri mkuu ,,,,na,,,hata kamati aiongozayo imefichua maovu mengi,,,,,niseme tu,,,mrema ni jasiri na mpambanaji,,,,alipoona hata wanamageuzi wanapambana naye,,,,,akawalia timing,,,,,akajishusha kwa ccm,,akafunga goli akapata ubunge chama kikabaki juu na yeye juu. Kuna mengi wana siasa mnapaswa kujifunza kwake:

La kwanza ni kuwekeza kwenye mioyo ya watu.

Pili kuijua jamii unayotaka kuitumikia kabla ya kuingia kichwa kichwa na siasa za msimu za mihemko kama miziki ya ubongo wa fleva ndio maana mtu kama Dr Slaa, Mbowe, Mwingamba na katibu wake mchungaji Golgwa; kina H Mdee, Mnyika nk nk wanaweza kudumu sana kwenye siasa,,,,,,,,

Tumuenzi Mrema na tunaposema mapungufu yake kama nyerere tusisahau wema wake uzalendo wake,,,,na uwanja wa siasa watu wanaocheza sasa umejengwa na mrema ,,,,,sitasubiri akitangulia mbele ya haki,,,nianze unafiki,,,,,,,mpeni haki yake,,,

:spy:
 
bila kutukana wanaojua mchango wa agustino lyatonga mrema,, katika nji hii bila kuweka propaganda waje humu,,,,
 
Mrema ni dume la mbegu aka jogoo, japo anamapungufu yake lakini ni mmojawapo ya watu walio imarisha upinzani. Acheni unafiki ni nani aliyetetea mama zetu wasipigwe na baba zetu enzi zile? yuko wapi waziri kama mrema wa enzi zile aliyeweza kutoa siku saba na amri yake kutekelezwa? yuko wapi waziri anayeweza kumkamata mke wa raisi airport kwa magendo zaidi ya Mrema? MREMA IYO NI PUN'GA.
 
2007-08-27
Na Simon Mhina


Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustine Mrema, amesema wapinzani wameunda vikosi viwili, cha anga na nchi kavu kwa ajili ya kuishambulia CCM.

Aidha, amesema ili kutekeleza azma hiyo, wameshakamilisha mipango ya kupata helikopta zingine nne.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, mwanasiasa huyo alisema mipango ya wapinzani kuzunguka nchi nzima na kuwaeleza wananchi juu ya kilichomsibu Mbunge Zitto Kabwe, imepangwa na viongozi wote.

Alisema maneno aliyonukuliwa akiyasema Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia yametungwa na CCM.

"Mimi CCM naijua sana, wameshajua wamejifunga wenyewe na sisi tunataka tuongezee bao lingine! Wameunda vitengo vingi vya propaganda, kikiwemo kile cha kwenye vyombo vya habari," alisema.

Hata hivyo, Bw. Mrema alisisitiza kuwa mbinu hizo chafu haziwezi kuwavunja nguvu kwa vile sio mpya, na kwamba CCM walizitumia dhidi yake na upinzani kwa miaka mingi.

"Propaganda ya kwanza ilikuwa kwamba Mrema ni CCM, ya pili wakasema Mrema ni mbinafsi, sasa wameona tumeungana, wanaanzisha fitina, lakini wamekwama," alisema.

Alisisitiza kuwa mwaka 2010, wataweka mgombe mmoja wa urais na mbunge mmoja wa upinzani kila jimbo.

Bw. Mrema alisema wapinzani wamegundua kila walikopita kwamba wananchi wamefurahishwa na muungano wao.

Alisema itakuwa ni kituko cha mwaka kwa viongozi wa upinzani kuvunja umoja huo.

Hata hivyo, alisema hakuna uwezekano wa umoja huo kuvurugika kwa sababu hakuna mkakati wanaopanga, bila kushirikishana wote.

Kuhusu 'brigedi' za mashambulizi, Bw. Mrema alisema wameamua kuunda kikosi cha anga na kile cha ardhini.

Akifafanua, alisema kama ilivyo katika vita ya kawaida, mashambulizi ya anga yanarahisisha, lakini hayawezi kuleta ushindi, bila kushuka chini.

Alisema kikosi cha anga ambacho kitatumia helkopta hizo, kitaongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Bw. Freeman Mbowe.

Alisema kikosi hicho, kitakachowajumuisha makomandoo kadhaa kama Zitto Kabwe, kitakuwa na lengo la kufanya mashambulizi ya nguvu katika vijiji na miji, ambayo ni ngome ya CCM, tena kwa haraka na kwa muda mfupi.

Alisema kikosi cha ardhini, ambacho ndicho chenye jukumu kubwa, kitakuwa na viongozi watatu, Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), James Mbatia (NCCR) na yeye mwenyewe.

Alisema viongozi hao watakuwa na jukumu la kupita kwa miguu sehemu ambazo zilifikiwa na helkopta, kwa ajili ya kuzisafisha na kuziteka.

Alisema safari hizo zimeshaanza na CCM wameshagundua mkakati huo na kuona hatari inayowakabili, na ndio maana wameanza propaganda kupitia vyombo vya habari.


SOURCE: Nipashe
johnthebaptist pole pole ajifunze kwa Lyatonga. Awaachie ccm chama chao
 
bila kutukana wanaojua mchango wa agustino lyatonga mrema,, katika nji hii bila kuweka propaganda waje humu,,,,
Kama alivyosema mleta mada, Mrema baada ya kutimuliwa CCM kunako 1994 baada ya kushindwa kuheshimu maamuzi halali ya chama alikwenda upinzani. Chama kilichokuwa na nguvu miaka hiyo ni NCCR Mageuzi, kukiwa na akina Mabere Marando na wengine. Akina Steven Wassira waliingia baadaye baada ya kusigana CCM. Mrema alileta amsha amsha kubwa sana kwa upinzani na kuhuisha juhudi za kuunda upinzani imara.
 
Back
Top Bottom